JK ame poteza "star power"

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
836
Hapa naomba nitumie mfano wa kimichezo. Kwenye timu yoyote mchezaji muhimu si yule tu ambae akiwa uwanjani timu huchezi vizuri bali pia ni yula ambae kama asipo kuwa dimbani unaona timu haichezi kama kawaida.

In short kwa sasa naanza kuona kama vile JK ana kosa umuhimu. Akiwa uwanjani timu haichezi vizuri na hata aki kosekana dimbani haionyeshi kubadilisha chochote kwenye timu.

Sasa katika hali ya kawaida mchezaji aliekuwa kiungo muhimu ana bidi aamue kustaafu au kuji kuta aki poteza kabisa heshima aliyo jijengea na kuji kuta mwisho wa kucheza ukifika hamna anaemkumbuka.

Kwa hali ya sasa ninge sana JK afanye mustakabali wake wa umuhimu wake katika siasa za Tanzania. Je ana taka kukumbukwa kwa heshima (japo kidogo) aliyo bakiza? Au ana taka ifike kipindi tumsahau kabisa.

Kama ataamua kubaki (historia ya viongozi wa Afrika inaonyesha ata amua kubaki) basi inabidi afanye mazoezi ya ziada kuhakikisha kiwango kina panda (kama kili wahi kuwepo). Asije akawa kama kaka etu Beckham ambe anauza sura kwenye vyombo vya habari lakini uwanjani wote tuna fahamu hakuna kitu kilicho baki (samahani mashabiki wa Becks).
 
Kweli kabisa mwanafalsafa1, lakini bado ana muda kidogo wa kuweza kurudisha kiwango chake na kurudisha imani kwa wananchi.
 
Kweli kabisa mwanafalsafa1, lakini bado ana muda kidogo wa kuweza kurudisha kiwango chake na kurudisha imani kwa wananchi.

Mkuu unajua tena uraisi si kama ubunge, una kikomo. Sasa hivi mheshimiwa yupo katika mwaka wake wa sita akiwa ame bakisha minne. Sasa muda wa kurudisha kiwango na kuonyesha kiwango ni mdogo mno. He has to act NOW!

In my opinion hakuna raisi aliye kuwa na opportunities nyingi za kuonyesha kiwango kama JK. Kuna swala la Richmond, Dowans, "vijisenti" nk. Zote hizo angeonyesha initiative tu hata za kuwa fukuza wahusika na kuwa kemea hadharani (hata kama nyuma ya pazia wangekua wana chekeana) basi mbele ya Watz angekua ame accomplish something. Sasa naona mheshimiwa ana achia opportunities zote zimpite.

Mimi naanza kuhisi kuanza kwake kushuhulikia mambo ya Ivory Coast ni kucompensate kwa ajili ya nyumbani. Kwa vile amesha jua akisha ondoka ni wachache sana watamkumbuka vyema nyumbani ni bora ajenge legacy kimataifa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom