JK Safarini tena UK

JK Safarini tena UK

Nenda Jk. Nenda Baba! Katuletee wawekezaji na fursa nyingine kwani Tanzania siyo kisiwa.
 
Hata kama kaalikwa labda jamaa ndo anaenda kuwashawishi watuletee viwanda na hapa kwetu.
Hata kama mtakataa Ukweli utajitokeza tu maana ukweli ni kama Kikohozi na moshi unaofuka:-
1. hata siku moja hakuna urafiki kati ya matajiri na maskini
2. Urafiki huo wa kualikwa kwa matajiri ni hatari kwa nchi kama yetu
3. Kwani umeona kwenye bajeti yetu ya mwaka 2013/14 waziri Mgimwa ameyaorodhesha
makampuni makubwa wanalipa na kuchangia kodi yoyote katika uchumi wetu
4. Kwani makampuni yanajileta yenyewe si jamaa anawaalika na tunaambiwa kwamba
wawekezaji wanachangia kuinua uchumi wetu wakati hawalipi kodi. Ama kweli hii ni nchi
ya Kalaghabao.
5. Wajinga ndio waliwao tumtegemee Mungu tu serikali hii haina dhamira ya dhati
kuboresha maisha ya walalahoi.


Unajua watu wanaweka ushaki kila mahali bila kujali maslahi ya nchi viongozi wakubwa wanapofanya ziara wanafanya na tathimini gharama na tija ya safari husika sasa ukialikwa kila mwezi utakuwa unasafiri tu kisa umealikwa,
 
Jamaa!ni noma au ana vimada hukO sio bure! Kwa hiyo nchi kamuachia mzee wa kulia:car:
 
Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa wakuu wachi walioalikwa kuhudhuria mkutano wa nchi zenye Viwanda Vingi G8,mkutano unaanza kesho UK.
my Take;
Safari kama hii ina Tija gani,na Jk anafuraha gani ya kuhudhuria mkutano wa wenye viwanda wakati ambapo serikali imeshindwa kuendeleza viwanda vya ndani.
Source;ITV


Wajinga ndio waliwao. Safari ya kikwete haina tija kwetu zaidi ya kwenda kuweka mipango ya kupora rasilimali zetu. Nimesikia kikwete anaenda na waziri wa madini na nishati (muhongo) na waziri wa ardhi, nyumba, na maendeleo ya makazi (tibaijuka). Swali la kujiuliza, kwa nini aalikwe kikwete na si mugabe au kenyetta, au museveni? Kwenda na hawa mawaziri kunanipa shaka!!
 
Umaarufu kazi sana, akialikwa makelele, asipoalikwa eti kachokwa akialikwa nako shida, sasa hakuna migomo, maandamano kilichobaki ni kutafuta vi thread kama hivi kutoa kihoro chao cha kukosa Urais!
 
mwenyewe ashawahi sema mnataka nikialikwa nisemeje? niwaambie wananchi wangu hawataki nitoke!
hana huo ujanja,lazima atoke ili CCM iweze endesha nchi..serikali imepanga abudget bil akuwa hata na miaa kwani mafisadi wameshagawana hela zote.Sasa wanaokota kama traffic na mlo wa siku
 
Anakwenda okoa serikali kw angwe iliyobaki...obama haji na hela zake serikali itajikopesha wapi?Hadi sasa serikali inachukua hela hazina kila isku na kuitumia kesho yake.Serikali imefilisika.
 
wivu wa kike, jk kaalikwa.
Kila ukialikwa inabidi uende?
Jaji Warioba aweke kipengele cha safari ngapi Rais wa Jamhuri anatakwa azifanye kwa mwaka;USA waliliona hilo mapema wakaweka sheria!
JK kawashinda ma Rais wote wa TZ ukichanganya safari zao!
 
wivu wa kike, jk kaalikwa.
Kila ukialikwa inabidi uende?
Jaji Warioba aweke kipengele cha safari ngapi Rais wa Jamhuri anatakwa azifanye kwa mwaka;USA waliliona hilo mapema wakaweka sheria!
JK kawashinda ma Rais wote wa TZ ukichanganya safari zao!
 
Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa wakuu wachi walioalikwa kuhudhuria mkutano wa nchi zenye Viwanda Vingi G8,mkutano unaanza kesho UK.
my Take;
Safari kama hii ina Tija gani,na Jk anafuraha gani ya kuhudhuria mkutano wa wenye viwanda wakati ambapo serikali imeshindwa kuendeleza viwanda vya ndani.
Source;ITV
Kwa sasa utakiwi kuogopa JK kwenda kokote uwezo wake tumeshaujua and he has done enough damage internally. Kilichobaki ni kusubiri muda wake uishe haraka sana tuokoe kilichobaki, unachotakiwa kukipigania kwa sasa ni misingi imara ya kulinda mariasili za taifa na kiongozi ajae asiwe le-le-mama kabisa, these people are coming and the consequences are gonna be severe and something wich we have never witnessed before; story yake nikitabu pekee ndio kinchoweza kufafanua (chukua acha huo ndio ukweli wenyewe).

As a nation we need someone who understands the international arena and has a clear plan for a Tanzanian development (with policies) . So far from CCM amna aliejitokeza mwenye huwezo as a visionary na upinzani ndio kabisa; Slaa is good for evoking democratic rights but he is way off from being a national leader, with regards to 'Mh. Mbowe' just dont even put him in the equation he nutting.

Atakapo tuacha JK sio kuzuri kabisa na hali ya uchumi wa ndani kwa sasa na watu wanaoivizia Tanzania, we cant take chances anymore with the next president or else nchi inatuponyoka.
 
Ni kweli mkuu halafu wengne wanafurahia mialiko ya mabeberu wakati huko ndio zinakozaliwa sera za kinyonyaji kwa nchi zetu kwa maslahi yao,Sijui kama huwa wanafikiria madhara au ndio wanaona ujiko tu safari zisizo na tathimini makini.
 
Umaarufu kazi sana, akialikwa makelele, asipoalikwa eti kachokwa akialikwa nako shida, sasa hakuna migomo, maandamano kilichobaki ni kutafuta vi thread kama hivi kutoa kihoro chao cha kukosa Urais!

Kama uko karibu na Rais muulze manufaa ya safari zake kama hii ya kuitwa na Mabeberu ndio utajua kwani umefikiria marais wasiosafiri sana umelinganisha vipi uchumi wao na Tz au unafikiri wazungu wanaipenda sana Tz wale kazi yao ni kukutumia kwa manufaa yao tu hakuna kitu cha kujivunia hapo.
 
Jason bourne said:
14/06/2013 - SAFARI ya 351 ya rais Jakaya Kikwete tangu aingie madarakani 2005!
Rais anawasili Uingereza kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu, pamoja na mambo mengine, rais atahudhuria sherehe za kuzaliwa kwa Malkia wa Uingereza!
Hii ni safari yake ya 351 toka aapishwe kuwa Raisi wa nchi hii mwaka 2005! Kwa hesabu za haraka haraka kama kila safari inachukua wastani wa siku tatu, katika miaka saba ya uongozi wake amekuwa nje ya nchi kwa siku 351x3 sawa na siku 1053! Kwa lugha nyingine iliyo chungu ni kwamba kwa miaka mitatu Raisi wetu yuko ugenini! Rais wetu anaishi kwa watu!

Hilo moja lakini la pili ni kwamba kulingana na vyanzo vya kuaminika kila safari yake moja gharama yake inakaribia shillingi 300,000,000/= kwa wastani! Milioni mia tatu...kwa iliyo chungu zaidi na isiyoweza kumezeka labda iwe kwa kusokomezewa ni kwamba katika hizo safari zake 351 ametafuna 300,000,000x351 sawa na shilingi 105,300,000,000/=!

Hilo la pili lakini la tatu linalotia hofu ni njama inayofanywa na walafi wajanja wanaofaidika na hizo safari zisokuwa na tija kwa taifa za kumuongezea miaka mingine miwili! Kwa lugha chungu isiyovumilika, kasi mpya ya kuwashughulikia wale wote wenye uthubutu wa kuhoji kulikoni, litatuachia taifa linaloongoza kwa idadi kubwa ya wasiokuwa na meno wala kucha!
 
Purpose and expencive! Kafikiria?

Ajabu taifa kubwa ndio linazingatia sababu na gharama za safari za rais wa nchi while sisi maskini tumeamua kufuja pesa za walipa kodi kwa safari zisizo na tija.
 
