JKT wamekanusha vikali kuwepo na vifo kwenye mafunzo ya muda mfupi ya vijana waliomaliza kidato cha sita, habari hizo zilitolewa ktk mtandao huu wa jf na mmoja wa watumiaji. hivyo siri ya jeshi je ilivuja?
====================
Wasemaji wa Jeshi la Ulinzi Tanzania (JWTZ), Luteni
Kanali Elick Komba (kushoto) na Meja Emmanuelo Murugi,
wakizungumza na waandishi wa habarijijini Dar es Salaam
jana kutoa ufafanuzi kuhusiana na madai ya vifo vya baadhi ya
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limekanusha taarifa zinazosambazwa kupitia simu na mitandao ya kijamii kuwa vijana watatu wamefariki baada ya kufanyiwa vitendo vya kikatili katika mafunzo yanayoendelea kwenye kambi ya JKT Oljoro, Arusha.
Msemaji wa JKT, Luteni Kanali Erick Komba, alikanusha taarifa zinazoenezwa juu ya kuhusika kwa jeshi hilo na vifo hivyo kikiwamo kifo cha mwanamke aliyefariki katika kambi hiyo.
Kanali Komba alisema kumezuka taarifa zenye nia ya kulichafua JKT na kupotosha jamii baada ya kifo cha Honorata aliyefariki kwa upungufu wa damu (anaemia).
"Taarifa zilizosambazwa ni uzushi, hakuna vifo vya vijana watatu vilivyotokana na ukatili katika kambi ya JKT Oljoro. Ukweli ni kwamba amefariki kijana mmoja anayeitwa Honorata Oiso," Kanali Komba aliwaambia waandishi wa habari jana.
"Kuna mtu anayetumia kifo hiki kusambaza ujumbe wa uongo kwa jamii. Wazazi wake wamethibitisha ukweli juu ya kifo cha mtoto wao," aliongeza.
Source: Nipashe
====================
Wasemaji wa Jeshi la Ulinzi Tanzania (JWTZ), Luteni
Kanali Elick Komba (kushoto) na Meja Emmanuelo Murugi,
wakizungumza na waandishi wa habarijijini Dar es Salaam
jana kutoa ufafanuzi kuhusiana na madai ya vifo vya baadhi ya
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limekanusha taarifa zinazosambazwa kupitia simu na mitandao ya kijamii kuwa vijana watatu wamefariki baada ya kufanyiwa vitendo vya kikatili katika mafunzo yanayoendelea kwenye kambi ya JKT Oljoro, Arusha.
Msemaji wa JKT, Luteni Kanali Erick Komba, alikanusha taarifa zinazoenezwa juu ya kuhusika kwa jeshi hilo na vifo hivyo kikiwamo kifo cha mwanamke aliyefariki katika kambi hiyo.
Kanali Komba alisema kumezuka taarifa zenye nia ya kulichafua JKT na kupotosha jamii baada ya kifo cha Honorata aliyefariki kwa upungufu wa damu (anaemia).
"Taarifa zilizosambazwa ni uzushi, hakuna vifo vya vijana watatu vilivyotokana na ukatili katika kambi ya JKT Oljoro. Ukweli ni kwamba amefariki kijana mmoja anayeitwa Honorata Oiso," Kanali Komba aliwaambia waandishi wa habari jana.
"Kuna mtu anayetumia kifo hiki kusambaza ujumbe wa uongo kwa jamii. Wazazi wake wamethibitisha ukweli juu ya kifo cha mtoto wao," aliongeza.
Source: Nipashe