Jitahidi mwanao asisome masomo ya Sanaa

Jitahidi mwanao asisome masomo ya Sanaa

Mbona unanitisha sasa watoto niwabadilishe? Tatizo ni kuwa wanataka masomo ya arts!
hapana, usitishike, ila angalia katika huko arts nini hasa wanakitaka, sio kwa mkumbo....
na ujue mara nyingi watoto wanapenda urahisi halafu wanajiachia, hata wakienda huko wasome kile ambacho wewe unakiona sokoni kwa sasa au unachofikiri kuwa baadae sokoni kitakuwa na maana zaidi...
 
hapana, usitishike, ila angalia katika huko arts nini hasa wanakitaka, sio kwa mkumbo....
na ujue mara nyingi watoto wanapenda urahisi halafu wanajiachia, hata wakienda huko wasome kile ambacho wewe unakiona sokoni kwa sasa au unachofikiri kuwa baadae sokoni kitakuwa na maana zaidi...

Asante, you are absolutely right, mmoja tuliminyana sana akitaka kusoma economics alipofika form 4 (alitaka achague EGM) nikasema if it is arts I am not going to cough millions , you can manage good passes with Kayumba schools. Akaona niko serious akachukua PCB, sasa ananishukuru sana kuwa baba uliona mbali, she is about to finish medicine. Wengina nao wanataka arts! ngoja niminyane nao!
 
Hii maada bhana. Lakini naona mkuu amesahau kitu kimoja muhimu sana. Angeiuliza kwanza nini maana ya elimu,nadhani wa kukurupuka asingeleta hii maada.

Kwa kifupi Elimu ni ile inayobakia kichwani baada ya kusoma makablasha mengi kama chands,lambat,bs...&c. Ukiwa na elimu ya uzamivu(Ph.D) kwa mfano,halafu ukawa unaleta threads kama hizi,tunakuona wewe hujaelimika,upo sawa na aliyekataa shule akiwa darsa la pili.

Jipange tena mkuu,utuletee maada iliyoshiba udadafuzi wa hoja,si kuleta nyuzi mbovu kama hizi kwa great thinkers hapa janvini.
 
Daaa aisee kuna ka ukweli hapa,kuna challenge hapa Pia

,coz za science ni uhakika wa Maisha yaani ajira, ila kupato chake ni kidogo au cha kusotea,kozi za biashara ikikupata kwenye anga zako duuu unatoka na mshahara unaoeleweka,

Pia hizi kozi ni za Msimu,sasa hivi Science pay Much,ila baada ya Miaka 5 Mbele duu,Kozi za biashara wanaweza nao kutoka tena sana tuu,miaka ya 2000-2010 kozi za biashara na Arts zilifana sana Kama Hr,Uhasibu,ugavi,usafirishaji,nk 2010-2015 duu hoi,science ndo zinafana,nime predict 5 ijayo kwa sababu ya miradi ambayo itakuwa imekamilika Kama Reli ya Kati to Rwanda,Reli ya tanga mpaka bahari ya Atlantic,bandari ya bagamoyo,na miradi mingine ambayo italeta Multiplier effect ktk uchumi!unaweza kuangalia Miradi mikubwa Tanzania utapata data!

So finally kozi za science muda wote ajira zipo regardless ya kipato chake na nafasi zake!

Umesema kweli...kuna mdogo wangu yuko UK anafanya MSc. Investment & Finance. I'm positive akirudi lazima anatoboa.....kulingana na situation inavyokwenda now hapa tz.
 
Guidance ni muhimu, lakin mwisho wa siku ni vizur mtu akasomea kile anachokipenda na kukimudu. Tujikite kusoma na kupata stadi, sio kusoma tu ili uajiriwe maana hata ajira zenyewe ni shida.

Kozi za sanaa ni nzuri sana na zinalipa kuliko hata Sayansi. Tatizo ni ile dhana kongwe kuwa masomo ya sanaa ni rahisi, hivyo watoto wetu wanabweteka. Mtu wa sanaa lazima awe na uwezo mkubwa wa kuandika, kuongea, kusikiliza na kujenga hoja. Hizi stadi sio rahisi kuwa nazo, hasa kwa mfumo wa elimu hapa Tanzania.

Mfano mzuri wa mtu aliyesomea vyema sanaa ni Tundu Lissu. Hata machizi kama Lusinde wanaukubali uwezo wake. Bahat mbaya watu wengi wanamfahamu Lissu wa enzi hizi wa chadema, na sio yule mwanaharakat wa mazingira na wachimbaji wadogo wa madini. Ana mchango mkubwa kwenye sekta ya madini, japo weng hawajui.
 
