Serikali Ondoeni Elimu ya Kidato 6 Vyumba hivyo vitumike kwa mashule ya VETA, Ushauri wa Prof. Kamuzola unafaa kwa hili.

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Wana JF,

Tanzania ni nchi yenye wanafunzi wanaosoma masomo mengi na mabovu, kwani hayana malengo thabiti ya kuiweka tanzania katika mikono salama ya sayansi na teknolojia. tangu kuanza kwa masomo ya awali unakuta watoto wanaingizwa kichwani vitu vilivyowazidi na wanakuwa wanavirudia kutokana na kupanda kwao daraja wanapokuwa masomoni. Hakika watanzania tunao mkwamo wa kutoangalia talent za vijana wetu kujua wanaweza nini ndicho tuwafundishe.

Ukiangalia kwa makini, sehemu nyingi ya watu waliosomea veta ndio wanaosukuma gurudumu la maendeleo kuliko waliosoama vyuo vikuu kwani wengi wako na makaburasha wanaangaika kupata ajira za waliopunguzwa serikalini au walikufa, au waliostaafu.

Hawa vijana mpaka wanapata ajira wanakuwa wameshachoka sana, umri unakuwa umewapita, kazi wanazifanya kwa uoga ufanisi hakuna kwa kuwa wanawaza kuwa na vitu walivyovikosa, wakiwa wanaangaikia ajira. ndio maana wengi wanakosa uadirifu wanakuwa wezi kweli kweli.

Tufike hatua kama mtu amepata maksi nzuri badala kwenda form five na Six, aende chuo kikuu chochote na waliopata maksi za kawaida basi waingie veta. kwa wale waliona wamefeli sana wanatakiwa kurudia hili wapate nafasi za veta hawa ndiowarudie mitiani kufuzu kuingia vyuo vya veta.

Hukovetawatakaofaulu vizuri ndio waingie chuo kikuu. hii itasaidia watu wengi kupata ujuzi wa kitu chochote cha kumwingizia riziki hata kama baadaye anataka kazi nyingine, angalalau anakuwa maeishazalisha kitu. hapa lazima tuwe na maendeleo.

Angalia wimbi la bodaboda , kuna mafundi wengi huko kama kungekuwepo mitaala mizuri wengi wangekua mashuleni wakijifunza stadi za kazi, badala yake, hawa ndio wengi wako mhimbili hawa mikono, hawana miguu, wengine wanaugulia kujaa maji vifuani.

Bodaboda ni ajira ya vipo hakuna mbadala. tufike hatua tutumie mawazo ya Profesa Kamzora kwa utafiti wake alioufanya kupitia jamii ya wahindi. Wahindi wengi hawapo mavyuoni wengi hawafiki kidato cha sita, wanacheza na fursa, halafu ndio wanaokuja kuongoza kwenye vitu vya kisayansi kwa sababu wamebobea kwenye masomo machache yenye tija, wanayachagua kwa uwezo walionao sio kwa kulazimika na hali uliyonayo.

======

Prof Kamuzora RAS Kagera:

Tatizo lile lile nililolisema awali. Falsafa ya Elimu yetu ni kuwa watu wanasomea taifa na si kusomea maisha yao. Hivyo, wote mnaingizwa kwenye behewa kuelekea kwenye combinations ambazo Taifa limechagua yaani PCM, PCB, PGM, CBG, CBN, ECA, EGM, HGL, HGE, HGK. Ukikosa nafasi kwenye behewa sasa ndio ukatafute hizo fursa zingine za NACTE na VETA.

Falsafa hii na mfumo huu una athari za kisaikolojia. Kwanza unafanywa watu wakikosa nafasi kwenye behewa la form five wajione kuwa ni watu waliofeli na waliopoteza ndoto za maisha. Pili, inafanya elimu ya NACTE na VETA kuonekana kama ni sitara na hifadhi kwa waliokosa nafasi behewani. Matokeo yake, tunapeleka huko kwenye NACTE na VETA waliopoteza matumaini. Yaani tumegeuza NACTE na VETA kuwa ni elimu mbadala na si chaguo tu kama kwenda form 5.

