JK ateua Mkurugenzi Mtendaji TANESCO

JK ateua Mkurugenzi Mtendaji TANESCO

Wakati Wachagga wakiwekeza kwenye Elimu kabila zingine ziko busy kurogana.........fact however bitter it is!

Nilikuwa nimependa jinsi watu walivokuwa wamechangia bila kuingilia udini wala ukabila, wewe unataka kuharibu mtiririko kabisa
 
Eng Mramba amekuwa kaimu wa nafasi hiyo kwa mda mrefu tangu alipofukuzwa kazi Eng Mhando,

Ninamfahamu vizuri na ni rafiki yangu wa karibu, uzuri zaidi nikuwa jamaa ni mtu wa kiroho yani ni mlokole halisi asiyependa njia za mkato, Amekumbana na urasimu wa wanabodi wakiongozwa na Gen Mboma hasa wakishinikiza ishu za dowansi lakini wameshindwa na sasa tanesco imeongezw ukusanyaji wa mapato kutoka milioni 12 kwa siku hadi 50milioni kwa siku, haya ni mafanikio makubwa kwake.

Kwa utendaji na uadilifu sina hofu nae labda abadilike baada ya kukabidhiwa kiti rasmi,

Eng. Mramba hongera sana. Tafadhali usiuaibishe ulokole Kama ambavyo baadhi wamefanya. Endelea kusimamia kweli na haki. Na Mungu hatakuacha wewe na uzao wako.

Tafadhali cheo kisikubadililishe ukamuacha Bwana. Pia ukumbuke watanzania WOTE wanaamini uadilifu wako utaleta matunda mazuri. Nani ajuae Tanesco itatupa Big Results Now (BRN). Jamani apewe ushirikiano hapo mahali sio pepesi. Zaburi 108:13

All the best.
Queen Esther
 
hongera sana injinia Mramba, Allah akujaalie afya njema na kukufanyia wepesi katika majukumu yako Inshaallah!
 
Nimeamini dhana ya vijana wanaweza,coz mraba ni kijana aliyeteuliwa kukaimu nafasi hiyo so kama angeli prove failure pewa
kuendelea na hiyo possition,KIKUBWA NI KWA WAFANYAKAZI WA TANESCO KUTOA USHIRIKIANO:welcome:
 
Jamani ni nini hii?
Nilitegemea amteue Mhandisi Boniface Njombe kuwa Mkurugenzi Mtendaji.

Jamaa huyu anatisha kwa utendaji na ni mtu wa principles maishani mwake.

Hahongeki, hasaundiki, anachojua yeye ni kazi, haki bin haki. Kuna wakati alifanya kazi mkoa fulani, wa kabila lake wakadhani atawasaidia na matatizo yao, aliwaacha hoi na kuwatimulia vumbi akiwabana na taratibu za utumishi wa umma.

Lakini anyway, penye miti hapana wajenzi.
Sasa huyo si atawaharibia dili...!!! wa hivyo huwa wanaachwa
 
Jamani ni nini hii?
Nilitegemea amteue Mhandisi Boniface Njombe kuwa Mkurugenzi Mtendaji.

Jamaa huyu anatisha kwa utendaji na ni mtu wa principles maishani mwake.

Hahongeki, hasaundiki, anachojua yeye ni kazi, haki bin haki. Kuna wakati alifanya kazi mkoa fulani, wa kabila lake wakadhani atawasaidia na matatizo yao, aliwaacha hoi na kuwatimulia vumbi akiwabana na taratibu za utumishi wa umma.

Lakini anyway, penye miti hapana wajenzi.

Mtu anashindwa kusaidia ndugu zake alafu unakuja hapa kumsifia?? Charity begin at home.
 
Jamani ni nini hii?
Nilitegemea amteue Mhandisi Boniface Njombe kuwa Mkurugenzi Mtendaji.

Jamaa huyu anatisha kwa utendaji na ni mtu wa principles maishani mwake.

Hahongeki, hasaundiki, anachojua yeye ni kazi, haki bin haki. Kuna wakati alifanya kazi mkoa fulani, wa kabila lake wakadhani atawasaidia na matatizo yao, aliwaacha hoi na kuwatimulia vumbi akiwabana na taratibu za utumishi wa umma.

Lakini anyway, penye miti hapana wajenzi.

huyo unamjua wewe na utendaji wake, kama alishindwa kuwasaidia wa kwao unadhani anaweza kulisaidia taifa zima??
 
Ni kujitafutia lawama tupu kwa wananchi!! kupewa shirika walikolikamua wenyewe hadi tone la mwisho!!
 