Iv kuna umuhimu wa mtt kwenda o level...a level then chuo kikuuu??? Maana mm Sio siri nmesoma arts.....nilivomaliza olevel nkaenda arts hgk ila nilisoma Huko n tofaut kabisa na nilivhosoma chuo....Je kuna hasara gan kumtoa mtt olevel kisha kumpeleka certificate....diploma in the same fld then chuo????
Tumekariri mkuu na kuna fikra vichwani kwetu hasa sie tuliobahatika kufika A-level kuwaona wale waliopitia certificate mpaka juu kama vilaza kumbe wakati mwingine sio wote ni suala la chance, kama mzazi una uwezo nadhani hoja yako ya mtu kupitia certificate mpaka chuo ina mashiko maana wengi wanakomaa na A-level kutokana na kupata fursa ya vitu kama mikopo na mambo kama hayo vinginevyo kama mtu O-level kafaulu vizuri bahati mbaya somo moja limegoma akashindwa kupata combination anayotaka ni vema tu ukapiga certificate then Diploma then chuo kikubwa mzazi uwe una hela maana mwenye Diploma na wa kidato cha sita ukiwaweka pamoja kwenye kutafuta mkopo kipaumbele ni kwa kidato cha sita kwa kuwa yeye anahesabiwa kama hana ujuzi / utaalamu wowote compared na mtu mwenye Diploma
 
Hii maada bhana. Lakini naona mkuu amesahau kitu kimoja muhimu sana. Angeiuliza kwanza nini maana ya elimu,nadhani wa kukurupuka asingeleta hii maada.

Kwa kifupi Elimu ni ile inayobakia kichwani baada ya kusoma makablasha mengi kama chands,lambat,bs...&c. Ukiwa na elimu ya uzamivu(Ph.D) kwa mfano,halafu ukawa unaleta threads kama hizi,tunakuona wewe hujaelimika,upo sawa na aliyekataa shule akiwa darsa la pili.

Jipange tena mkuu,utuletee maada iliyoshiba udadafuzi wa hoja,si kuleta nyuzi mbovu kama hizi kwa great thinkers hapa janvini.
imekaa bomba tu mkuu maana imefanya watu watiririke na kujazia mapungufu ambayo kwa namna moja ama nyingine yameonekana kwa mleta uzi lakini mwisho wa siku kutokana na uzi huu tumenufaika kwa mawazo mengine mazuri zaidi kwani sifa ya binadamu ni kutofautiana mitazamo alafu kwa kushirikiana na wengine tuaboresha lile wazo la misngi na kutoka na kitu kizuri na ndio maana huwa tuna makongamano, mikutano na social networks kwa kuwa vichwa vyetu vipo tofauti
 
Nanukuuu "Kama unataka kula nchi nenda arts kama unataka ajira nenda science maana hata katika kipindi chetu tuliosoma Mkondo wa SHE(swahili,History,English) walitudharau sana lakini ukiangalia wanaokula nchi (National Cake) ni Sisi tuliosoma Arts" Mwisho wa kunukuuu hiyo ni kauli ya mmoja wa kigogo wa nchi hiii.
Katika nchi zetu hizi zinazoendelea Ajira ni Magumashi sana Ukitaka kuamini hiki ngoja u-graduate nakurudi mtaani kisha mtafutane ndio utaelewa.....
 
Nanukuuu "Kama unataka kula nchi nenda arts kama unataka ajira nenda science maana hata katika kipindi chetu tuliosoma Mkondo wa SHE(swahili,History,English) walitudharau sana lakini ukiangalia wanaokula nchi (National Cake) ni Sisi tuliosoma Arts" Mwisho wa kunukuuu hiyo ni kauli ya mmoja wa kigogo wa nchi hiii.
Katika nchi zetu hizi zinazoendelea Ajira ni Magumashi sana Ukitaka kuamini hiki ngoja u-graduate nakurudi mtaani kisha mtafutane ndio utaelewa.....
hao arts wanaokula nchi ni asilimia ngapi ya waliosoma arts?. hao arts wanaokula nchi na arts wanaotafuta kazi nani ni wengi?
 
ngoja nikuache maana naona una uelewa mgumu sana. unashindwa kujua kama huo ni mfano. pia unashindwa kutofautisha kulazimisha na kujenga mazingira/kujitahidi.