Katika hili nitapenda kutoa mfano wa jamii ya watanzania wenye asili ya asia. Hivi hawa wanaishiaga wapi? Mbona wengi hawaendi form 5 na hata wanaoenda hawasomi HGL, HGK na HGE bali utawakuta aidha kwenye PCB, PCM na ECA na EGM? Na je mbona huko chuo hawaonekani kwenye vitivo vya Sheria, Sayansi ya Siasa, Sociolojia na Historia na Archaeology? Mbona ni kama hawapo kabisa kwenye Masters degree zinazotolewa na Chuo Kikuu kipendwa cha UDSM na pia hawapatikani kule kwenye Masters za jioni za Mzumbe wala zile za Open University? Lakini mbona pamoja na kutowaona huko kote hatuwaoni mtaani wakipita na bahasha za khaki zenye photocopy za vyeti na barua za kuomba ajira?

Wenzetu hawa walishajinasua siku nyingi katika mtego wa fikra tuliouingia wa kusomeshea watoto kwenda kujaza nafasi za wanaostaafu na kufa katika sekta ya umma. Wenzetu wanajifunza stadi zaidi. Anayetaka uhasibu, akifika form four anajisajili kwenye mitihani ya Bodi za Uhasibu (NBAA na ACCA) anaendelea huko. Wengine watakwenda kujifunza masuala ya kukatisha tiketi za ndege IATA system, wengine watakwenda kujifunza stadi za Hardware na Software Engineering na stadi nyingine nyingine. Wengine watasomea u-pilot, wengine insurances nk. Leo nenda kwenye nursery schools walimu wengi ni watanzania waasia kwa kuwa wanakwenda kusomea fani hiyo. Kwao behewa la form 5 ni moja tu kati ya mabehewa mengine na si behewa takatifu au la wateule.

Wenzangu na sisi tunakwenda na behewa, tunaingia chuo tunapigwa sumu ya DS 101 tunakuwa wanamapinduzi na wachukia mabeberu huku tukisoma archaeology, Sociology, Political Science na Kiswahili mwisho wa siku tunasubiri Sekretariati ya Ajira itangaze kazi tunajikuta inaajiri asilimia 10 tu ya waliomaliza chuo. Mwishowe hao hao wasomi wanarudi kuajriwa na mabepari waliokuwa wanawachukia wakiwa chuo🤣🤣🤣🤣🤣.

Kuna kitu tunakosea mahala.

Credit to profesa Kamuzora
 
Hoja yako ni nzito na inahitaji tafakuri pana.
Mimi nashauri kuwa mtaala wa form five na six ujumuishe ufundi stadi katika fani husika.
mfano mwanafunzi wa form six anayechukua PCB anatakiwa akimaliza form six awe na uwezo flani wa kiutendaji kama muhitimu wa Veta.let say awe hata na utaalamu msingi wa kutoa huduma za dharura au kuwa mhudumu wa afya akiwa zahanati au kutengeneza vifaa vidogo vya kieletronic na mambo mengine equevalent na haya kadri jopo la wataalamu litakavyosuggest.
Hii itamfanya mwanafunzi huyu akifeli form six aweze kujiajiri au kuajirika.
Kwa sasa ukimchukua mwanafunzi wa udaktari aliyeopo mwaka wa Tano na bahati mbaya akafeli katika mwaka wake huo wa tano basi atajikuta hana uwezo au sifa ya kuajiriwa au kujiajiri popote kwenye field ya afya despite knowledge aliyoikusanya kwa miaka yote hiyo..badala yake yule aliyefeli form four na kuingia chuo cha KAM Medics kwa mwaka mmoja anaajirika.
 
