Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
na Mwandishi wetu
RAIS Jakaya Kikwete ameondoka nchini jana kwenda Hispania kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa kujadili maendeleo ya Afrika na nafasi na wajibu wa siasa za kimaendeleo katika nchi za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara.
Mkutano huo wa siku moja, unaojulikana kama The African Progress Conference, unafanyika leo kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Palacio de Congresos de Madrid, mjini Madrid.
Akiwa huko, Rais Kikwete ataungana na viongozi wengine wa Afrika kujadili maendeleo ya Afrika katika mkutano huo wa aina yake kuandaliwa duniani.
Miongoni mwa viongozi ambao wataungana na Rais Kikwete katika mkutano huo ni pamoja na mwenyeji wake, Rais Jose Luis Rodriguez Zapatero wa Hispania, Rais wa Cape Verde, Pedro Pires, Waziri Mkuu wa Ethiopia, Meles Zenawi, Naibu Rais wa Afrika Kusini, Motlanthe Kgalema na Rais wa zamani wa Jamhuri ya Liberia, Amos Sawyer.
Mbali na kuhutubia mkutano huo utakaowashirikisha wanasiasa, watunga sera, wanazuoni na wasomi, wawakilishi kutoka taasisi zisizokuwa za serikali zinazojihusisha na kufikria jinsi gani ya kuharakisha maendeleo ya Afrika, Rais Kikwete pia atashiriki katika majadiliano ya mwisho ya mkutano huo.
Washiriki wengine wa mkutano huo wanatoka nchi za Tanzania, Ghana, Ivory Coast, Cape Verde, Kenya, Uingereza, Afrika Kusini, Mali, Ethiopia, Ureno, Msumbiji, Senegal, Ubelgiji, Equatorial Guinea na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Akiwa huko, Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo na Mfalme wa Hispania, D. Juan Carlos wa Kwanza na Rais Zapatero.
Source: Tanzania Daima
RAIS Jakaya Kikwete ameondoka nchini jana kwenda Hispania kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa kujadili maendeleo ya Afrika na nafasi na wajibu wa siasa za kimaendeleo katika nchi za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara.
Mkutano huo wa siku moja, unaojulikana kama The African Progress Conference, unafanyika leo kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Palacio de Congresos de Madrid, mjini Madrid.
Akiwa huko, Rais Kikwete ataungana na viongozi wengine wa Afrika kujadili maendeleo ya Afrika katika mkutano huo wa aina yake kuandaliwa duniani.
Miongoni mwa viongozi ambao wataungana na Rais Kikwete katika mkutano huo ni pamoja na mwenyeji wake, Rais Jose Luis Rodriguez Zapatero wa Hispania, Rais wa Cape Verde, Pedro Pires, Waziri Mkuu wa Ethiopia, Meles Zenawi, Naibu Rais wa Afrika Kusini, Motlanthe Kgalema na Rais wa zamani wa Jamhuri ya Liberia, Amos Sawyer.
Mbali na kuhutubia mkutano huo utakaowashirikisha wanasiasa, watunga sera, wanazuoni na wasomi, wawakilishi kutoka taasisi zisizokuwa za serikali zinazojihusisha na kufikria jinsi gani ya kuharakisha maendeleo ya Afrika, Rais Kikwete pia atashiriki katika majadiliano ya mwisho ya mkutano huo.
Washiriki wengine wa mkutano huo wanatoka nchi za Tanzania, Ghana, Ivory Coast, Cape Verde, Kenya, Uingereza, Afrika Kusini, Mali, Ethiopia, Ureno, Msumbiji, Senegal, Ubelgiji, Equatorial Guinea na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Akiwa huko, Rais Kikwete atakutana na kufanya mazungumzo na Mfalme wa Hispania, D. Juan Carlos wa Kwanza na Rais Zapatero.
Source: Tanzania Daima