JK Rais Bora kuliko wote Tanzania

JK Rais Bora kuliko wote Tanzania

Ahadi hewa! Yaani baba mzima na watoto pia wajukuu anazunguka nchi nzima kuwadanganya wananchi halafu mnamwita Rais bora? Ama kweli mmekosa cha kufanya!

Tumeahidi tumetimiza kuliko rais yeyote Tanzania
 
Rais pekee aliyekwisha ongeza mitambo ya umeme amma iko tayari nchini amma iko kwenye mchakato wa kuundwa, kurasimiwa amma kufungwa kuliko mwingine yoyote wa kabla yake.
Jibu swali: mgao wa umeme umekwisha? Leo ni Novemba 26 tunaelekea Desemba. Mwaka mzima Tanzagiza inarindima unaniambia ameongeza mitambo. Tanzagiza ya Kikwete hiyo.

Na shilingi inazidi kuporomoka. Hapo hujaweka inflation ambayo inakimbilia 20% wakati anachukua nchi Mkapa alikuwa ameishusha hadi 6%. Tanzania ya Kikwete hawachekani na Zimbabwe ya Mugabe, lakini kama mavuvuleza wa Patriotic Front wanavyoendelea kumsifia kizee ndivyo hivyo hivyo mavuvuzela ya Bongo yanaendelea kumsifia JK.
 
Nadhani anapima upepo baada ya CC, NEC and the rest kushindwa kufanya maamuzi ya maana Dodoma. Week nzima wamekaa hawa wakubwa wanatoka na kauli za kuisifia serikali kuruhusu wakulima kuuza mahindi nje!
Tatizo lako ulitaka kikao cha CC pamoja na NEC kiwafukuze wanachama ambao wewe ulitaka waondoke kwa matakwa yenu sasa unapoona hakuna ulichokitegemea unaanza kulalamika.
 
ni rais aliyepitia misukosuko mingi
ni rais alikumbana na upinzani mkali
ni rahisi aliyetoa uhuru wa kwa kila mtu asemalo
ni rais alietuletea misaada mingi kutoka kwa wahisani
ni rahisi ambaye anaongoza katika kipindi kigumu
ni rais anayepambana na ufisadi mf richmond,epa,nk
ni rais anayepambana na wanaofuja mali ya umma
ni rais msikivu na mpokea maoni ya wapinzani

namtakia kila la heri na kazi yake

umeonaee!
 
Jibu swali: mgao wa umeme umekwisha? Leo ni Novemba 26 tunaelekea Desemba. Mwaka mzima Tanzagiza inarindima unaniambia
ameongeza mitambo. Tanzagiza ya Kikwete hiyo. Na shilingi inazidi kuporomoka. Hapo hujaweka inflation ambayo inakimbilia 20% wakati anachukua nchi Mkapa alikuwa ameishusha hadi 6%. Tanzania ya Kikwete hawachekani na Zimbabwe ya Mugabe, lakini kama mavuvuleza wa Patriotic Front wanavyoendelea kumsifia kizee ndivyo hivyo hivyo mavuvuzela ya Bongo yanaendelea kumsifia kilaza.

Hayo mengine ya umeme atafanya Slaa na symbion yao

Lakini JK mengine kafanya zaidi ya Marais wote so bado anabaki best president ever!
 
Nasikia amefanikiwa sana katika kutatua tatizo la ajira na kudhibiti mfumuko wa bei!Teh,teh,teh
 
Kwishney nyie hakuna hoja mkipewa mafanikio mnabaki kutukana slaa @ work

Maendeleo tuliyoyapata kipindi cha JK nina wasiwasi yataharibiwa na atakayefuata..

Huo ndio wasiwasi wangu tu..

Mwisho wa ubaya ni aibu, aibu yenu haipo mbali maisha bora kwa kila mtanzania. Tumetubutu, tumeweza na tunasonga mbele.
 
Mwisho wa maji ni matope, pelekeni matope yenu huko.

Watu kama nyie huwa mnatamaa sana na madaraka na hiyo inatokana na huenda mna njaa kali sana,sasa mkipewa nchi ndiyo itakuwa balaa zaid

Namshukuru sana JK kwa kuimarisha usalama kila sehemu ili kutulinda wengine ambao hatuna mawazo mgando kama yenu.

