JK anamuandaa Edward Lowasa kuwa rais mwaka 2015

amejitahidi pamoja an ugeni, amejitutumua kiasi chake, atakuja kuwa memba mzuri wa JF
 
Kweli siasa ni mchezo mchafu. Unaweza kumsikia mwanasiasa anasema hiki ukafikiri anamaanisha kumbe ni kuhadaa wananchi tu, hii imedhihirika baada ya kupata tetesi kutoka Ikulu ya Dodoma kuwa anayeandaliwa kuwa Rais mwaka 2015 ni Edward Lowasa na sio Asha Rose Migiro wala Amani Karume.

Mtoa habari hizi ameeleza kuwa mipango hii inafanywa kwa ustadi mkubwa sana kiasi kwamba sio rahisi watu kufahamu kinachoendeleo hivi sasa.

Ameendelea kusema, mbinu alizozifanya na atakazoendelea kuzifanya ni pamoja na;

  1. Kujifanya ni adui mkubwa wa Lowasa kwa sasa ili watu waamini hivyo
  2. Kumlejesha Asha Rose Migiro nyumbani ili aanze kuonekana kwa watu ambapo hivi karibuni atamteua kuwa mbunge na hatimaye waziri (Kumbuka JK bado ana nafasi 7 za wabunge, zilikuwa zinamsubiri mama huyu).
  3. Hata mabadiriko ya baraza la mawaziri lililoandikwa sana kwenye vyombo vya habari lilikuwa linamsubiri Asha.
  4. Anasema, '' UKWELI NI KWAMBA ASHA HAADALIWI KUWA RAIS BALI WAZIRI MKUU''
  5. Ananiambia, Siri ya JK na Lowasa ni kubwa Mno mpaka uijue unakuwa umeaminiwa sana na hawa watu.
  6. Lowasa atajulikana mwishoni kabisa kwenye maamuzi ya CC ambayo mtu pekee wa kuamua ni JK mwenyewe kwavile hana mtu mwingine wa kumpinga mle.
  7. Kuwaondoa Marais wastaafu kwenye CC ndiyo ulikuwa mtihani wake mgumu sana na sasa kafaulu na baada ya mchakato huo wazee hao watarudishwa tena CC.

Nawasilisha.

hapo kwenye redi, alafu wewe umezipata wapi hizi??????????
au ndo mtu mwenyewe wa karibu?????????
anyway, kama halipo basi linakuja
 
Kweli siasa ni mchezo mchafu. Unaweza kumsikia mwanasiasa anasema hiki ukafikiri anamaanisha kumbe ni kuhadaa wananchi tu, hii imedhihirika baada ya kupata tetesi kutoka Ikulu ya Dodoma kuwa anayeandaliwa kuwa Rais mwaka 2015 ni Edward Lowasa na sio Asha Rose Migiro wala Amani Karume.

Mtoa habari hizi ameeleza kuwa mipango hii inafanywa kwa ustadi mkubwa sana kiasi kwamba sio rahisi watu kufahamu kinachoendeleo hivi sasa.

Ameendelea kusema, mbinu alizozifanya na atakazoendelea kuzifanya ni pamoja na;

  1. Kujifanya ni adui mkubwa wa Lowasa kwa sasa ili watu waamini hivyo
  2. Kumlejesha Asha Rose Migiro nyumbani ili aanze kuonekana kwa watu ambapo hivi karibuni atamteua kuwa mbunge na hatimaye waziri (Kumbuka JK bado ana nafasi 7 za wabunge, zilikuwa zinamsubiri mama huyu).
  3. Hata mabadiriko ya baraza la mawaziri lililoandikwa sana kwenye vyombo vya habari lilikuwa linamsubiri Asha.
  4. Anasema, '' UKWELI NI KWAMBA ASHA HAADALIWI KUWA RAIS BALI WAZIRI MKUU''
  5. Ananiambia, Siri ya JK na Lowasa ni kubwa Mno mpaka uijue unakuwa umeaminiwa sana na hawa watu.
  6. Lowasa atajulikana mwishoni kabisa kwenye maamuzi ya CC ambayo mtu pekee wa kuamua ni JK mwenyewe kwavile hana mtu mwingine wa kumpinga mle.
  7. Kuwaondoa Marais wastaafu kwenye CC ndiyo ulikuwa mtihani wake mgumu sana na sasa kafaulu na baada ya mchakato huo wazee hao watarudishwa tena CC.

Nawasilisha.

Sijui hata nichangie nini!!
 
Hata mimi sitashangaa maana kikundi cha JK hakina ubavu wa kumzuia huyu fisadi papa watampisha apite kama alivyowafanya Arumeru kwa mkwe wake. Wamruhusu tu aje apambane na wanaume wa nguvu ya umma. Watu watamfilisi kila kitu 2015 na kura watamnyima maana wakimpa atatuuza mpaka wananchi ili kurudisha fedha yake. Chadema waanzie Arumeru kumwashia indicator za 2015.
 
Ni tetesi lakini naamini hivyo. JK ana kila sababu ya kufanya hivyo kwa madudu aliyofanya na Lowassa, wa kumlinda yeye ni lowassa tu. Sitta atawafunga, Membe hana ubavu wa kuhimili vishindo vya raia wakati huo. Lowassa ndiye chaguo lake pekee kwa ajili ya kujilinda na sio maendeleo ya nchi. Hata hivyo naamini CDM watachukua nchi na utakuwa mwisho wa hao mafisadi.
 
