JK; na mimi ujue naitwa Muhando

JK; na mimi ujue naitwa Muhando

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,367
Reaction score
100,408
Jamani, naombeni mnisaidie kufikisha ujumbe huu kwa Rais wangu mpendwa kuwa kuanzia leo nimeamua kubadili Jina na kuitwa Whatever Muhando; najua baadhi yenu mtashangaa ila kuna ukweli mtupu kuwa RAHISI wetu anapendelea saaana kuwapa ulaji wale wote wenye majina ya Mikando ( plural)

Nimeenda kwa Mchungaji wangu na amekubali nibadili jina langu la asili na kuchukua jina hilo jipya ambalo litaniwezesha kupata Ukurugenzi wowote ule toka kwa kiranja mkuu. majina ya Muhando yana sifa kuu zifuatazo: Ni majina maalumu kwa ajili ya kupata Ukurugenzi, Pili, Wana-sifa ya kuwakusanya ndugu zao wote wanaotumia majina yao bila kuulizwa na mtu; si wana sifa bwana??? kwa mfano pale kwa TaaaBaaaCaaaaa; wapo wakinda Mihando wapatao wanne, huko kwene umeme sasa watafika 20, na ndio maana nikaaamua kubadili jina na kuitwa....Muhando.

Ikishindikana mimi kupata nafasi yoyote, naapa mwanangu wa kwanza ninayemtarajia hivi karibuni nitamuita Jina la Babu yake: Tigo Mhando. Hii itasaidia nae aingie kwenye orodha ya majina yanayo mkuna kiranja Mkuu.

Raisi wangu, nikumbuke hata kwenye Ukurugenzi wa Always Time Cancellation ( ATCL) au kule kwenye miundo mbinu ya mabarabara baada ya kumfukuza yule mtani wangu...
 
Pia,
Mwambieni nitamtafutia kiwanja cha kujenga kule Lushoto, kama kaka Beeee na Sumari/ sorry nafikiri ni kaka Asomaye, na wale wengine waliokuwa wakuu wa mkao wangu, oohh, sorry, mkoa wangu.

Mwambie sijajikana utu wangu, Nimimi

Shemdodo Orijino
 
Jamani, naombeni mnisaidie kufikisha ujumbe huu kwa Rais wangu mpendwa kuwa kuanzia leo nimeamua kubadili Jina na kuitwa Whatever Muhando; najua baadhi yenu mtashangaa ila kuna ukweli mtupu kuwa RAHISI wetu anapendelea saaana kuwapa ulaji wale wote wenye majina ya Mikando ( plural)

Nimeenda kwa Mchungaji wangu na amekubali nibadili jina langu la asili na kuchukua jina hilo jipya ambalo litaniwezesha kupata Ukurugenzi wowote ule toka kwa kiranja mkuu. majina ya Muhando yana sifa kuu zifuatazo: Ni majina maalumu kwa ajili ya kupata Ukurugenzi, Pili, Wana-sifa ya kuwakusanya ndugu zao wote wanaotumia majina yao bila kuulizwa na mtu; si wana sifa bwana??? kwa mfano pale kwa TaaaBaaaCaaaaa; wapo wakinda Mihando wapatao wanne, huko kwene umeme sasa watafika 20, na ndio maana nikaaamua kubadili jina na kuitwa....Muhando.

Ikishindikana mimi kupata nafasi yoyote, naapa mwanangu wa kwanza ninayemtarajia hivi karibuni nitamuita Jina la Babu yake: Tigo Mhando. Hii itasaidia nae aingie kwenye orodha ya majina yanayo mkuna kiranja Mkuu.

Raisi wangu, nikumbuke hata kwenye Ukurugenzi wa Always Time Cancellation ( ATCL) au kule kwenye miundo mbinu ya mabarabara baada ya kumfukuza yule mtani wangu...

Yes you are Great Sinker
 
Heeeeee, heeeeee, kweli nimekubali kuwa hawajamaa ni Great Sinker/Thinker; Yote nadhani sawa hata tukiwaita Sinner oohh sorry ni Sina. Ulimi hauna mfuko/mfupa
 
Mbona mmeshaambiwa tena hapa kwenye thread nyingine huko nyuma kuwa Tido Mhanda (?Muhando) na huyo dada Mhando (?Muhando) hawana undugu??

Kama watu wana sifa zinazohitajika hiyo tu ni sababu ya kutoajiriwa??

Yaani waTanzania bwana, wakiwepo watu wa kabila moja sehemu moja ya kazi taabu, ndugu taabu, wenye majina ya kufanana taabu!!

Grow up!!
 
wikend huondoka na vicheko vyetu walah
hahahaha
 
Mmhh, mdau huyu kawa mkali kweli kweli, nadhani hajaelewa mada yenyewe, swala si undugu ni Majina na ndio theme ya Thread.....huyu atakuwa mjukuu wake tu, na analake jimbo/ sorry ana lake jambo
 
sio massawe wote ni ndugu, au juma wote ni ndugu au mbura wote ni ndugu! ni majina tu, cha msingi ni hao watajwa wana vigezo au?
 
Heeeee heee, msumari huo.....umewachoma.

Wapi mie sijui
 
Mbona mmeshaambiwa tena hapa kwenye thread nyingine huko nyuma kuwa Tido Mhanda (?Muhando) na huyo dada Mhando (?Muhando) hawana undugu??

Kama watu wana sifa zinazohitajika hiyo tu ni sababu ya kutoajiriwa??

Yaani waTanzania bwana, wakiwepo watu wa kabila moja sehemu moja ya kazi taabu, ndugu taabu, wenye majina ya kufanana taabu!!

Grow up!!

Baelezeee
 
Kufikiri majina yana uhusiano na vyeo ni sawa na kutofikiri kabisa . Great Thinker? Kafikirie umpa mazee.
 
Mosi, Hivi kwani TANESCO waliteuana au kazi ilitangazwa ?

Pili, ukishakubali kumpa Rais blank cheque ya kuteua, unapoteza kila sababu ya kuhoji uteuzi wake. Sanasana utaonekana kituko.
 
Hiyo kitu nimewahi kujiuliza sana kuhusiana na hilo jina kukutana nalo kwenye ofisi nyingi baadae nikapata jawabu kwamba kupata kazi/ajira fulani lazima kuwepo vigezo fulani vinavyoendana na kazi husika. Hivyo nikahisi kuwa wenye hayo majina Cvs zao zinawaruhusu kama ni kinyume na hilo mpwa nakupongeza kubadili jina.
 
Hiyo kitu nimewahi kujiuliza sana kuhusiana na hilo jina kukutana nalo kwenye ofisi nyingi baadae nikapata jawabu kwamba kupata kazi/ajira fulani lazima kuwepo vigezo fulani vinavyoendana na kazi husika. Hivyo nikahisi kuwa wenye hayo majina Cvs zao zinawaruhusu kama ni kinyume na hilo mpwa nakupongeza kubadili jina.
 
Waalaah, nakuambia haya majina yana raha yake, muulize hata yule shehe wetu wa yaya, yule muona mbali atakuambia kuwa jina lako, litakufanya usipate kazi kwa huyu Blazameni...smiling face
 
Back
Top Bottom