Mimi namkubali JK kwa mengi sana aliyoyafanya, namnukuu Mwl Nyerere kwa maneno yake kuwa Tatizo lenu mnaacha mema mnachukua ya kijinga

Kikweteeeeeeeeee oyeeeeeeeeeeeee!!!
Kidumu chama cha mapinduzi
 
Kuzidisha Barabara
Kuzidisha Shule
Kuzidisha afya
Kuzidisha Uchumi
Kuzidisha Demokrasia
Kuzidisha Maji
Kuzidisha Kazi
Kuzidisha Viwanda
Utalii
Kupigana na Rushwa
Kwa haraka haraka hayo hapo juu kafanya kuliko Rais yoyote wa kabla yake.

kwani kwako ni multiplication siyo value.
ama kweli vipimo vyetu vyachekesha
:juggle:
 
Rais pekee aliyekwisha ongeza mitambo ya umeme amma iko tayari nchini amma iko kwenye mchakato wa kuundwa, kurasimiwa amma kufungwa kuliko mwingine yoyote wa kabla yake.
Hayati Mwalimu Nyerere alipong'atuka alituachia megawatt 500 plus za umeme. Marais wote waliofuata baada yake wameongeza megawatt 300 tu. Fanya utafiti kabla ya kuandika.
 
Teh teh teh teh teh teh teh teeeeh:lol:! kweli jina lako linasanifu akili yako
 
Watu kama nyie huwa mnatamaa sana na madaraka na hiyo inatokana na huenda mna njaa kali sana,sasa mkipewa nchi ndiyo itakuwa balaa zaid

Namshukuru sana JK kwa kuimarisha usalama kila sehemu ili kutulinda wengine ambao hatuna mawazo mgando kama yenu.

Mimi namkubali JK kwa mengi sana aliyoyafanya, namnukuu Mwl Nyerere kwa maneno yake kuwa Tatizo lenu mnaacha mema mnachukua ya kijinga

Kikweteeeeeeeeee oyeeeeeeeeeeeee!!!
Kidumu chama cha mapinduzi
Hata kama tuna njaa lakini hiajafikia ya kuuza nchi kwa suti!!!!!!
 
Hayati Mwalimu Nyerere alipong'atuka alituachia megawatt 500 plus za umeme. Marais wote waliofuata baada yake wameongeza megawatt 300 tu. Fanya utafiti kabla ya kuandika.
500MG za uhakika, lakini waliofuata hasa huyu wa amau ya tatu na nne ameongeza ufisadi katika sekta hiyo unaotaka kumgharimu madaraka!
 
miaka ya nyuma kulikuwa kikatuni gazeti fulani jamaa anajiita bingwa wa rivasi, ndiyo hii. FF hata wewe umeamua kumtukana JK waziwazi namna hii?
 
Ni Rais aliyepitia Misukosuko mingi
Ni Rais alikumbana na upinzani mkali
Ni rahisi aliyetoa uhuru wa kwa kila mtu asemalo
Ni Rais alietuletea misaada mingi kutoka kwa wahisani
Ni rahisi ambaye anaongoza katika kipindi kigumu
Ni Rais anayepambana na ufisadi Mf richmond,EPA,nk
Ni Rais anayepambana na wanaofuja mali ya umma
Ni Rais Msikivu na mpokea maoni ya wapinzani

Namtakia kila la heri na kazi yake

Mkuu, una undugu na Malaria Sugu a.k.a MS ? Nauliza tu.
 
Sioni haja ya kupinga wazo lako,kwani haki uliyonayo kikatiba ktk maoni inanifunga as hata wavivu wa kufikiri kama ww mmetambuliwa,Nyerere was and is still the BEST President.Ni matusi kumlinganisha na mkwezi n ni KOSA la jinai.
 
Mkuu, una undugu na Malaria Sugu a.k.a MS ? Nauliza tu.

Mkuu sina Undugu naye isipokuwa mawazo yangu na ya maralia sugu ni mawazo na fikra sahihi

WanaJF wengi hapa jukwaani mnatakiwa kukishukuru chama chetu cos wengi wenu mmelelewa na kusomeshwa na CCM nashangaa sana kwa maneno yanavyowatoka vinywani mwenu

Hata siku moja haiwezekani Mtoto akiota ndevu tu basi anakuwa na anjifanya mjuaji kuliko mzazi

Mafanikio yangu yote ni kwa sababu ya Chama chetu.

Tumethubutu tumeweza na tunasonga mbele
 
Back
Top Bottom