JKT KWA MUJIBU WA SHERIA 2019.

JKT KWA MUJIBU WA SHERIA 2019.

We are what we eat and do; balanced diet, exercises and natural remedies; no smoking, no alcohol and toxic intakes. Jaribu utaona (kama hujachelewa).


changamoto muda ratiba iko hovyo unaweza kujitahidi one month ila kwa mbinde.

kila baada ya 1.5 mpka 2 month hapo kati lazima unakuta nimeshakunywa alcohol mara 3 mpka 4.

kitu kinanibeba sijaachia mwili
 
Sijui kwa sasa nini kinaweza kutokea iwapo anayetakiwa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria hatakwenda JKT. Kabla ya JKT kuahirisha mafunzo kwa mujibu wa sheria; yeyote aliyekwepa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria (Form six leavers na Form four aliyepitia kozi inayozidi miezi sita), yule Form six leaver asingepata nafasi ya kwenda University (Ukizingatia kuwa wakati ule kulikuwa na UDSM pekee) wala asingepata Direct Employment popote; na yule wa Form four na kozi iliyozidi miezi sita asingepata ajira serikalini.
JKT ya wakati ule (mimi nilikwenda Juni 1983 hadi Juni 1983 OPR NGUVU KAZI - 835 KJ) ilikuwa ni mwaka mmoja kamili; acha sasa hivi miezi sijui mitatu au sita!! Mbona ni burudani tu hiyo?
Enzi zile miezi 6 net ni ya recruitment; kwata na ngarambe za ukweli (no joke). Lakini ndani ya kipindi hicho mtu unajifunza mambo mengi sana yenye manufaa kwa maisha yako binafsi, japo mwanzoni utaona ni mateso; but at the end siku unayoondoka kambini unaweza kutokwa na machozi unapoagana na maafande uliowaona kuwa wanoko wakati wa mafunzo.
Ushauri wangu kwa vijana mnaotakiwa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria, nendeni; hamtajutia bali at the end mtafurahia wala hamtajutia.
Dada yangu mkubwa alikwenda miaka JKT Kwa mujibu wa sheria inaanzishwa. Anasema asubuhi walipewa nusu loaf ya mkate na chai, weekend unaweza kipande cha sabuni mbuni. Wakati huo ilikuwa miezi sita
 
Kisheria, unapaswa kwenda. Usipoenda unakuwa umeivunja sheria. Watakufanyaje? Hakuna anayejua.

Ila kimantiki, hakuna faida yoyote.
Yanayosemwa kuhusu uzalendo, ni maneno matamu tu.
Kupata scholarship au ajira ya serikali itakuwa ngumu sana
 
Dada yangu mkubwa alikwenda miaka JKT Kwa mujibu wa sheria inaanzishwa. Anasema asubuhi walipewa nusu loaf ya mkate na chai, weekend unaweza kipande cha sabuni mbuni. Wakati huo ilikuwa miezi sita
Enzi zetu OPR. NGUVU KAZI 1983/84 MWAKA MMOJA; kwa kambi niliyokuwa mimi 835 KJ Mgambo JKT Handeni, mambo ya loafs of bread na chai kwa kuruta na Service man/ girl ilikuwa hakuna. Hayo yalikuwa yanafanyika Officer's na Sargent's Mess wakihudumiwa na ma-service girl. Huku jiko kuu ulikuwa ni mwendo wa uji sugarless, ukipenda weka chumvi au/na limao. Kuna wakati tulikunywa uji wa serena (mtama mwekundu). Ration yako lazima uile; usipokuwepo (kwa taarifa), share yako utaikuta hata kama ni kuanzia uji, cha mchana na cha jioni. Siku za nyama zilikuwa mbili kwa wiki, J'tano na Ijumaa; lakini siku hizo zilikuwa mbaya sana kwa kuruta; mikwara ilianza tangu asubuhi; harassment za kutosha kwenye kwata, mpaka unapofika wakati wa lunch kuruta wako nyang'anyang'a; pale usawa wa gudulia afande ni mkali ile mbaya; kwenye gudulia la nyama wengi walikuwa wanaambulia mchuzi au finyango moja. Lengo la maafande ni ku-save nyama nyingi inavyowezekana, ili wazivushe kwenye vitini kwenda makwao!! Ukitaka nyama ni kutoroka (kujongomea) kuanzia alfajiri kwenda kijijini Gendagenda, Kwa Msanga, Kwa Bojo kwenda kula kuku au ndezi (a.k.a. panya buku) kwa wanakijiji kwa kubadilishana na mess tin (mustin) ya maharage mekundu yaliyoibiwa ration store. Baada ya msosi huo wa ugali kwa ndezi au jogoo; unashushia na pombe ya mnazi au boha, kabla ya kurudi kambini giza ukiwa na mzigo wa miwa au/na Nazi. Unaweza kulazimika kutoroka wiki nzima au zaidi mkitafutana na maafande; ni mwendo wa kubadili bweni la kulala na vitanda; mpaka anakata tamaa; siku mkigongana anaishia kuaema tu wewe kuruta wewe....!! Hiyo raundi inapita; another episode comes and goes, mwishowe unatoboa. Hakuna cha Me wala Ke; wote mtindo mmoja.
 
