JK Safarini tena UK

JK Safarini tena UK

Ngoja nizungukie jukwaa lengwa niangalie ni safari yake ya ngapi kwani bila kukosea kwa kumbukumbu ya Jason bourne ni safari ya 420.
Mmmmmh!
 
Last edited by a moderator:
wivu wa kike, jk kaalikwa.

Poor you boy-girl!! Amealikwa..eenh, nani analipa nauli ya kwenda kwenye huo mkutano wa G8? Ujinga uliopitiliza ni mauti yako, this guy, JK, ameharibu na anaendelea kuharibu nchi yetu huku tukiwa tunamwona and, terribly, some people of your kind eti unatukana wakosoaji wanaoona UDHAIFU wa dhahiri wa this so-called the President.....damn you..!!
 
"Nikiondoka napenda nikumbukwe kama Bwana MAENDELEO" Jakaya Mrisho Kikwete Fourth President of United Republic of Tanzania
 
wivu wa kike, jk kaalikwa.

Wivu wa kike!!! Ghooosh...! Wewe una wivu wa kiume!!! Habu ngoja nikusaidie kukuelimisha wewe na wenye mawazo kama yako!!! Nifuatishe kwa makini katika comment yangu!
Bwana YESU alipokuwa akisulubiwa alivikwa joho jekundu na taji ya miiba. Kisha watesi wake wakapiga magoti mbele yake na kumdhihaki 'Salamu Mfalme wa Wayahudi'...kisha wakampiga piga kichwani na magongo kushindilia ile miiba kichwani, wakamtemea mate na kumsulubisha sana!!!! Hivi ndivyo wazungu wanaichezea Tanzania. Nchi yetu imevikwa joho jekundu na taji la miiba. Wanajifanya watatutukuza kumbe wanafiki wanatusulubisha kwa kupora raslimali zetu.
Hebu tuwaangalie hawa G8 (watesi wetu) namna walivyotuvika joho jekundu na namna wanavyotusulubisha!!!
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimechaguliwa na nchi za G8 kuwa ni nchi iliyofanya vema katika tasnia ya uziduaji (EITI) yaani uwazi (Transparency) katika sekta ya Madini, Gesi asilia na Mafuta!!! (Hapa jiulize Transparency gani wanayoisema hawa watesi wetu kama mikataba ya madini, gesi na mafuta ni SIRI. wananchi hawaambiwi nini kilichomo ndani yake!!!). Sasa hao watesi (G8) wamesema watashirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa misaada kwa Idara mbalimbali za serikali na Asasi za kiraia, NGO na makundi ya kiharakati!!! (Nchi za G8 zimekuwa zikifadhili makundi ya kiharakati ili ku-distabilize hali ya amani na utulivu katika nchi zenye maslahi yao ili wavune kilaini).

Sasa hebu tuzitambue nchi za G8...ni pamoja na Canada, Uingereza, Marekani, Norway, Sweden, Japan na Ujeruman. nchi hizi zina makampuni makubwa Tanzania yaliyowekeza katika sekta ya madini, gasi asilia na Mafuta. Tazama...
CANADA: Makampuni yake TZ ni African Barrick Gold(ina migodi mikubwa ya Tulawaka, Buzwagi, North Mara, Bulyanhulu) na makampuni ya mafuta na gasi ya Orca Exploration Group, Antrim Resources, Artumas Group.
UK: BG Group, Dominion Oil & Gas, Pan African Energy, Petrodel Resources/ Heritage Oil, HYROTANZ, Tullow Oil.
NORWAY: Statoil
USA: ExxonMobil na Anadarko Corporation.
SWEDEN: Miradi ya ukoloni mpya kupitia mzingira na hewa ukaa (REDD)

hiyo ni mifano michache ya makampuni ya G8 nchini Tanzania.
Sasa mwaliko wa JK kwenda huko UK tena na Prof. Muhongo hapo nawaachia mchanganye akili zenu mjue maana yake nini!!!! Wamekwenda kuhudhuria mkutano wa G8 kuhusu masuala ya uziduaji katika sekta ya Madini, gesi asilia na Mafuta! Hakuna jambo jipya chini ya jua. tunatendwa kama Bwana YESU alivyotendwa! Raslimali zetu zinakwenda hivyo!
 