Kuna Lugha ilikuwa inatumika kwamba hela zinatoka kwa masikini wa ulaya(walipa kodi) zinakuja kwa Matajiri wa Afrika(Watawala) hawa jamaa hawana uchungu kabisa inamaana kuna siku imeongezeka ambayo Rais atahudhuria birthday ya Malkia halafu atafurahi kweli, alafu kuna watu humu wanataka tusiseme kitu kuhusu hizi safari bahati mbaya sana unawezakuta ni vijana kabisa na hawaoni hatari ya miaka ijayo tutakapoamka ardi inamilkiwa na mabepari wamezungusha fensi za umeme kwenye ardhi yao vijana wa kitanzania wapange foleni kuomba kibarua,Ina maana marais waliotangulia waliwezaje kufanya kazi bila safari zisizo na msingi.
 
Hii ni safari yake ya 351 toka aapishwe kuwa Raisi wa nchi hii mwaka 2005! Kwa hesabu za haraka haraka kama kila safari inachukua wastani wa siku tatu, katika miaka saba ya uongozi wake amekuwa nje ya nchi kwa siku 351x3 sawa na siku 1053! Kwa lugha nyingine iliyo chungu ni kwamba kwa miaka mitatu Raisi wetu yuko ugenini! Rais wetu anaishi kwa watu!

Hilo moja lakini la pili ni kwamba kulingana na vyanzo vya kuaminika kila safari yake moja gharama yake inakaribia shillingi 300,000,000/= kwa wastani! Milioni mia tatu...kwa iliyo chungu zaidi na isiyoweza kumezeka labda iwe kwa kusokomezewa ni kwamba katika hizo safari zake 351 ametafuna 300,000,000x351 sawa na shilingi 105,300,000,000/=!

Hilo la pili lakini la tatu linalotia hofu ni njama inayofanywa na walafi wajanja wanaofaidika na hizo safari zisokuwa na tija kwa taifa za kumuongezea miaka mingine miwili! Kwa lugha chungu isiyovumilika, kasi mpya ya kuwashughulikia wale wote wenye uthubutu wa kuhoji kulikoni, litatuachia taifa linaloongoza kwa idadi kubwa ya wasiokuwa na meno wala kucha!

Matatzo yote tulyonayo Rais anasafri kwenye birtday mara South Sudan,South Afrka safar hii atakaa UK kuhudhuria bday ya Malkia,Ni hatari sana.
 
Hii ni safari yake ya 351 toka aapishwe kuwa Raisi wa nchi hii mwaka 2005! Kwa hesabu za haraka haraka kama kila safari inachukua wastani wa siku tatu, katika miaka saba ya uongozi wake amekuwa nje ya nchi kwa siku 351x3 sawa na siku 1053! Kwa lugha nyingine iliyo chungu ni kwamba kwa miaka mitatu Raisi wetu yuko ugenini! Rais wetu anaishi kwa watu!

Hilo moja lakini la pili ni kwamba kulingana na vyanzo vya kuaminika kila safari yake moja gharama yake inakaribia shillingi 300,000,000/= kwa wastani! Milioni mia tatu...kwa iliyo chungu zaidi na isiyoweza kumezeka labda iwe kwa kusokomezewa ni kwamba katika hizo safari zake 351 ametafuna 300,000,000x351 sawa na shilingi 105,300,000,000/=!

Hilo la pili lakini la tatu linalotia hofu ni njama inayofanywa na walafi wajanja wanaofaidika na hizo safari zisokuwa na tija kwa taifa za kumuongezea miaka mingine miwili! Kwa lugha chungu isiyovumilika, kasi mpya ya kuwashughulikia wale wote wenye uthubutu wa kuhoji kulikoni, litatuachia taifa linaloongoza kwa idadi kubwa ya wasiokuwa na meno wala kucha!
Kwa kweli safari 351 katika miaka 8 ni nyingi sana kwa level ya Rais wa Nchi, sidhani kama kuna Rais yeyote Duniani aliyewahi kufikisha angalau nusu ya safari hizi. Nadhani atakuwa ana matatizo ya msongo kidogo, safari 351 za ndege si mchezo jamani.
 
Back
Top Bottom