JK kuachana kabisa na suala la katiba mpya iwapo Bunge litakataa marekebisho

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Wanajamvi:

Habari kutoka vianzo vyangu vya habari (msiniulize ni vyanzo vipi) ni kwamba kuna uwezekano mkubwa kwa JK kuachana kabisa na wazo la Katiba mpya katika kipindi chake cha utawala kilichobakia.

Hii itatokea iwapo Bunge litakwamisha marekebisho ya Katiba yaliyopelekwa Bungeni. habari zilizozagaa ni kwamba Wabunge wa CCM, ambao ndiyo wengi wanasema wataukwamisha muswada huo wa marekebisho ya katiba kutokana na kutoafikiana na JK kuhusu posho, na pia kwa sababu eti marekebisho hayo yalitoka kwa viongozi wa CDM.

Habari zaidi zinasema baada ya JK kusaini ule Muswada wa awali, alipata shinikizo kubwa kutoka pande mbali mbali wakiwemo kwa wafadhili, kwamba Sheria ile haifai jinsi ilivyopitishwa na kwamba ni lazima ifanyiwe marekebisho ili kupata katiba iliyo bora, kwani hii ni nafasi pekee ya nchi kupata katiba iliyo bora kama kweli inataka kuepuka kukumbwa na machafuko hapo mbeleni.


Kwa hivyo iwapo marekebisho yatakataliwa, basi JK ataachana na ile sheria mama iliyopitishwa kwani hataishughulikia kwa maana ya kutoteuwa wajumbe wa kuratibu maoni na pia wajumbe wa Bunge la Katiba -- hivyo fursa yote itakuwa imepotea, naye atajikosha kwa wafadhili na wadau wengine kwamba yeye hana tena makosa isipokuwa Bunge.

Kulikuwapo hatua nyingine pia iwapo marekebisho hayatapitishwa, kulivunja Bunge na kuitisha uchaguzi mwingine, kama vile alivyofanya Mwl Nyerere mwaka 1973 Bunge lilipokataa kupitisha Sheria ya Kodi ya Mapato kuirithi ile ya iliyokuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.

Hatua hiyo ya kuitisha uchaguzi mpya meonekana kuwa na gharama kubwa.




 
Sawa nimekusoma lakini wabunge wa CCM lazima watambue mchezo wao ndiyo mauti yetu.
 
Bora kulivunja bunge ili tuingie kwenye uchaguzi mwingine! Magamba ndo watakapoisoma namba vilivyo. Katiba mpya isipopatikana nako kuna moshi nje nje unafukuta!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Hakuna kubembelezana sisi ndio wenye nchi kama wataukwamisha nguvu ya ziada itumike kama maandamano makubwa kulipinga bunge na tutoe tamko letu sisi wananchi la kutokuwa na imani na bunge mpaka lilithie matakwa yetu na ndipo hapo utakuwa mwanzo wa uvunjifu wa amani
 
Kumbuka wab unge walichaguliwa na watu na watu wanataka change. JK mwenyewe amesema watz ulofa ndo tatizo. Tusimlaumu jk kila time. Sisi wananji ndo tatizo kubwa. Ila namuomba avunje bunge na tusiwe na wabunge wote hao tena. Wasizidi mia au idadi za wilaya.
 
kwakofia alizonazo{rais,mwenyekiti wa ccm} mh JK anapaswa kufanya maamuzi makini lkn kuamua kuliacha suala la katiba mpya kutamfanya aendelee kuonekana ni kiongozi mbabaishaji na sio mtu wakufanya nae makubaliano kwani hawezi kutekeleza anachokiamini....tanzania yasasa inahitaji katiba mpya itakayoandikwa kupitia mchakato wawazi ambao watanzania wote watatoa maoni yao.
 
kwakofia alizonazo{rais,mwenyekiti wa ccm} mh JK anapaswa kufanya maamuzi makini lkn kuamua kuliacha suala la katiba mpya kutamfanya aendelee kuonekana ni kiongozi mbabaishaji na sio mtu wakufanya nae makubaliano kwani hawezi kutekeleza anachokiamini....tanzania yasasa inahitaji katiba mpya itakayoandikwa kupitia mchakato wawazi ambao watanzania wote watatoa maoni yao.