Wee jamaa una Wivu sana. Umesomea kwa kuungaunga. Waache vijana wasome Advanced lever bnana. Wengine tulipatia mademu huko na heshima mtaani

Sent using Jamii Forums mobile app
sina wivu hata kidogo kwa kuwa nami nimepitia huko, lakini naona ni kupoteza muda, unakuta tanzania ina wasomi wengi lakini hawajaweza ku-deliver chochote ukilinganisha na nchi nyingine, wasomi hawa wengi wameingia kwenye wimbi la ufisadi wa kujali matumbo yao. haya yote ni matokeo ya kusoma muda mrefu wanakuja kujikuta umri umeenda na serikali inahitaji mtu aihudumia miaka zaidi ya inshirni sasa unastaafu kwa miaka 60, wewe umeifanyia serikali mika 10 tu, uoni kwamba umetumika kidogo kuiidumia nchi yako, kuliko veta aliyefundishwa kulima korosho kwa ubora na TRA inamtegemea yeye kuingizia taifa mapato wakati wewe umezunguka na vyeti miaka sita ukila ugali wa wazee, wazee wamekusomesha bado unakula ugali wao miaka sita!!!
 
Mkuu mtoa mada, suala la watu kwenda advance level mimi bado naiona kama kikwazo kikubwa sana kwa vijana wetu kupanua akili. Chukulia ukweli kua shule nyingi za sekondari nchini hazina vitendea kazi hivyo mwanafunzi usoma kwa kukariri mwisho wa siku anaenda shule kidato cha tano na sita.

Huko kidato cha tano na sita mwendo ni kukariri mwishoni wanafunzi wanafanya pratical kwa kugoji then mwanafunzi huko anaenda chuo. Kufika chuo anakutana na vitu vipya vingi vyenye kuitaji muda mwingi na vitendo vya kutosha mwisho wa siku anafaulu kwa kukariri. Mwambie sasa huyo aliyepata A kwenye electrical machine design akusukie ata motor iliyoungua ndo utashangaa vibaya sana.

Mwanafunzi anayo alama A kwenye programming wenda kwa kutumia C++ sasa mpe kazi uone maajabu yake. Watunga sera wasipobadilika kwa kulazimisha wakufunzi kufanya tafiti kwa ulazima na mitala yetu kubadilishwa tutazidi kuchekesha sana
 
Hoja yako ni nzito na inahitaji tafakuri pana.
Mimi nashauri kuwa mtaala wa form five na six ujumuishe ufundi stadi katika fani husika.
mfano mwanafunzi wa form six anayechukua PCB anatakiwa akimaliza form six awe na uwezo flani wa kiutendaji kama muhitimu wa Veta.let say awe hata na utaalamu msingi wa kutoa huduma za dharura au kuwa mhudumu wa afya akiwa zahanati au kutengeneza vifaa vidogo vya kieletronic na mambo mengine equevalent na haya kadri jopo la wataalamu litakavyosuggest.
Hii itamfanya mwanafunzi huyu akifeli form six aweze kujiajiri au kuajirika.
Kwa sasa ukimchukua mwanafunzi wa udaktari aliyeopo mwaka wa Tano na bahati mbaya akafeli katika mwaka wake huo wa tano basi atajikuta hana uwezo au sifa ya kuajiriwa au kujiajiri popote kwenye field ya afya despite knowledge aliyoikusanya kwa miaka yote hiyo..badala yake yule aliyefeli form four na kuingia chuo cha KAM Medics kwa mwaka mmoja anaajirika.
Kumbe sometimes akili zako zinacharge...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu mtoa mada, suala la watu kwenda advance level mimi bado naiona kama kikwazo kikubwa sana kwa vijana wetu kupanua akili. Chukulia ukweli kua shule nyingi za sekondari nchini hazina vitendea kazi hivyo mwanafunzi usoma kwa kukariri mwisho wa siku anaenda shule kidato cha tano na sita.

Huko kidato cha tano na sita mwendo ni kukariri mwishoni wanafunzi wanafanya pratical kwa kugoji then mwanafunzi huko anaenda chuo. Kufika chuo anakutana na vitu vipya vingi vyenye kuitaji muda mwingi na vitendo vya kutosha mwisho wa siku anafaulu kwa kukariri. Mwambie sasa huyo aliyepata A kwenye electrical machine design akusukie ata motor iliyoungua ndo utashangaa vibaya sana.

