JKT KWA MUJIBU WA SHERIA 2019.

JKT KWA MUJIBU WA SHERIA 2019.

Kwa hiyo nchi inalindwa na JKT?? Tena mujibu wa sheria,

Sent using Jamii Forums mobile app
Nchi inalindwa na wananchi wenyewe; kila mmoja katika uga wake; wapo mstari wa mbele nako kuna makamanda, wapiganaji n.k. JKT ni sehemu ya jeshi la ulinzi ndio maana viongozi wake wote ni waajiriwa wa JWTZ bila chenga. Mhitimu yeyote wa JKT ni askari kamili wa akiba, ndio maana anapewa Force Number; wakati wowote ukihitajika utaripoti utakapoelekezwa kwenda kwa kazi utakayoagizwa. JKT ni chungu cha kupika vijana kwa majeshi mbalimbali nchini, liwe jeshi la ulinzi au majeshi ya usalama polisi na magereza; hata vyombo vingine vya usalama kama PCCB, TISS, Paramilitary wa National Parks, Private Guards n.k.
Hayo yote kwako yataonekana hayana maana kwa sababu una negative attitude na JKT. Usiende, just go enjoying your lavish dot com life wherever you are.
 
Nchi inalindwa na wananchi wenyewe; kila mmoja katika uga wake; wapo mstari wa mbele nako kuna makamanda, wapiganaji n.k. JKT ni sehemu ya jeshi la ulinzi ndio maana viongozi wake wote ni waajiriwa wa JWTZ bila chenga. Mhitimu yeyote wa JKT ni askari kamili wa akiba, ndio maana anapewa Force Number; wakati wowote ukihitajika utaripoti utakapoelekezwa kwenda kwa kazi utakayoagizwa. JKT ni chungu cha kupika vijana kwa majeshi mbalimbali nchini, liwe jeshi la ulinzi au majeshi ya usalama polisi na magereza; hata vyombo vingine vya usalama kama PCCB, TISS, Paramilitary wa National Parks, Private Guards n.k.
Hayo yote kwako yataonekana hayana maana kwa sababu una negative attitude na JKT. Usiende, just go enjoying your lavish dot com life wherever you are.
Hapo 100% umeizungumzia JKT hii ya kujitolea na sio hii ya mujibu wa sheria, ambapo ndio mapolisi , jwtz, tanapa, huchukua askari kutoka huko kwa ajili ya mafunzo. Nilipita Jkt mujibu wa sheria Op kikwete
 
Hapo 100% umeizungumzia JKT hii ya kujitolea na sio hii ya mujibu wa sheria, ambapo ndio mapolisi , jwtz, tanapa, huchukua askari kutoka huko kwa ajili ya mafunzo. Nilipita Jkt mujibu wa sheria Op kikwete
Mimi nilikuwa Opr. Nguvu Kazi 835 KJ Mgambo JKT Juni 1983 hadi Juni 1984; Fn. T49_ _ kwa mujibu wa sheria. Julai 1984 niliitwa na kuajiriwa JWTZ. Siyo mimi peke yangu, nilikutana hukona wenzangu wengine niliokuwa nao 835 KJ, Compulsory na wa kutoka vikosi vingine. Katika hali ya kawaida volunteers wengi walikuwa ni STD VII leavers; kwa fani kama za urubani, uhandisi au udaktari jeshini panahitajika vijana wenye elimu ya fizikia, hisabati, kemia n.k. Kama si vijana wa Form VI kuchukuliwa, wataalam hao kwenye majeshi watapatikanaje? Sikukatalii hoja yako kwamba ni volunteers pekee waliajiriwa kwenye majeshi; JKT imepitia hatua nyingi miaka kama 20 iliyopita, na kuna wakati hata compulsory hawakuingizwa kabisa.
 
Mimi nilikuwa Opr. Nguvu Kazi 835 KJ Mgambo JKT Juni 1983 hadi Juni 1984; Fn. T49_ _ kwa mujibu wa sheria. Julai 1984 niliitwa na kuajiriwa JWTZ. Siyo mimi peke yangu, nilikutana hukona wenzangu wengine niliokuwa nao 835 KJ, Compulsory na wa kutoka vikosi vingine. Katika hali ya kawaida volunteers wengi walikuwa ni STD VII leavers; kwa fani kama za urubani, uhandisi au udaktari jeshini panahitajika vijana wenye elimu ya fizikia, hisabati, kemia n.k. Kama si vijana wa Form VI kuchukuliwa, wataalam hao kwenye majeshi watapatikanaje? Sikukatalii hoja yako kwamba ni volunteers pekee waliajiriwa kwenye majeshi; JKT imepitia hatua nyingi miaka kama 20 iliyopita, na kuna wakati hata compulsory hawakuingizwa kabisa.
Hiyo sasa ndio ilikua JKT , sio hii ya kwetu ya miezi mi 3 hakuna cha ziada kikubwa tulichopata zaidi cheti ambacho hatukitumii popote pale iwe kuomba kazi au kitu chochote, tupo kwenye ulimwengu ambao muajiri anataka uzoefu wa miaka 2+ , na vyeti vya kitaaluma
 
