JK azidi kupasua anga Ulaya

Ki Mun

JF-Expert Member
Oct 6, 2014
3,443
4,384
Wakati Rais mstaafu Jakaya Kikwete akiendelea kusafiri kwenda mataifa mbalimbali kwa shughuli za kikazi na kufikisha nchi 10 alizokwisha tembelea, Rais John Magufuli leo ametimiza siku ya 143 tangu aapishwe kuingia Ikulu bila kukwea ndege kwenda ughaibuni.

Hiyo inaweza kuwa rekodi ya aina yake kwa kuwa haijawahi kutokea tangu Uhuru kwa Rais mstaafu kusafiri safari nyingi za nje ya nchi kushinda Rais aliyeko madarakani.

Hadi sasa, Rais John Magufuli ametumia siku zote za kuwa kwake madarakani kusimamia kampeni yake ya kuongeza mapato ya serikali na kukomesha vitendo vya ufisadi kupitia kile anachokiita ‘kutumbua majipu’.

Mbali na mataifa mbalimbali aliyokwishatembelea, rekodi zinaonyesha kuwa Machi 21 mwaka huu, Kikwete alikwenda nchini Tunisia kwenye mkutano wa nane wa nchi majirani na Libya ambapo yeye ni mwakilishi maalum wa Afrika wa usuluhishi wa mgogoro wa taifa hilo.

Kabla ya kwenda Tunisia, Kikwete alikuwa katika mji wa Salalah nchini Oman alikoshiriki Mkutano wa Kamati ya Bunge la Kuandika Katiba ya Libya na alishindwa kuhudhuria kuapishwa kwa Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Shein kutokana na kuwa nje ya nchi.

Katika mkutano wake na viongozi wa Libya, Kikwete alisisitiza kuwa suluhisho la kudumu la mgogoro wa Libya liko mikononi mwa wananchi wa Libya wenyewe.Juzi Rais huyo mstaafu aliwasili Dubai akitokea Tunisia kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kwa shughuli hizo hizo za upatanishi wa mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Libya.

Uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa tayari JK ameshakwea ‘pipa’ na kufika nchi za Ethiopia, Uingereza, Visiwa vya Comoro, Afrika Kusini, Ujerumani, Marekani, Oman, Libya, Tunisia na UAE huku baadhi ya safari hizo zikitokana na mialiko maalum anayopata.

Wakati Kikwete akiendelea kusafiri kutokana na majukumu mbalimbali yanayomkabili akiwa Rais mstaafu, Rais Magufuli ameendeleza rekodi yake ya kutosafiri.


Chanzo: Gazeti la Nipashe
27 March. 2016
 
Magufuli haitaji kusafir kwa sasa, mambo serikalini hayajakaa Sawa.
Mara yatakapokaa Sawa Atascadero tu.
Kikwete kwa majukumu aliyonayo ss suala la usuluhishi, kupanda ndege hakuepukiki.
Ni kweli kabisa. Nitamshangaa sana Rais Magufuli ikiwa atasafiri nje ya nchi katika kipindi hiki ambacho wananchi wanamhitaji zaidi
 
Wakati Rais mstaafu Jakaya Kikwete akiendelea kusafiri kwenda mataifa mbalimbali kwa shughuli za kikazi na kufikisha nchi 10 alizokwisha tembelea, Rais John Magufuli leo ametimiza siku ya 143 tangu aapishwe kuingia Ikulu bila kukwea ndege kwenda ughaibuni.

Hiyo inaweza kuwa rekodi ya aina yake kwa kuwa haijawahi kutokea tangu Uhuru kwa Rais mstaafu kusafiri safari nyingi za nje ya nchi kushinda Rais aliyeko madarakani.

Hadi sasa, Rais John Magufuli ametumia siku zote za kuwa kwake madarakani kusimamia kampeni yake ya kuongeza mapato ya serikali na kukomesha vitendo vya ufisadi kupitia kile anachokiita ‘kutumbua majipu’.

Mbali na mataifa mbalimbali aliyokwishatembelea, rekodi zinaonyesha kuwa Machi 21 mwaka huu, Kikwete alikwenda nchini Tunisia kwenye mkutano wa nane wa nchi majirani na Libya ambapo yeye ni mwakilishi maalum wa Afrika wa usuluhishi wa mgogoro wa taifa hilo.

Kabla ya kwenda Tunisia, Kikwete alikuwa katika mji wa Salalah nchini Oman alikoshiriki Mkutano wa Kamati ya Bunge la Kuandika Katiba ya Libya na alishindwa kuhudhuria kuapishwa kwa Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Shein kutokana na kuwa nje ya nchi.

Katika mkutano wake na viongozi wa Libya, Kikwete alisisitiza kuwa suluhisho la kudumu la mgogoro wa Libya liko mikononi mwa wananchi wa Libya wenyewe.Juzi Rais huyo mstaafu aliwasili Dubai akitokea Tunisia kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kwa shughuli hizo hizo za upatanishi wa mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Libya.

Uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa tayari JK ameshakwea ‘pipa’ na kufika nchi za Ethiopia, Uingereza, Visiwa vya Comoro, Afrika Kusini, Ujerumani, Marekani, Oman, Libya, Tunisia na UAE huku baadhi ya safari hizo zikitokana na mialiko maalum anayopata.

Wakati Kikwete akiendelea kusafiri kutokana na majukumu mbalimbali yanayomkabili akiwa Rais mstaafu, Rais Magufuli ameendeleza rekodi yake ya kutosafiri.

Chanzo: Gazeti la Nipashe
27 March. 2016

What is the meaning of this news story? Lengo la mwandishi na gazeti hili ni nini hasa kuhusu stori hii?
 
Muacheni Vasco Dagama azunguke kwani Msoga hakukaliki; kila siku watu wake aliowateua wanatumbuliwa majipu kutokana na vijimemo vyake alivyokuwa anawaelekeza wafanye nini!!
 
Hii story ya kiboya sana; kwa sababu haieleweki ni ujumbe gani mwandishi anataka tuupate. Anasema JK anasafiri sana lakini anamalizia kuwa safari hizi zinatokana na mialiko anayoipata. Mwandishi alitakiwa atuambie kikwete alikuwa na options gani; kukataa mialiko? ku-host mikutano hiyo Tanzania? nk. Pia angejishughulisha kufahamu safari hizi zimegharimiwa na nani, zimegharimu kiasi gani cha fedha nk na je JK kwa namna yeyote alishinikiza vikao hivyo kufanyika?...wakiitwa makanjanja wanalalamika
 
Back
Top Bottom