Wivu wa kike!!! Ghooosh...! Wewe una wivu wa kiume!!! Habu ngoja nikusaidie kukuelimisha wewe na wenye mawazo kama yako!!! Nifuatishe kwa makini katika comment yangu!
Bwana YESU alipokuwa akisulubiwa alivikwa joho jekundu na taji ya miiba. Kisha watesi wake wakapiga magoti mbele yake na kumdhihaki 'Salamu Mfalme wa Wayahudi'...kisha wakampiga piga kichwani na magongo kushindilia ile miiba kichwani, wakamtemea mate na kumsulubisha sana!!!! Hivi ndivyo wazungu wanaichezea Tanzania. Nchi yetu imevikwa joho jekundu na taji la miiba. Wanajifanya watatutukuza kumbe wanafiki wanatusulubisha kwa kupora raslimali zetu.
Hebu tuwaangalie hawa G8 (watesi wetu) namna walivyotuvika joho jekundu na namna wanavyotusulubisha!!!
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimechaguliwa na nchi za G8 kuwa ni nchi iliyofanya vema katika tasnia ya uziduaji (EITI) yaani uwazi (Transparency) katika sekta ya Madini, Gesi asilia na Mafuta!!! (Hapa jiulize Transparency gani wanayoisema hawa watesi wetu kama mikataba ya madini, gesi na mafuta ni SIRI. wananchi hawaambiwi nini kilichomo ndani yake!!!). Sasa hao watesi (G8) wamesema watashirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa misaada kwa Idara mbalimbali za serikali na Asasi za kiraia, NGO na makundi ya kiharakati!!! (Nchi za G8 zimekuwa zikifadhili makundi ya kiharakati ili ku-distabilize hali ya amani na utulivu katika nchi zenye maslahi yao ili wavune kilaini).

Sasa hebu tuzitambue nchi za G8...ni pamoja na Canada, Uingereza, Marekani, Norway, Sweden, Japan na Ujeruman. nchi hizi zina makampuni makubwa Tanzania yaliyowekeza katika sekta ya madini, gasi asilia na Mafuta. Tazama...
CANADA: Makampuni yake TZ ni African Barrick Gold(ina migodi mikubwa ya Tulawaka, Buzwagi, North Mara, Bulyanhulu) na makampuni ya mafuta na gasi ya Orca Exploration Group, Antrim Resources, Artumas Group.
UK: BG Group, Dominion Oil & Gas, Pan African Energy, Petrodel Resources/ Heritage Oil, HYROTANZ, Tullow Oil.
NORWAY: Statoil
USA: ExxonMobil na Anadarko Corporation.
SWEDEN: Miradi ya ukoloni mpya kupitia mzingira na hewa ukaa (REDD)

hiyo ni mifano michache ya makampuni ya G8 nchini Tanzania.
Sasa mwaliko wa JK kwenda huko UK tena na Prof. Muhongo hapo nawaachia mchanganye akili zenu mjue maana yake nini!!!! Wamekwenda kuhudhuria mkutano wa G8 kuhusu masuala ya uziduaji katika sekta ya Madini, gesi asilia na Mafuta! Hakuna jambo jipya chini ya jua. tunatendwa kama Bwana YESU alivyotendwa! Raslimali zetu zinakwenda hivyo!

Michango kama hii ndio inafanya JF Iheshimike,Asante mkuu kwa maelezo mazuri.
 
Sifa kuu za JK:
1. SHEREHE (Ngoma/maadhimisho/hotuba ndeeeefu)
2.KUPOKEA WAGENI (Njooni kina Mzee Bush/Li xi Ping/Obama...)
3.ZIARA (Kama ilivyo sasa...kwani ni lazima kwenda?)
 
. Wanajifanya watatutukuza kumbe wanafiki wanatusulubisha kwa kupora raslimali zetu.
Hapa jiulize Transparency gani wanayoisema hawa watesi wetu kama mikataba ya madini, gesi na mafuta ni SIRI. wananchi hawaambiwi nini kilichomo ndani yake!!!). Sasa hao watesi (G8) wamesema watashirikiana na Tanzania na kutoa misaada kwa Idara mbalimbali za serikali na Asasi za kiraia, NGO na makundi ya kiharakati!!! (Nchi za G8 zimekuwa zikifadhili makundi ya kiharakati ili ku-distabilize hali ya amani na utulivu katika nchi zenye maslahi yao ili wavune kilaini).


Sasa mwaliko wa JK kwenda huko UK tena na Prof. Muhongo hapo nawaachia mchanganye akili zenu mjue maana yake nini!!!! Wamekwenda kuhudhuria mkutano wa G8 kuhusu masuala ya uziduaji katika sekta ya Madini, gesi asilia na Mafuta! Raslimali zetu zinakwenda hivyo!

Kaka K.K. Nikupongeze kwa uchambuzi wako Ni Mchango wenye TIJA na mtazamo halisia! Ukweli huu unaudhi, unakera, unakatisha tamaa.Hivi Watanzania ni wapi tulipojikwaa hadi kufikia udhaifu huu? Utadhani tumelogwa? I am sorry lakini nyakati fulani nafikia kumlaumu sana Baba wa Taifa!