Tatizo una mawazo ya kizamani sana.Hebu badili huo mtazamo wako kwanza.
Kwanza elewa nini maana ya elimu,dhumuni la elimu na kwa nini kuna course mbalimbali za kusoma na jinsi zinavyotegemeana.
Narudia tena usijeongea tena upuuzi kama huu ulioandika hapa maana unathibitisha hiyo elimu uliyoipata haijakusaidia.
 
Ww ubashauri watu wasome chochote ili wakimaliza wajiajili ni mbulula kabisa unafikili kujiajili ni kama kuotea jua eti ? Hakuna mtu ambaye apendi kufanya kaz zake tatizo ni mitaji hongera mtoa ada
 
bado tupo mbali kimawazo,bila kusema mengi sidhani kama nitampeleka mwanangu shuleni akasome ili tu apate kazi,elimu ni zana ya ukuaji wa kifikra,kama bado umesoma halafu uchambuzi wako wa mambo ni sawa na mtu asiyesoma tutasema wewe hujaelimika,hata kama utakuwa ofisi gani.

narudia kusema watanzania tuanze kubadilika japo kidogo kidogo,hadi lini tutakaa kufikiri kwenda shule ni kupata ajira? wengine hawajaenda shule na wajomba zao wamewapa viti maofisini, elimu ni nyenzo ya kutukomboa kiakili, ajira inakuja baadae.

sitozungumzia sana kuhusu uwanja mpana wa wanasayansi au waliosoma arts kwa sababu binafsi siamini katika misingi hiyo ila tu nilisoma taarifa moja jana na ngoja nipaste hapa.

Hizi ndio faida za kusoma kupata kazi,kukariri maandishi ya vitabu katika misingi hiyo,tubadilike jamani.

[/FONT][/COLOR]

Hyo n kwel lakni cyo bongo
 
Bongo Movie na Bongo Fleva wanatufukuza hapa town hatare! Hivi hawa akina Diamond, Jux, JB, Lulu, Wema, Ray, Jaydee, Alikiba, nk walisoma course gani?
 
Ww ubashauri watu wasome chochote ili wakimaliza wajiajili ni mbulula kabisa unafikili kujiajili ni kama kuotea jua eti ? Hakuna mtu ambaye apendi kufanya kaz zake tatizo ni mitaji hongera mtoa ada

mwakifusu unafikiri below average kujiajiri ni ngumu kama wewe ni mvivu na una malengo madogo.. ngoja nikupe mfano... ukienda kijijini kwenu ukaamua kutumia elimu yako (Art au Science) ukafuta eneo la eka 2(Hata la kukodi) ukalima matiki maji kwa sh 500,000/=(kulima na kutunza) yatakapo kuwa vizuri baada ya miezi 3 utapata mpaka mil 12,au kama hyo ngumu unaweza ukatafuta elf 10 ukaagiza gunia la mkaa mkoani kwa sh 10(usafiri na kulinunua),na kuliuza dar sh 15,je ukienda huku unakuza biashara huwezi kufikia mpka ukawa milionea...!!?,fikiri kwanza maisha baada ya kustaafu..
 
Hayo unayo yataja yote unahususha pesa hv unatoa wapivhizo?
Pia sio kila kwao ni kijijini wengine maisha yao yote ,ndugu zao wote wapo mjn mambo ya kilimo ataweza wapi
 
Hayo unayo yataja yote unahususha pesa hv unatoa wapivhizo?
Pia sio kila kwao ni kijijini wengine maisha yao yote ,ndugu zao wote wapo mjn mambo ya kilimo ataweza wapi

MwaKifusu...!!! umezaliwa na kukulia dar, ila ni kweli asili yako ni Dar...!!? ndio huna pesa ya kununua kiwanja Dar je huwezi kupata mkoani...!!? Hata elfu 15 huwez pata kwa miezi 7,What is point of living in towns.. wakati huwezi kustahimili maisha yake...!?
 
Asante, you are absolutely right, mmoja tuliminyana sana akitaka kusoma economics alipofika form 4 (alitaka achague EGM) nikasema if it is arts I am not going to cough millions , you can manage good passes with Kayumba schools. Akaona niko serious akachukua PCB, sasa ananishukuru sana kuwa baba uliona mbali, she is about to finish medicine. Wengina nao wanataka arts! ngoja niminyane nao!
hongera, akimaliza afanye kadigirii kapili kabisa.....
 
Back
Top Bottom