unajua mnanichekesha sana yaani JK ndo wa kufanya maamuzi magumu?hahaaaa mweeee...kama unaytaka kujua JK makini soma majibu aliyotoa DAvos kwenye mahojiano ndo utajua JK makini au utumbo wa bata
 
Ok namna nzuri ya kutafuta maoni kuona option ya kuskip inaweza kufaaa chonde chonde ni mara mia Taifa likaingia kwenye gahrama ya uchaguzi wa wabunge watakao ondolea kwa kutokuwa n imani nao kuliko kuacha katiba.Katiba ndio gharama ya muafaka wa maisha ya mbele yetu watanzania.Wameshaona kuwa wanakwenda kukwamwa na keki waliyokuwa wanaitafuna wao kupitia wajuzi wa sheria walio upande wa CCM wanawapotosha na kuwatisha wabunge wasiojua sheria za katiba kuwa wana hali mbaya hivyo wanaamua kujiami.Wapande washuke, waluke wakae ,wachuchumae wasimame, wanune wacheke katiba ipo pale pale.Sana sana wakimkwamisha JK awashitakie kwetu,chini ya mgongo wa CDM tutawasurubu mpaka wajute kwa dhambi yao.
 
Sasa hapo ndiyo watakapoharibu mambo kabisa!Kuzuia mabadiliko ya katiba kwasasa ni kukataa maendeleo ya taifa!!!Hv ubunge ni biashara watu wameenda kuchuma fedha?Mnataka posho wakati wenyewe mnakili kuwa Tz ni masikini!Muogopeni mungu nyie wabunge,kumbukeni nyie siyo hata 1% ya watanzania mil43 wanaotaka mabadiliko!!
 
Bora kulivunja bunge ili tuingie kwenye uchaguzi mwingine! Magamba ndo watakapoisoma namba vilivyo. Katiba mpya isipopatikana nako kuna moshi nje nje unafukuta!

Naunga mkono suala la JK kufikiria kuvunja bunge iwapo wabunge wa chama chake hawataki mabadiliko chanya kwa maslahi ya nchi. Uroho wao wa madaraka unatupeleka pabaya. Ni bora tukaingia gharama mpya za uchaguzi kuliko kuingia gharama za damu zetu huko mbeleni kwa kukosa katiba nzuri.
 
Mimi kwa mawazo yangu kiama cha ccm na wabunge wake kimefika ndio maana kuna kutapatapa
 
Kwa mara ya kwanza nitamuoana JK ana akili. Ni bora kuachana kabisa na mchakato wa katiba mpya kama sheria itakayotumika kupata katiba mpya ni hiyo aliyo-sign ambayo ninaamini itatuletea BORA KATIBA na SIO KATIBA BORA. Ni kheri kuchelewa kupata katiba mpya kuliko kuburuzwa. Ingawa ni JK mwenyewe aliyefanya makosa kwa ku-sign hiyo sheria wakati hata yeye akijua kwamba ina makosa mapungufu makubwa, lakini kurudia kosa ndiyo kosa. Kama wabunge wake watakataa na kwasababu JK ni weak ni bora aachane na hili jambo.

Ingekuwa wakati wa Nyerere wala hao wabunge wasingethubutu, rejea hoja ya G55 kuhusu serikali ya Tanganyika jinsi walivyonyamazishwa. Siwezi kuamini kwamba wabunge wa CCM wanaweza kupata ujasiri wa kumkatalia mwenyekiti wao, haijawahi kutokea katika miaka 35 ya uhai wa CCM! I doubting Thomas
 
Sawa nimekusoma lakini wabunge wa CCM lazima watambue mchezo wao ndiyo mauti yetu.

Siamini kama ulikuwa hujui wabunge wa ccm na ccm yenyewe hawako kwa maslahi ya wananchi wala ya nchi. Kama ulikuwa hujui ebu jikusanye chunguza halafu amua. Kwanza Katiba Mpya wamedandia na inakinzana na maslahi yao. Hata hivyo kama wote tungekuwa na maslahi ya taifa basi tungeshirikiana na kushikamana kwenye maswala ya Kitaifa. HALITAWEZEKANA TUKIWA NA CCM MADARAKANI.
 
Hivi akivunja bunge si inabidi na yeye mwenyewe aachie ngazi uitishwe uchaguzi mpya? Wanaojua nisaidieni.
 
Back
Top Bottom