 
....ndipo hapo huwa napata shida sana kuwaelewa wabunge wetu....maana tupende tusipende hizi safari ni mzigo mzito katika matumizi ya serikali.....Leo hii tunajadili bajeti na jinsi inavyokosa hela za kutosha.....alafu rais anaendekeza safari kila kukicha.....Lazima ifike mahali kufanyike tathmini ya hizi safari za JK....maana anaeumia na kuchangia safari hizi ni mlipa kodi wa TZ anaelalalmika kila siku kwamba serikali yake haimjali...

....kwa nchi yenye kutegemea misaada kama TZ ni jambo la ajabu sana kumwona rais anasafiri kilia kukicha.....alafu bunge wala halihoji???....

Juzi tu kule marekani wabunge wamepiga kelele gharama za safari ya Obama mbugani TZ...na wamarekani wamefikia hata kuondoa safari za Obama mbugani TZ....Leo sisi tunaojiita maskini rais wetu kila leo yuko kwenye safari!! this is ridiculous!! alafu watu wanaona sawa tu.....haiwezekaani.....huyu jamaa juzi tu hata wk haijapita alikua Japan na Singapore...hizo zote ni hela za mlipa kodi....hivi nani analipia hizi safari???
 
Kaka K.K. Nikupongeze kwa uchambuzi wako Ni Mchango wenye TIJA na mtazamo halisia! Ukweli huu unaudhi, unakera, unakatisha tamaa.Hivi Watanzania ni wapi tulipojikwaa hadi kufikia udhaifu huu? Utadhani tumelogwa? I am sorry lakini nyakati fulani nafikia kumlaumu sana Baba wa Taifa!


Mmmh huo ndio ukweli! Ukiona mzungu anakuwa karibu na wewe ujue kuna kitu kakiona kwako na wewe amekuona huna akili. Ukiona mzungu anakuchukia ujue kaona kitu kwako lakini amekuta wewe ni mjanja. hudanganyiki! wewe fuatilia kwa makini uhusiano wa Tanzania na mataifa ya Magharibi na Marekani. Utaona Tanzania tukipewa vyeo vyeo katika vyombo/ mashirika ya kimataifa! hayo ni majoho mekundu tu lakini tunasulubiwa kwa kuporwa raslimali zetu. siku seriakali ya TZ (kwa muujiza wa Mungu) ikiwa janja utaona Tanzania inaanza kuingizwa katika makundi ya nchi hatari ya kigaidi duniani! upuuzi mtupu!
 
Leadership isn’t just a job. It’s a lifetime commitment to other people’s excellence
What legacy is he going to leave behind????
 
Sio tatizo nchi magharibi kufanya biashara na sisi tatizo ni pale tunapoingia mkataba Huku tunapata asilimia 5 na asilimia tano inaenda uswisi yaaani hamna tofauti na mikataba ile ya enzi zile za kikoloni unapewa nguo watu wanabeba diamond yaaani gesi madini utalii petrol vinaweza kuendesha nchi hii hizo trillion 18 zinaweza patikana humo tu inatia hasira sana nchi inavyowabana walalahoi machinga na kodi na hawa g8 tunaitwa kwenda kupewa 5 percent pumbaf Kabisa
 
Acha kudanganya watu wewe!!!!

Tangu lini Norway na Sweden zikawa ktk G 8???

G 8 Ni (UK, France, German, USA, Canada, China, Italy na Russia)!!


Wivu wa kike!!! Ghooosh...! Wewe una wivu wa kiume!!! Habu ngoja nikusaidie kukuelimisha wewe na wenye mawazo kama yako!!! Nifuatishe kwa makini katika comment yangu!
Bwana YESU alipokuwa akisulubiwa alivikwa joho jekundu na taji ya miiba. Kisha watesi wake wakapiga magoti mbele yake na kumdhihaki 'Salamu Mfalme wa Wayahudi'...kisha wakampiga piga kichwani na magongo kushindilia ile miiba kichwani, wakamtemea mate na kumsulubisha sana!!!! Hivi ndivyo wazungu wanaichezea Tanzania. Nchi yetu imevikwa joho jekundu na taji la miiba. Wanajifanya watatutukuza kumbe wanafiki wanatusulubisha kwa kupora raslimali zetu.
Hebu tuwaangalie hawa G8 (watesi wetu) namna walivyotuvika joho jekundu na namna wanavyotusulubisha!!!
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimechaguliwa na nchi za G8 kuwa ni nchi iliyofanya vema katika tasnia ya uziduaji (EITI) yaani uwazi (Transparency) katika sekta ya Madini, Gesi asilia na Mafuta!!! (Hapa jiulize Transparency gani wanayoisema hawa watesi wetu kama mikataba ya madini, gesi na mafuta ni SIRI. wananchi hawaambiwi nini kilichomo ndani yake!!!). Sasa hao watesi (G8) wamesema watashirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa misaada kwa Idara mbalimbali za serikali na Asasi za kiraia, NGO na makundi ya kiharakati!!! (Nchi za G8 zimekuwa zikifadhili makundi ya kiharakati ili ku-distabilize hali ya amani na utulivu katika nchi zenye maslahi yao ili wavune kilaini).

