JK aomba walimu toka Jamaica

JK aomba walimu toka Jamaica

Mkuu hata mimi hiyo imenishangaza sana au alikuwa ill adviced hata sielewi, JK mwenyewe kasoma economics kwa hiyo hata somo la hesabu inaliweza sana akipata muda wa kujitayarisha, huo ulikuwa ni utangulizi wangu kwanza - sasa tuje kwenye masoma ya HESABU na FISIKIA/SAYANSI raia walio somea fani ya Engineering wote wanayamudu masomo hayo kwa ufanisi mkubwa sana, mkuu Watanzania wana uwezo mkubwa sana katika masomo hayo wakipewa motisha wa kutosha.

Mimi nina mfano hai, nilibahatika kwenda kusoma katika nchi za magharibi shahada yangu ya kwanza ya Engineering enzi hizo, kitu kilicho washangaza Wazungu ni uwezo mkubwa wa Watanzania katika kumudu somo la Hesabu, na si hisabati tu hata fisikia na kemia - wanafunzi kutoka Kenya, Uganda, Zambia nk walikuwa awaoni ndani - hapo ndipo nilikuja gunduwa kwamba Kambarage alikuwa mahiri katika suala la Elimu nchini na alikuwa anawapa walimu motisha wa kutosha na walikuwa na nidhamu ya hali ya juu kweli kweli.

Mimi nashauri kitu cha kufanya ni kumueleza Waziri wa Elimu Mh.Kawambwa ajaribu kuwasiliana na ma Engineeer nchini ambaoa wako kazini na wale walio staafu, alafu ajaribu kuwasikiliza wanaweza kusaidia kivipi katika masomo hayo muhimu ya kisayansi - unajua mambo mengine unapaswa kuwa mbunifu wakati mwingine; wajaribu kumuhiga Mh.Mwakyembe - mambo mengine mengi Watanzania tuna uwezo wa kuyatatua sisi wenyewe bila ya kutegemea nchi za nje - ukosefu wa UBUNIFU na kutojiamini ndio naona ndilo tatizo kubwa nchini, chukulia suala kama hili la ukosefu wa walimu wa hisabati na sayansi kwani walikuwa awajuhi kwamba ma Engineer wanaweza kusaidia katika HILO??

Mkuu unaona mbali, chamsingi ni kuboresha mishahara ya walimu pia. Kwani walimu wapo isipokuwa wengine wameamua kuwa ma-tellers ktk mabenki. Ualimu umekuwa na maslahi duni sana.
 
Da tukipata walimu kama kumi wa mchezo wa mbio lazima tutoke kimchezo. Tena ngona nimtafute Joe Stivin tukawekeze kule kwake.
 
Ina maana Jamaica katika sayansi wako vizuri sana kiasi tuwaombe msaada katika eneo hili?
 
Mimi nina mfano hai, nilibahatika kwenda kusoma katika nchi za magharibi shahada yangu ya kwanza ya Engineering enzi hizo, kitu kilicho washangaza Wazungu ni uwezo mkubwa wa Watanzania katika kumudu somo la Hesabu, na si hisabati tu hata fisikia na kemia - wanafunzi kutoka Kenya, Uganda, Zambia nk walikuwa awaoni ndani - hapo ndipo nilikuja gunduwa kwamba Kambarage alikuwa mahiri katika suala la Elimu nchini na alikuwa anawapa walimu motisha wa kutosha na walikuwa na nidhamu ya hali ya juu kweli kweli. Mimi nashauri kitu cha kufanya ni kumueleza Waziri wa Elimu Mh.Kawambwa ajaribu kuwasiliana na ma Engineeer nchini ambaoa wako kazini na wale walio staafu, alafu ajaribu kuwasikiliza wanaweza kusaidia kivipi katika masomo hayo muhimu ya kisayansi - unajua mambo mengine unapaswa kuwa mbunifu wakati mwingine; wajaribu kumuhiga Mh.Mwakyembe - mambo mengine mengi Watanzania tuna uwezo wa kuyatatua sisi wenyewe bila ya kutegemea nchi za nje - ukosefu wa UBUNIFU na kutojiamini ndio naona ndilo tatizo kubwa nchini, chukulia suala kama hili la ukosefu wa walimu wa hisabati na sayansi kwani walikuwa awajuhi kwamba ma Engineer wanaweza kusaidia katika HILO??
Nakuhunga mkono kwa wazo lako. Kweli kabisa kuhusu watz tupo fiti hila mfumo mbovu ktk sekta ya elimu na serikali kwa ujumla ndochanzo cha matatizo yote haya.Embu siku moja serikali ifanye mabadiliko ya maana hili Tz tupae kama wenzetu. Mbona Mwalimu Nyerere aliweza? Hivi duniani tunajua tumekuja kushangaa magorofa na magari ya wazungu au tunaitajika kufanya maendeleo halafu tuondoke zetu? Albert Einstein haliwai kusema maneno mazuri sana "I have done my share, it is time to go. I will do it elegantly." Hivyo tufanye kazi kwa bidii bila kuchoka hata kama wanatnyonya hila nafsi zao zinawasuta na pia najua wanaumia sana kwenye mioyo yao.
 
