JK ateua Mkurugenzi Mtendaji TANESCO

JK ateua Mkurugenzi Mtendaji TANESCO

Eng Mramba amekuwa kaimu wa nafasi hiyo kwa mda mrefu tangu alipofukuzwa kazi Eng Mhando,

Ninamfahamu vizuri na ni rafiki yangu wa karibu, uzuri zaidi nikuwa jamaa ni mtu wa kiroho yani ni mlokole halisi asiyependa njia za mkato, Amekumbana na urasimu wa wanabodi wakiongozwa na Gen Mboma hasa wakishinikiza ishu za dowansi lakini wameshindwa na sasa tanesco imeongezw ukusanyaji wa mapato kutoka milioni 12 kwa siku hadi 50milioni kwa siku, haya ni mafanikio makubwa kwake.

Kwa utendaji na uadilifu sina hofu nae labda abadilike baada ya kukabidhiwa kiti rasmi,
 
Huyu Eng. Mramba ni mtu makini na asiyehongeka kirahisi (kwa kumbukumbu zangu za nyuma.). Nina furahi kusikia kwamba hata Eng. boniface njombe ni mtu wa kaliba hiyo hiyo. Labda jambo la kujiuliza hapa ni , Je hawa watu wataruhusiwa kufanyakazi kwa kuzingatia weledi wao? Je hawa watu watawezeshwa kufikia malengo ya shirika? Ningeomba yeyote mwenye taarifa za zaidi kuhusu huyu Eng. Mramba aziweke hapa.
Eng Mramba anachukia rushwa ndiyo sababu Gen Mboma anamgwaya. Hii ni moja ya teuzi chache makini msanii Kikwete alizowahi fanya. Hongera Felchism
 
Ukisoma Mwanahalisi....oh sorry.. Mawio la last week linaeleza kuwa huyu jamaa yupo katika mgogoro na mwenyekiti wa bodi ya Tanesco Jenerali mst Robert mboma ambapo mboma anasema jamaa anatakiwa kuachia ngazi lakini anatetewa na katibu mkuu wa nishati bw maswi. Tafuta Mawio la last week lina habari ya kina ya huyu mtu

Sasa kwa kitendo cha Raisi kumpigia Mstari maanke si kampuuza Mbona? sasa kwa nini Mboma kama ni mkweli asiachie yeye?
 
hv wakimsikia wale wahubili wa ukanda na udini si watamtenga kwenye kikundi chao kile cha ma CCM watasema sana ila wachaga nomaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Rais Kikwete jioni hii amemtangaza rasmi Mhandisi felchesmi mramba kuwa mkurugenzi mtendaji wa Tanesco uteuzi ambao umeanza rasmi leo hii
Labda kwa mengine ila kwa ubadhirifu huyu jamaa ninamjua kuwa sio mbadhirifu kabisa maana ni mtumishi wa Mungu aliyetukuka... labda abadilike. Nimewahi kuwa nae kwenye kanisa moja la Assemblies of God(TAG) na kwa kwa kweli si wa kumtilia shaka uaminifu wake ... naamini kwa hapa mafisadi walie tu..
 
Hongera Mate Wa Kibaha Secondary Eng Felchism Mramba uadilifu wako ni Tunu kwa TANESCO na Taifa. Umefata nyayo za Dr Kazaura Kamugisha Dir General TTCL. I'm proud of you guys.
For sure, I admire this guy. Humble,servant of God,kwa kweli taifa linahitaji watu safi kama huyu... bahati mbaya tu ni huu mfumo wa serikali badhirifu ya ccm,nakuombea Ndugu Mramba uyashinde mabaya yote....
 
Eng Mramba amekuwa kaimu wa nafasi hiyo kwa mda mrefu tangu alipofukuzwa kazi Eng Mhando,

Ninamfahamu vizuri na ni rafiki yangu wa karibu, uzuri zaidi nikuwa jamaa ni mtu wa kiroho yani ni mlokole halisi asiyependa njia za mkato, Amekumbana na urasimu wa wanabodi wakiongozwa na Gen Mboma hasa wakishinikiza ishu za dowansi lakini wameshindwa na sasa tanesco imeongezw ukusanyaji wa mapato kutoka milioni 12 kwa siku hadi 50milioni kwa siku, haya ni mafanikio makubwa kwake.

Kwa utendaji na uadilifu sina hofu nae labda abadilike baada ya kukabidhiwa kiti rasmi,
Mkuu umenena vema sana,the guy is a man of God.
 
Hayo unayosema yanaweza kuwa sahihi kwa sababu wewe ndiye unayemfahamu huyo Njombe. Ila mimi namfahamu Mramba, nimesoma naye, nimefanya naye kazi over the years, nakuhakikishia the guy is good ! Nadhani hizo sifa ulizozitaja kwa huyo Boniface, mramba anazo vile vile.....

Jamani ni nini hii?
Nilitegemea amteue Mhandisi Boniface Njombe kuwa Mkurugenzi Mtendaji.

Jamaa huyu anatisha kwa utendaji na ni mtu wa principles maishani mwake.

Hahongeki, hasaundiki, anachojua yeye ni kazi, haki bin haki. Kuna wakati alifanya kazi mkoa fulani, wa kabila lake wakadhani atawasaidia na matatizo yao, aliwaacha hoi na kuwatimulia vumbi akiwabana na taratibu za utumishi wa umma.

Lakini anyway, penye miti hapana wajenzi.
 
Sijui ataweza kuharakisha ufungaji wa umeme kwa watu tulioomba tangu JANUARI! Tangu january nimeomba kufungiwa umeme tena watu wa tatu tunahitaji nguzo 1 tu!! Lakini inatia hasira..MPAKA NAICHUKIA TANESKO.
 
Jembe lililokuwa limebaki TANESCO, nadhani sasa wenye majenereta wayapeleke Sudan Kusini, Tz hakutakuwa na mgao tena wa kushinikizwa kuzima umeme ili majenereta yauzwe!
 
kwa comment za watu inaonyesha Mboma sio muadilifu.
Hongera Mramba kazi njema.
 
Nitamuona wa maana kama akitengua ombi lao la kutuongezea bei ya umeme waliloliwasirisha EWURA. Vinginevyo ni siasa tu as usual.
 
Wamethubutu, wameweza na sasa wanaendelea zao.

Ikiwa wamediriki kupandisha bei ya umeme katikati ya mgao wa aibu, ni nini kisichowezekana kwa Kikwete na TANESCO?

I rest my case.
 
Back
Top Bottom