Mimi sishangai hili
OMBI...Lakini nitakachoshangaa ni kama NCHI yetu bado Watu wanajifanya
kwamba hawajui ni NAMNA GANI YA KUWAPATA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI
Kuletewa walimu toka Jamaica sio suluhisho ZURI!
Ni kweli tuna TATIZO LA KUSULUHISHWA HARAKA ili tuweze kupata Walimu wa
Sayansi.
Tatizo ni kwamba Nchini mwetu,kuna Watu wamekaa na kujifanya hawajui
kwamba kuna tatizo la masomo ya Sayansi kuogopwa na Vijana/watoto
wengi;hivyo zinahitajika jitihada za makusudi kabisa kabisa ili kuweza
kuokoa jahazi.
Ukweli ni kwamba🙁Uso nimeukunja hapa,utake usitake)
1.Sayansi ni NGUMU zaidi ya ART
2.Kuanzishwe Olimpiki za masomo ya Sayansi mashuleni,watoto wengi zaidi
wavutwe kupenda sayansi kama vile kuwapa zawadi na medali wale
wanaofaulu vema masomo ya sayansi
3.Watu wahimizwe kusoma sayansi kuanzia form 2,wanaofaulu masomo ya
Sayansi vizuri wapewe zawadi ikiwezekana hata kulipiwa ada
4.Waalimu wa Sayansi wapewe upendeleo maalumu sehemu yeyote wanayopangwa
Hii yote itasaidia hawa watu kuigwa....Watoto mashuleni watajua kwamba
kusoma Sayansi vema ama nikiwa Mwalimu Sayansi mambo yangu yatakuwa sio
haba.
Siku hizi kila mtu anataka awe Mwanasiasa...Kwanini?Kwa sababu Siasani
ndio kuna motivation zote hizo...hela nzuri,gari nzuri,maisha
mazuri.,....nani hataki hayo maisha?halaf ubaya ni kwamba kila kukicha
sie pamoja na watoto tunasikia wanasiasa wengi hata hawajasoma...kumbuka
zama hizi sio kama zamani ambapo information kama hizi ilikuwa ngumu
kuzipata,na hata magazeti ya Chama hayakuwa yanandika,na wengine
tuliokuwa vijijini enzi hizo mnasubiri magazeti ya wakatoliki ya
Kiongozi ambayo yana makala za Mbunda msokile as a hot topic
kwishneeey....sala kibwaaao!
Ninakumbuka Baba yangu enzi hizo nilimuuliza kama nataka "U- Nyerere@
nifanyeje,yeye akaniambia ni lazima niwe wa kwanza darasani kuanzia
darasa la kwanza mpaka la saba!niliamini hivyo....mwambie mtoto wa siku
hizi hayo!Looo
Watu wameanza kutoka Kozi za Sayansi(Ma engineer,Madaktari wanasoma
MBA,Bcom---maksi zao za nyuma zinawaruhusu,i mean za Alevel),kwa sababu
wanagundua late kwamba waliingia chaka kuchagua Kozi ambazo zina "sifa
za Kijinga"...sifa nyingi halafu unaponda kwa mguu,wakati yule uliyekuwa
unamcheka enzi hizo kwamba anasoma "art",leo hii anakwambia "Pole Bwana
Mkubwa hebu nikufikishe mbele kidogo"?
Unajua tatizo linakuja kwamba mechanism ya kuwapata walimu ni ya aina
yake.....wale watu ambao hawajafaulu vizuri,ndio wanaochukuliwa kwenda
Ualimu.....na mara nyingi unakuta kwamba watu wanaojiweza kwenye
science,in one way or the other hata masomo mengine wanayaweza...lakini
watu wasioiweza sayansi,hakuna guarantee kwamba wanaweza hata masomo
mengine,ni either hawayawezi yote,ama wanaweza ya Art tu....hivyo ni
bora kuwakazania wanafunzi wakiwa bado wadogo wasiiiogope sayansi,kwani
inahitaji nguvu za ziada kuweza kufanya watoto waipende....art watajua
tu njiani,lakini huwezi ukawaacha ukasema sayansi wataijua njiani.
Ni lazima Sayansi itambuliwe kama Special subjects zinazohitaji special
treatment,iki involve programe,na washika dau wake,yaani walimu wa
sayansi na wanafunzi wanaopenda sayansi
Unless tutaendelea kujificha vichwa udongoni na kuacha i kibinda nkoi
iko nje,tukidhani kwamba hatuonekani,kumbe sie ndio hatuoni
kinachoendelea.....Kuwapata walimu wa sayansi sio mchezooooo,kunahitaji
gharama na nguvu ya ziada isiyohitaji aibu ya kwamba "tutakuwa
tunawatenga ama kuwadhalilisha waalimu wa makundi masomo mengine"
Am out