Nitakachosikitika ni pale hao Mwl toka Jamaica atakuwa analipwa mara 4 ya huyu wa Tz ingawa huyu atakuwa nafanya kazi nzuri kuliko huyo mgeni. Yangu macho.
Mimi sishangai hili OMBI...Lakini nitakachoshangaa ni kama NCHI yetu bado Watu wanajifanya kwamba hawajui ni NAMNA GANI YA KUWAPATA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI
Kuletewa walimu toka Jamaica sio suluhisho ZURI!
Ni kweli tuna TATIZO LA KUSULUHISHWA HARAKA ili tuweze kupata Walimu wa Sayansi.
Tatizo ni kwamba Nchini mwetu,kuna Watu wamekaa na kujifanya hawajui kwamba kuna tatizo la masomo ya Sayansi kuogopwa na Vijana/watoto wengi;hivyo zinahitajika jitihada za makusudi kabisa kabisa ili kuweza kuokoa jahazi.
Ukweli ni kwamba
🙁Uso nimeukunja hapa,utake usitake)
1.Sayansi ni NGUMU zaidi ya ART
2.Kuanzishwe Olimpiki za masomo ya Sayansi mashuleni,watoto wengi zaidi wavutwe kupenda sayansi kama vile kuwapa zawadi na medali wale wanaofaulu vema masomo ya sayansi
3.Watu wahimizwe kusoma sayansi kuanzia form 2,wanaofaulu masomo ya Sayansi vizuri wapewe zawadi ikiwezekana hata kulipiwa ada
4.Waalimu wa Sayansi wapewe upendeleo maalumu sehemu yeyote wanayopangwa
Hii yote itasaidia hawa watu kuigwa....Watoto mashuleni watajua kwamba kusoma Sayansi vema ama nikiwa Mwalimu Sayansi mambo yangu yatakuwa sio haba.
Siku hizi kila mtu anataka awe Mwanasiasa...Kwanini?Kwa sababu Siasani ndio kuna motivation zote hizo...hela nzuri,gari nzuri,maisha mazuri.,....nani hataki hayo maisha?halaf ubaya ni kwamba kila kukicha sie pamoja na watoto tunasikia wanasiasa wengi hata hawajasoma...kumbuka zama hizi sio kama zamani ambapo information kama hizi ilikuwa ngumu kuzipata,na hata magazeti ya Chama hayakuwa yanandika,na wengine tuliokuwa vijijini enzi hizo mnasubiri magazeti ya wakatoliki ya Kiongozi ambayo yana makala za Mbunda msokile as a hot topic kwishneeey....sala kibwaaao!
Ninakumbuka Baba yangu enzi hizo nilimuuliza kama nataka "U- Nyerere@ nifanyeje,yeye akaniambia ni lazima niwe wa kwanza darasani kuanzia darasa la kwanza mpaka la saba!niliamini hivyo....mwambie mtoto wa siku hizi hayo!Looo
Watu wameanza kutoka Kozi za Sayansi(Ma engineer,Madaktari wanasoma MBA,Bcom---maksi zao za nyuma zinawaruhusu,i mean za Alevel),kwa sababu wanagundua late kwamba waliingia chaka kuchagua Kozi ambazo zina "sifa za Kijinga"...sifa nyingi halafu unaponda kwa mguu,wakati yule uliyekuwa unamcheka enzi hizo kwamba anasoma "art",leo hii anakwambia "Pole Bwana Mkubwa hebu nikufikishe mbele kidogo"?
Unajua tatizo linakuja kwamba mechanism ya kuwapata walimu ni ya aina yake.....wale watu ambao hawajafaulu vizuri,ndio wanaochukuliwa kwenda Ualimu.....na mara nyingi unakuta kwamba watu wanaojiweza kwenye science,in one way or the other hata masomo mengine wanayaweza...lakini watu wasioiweza sayansi,hakuna guarantee kwamba wanaweza hata masomo mengine,ni either hawayawezi yote,ama wanaweza ya Art tu....hivyo ni bora kuwakazania wanafunzi wakiwa bado wadogo wasiiiogope sayansi,kwani inahitaji nguvu za ziada kuweza kufanya watoto waipende....art watajua tu njiani,lakini huwezi ukawaacha ukasema sayansi wataijua njiani.
Ni lazima Sayansi itambuliwe kama Special subjects zinazohitaji special treatment,iki involve programe,na washika dau wake,yaani walimu wa sayansi na wanafunzi wanaopenda sayansi
Unless tutaendelea kujificha vichwa udongoni na kuacha i kibinda nkoi iko nje,tukidhani kwamba hatuonekani,kumbe sie ndio hatuoni kinachoendelea.....Kuwapata walimu wa sayansi sio mchezooooo,kunahitaji gharama na nguvu ya ziada isiyohitaji aibu ya kwamba "tutakuwa tunawatenga ama kuwadhalilisha waalimu wa makundi masomo mengine"
Am out