Eng Mramba anachukia rushwa ndiyo sababu Gen Mboma anamgwaya. Hii ni moja ya teuzi chache makini msanii Kikwete alizowahi fanya. Hongera Felchism

Unamaanisha nini unapomdharau rais wako namna hiyo? inamaana amekuwa ney wa mitego sio???
ovyoo kweli
 
cha kwanza ni kuondoa mchezo wa kuwapa watu kazi ya kuzisambaza nguzo za umeme,kwanini Tanesco wenyewe wasifanye kazi hiyo? inakuwaje unampa mtu kazi ya kuiuzia Tanesco nguzo tena nguzo hizo zinatoka njombe,zinapelekwa SA na kurudishwa Tanzania na kuuzwa kwa bei kubwa.lakini pia niwakati sasa wa Tanesco kuachana na utumiaji wa nguzo za miti,ni vyema wakatumia nguzo zinazotenezwa na cement,hii inafanyika china na majirani zake,ukitumia nguzo za aina hii,huitaji kubadilisha kila wakati,huitaji kuogopa moto na zinadumu kwa muda mrefu.tatizo la vishoka Tanesco limekuwa kubwa sana,ni wakati sasa wa eng huyu mramba kupambana nalo,ni vyema tanesco wakawaeleza wananchi ufikapo tanesco nani anahusika na nini na mafundi wao wapewe vitamburisho vitakavyo weza kufanya watu kuwatambua wafanyakazi wa TANESCO bila shida
Kuhusu nguzo za cement, kweli ni imara sana. Niliwahi kuona nguzo hizo kule mkoani Tanga. Bahati mbaya wezi wamebomoa nguzo hizo na kuiba nondo zote zilizotumika kujenga nguzo husika. Zinafaa sana labda tu gharama za kutengeneza hizo concrete poles inasemekana ni aghali sana.
 
Wewe ungesomea engineering labda ungefikiriwa. Hii nafasi inahitaji Mhandisi tena aliyefauu vizuri. We kalaga baho.

Nafikiri nafasi hii inahitaji manager mzuri mwenye rekodi nzuri ya usimamizi (ufaulu si sifa ya msingi) na si lazima awe mhandisi. Mhandisi kazi yake ni kuzalisha, kusafirisha, na kusambaza umeme. Mtendaji Mkuu kazi yake ni kuongoza/kusimamia (define vision and rally everybody behind a common purpose).
 
uyu hana uhusiano na yule alykuaga gavana wa benki yetu kubwa??
 
eeh! haya kaandamane basi km hutaki! aah wabongop hamna jema?mpeni hongera na kumuombea mambo ya kheri ili hata aweze kufikia kuleta unafuu ktk suala la bei za umeme...msifikiriage mambo negative tu, fikirieni na positive pia ili mfanikiwe kha!
Kwa kuongeza bei ya umeme? Not the Allah I know.
 
Kuhusu nguzo za cement, kweli ni imara sana. Niliwahi kuona nguzo hizo kule mkoani Tanga. Bahati mbaya wezi wamebomoa nguzo hizo na kuiba nondo zote zilizotumika kujenga nguzo husika. Zinafaa sana labda tu gharama za kutengeneza hizo concrete poles inasemekana ni aghali sana.

Ni kweli kabisa ndugu yangu,tabia ya wizi ni tatizo kubwa ktk jamii yetu,kama tunahitaji kuwa na aina hii ya nguzo kwanza ni vyema tukubali kuto ogopa wezi lakini pili hatuwezi kwepa gharama,sema tu,baada ya tajiri wa kinigeria kutujengea kiwanda cha utengenezaji wa malighafi za saruji upo uwezekano mkubwa cement isiwe na gharama kubwa na hapo ndipo kazi ya kuachana na nguzo za miti itakapoanza.
Elimu ikitolewa kwa watu wetu kuhusu utunzaji wa mali za umma hususani hizo nguzo upo uwezakano zikakwepa kubomolewa na kama inawezekana sheria ziwe wazi juu ya hawa wahujumu miundo msingi ya umma.
 
Hii ni commentya kijima kabisa na fyongo, yenye nia tofauti kabisa na mada ya awali...ukiitazama kwa jicho la 3 utaona kuwa ina mkono uliofichama
asante mkuu lakini huo ni mtazamo wangu tu na ndio maana nimetoa mifano ya walokole tena viongozi wao kwa maana ya wachungaji na manabii lakini wanafanya vitu visivyostahili katika jamii kiasi cha kuamini kuwa kuwa kwao walokole wanatakiwa kuwa perfect. Ungekuja na hoja yenye kuthibitisha ulokole ni hoja ningekuheshimu zaidi na zaidi

kaka panua fikra kidogo kwani akitokea muislam mmoja kala kitimoto ndio tunajenga hoja kuwa hakuna uislam, au hakuna muislam aliye muaminifu, hiyo ni fallacy- hasty generalisation

Very right mkuu. And Hasty Generalization is to believe that once you become 'mlokole' you will be free from sin especially ufisadi. This is very very wrong mkuu! Anyone can become fisadi despite being Mlokole or Mpagani.
 
tunamtakia kila la heri , tunatarajia kuanzia sasa NGUZO ZA UMEME zitatoka MUFINDI badala ya S. Africa .
 
Back
Top Bottom