Kupata scholarship au ajira ya serikali itakuwa ngumu sana
Ajira serikalini atapata tu bila shida yoyote ile hata asipo kwenda

Manake sio kwamba wote wanaomaliza form 6 wanakwenda JKT ni baadhi tu, Ingekuwa ni wote hapo ndo tungesema hiko kitu kinaweza kuwa applied.

Lakini labda kama unaongelea ajira za kiaskari au za majeshi.
 
Kuna dada yetu hakwenda 2016 na mwaka huu ana graduate....
 
We are what we eat and do; balanced diet, exercises and natural remedies; no smoking, no alcohol and toxic intakes. Jaribu utaona (kama hujachelewa).
Shikamoo mama. Ila hayo mavazi sio fair kwa sisi vijana wako. Na wakwe zako wanatuvalia hivyo hivyo na ulivyo na mwili mdogo dah mama....
 
Nilimaanisha miaka 36 tangu nimalize JKT; nilikwenda nikiwa na miaka 21, I'm now 57 but still going strong!! (Joking)
OK sawa Mkuu,nadhani kwa sasa hata chai huweki sukari,utakuwa unatumia asali kwa sana,ahaaaa ahaaaa
 
Mimi nilienda jkt mwaka Jana na kuna wenzangu hawakuenda lakin wamepata chuo pamoja na mkopo,,lakin ukienda jeshin kuna faida pia kuna changamoto mbalimbali kwa mfano sisi tulipata shida sana wakat wa kuapply vyuo na weng wetu walikosa vyuo kutokana na kuwa jeshin
Upande mwengine kuna fursa mbalimbali kwa mfano mwaka Jana tuliokuwepo kambi ya nachingwea kulikua na usaili wa kwnda kusomea mafunzo ya afisa kadet( nyota moja) kwaio Kama hukuenda jesh huwez kupata fursa hiyo kwaio wenye uhitaj walichukuliwa na Sasa wapo Arusha kwenye course wakitoka wanakua watu wengine kabisa ambao wanakua wameshapiga hatua kimaisha so my advice Kama unaona kuna umuhimu nenda na Kama unahisi ni kupoteza muda unaweza ukaacha na kufanya mambo mengine ambayo yatakuingizia kipato
 
Shikamoo mama. Ila hayo mavazi sio fair kwa sisi vijana wako. Na wakwe zako wanatuvalia hivyo hivyo na ulivyo na mwili mdogo dah mama....
Marahaba kijana; hujambo? Unaonekana kukerwa na mavazi yangu, pole. Mme wangu hunifanyia shopping ya nguo zangu na mara nyingi hunichagulia nivae nini nami hufanya hivyo kwake. Ni muhimu kwa furaha ya maisha yetu ya ndoa. Haiwezekani kuondoa au kuthibiti dhana ya kila anayetuona; muhimu kwetu ni kutokuingilia maisha ya watu wengine na familia yetu kuwa na furaha. Uwe na amani.
 
Shikamoo mama. Ila hayo mavazi sio fair kwa sisi vijana wako. Na wakwe zako wanatuvalia hivyo hivyo na ulivyo na mwili mdogo dah mama....
[/QUOT
Pole kijana wangu; mme wangu ndiye huninunulia nguo azipendazo nivae; mimi ni ua lake; I stay in any vase he prefers.
 
Mimi nilienda jkt mwaka Jana na kuna wenzangu hawakuenda lakin wamepata chuo pamoja na mkopo,,lakin ukienda jeshin kuna faida pia kuna changamoto mbalimbali kwa mfano sisi tulipata shida sana wakat wa kuapply vyuo na weng wetu walikosa vyuo kutokana na kuwa jeshin
Upande mwengine kuna fursa mbalimbali kwa mfano mwaka Jana tuliokuwepo kambi ya nachingwea kulikua na usaili wa kwnda kusomea mafunzo ya afisa kadet( nyota moja) kwaio Kama hukuenda jesh huwez kupata fursa hiyo kwaio wenye uhitaj walichukuliwa na Sasa wapo Arusha kwenye course wakitoka wanakua watu wengine kabisa ambao wanakua wameshapiga hatua kimaisha so my advice Kama unaona kuna umuhimu nenda na Kama unahisi ni kupoteza muda unaweza ukaacha na kufanya mambo mengine ambayo yatakuingizia kipato
Walitumia criteria gani kuwachukua hao kwenda monduli
Na je walipita kambi hio tu au kambi zote TZ
 
Machungwa, machenza, madansi, malimao, ndimu vyote hivyo tulivikuta na vingine tukaongezea. Ulikuwepo ujenzi wa kiwanda cha juice na tulimenyeka kwelikweli kufyatua matofali huko juu karibu na kwa Afande C.O. Lt. Col. Mtono; Adjutant alikuwa Lt. Mushi; O.P.T.O. Lt. Mande; U.P.M. Lt. Nyenyema na Pay Sgt S/Sgt Milanzi; bila kuwasahau RSM Sgt Busongo na Mpishi Mkuu CPL Ndetaulo; MP Commamder CPL Dick na Green Kwanja RP Justine (alikuwa mnoko ile mbaya). Acha tu; yalikuwa maisha ya aina yake yaliyotufundiasha mambo mengi kweli kwenye maisha ya kawaida; VIVA JKT.
Baadhi ya watu uliowataja, hata mimi nilikutana naa hapo Mgambo JKT mwaka 1981. Wakati huo, Busongo hakuwa RSM. Ndetaulo na Mtono walikuwapo.
 
Back
Top Bottom