Sasa hebu tuzitambue nchi za G8...ni pamoja na Canada, Uingereza, Marekani, Norway, Sweden, Japan na Ujeruman. nchi hizi zina makampuni makubwa Tanzania yaliyowekeza katika sekta ya madini, gasi asilia na Mafuta. Tazama...
CANADA: Makampuni yake TZ ni African Barrick Gold(ina migodi mikubwa ya Tulawaka, Buzwagi, North Mara, Bulyanhulu) na makampuni ya mafuta na gasi ya Orca Exploration Group, Antrim Resources, Artumas Group.
UK: BG Group, Dominion Oil & Gas, Pan African Energy, Petrodel Resources/ Heritage Oil, HYROTANZ, Tullow Oil.
NORWAY: Statoil
USA: ExxonMobil na Anadarko Corporation.
SWEDEN: Miradi ya ukoloni mpya kupitia mzingira na hewa ukaa (REDD)

hiyo ni mifano michache ya makampuni ya G8 nchini Tanzania.
Sasa mwaliko wa JK kwenda huko UK tena na Prof. Muhongo hapo nawaachia mchanganye akili zenu mjue maana yake nini!!!! Wamekwenda kuhudhuria mkutano wa G8 kuhusu masuala ya uziduaji katika sekta ya Madini, gesi asilia na Mafuta! Hakuna jambo jipya chini ya jua. tunatendwa kama Bwana YESU alivyotendwa! Raslimali zetu zinakwenda hivyo!
 
Anakata mawingu kwa kwenda mbele; majuzi tu tuliambiwa yuko Japan na my wife wake, ghafla wakaibukia Singapore, mara my wife wake yuko US, sasa tunaambiwa mzee atapishana na my wife hapo London ama sijui atampitia ili waende wote kwenye huo mnuso wa G8, no one knows.

Swali la kujiuliza ni kuwa; kama Kikwete alikiri mwenyewe kuwa hajui sababu ama chanzo cha umaskini wa Watanzania; sasa huko anakoenda kukaa na hao wenye dunia ataongea nini zaidi ya kujichekesha na kushangaa.

Ee Mwenyezi Mungu ibariki Tanzania na watu wake.
 
JK ana heshima gani? Kwa nani? Amebaki anakula nchi kwa safari zisizo tija kwetu Wala Taifa kwa jumla
 
Acha kudanganya watu wewe!!!!

Tangu lini Norway na Sweden zikawa ktk G 8???

G 8 Ni (UK, France, German, USA, Canada, China, Italy na Russia)!!

Norway na Sweden haziko katika kundi la G8 sawa lakini nchi hizo zime-team up na nchi za G8 katika masuala ya EITI. Na mkutano anahudhuria Kikwete utahusu masuala ya Tasnia ya Uziduaji (EITI) na ambapo Uingereza itakuwa mwenyekiti ajaye wa G8. Sasa jiulize kwa nini Norway na Sweden zime-team up na hizo nchi ulizotaja. Kwa maslahi ya nani?!!!
Kwa kukusaidia kidogo: wakati vyombo vya Ulinzi na Usalama vya TZ vimekodoa macho kuhakikisha CDM haishindi urais 2015, vyombo vya hizo nchi za G8 pamoja na Norway na Sweden viko makini kuchunguza na kukusanya taarifa za kina juu ya raslimali zetu! kama unabisha bisha maana utakuwa unatekeleza haki yako kikatiba!
 
Rais Jakaya Kikwete ni miongoni mwa wakuu wachi walioalikwa kuhudhuria mkutano wa nchi zenye Viwanda Vingi G8,mkutano unaanza kesho UK.

Source: ITV

my Take;
Safari kama hii ina Tija gani,na Jk anafuraha gani ya kuhudhuria mkutano wa wenye viwanda wakati ambapo serikali imeshindwa kuendeleza viwanda vya ndani.

Katika mikutano ya aina hiyo lazima wawepo watu wa kutumwa. Labda aende kwa hilo lakinin vinginevyo sioni sababu zaidi ya ule uVasco da Gama wake!
 
Back
Top Bottom