Sijui kwa sasa nini kinaweza kutokea iwapo anayetakiwa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria hatakwenda JKT. Kabla ya JKT kuahirisha mafunzo kwa mujibu wa sheria; yeyote aliyekwepa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria (Form six leavers na Form four aliyepitia kozi inayozidi miezi sita), yule Form six leaver asingepata nafasi ya kwenda University (Ukizingatia kuwa wakati ule kulikuwa na UDSM pekee) wala asingepata Direct Employment popote; na yule wa Form four na kozi iliyozidi miezi sita asingepata ajira serikalini.
JKT ya wakati ule (mimi nilikwenda Juni 1983 hadi Juni 1983 OPR NGUVU KAZI - 835 KJ) ilikuwa ni mwaka mmoja kamili; acha sasa hivi miezi sijui mitatu au sita!! Mbona ni burudani tu hiyo?
Enzi zile miezi 6 net ni ya recruitment; kwata na ngarambe za ukweli (no joke). Lakini ndani ya kipindi hicho mtu unajifunza mambo mengi sana yenye manufaa kwa maisha yako binafsi, japo mwanzoni utaona ni mateso; but at the end siku unayoondoka kambini unaweza kutokwa na machozi unapoagana na maafande uliowaona kuwa wanoko wakati wa mafunzo.
Ushauri wangu kwa vijana mnaotakiwa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria, nendeni; hamtajutia bali at the end mtafurahia wala hamtajutia.
Kama OP's zenu ndio mliopanda machungwa pale mgambo hakika mbalikiwe sana...
ngurutu wanashambulia chungwa hadi wanabloo wenyewe
 
Kama OP's zenu ndio mliopanda machungwa pale mgambo hakika mbalikiwe sana...
ngurutu wanashambulia chungwa hadi wanabloo wenyewe
Machungwa, machenza, madansi, malimao, ndimu vyote hivyo tulivikuta na vingine tukaongezea. Ulikuwepo ujenzi wa kiwanda cha juice na tulimenyeka kwelikweli kufyatua matofali huko juu karibu na kwa Afande C.O. Lt. Col. Mtono; Adjutant alikuwa Lt. Mushi; O.P.T.O. Lt. Mande; U.P.M. Lt. Nyenyema na Pay Sgt S/Sgt Milanzi; bila kuwasahau RSM Sgt Busongo na Mpishi Mkuu CPL Ndetaulo; MP Commamder CPL Dick na Green Kwanja RP Justine (alikuwa mnoko ile mbaya). Acha tu; yalikuwa maisha ya aina yake yaliyotufundiasha mambo mengi kweli kwenye maisha ya kawaida; VIVA JKT.
 
Sijui kwa sasa nini kinaweza kutokea iwapo anayetakiwa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria hatakwenda JKT. Kabla ya JKT kuahirisha mafunzo kwa mujibu wa sheria; yeyote aliyekwepa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria (Form six leavers na Form four aliyepitia kozi inayozidi miezi sita), yule Form six leaver asingepata nafasi ya kwenda University (Ukizingatia kuwa wakati ule kulikuwa na UDSM pekee) wala asingepata Direct Employment popote; na yule wa Form four na kozi iliyozidi miezi sita asingepata ajira serikalini.
JKT ya wakati ule (mimi nilikwenda Juni 1983 hadi Juni 1983 OPR NGUVU KAZI - 835 KJ) ilikuwa ni mwaka mmoja kamili; acha sasa hivi miezi sijui mitatu au sita!! Mbona ni burudani tu hiyo?
Enzi zile miezi 6 net ni ya recruitment; kwata na ngarambe za ukweli (no joke). Lakini ndani ya kipindi hicho mtu unajifunza mambo mengi sana yenye manufaa kwa maisha yako binafsi, japo mwanzoni utaona ni mateso; but at the end siku unayoondoka kambini unaweza kutokwa na machozi unapoagana na maafande uliowaona kuwa wanoko wakati wa mafunzo.
Ushauri wangu kwa vijana mnaotakiwa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria, nendeni; hamtajutia bali at the end mtafurahia wala hamtajutia.
Miaka 10 badaye ndy nimetafutwa!! Mi ndy kwanza wa 2014!!
Heshima yako Baba!!
 