Mwanafunzi anayo alama A kwenye programming wenda kwa kutumia C++ sasa mpe kazi uone maajabu yake. Watunga sera wasipobadilika kwa kulazimisha wakufunzi kufanya tafiti kwa ulazima na mitala yetu kubadilishwa tutazidi kuchekesha sana
Ipo mifano ya shule maalumu za kiufundi kama Moshi Technical sielewi kwa nini hazitoi wanafunzi wenye knowledge hizi kama ilivyokuwa enzi hizo.
Kila fani ingewekewa shule maalum zenye mfanano huu basi tungeweza kuondokana na hali hii ya sasa.
Nyerere alikuwa na maono na majibu ya haya tunayoyauliza ila mabeberu na mabepari yalituchafulia nchi.
 
Mkuu mtoa mada, suala la watu kwenda advance level mimi bado naiona kama kikwazo kikubwa sana kwa vijana wetu kupanua akili. Chukulia ukweli kua shule nyingi za sekondari nchini hazina vitendea kazi hivyo mwanafunzi usoma kwa kukariri mwisho wa siku anaenda shule kidato cha tano na sita.

Huko kidato cha tano na sita mwendo ni kukariri mwishoni wanafunzi wanafanya pratical kwa kugoji then mwanafunzi huko anaenda chuo. Kufika chuo anakutana na vitu vipya vingi vyenye kuitaji muda mwingi na vitendo vya kutosha mwisho wa siku anafaulu kwa kukariri. Mwambie sasa huyo aliyepata A kwenye electrical machine design akusukie ata motor iliyoungua ndo utashangaa vibaya sana.

Mwanafunzi anayo alama A kwenye programming wenda kwa kutumia C++ sasa mpe kazi uone maajabu yake. Watunga sera wasipobadilika kwa kulazimisha wakufunzi kufanya tafiti kwa ulazima na mitala yetu kubadilishwa tutazidi kuchekesha sana
Mkuu mchango wako nimeupenda sana. Vyuo vingi vyenye sifa ni Idara angalau ya kuto madaktari ndio wanafaulu kuleta kitu bora, lakini vyuo vingi vinazidiwa na wanafunzi wa VETA wanaofaulu kudesigne hata kwa kuiga vifaa mbailimbali, angalia mafundi walijiajiri wanatengeneza vitanda vya chuma wamewaiga wachina , njoo pale kwa Mhindi mmoja Jaafel (jina sikumbuki vizuri) ana workshop mzuri sana ametumia vijana wa VETA kudisigne vitu mbali mbali, sasa hivi ndiye ana tenda nyingi mavyoni na serikalini wananunua fanicha kwake, Angali ujio wa matrector tanzania, nenda pale JKT Mwenge, yale majembe, na vifaa vingine vingetengenezwa hapa tanzania wao waagize engine tu na excel, lakini vyote tunaagiza wakati machuma yale hata ambao hawakwenda shule wangeyajenga, kama mtu anajenga body za masemi tela kwa nini tunaingiza tena masemi yaliyoundwa badala ya kutumia chuma chetu kujenga hapa hapa, ifike hatuavinavyowezekana hapa vitengenezwe hapa hapa, na wale wanaozunguka na bahasha za vyeti kusubili wastaafu , au wenye ajira wafe nao wapate kujiajiri.
 
