Hii picha imerudi tena! Companero uko wapi?
Wednesday, 10 August 2011 20:48 |
0digg Rais Jakaya Mrisho Kikwete Mwandishi WetuSERIKALI imetangaza kuwa itatoa msaada wa tani 300 za mahindi, ili kuwasaidia watu 3.5 milioni wa Somalia kupunguza makali ya ukosefu mkubwa wa chakula unaowakabili. Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, ilieleza kuwa Tanzania pia imeahidi kutoa misaada mingine kwa nchi hiyo kwa kadri uwezo wa nchi unavyoruhusu . Mchango wa Tanzania umetangazwa wakati wa mazungumzo rasmi kati ya Serikali ya Tanzania na ile ya Jamhuri ya Somalia, na wakati wa futari ambayo Rais Jakaya Kikwete, alimwandalia mgeni wake Rais wa Somalia, Sheikh Sharif Sheikh Ahmed ambaye alikuwa katika ziara ya siku mbili ya kikazi nchini. "Tunasikitika sana kuona matatizo makubwa ya ukosefu mkubwa wa chakula yanayoikabili nchi yako. Kama unavyojua Tanzania ni nchi maskini na uwezo wetu siyo mkubwa. Lakini tuna methali hapa isemayo kutoa ni moyo siyo utajiri. Kwa hiyo kwa moyo huo wa mtu maskini, tumeamua kutoa mchango wetu mdogo wa tani 300 za mahindi ambazo ni sawa na magunia 3,000 ili kusaidia ndugu zetu wa Somalia kukabiliana na hali ya njaa kubwa," Rais Kikwete alimwambia Rais Sheikh Ahmed. Tanzania kusaidia tani 300 za mahindi Somalia |