Ni tetesi lakini naamini hivyo. JK ana kila sababu ya kufanya hivyo kwa madudu aliyofanya na Lowassa, wa kumlinda yeye ni lowassa tu. Sitta atawafunga, Membe hana ubavu wa kuhimili vishindo vya raia wakati huo. Lowassa ndiye chaguo lake pekee kwa ajili ya kujilinda na sio maendeleo ya nchi. Hata hivyo naamini CDM watachukua nchi na utakuwa mwisho wa hao mafisadi.
Hivi cdm itakuwepo wakati huo ?
 
Hapa kuna asilimia kubwa sana ya ukweli. Sisi wengine tuliliona hili mara tu baada ya wastaafu kuondolewa kwenye CC.
 
frustration = expectation/outcome
Not always true....je kama your expectation ni kama ilivyokuwa kwa mbunge wa Ilemela (Kiwia or whatever his name is) ambaye alitegemea kuangushwa kwa kishindi na Diallo,, lakini outcome ikawa ushindi?? Frustration si mahala pake
 
Haya mambo wakati mwingine nii burudani sana,uzuri ukiwa ndani uwezi kuona nje na wakati mwingine Mungu anaongea na walio nje kuwaonyesha wa ndani.Ndio maana kukiwa na mechi ya mpira wakati mwingine watazamaji umlazimisha kocha kwa kumwambia toa huyo!!!!!!!!.....toa huyo tena wakishambulia kwa mbija kubwa sana pfyuuuuuuu!!!!!!!!!!!!pfuuuuuuuuuuu!!!!!. Mwisho wa yote kocha usikia makelele ya mashabiki na umtoa mcheza nje.Mchezo huo ama style hiyo imekwenda mpaka sasa imefikia hatua hata makocha wamefikia kuwa nao hatima ya kuendelea kuwemo uwanjani kama makocha wa timu ya mashabiki ni kuweka ushindi kwenye timu ya mashabiki,vinginevyo kitakachofuata baada ya kubolonga mara kadha wa kadha ni kushinikiza kocha atoswe kama ilivyotokea kw maxio maximo. [Kocha Mbrazil]

Haya yanayosemwa sana siku hizi mitaani kuwa fulani anatyarishwa kuwa Rais kimepanda kikashuka,hakika kama mtanzania nianetafakari kupitia ukweli halisi na si kwa kuwa fulani anafedha na watu wa kumfanya awepo pale wanasahau kuwa fedha sio kila kitu.

Mwaka 1985 Baba wa Taifa alikuwa na chaguo lake ambalo alitaka kumlithisha kuwa Rais mwaka huo lakini pamoja na nguvu zote hizo za Umwalimu wake kwa Serikali dhamira yake haikufanikiwa. Mwaka 1995 Rais ambae alikuwa madarakani alikuwa na chaguo lake ambae alipenda amlithishe pia,lakini siye aliyekuja kuwa Rais wa Tanzania kipindi hicho.Mwaka 2005 Rais na wale waliokuwa madarakani walikuwa na machaguo yao mwaka huo ambao waliwaanda kuwaweka madarakani lakini matokeo yake alieingia sie aliekuwa chaguo lao hata kama wako chama kimoja.

Leo hii tunaenda mwaka 2015,tunajua kama binadamu Mungu alivyotuumba tuna utashi na chaguzi zetu binafsi lakini, katika swala la urais Mungu nae ucheza turufu yake kwa sababu anazozitaka yeye na sio sisi binadamu watu wazima uwa na msemo wao wewe unapanga na Mungu anapanga.Hili la Rais kuhusishwa na kumwandaa huyu jamaa kama ni kweli au La hakika ni utashi tu na si jambo la ajabu na yeye si mtu wa kwannza uzuri mwenyewe anajua jinsi alivyokutana na vizuizi mpaka akafika hapo ndivyo hivyo huyo wasie mtaka hao wengine awe Rais wa mwaka 2015,hatatoka kwa Watawala bali watawala watalazimika kumsimamisha ili iwe ni heri ya nusu shari kuliko shari kamili.Muda ukifika mbona kitaeleweka tu.Kuna mmoja huyo alitayarisha timu idara zaote Serikalini akiwa anategemea Urais wa 2005 lakini chakachua ni kuchakachue iliyopita uwezi kuamini, urais aliusikia kwenye bomba.

Uzuri wa maswala hayo utoa ajira kwa baadhi ya watanzania na wengine kujipatia kipato kupitia michakato hiyo hivyo yote heri,lakini uzaniaye ndiye kumbe siye na uzaniaye sie kumbe ndie, kwenye msafara wa mamba kenge nao wamo.Huwezi kutumia Devil style Strategy [Fisadi] kumpandisha chati Mtu wa Kiti cha Urais [Utakatifu],sijawi kuona aina hiyo ya mikakati.Kwa kuwa wanapenda sana kufananisha na style ya southh africa ya Jacob Zuma,wanasahau wale jamaa walikuwa na mtafaruku wa kweli,na hatimae imejibu kwa kijana malema.Na pia kihistoria Tanzania ni Taifa lenye watu wengi wenye uzoefu kisiasa ambao jicho lao kwa mtu anaitwa Rais liko pana sana kuliko ilivyo kawaida.
 
Back
Top Bottom