Raisi wetu anaomba mpaka nchi maskini? Hivi sisi na jamaica tunatofauti gani? Tena tunawazidi kwa rasilimali.. (mbona tunatiana aibu jama?)
 
Jk kwel hii tabia ya kutufanya omba omba dunian wakati Watanzania tunakila rasilmal za kila aina ni kutudhalilisha na kutuibisha.

Kwel watz tumeishiwa had tuombe walimu wa sayans na hisabat jamaica?
Mimi kama mwalimu wa masomo ya sayans naomba niseme kuwa walimu wa hayo masomo tupo weng tu.
Mitaan.

Tatizo ni dharau yako na serikal yako juu ya walimu,mishahara midogo,malimbikizo ya stahik zetu,mazingira mabovu ya kufanyia kaz.

Walimu tupo private schools and tasis nyingine.nibora mwalimu kufundisha tuition centre kama tatu au nne kuliko kuajiriwa na serikal ya JK.
Boreshen hayo ndo tutakuja kama si hivyo safar njema na wajamaica wako ila walimu wa sayans na hesabu tupo kuhakikisha ilo tembelea vituo binafsi na shule binafsi uone kama kuna uhaba wa walimu.
Nawasilisha.
Mwl Muta
 
Nimeona hii habari nikasikitika sana....Hivi kasema hivyo kweli au wanamsingizia....? Walimu wetu wenyewe tunashidwa kuwalipa hao wajamaica tutawalipa nini...?au ndo hela itakuwepo ya kuwalipa wajamaica lakini kulipa wakwetu haipo...Mimi nafahamu walimu wengi sana wameacha kazi ya ualimu kwasababu ya maslahi madogo...sasa jamaa anataka wa Jamaica...?!!!!!!!
 
Ni kweli usemavyo ndugu yangu, Jamaica ni wavuta bangi kuliko mahali popote labda kama anataka walimu wa reggae music. Umeona hali ya Mzumbe special school? Kwa mtaji huo ndani ya utawala wa CCM tuhesabu tumezikwa wakenya na waganda watatunyang'anya hata kazi za ulinzi.
 
Hivi kama hawa tu kuwalipa inakua shida...hao wa Jamaica utawalipa nini..?(kwanza ni kwa dola au madafu)....au ilikua changamsha kijiwe...?Sis waafrika tumekuaje sisis..?au DNA zetu zinashida kidogo..?US au UK wakifanya Brain Drain wanakuwa wafanyakazi wao wanawalipa vya kutosha ndo wanaiba na nchi nyingine...Sasa hapa walimu hawalipwi... wametoka kugoma hata hawkusikilizwa wewe unasema unataka wa Jamaica...Hii miaka kumi wabongo tumekula HASARA
 
Kwa mtaji wa huo msaada unaotarajiwa kutoka Jamaica, taifa masikini mwenzetu katika lile kundi la mataifa ya Ulimwengu wa Tatu licha ya kujawa na walimu Grade A na Diploma kibao nchini ambao hawajapata posting tangu enzi za Waziri Mungai, Tanzania sasa tujiandae kupata kundi kubwa mno la 'Ma-JUSTIN KALIKAWE' na 'VIKOSI VYA MIZINGA' kwenye matokeo ya form four maadam walimu sasa ni kuagizwa kwa Magwiji wa Regge na Ragamaffin duniani.
 
hayo marupurupu watakayo mlipa mjamaika mwalimu wanipe mimi nitaenda kufundisha usiku na mchana kwa hari kubwa na watoto watafaulu na kupenda masomo ya sayansi,sio kunilipa pesa nusu ya per diem ya ofisa wa serikali aliye semina bagamoyo.Yaani rais wetu unatia aibu sasa badala ya kuwenga misingi endelevu ya kutatua tatizo,unatafuta tiba ya muda mfupi isiyotoa suluhisho la kudumu.Tumia resources za ndani JK usitegemee vya kuomba
 
Raisi wetu anaomba mpaka nchi maskini? Hivi sisi na jamaica tunatofauti gani? Tena tunawazidi kwa rasilimali.. (mbona tunatiana aibu jama?)

Hivi kwani katika hizi Protocol ukiwa Rais\kiongzi wa nchi huruhusiwi kukaa kimya kama huna cha maana cha kumwambia fellow national leader?
 
somo la reggae music liingizwe kwenye mtaala plz na bado aombe na mateacher toka mexico nasikia ni wazuri sana kwa marijuana

tatizo si kwamba hakuna watu wanaoweza kufundisha hayo masomo bali watu hawataki kufundisha kwa sababu kunahusishwa na umasikini/ tatizo ni umaskini na ulofa katika ualimu na si kutokuwapo kwa watu hao. kuondoa hilo ni kujaza amapesa katia taaluma hii na walimu watajaa tu
 
Hivi tuna upungufu wa walimu au maslahi ya walimu ndo yanatakiwa yaangaliwe na kuboreshwa? JK haishi kutushangaza.
 
Back
Top Bottom