Hoja yako ni nzito na inahitaji tafakuri pana.
Mimi nashauri kuwa mtaala wa form five na six ujumuishe ufundi stadi katika fani husika.
mfano mwanafunzi wa form six anayechukua PCB anatakiwa akimaliza form six awe na uwezo flani wa kiutendaji kama muhitimu wa Veta.let say awe hata na utaalamu msingi wa kutoa huduma za dharura au kuwa mhudumu wa afya akiwa zahanati au kutengeneza vifaa vidogo vya kieletronic na mambo mengine equevalent na haya kadri jopo la wataalamu litakavyosuggest.
Hii itamfanya mwanafunzi huyu akifeli form six aweze kujiajiri au kuajirika.
Kwa sasa ukimchukua mwanafunzi wa udaktari aliyeopo mwaka wa Tano na bahati mbaya akafeli katika mwaka wake huo wa tano basi atajikuta hana uwezo au sifa ya kuajiriwa au kujiajiri popote kwenye field ya afya despite knowledge aliyoikusanya kwa miaka yote hiyo..badala yake yule aliyefeli form four na kuingia chuo cha KAM Medics kwa mwaka mmoja anaajirika.
Nimependa sana mawazo yako Mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ipo mifano ya shule maalumu za kiufundi kama Moshi Technical sielewi kwa nini hazitoi wanafunzi wenye knowledge hizi kama ilivyokuwa enzi hizo.
Kila fani ingewekewa shule maalum zenye mfanano huu basi tungeweza kuondokana na hali hii ya sasa.
Nyerere alikuwa na maono na majibu ya haya tunayoyauliza ila mabeberu na mabepari yalituchafulia nchi.
sentensi ya mwisho ndio ukweli mtupu lakini kuna watu watapinga na watailaumu CCM kuwa ndio inefanya hivyo
 
Wana JF,

Tanzania ni nchi yenye wanafunzi wanaosoma masomo mengi na mabovu, kwani hayana malengo thabiti ya kuiweka tanzania katika mikono salama ya sayansi na teknolojia. tangu kuanza kwa masomo ya awali unakuta watoto wanaingizwa kichwani vitu vilivyowazidi na wanakuwa wanavirudia kutokana na kupanda kwao daraja wanapokuwa masomoni. Hakika watanzania tunao mkwamo wa kutoangalia talent za vijana wetu kujua wanaweza nini ndicho tuwafundishe.

Ukiangalia kwa makini, sehemu nyingi ya watu waliosomea veta ndio wanaosukuma gurudumu la maendeleo kuliko waliosoama vyuo vikuu kwani wengi wako na makaburasha wanaangaika kupata ajira za waliopunguzwa serikalini au walikufa, au waliostaafu.

Hawa vijana mpaka wanapata ajira wanakuwa wameshachoka sana, umri unakuwa umewapita, kazi wanazifanya kwa uoga ufanisi hakuna kwa kuwa wanawaza kuwa na vitu walivyovikosa, wakiwa wanaangaikia ajira. ndio maana wengi wanakosa uadirifu wanakuwa wezi kweli kweli.

Tufike hatua kama mtu amepata maksi nzuri badala kwenda form five na Six, aende chuo kikuu chochote na waliopata maksi za kawaida basi waingie veta. kwa wale waliona wamefeli sana wanatakiwa kurudia hili wapate nafasi za veta hawa ndiowarudie mitiani kufuzu kuingia vyuo vya veta.

Hukovetawatakaofaulu vizuri ndio waingie chuo kikuu. hii itasaidia watu wengi kupata ujuzi wa kitu chochote cha kumwingizia riziki hata kama baadaye anataka kazi nyingine, angalalau anakuwa maeishazalisha kitu. hapa lazima tuwe na maendeleo.

Angalia wimbi la bodaboda , kuna mafundi wengi huko kama kungekuwepo mitaala mizuri wengi wangekua mashuleni wakijifunza stadi za kazi, badala yake, hawa ndio wengi wako mhimbili hawa mikono, hawana miguu, wengine wanaugulia kujaa maji vifuani.

Bodaboda ni ajira ya vipo hakuna mbadala. tufike hatua tutumie mawazo ya Profesa Kamzora kwa utafiti wake alioufanya kupitia jamii ya wahindi. Wahindi wengi hawapo mavyuoni wengi hawafiki kidato cha sita, wanacheza na fursa, halafu ndio wanaokuja kuongoza kwenye vitu vya kisayansi kwa sababu wamebobea kwenye masomo machache yenye tija, wanayachagua kwa uwezo walionao sio kwa kulazimika na hali uliyonayo.
Mimi naona badala ya advance tuwe na vyuo vya ufundi kama DIT na MUST na ATC hivi viwe katika fani zote sio sayansi tu viwe mbadala wa advance angalia elimu katika mataifa kama Urusi
 
Back
Top Bottom