Machungwa, machenza, madansi, malimao, ndimu vyote hivyo tulivikuta na vingine tukaongezea. Ulikuwepo ujenzi wa kiwanda cha juice na tulimenyeka kwelikweli kufyatua matofali huko juu karibu na kwa Afande C.O. Lt. Col. Mtono; Adjutant alikuwa Lt. Mushi; O.P.T.O. Lt. Mande; U.P.M. Lt. Nyenyema na Pay Sgt S/Sgt Milanzi; bila kuwasahau RSM Sgt Busongo na Mpishi Mkuu CPL Ndetaulo; MP Commamder CPL Dick na Green Kwanja RP Justine (alikuwa mnoko ile mbaya). Acha tu; yalikuwa maisha ya aina yake yaliyotufundiasha mambo mengi kweli kwenye maisha ya kawaida; VIVA JKT.
Baba nakuona..
 
Nenda Mdogo wangu
Kule utajifunza vingi Sana..
Nidhamu , uzalendo ... Mafunzo ya kijeshi n. k
 
Tatizo kubwa JKT ya sasa imerudishwa "kisiasa" zaidi kuliko kiuhalisia. Kwa sasa budget yao hiwawezeshi kuita kila kijana aliyemaliza F6. Matokeo yake wanacheza kamari tu na ndio maana hawafuatilii nani hakwenda (labda mambo yabadilike).
Kuna hili la mikopo isiyo eleweka- kama umepata nafasi ya kutengeneza hela kidogo na huna hakika na mkopo au una hakika hutapata unafikiri ni kipi cha msingi zaidi kwenda JKT au utafute hela ikusaidie chuo. Enzi zetu ilikuwa ni sifa kubwa kwenda JKT (miezi 3 mafunzo ya kijeshi na 3 kupiga kazi) kabla hawajabadilisha kwenda mwaka mmoja. Ukifaulu chuo ( E mbili zilitosha kabisa hata medicine) na hatukuwa na mkopo bali serikali ililipa. Ukimaliza chuo kwa miezi 18 unakuwa chini ya JKT na serikali inakata percent ya mshahara wako. Hapo unaona kwa nini uwe mzalendo wa kwenda au kujipeleka JKT. Nauli walitoa wao.
Kwa hali ya sasa inabidi uamue tu ukiona mantiki ya kwenda unakwenda ingawa sijui kama unaweza kujifunza au kufundishwa uzalendo ukiangalia siasa zetu za sasa. Ukakamavu ndio utapata ingawa kuna njia nyingine za kupata ukakamavu.
Mwisho kabisa umesha sikia - waziri wetu wa ulinzi wa sasa enzi hizo alipo maliza F6 alikwepa JKT kwa kisingizio cha kwenda nnje kusoma na hadi leo hajakwenda huko kama kuruta.
 
Sijui kwa sasa nini kinaweza kutokea iwapo anayetakiwa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria hatakwenda JKT. Kabla ya JKT kuahirisha mafunzo kwa mujibu wa sheria; yeyote aliyekwepa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria (Form six leavers na Form four aliyepitia kozi inayozidi miezi sita), yule Form six leaver asingepata nafasi ya kwenda University (Ukizingatia kuwa wakati ule kulikuwa na UDSM pekee) wala asingepata Direct Employment popote; na yule wa Form four na kozi iliyozidi miezi sita asingepata ajira serikalini.
JKT ya wakati ule (mimi nilikwenda Juni 1983 hadi Juni 1983 OPR NGUVU KAZI - 835 KJ) ilikuwa ni mwaka mmoja kamili; acha sasa hivi miezi sijui mitatu au sita!! Mbona ni burudani tu hiyo?
Enzi zile miezi 6 net ni ya recruitment; kwata na ngarambe za ukweli (no joke). Lakini ndani ya kipindi hicho mtu unajifunza mambo mengi sana yenye manufaa kwa maisha yako binafsi, japo mwanzoni utaona ni mateso; but at the end siku unayoondoka kambini unaweza kutokwa na machozi unapoagana na maafande uliowaona kuwa wanoko wakati wa mafunzo.
Ushauri wangu kwa vijana mnaotakiwa kwenda JKT kwa mujibu wa sheria, nendeni; hamtajutia bali at the end mtafurahia wala hamtajutia.


huyoo kwenye avatar yako ni mke wako au ni wewe??
 
Kisheria, unapaswa kwenda. Usipoenda unakuwa umeivunja sheria. Watakufanyaje? Hakuna anayejua.

Ila kimantiki, hakuna faida yoyote.
Yanayosemwa kuhusu uzalendo, ni maneno matamu tu.
Wewe faida unataka iwe pesa tu sababu una njaa ya pesa
 
Unakosea kumpotosha Dogo.
Acha aende akajifunze.
Nailikua najaribu tu kumjibu kulingana na alivyo uliza kwani ni ukweli uliothabiti kwamba hamna madhara yoyote kwenye kupata mkopo ama kupata chuo kama asipokwenda JKT

Ila kama ni mkakamavu aende tu lakn kama oya oya na hataki kuchosa mwili wake kabisa namshauri abaki nyumbani tu.
 
Back
Top Bottom