Jirani yetu limbukeni anatuboa

Jirani yetu limbukeni anatuboa

Tanzania Mpya

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2012
Posts
252
Reaction score
145
Tabia zingine bwana sijui ni za asili? Tuna jirani yetu anatusumbua sana, yaani anasikiliza muziki kwa sauti kubwa sana na hana usiku wala mchana! Anaanza saa 11 asubuhi na anaweka sauti kubwa muda wote mpaka saa 5 au 6 usiku, yaani kelele tu. Yeye na mke wake wote wako hivyo na wana watoto wadogo sana, inanishangaza kwa kweli.

Mkewe huweka taarabu, mipasho kwa sauti kubwa sana, jamaa mwenyewe mfano asubuhi hii kaweka cd ya Remi Ongala (nafikiri kainunua jana) basi kaweka sauti kubwa sana wakati yeye mwenyewe kakaa nje ya nyumba yake akisikilizia. Jamaa ni Mndengereko, sasa sijui ni asili ya uswahili? Siku nyingi tu nilitaka nimfuate kumjulisha tatizo hili, lakini wife anasema huyu kuna analotafuta kwa majirani kwa hiyo tumuache tu na ulimbukeni wake.

Naomba ushauri wenu wadau, tutaishi hivi mpaka lini?
 
Hilo tatizo hata mimi linanisibu, nasubiria ushauri pia, manake mtu mzima kumfundisha kazi kweli kweli
 
hata mie ni jirani mpenda sauti kubwa
kama umepanga anza kutafuta ustaarabu wa kuwa na kwako.

Hata ukimwambia kupunguza, atapunguza leo, kesho anasahau.
Ni tabia tu
 
Unaishi kigamboni nini!?? Hapo kwenye taarabu ni kama tuna-share jirani aisee!
 
Hahah kumbe ni Mdengereko....!!!
Baada ya ulimwengu kuhamia dijitali basi hata wao wamehama kutoka ngoma za "Mdundiko, Segere" nk na kuja kwenye ulimwengu wa kubofya...

Ila hao dawa yao ni moja tu, ongea na vishoka wa mtaani wapige shoti nyumbani kwake, hizo tabu hutazipata tena
 
he he he, mbona mie si mdengereko ila kwa sauti tu, sijambo.

Hahah kumbe ni Mdengereko....!!!
Baada ya ulimwengu kuhamia dijitali basi hata wao wamehama kutoka ngoma za "Mdundiko, Segere" nk na kuja kwenye ulimwengu wa kubofya...
 
Hata kwetu wapo!! kuna mzee mmoja wa kipemba anatuboa kweli yeye ni mwislamu basi anafungulia radio ya dini kama ugomvi.
 
Tulichofanya majirani, tuliungana tukaenda kwa mjumbe aliposhtakiwa na majirani akajirekebisha lol, nendeni serikalini.
 
Tabia zingine bwana sijui ni za asili? Tuna jirani yetu anatusumbua sana, yaani anasikiliza muziki kwa sauti kubwa sana na hana usiku wala mchana! Anaanza saa 11 asubuhi na anaweka sauti kubwa muda wote mpaka saa 5 au 6 usiku, yaani kelele tu. Yeye na mke wake wote wako hivyo na wana watoto wadogo sana, inanishangaza kwa kweli.

Mkewe huweka taarabu, mipasho kwa sauti kubwa sana, jamaa mwenyewe mfano asubuhi hii kaweka cd ya Remi Ongala (nafikiri kainunua jana) basi kaweka sauti kubwa sana wakati yeye mwenyewe kakaa nje ya nyumba yake akisikilizia. Jamaa ni Mndengereko, sasa sijui ni asili ya uswahili? Siku nyingi tu nilitaka nimfuate kumjulisha tatizo hili, lakini wife anasema huyu kuna analotafuta kwa majirani kwa hiyo tumuache tu na ulimbukeni wake.

Naomba ushauri wenu wadau, tutaishi hivi mpaka lini?


mpelekeni serikali za mitaa akashughulikiwe
 
Hayo yalinikuta nikiwa chuo Mlimani (hall 3). Lakini majirani wenyewe walikuwa ni kutoka Mbeya.
walikuwa wanawahi sana kuamka, radio ni full blast halafu mtu anaenda bafuni kuoga!
 
Ningekuwa mimi dawa yao ni kuwa na mziki mkubwa zaidi yao,natafuta siku akiwa anaumwa nami nafungulia muziki kwa sauti ya juu,atajirekebisha tu.

ahahahaahhaaaaaaaaaaaaaaaa_hii inaitwa dawa ya moto ni moto,....lo!
 
Mimi nilikomesha tabia ya hivyo kwenye nyumba ninayoishi
watu walikua wanafungulia ufa mshenzi mm nikawa nakodi ufa
kubwa kwa jamaa yangu mmoja mwenye duka la electronics
nikawakomesha wenyewe wakaja kunifuata jamani sauti nikawaambia
waanze wao kwanza kuwa wastaarabu mpaka
leo heshima.
 
Unakuta wakiwa kwenye majamboz mke anapiga kelele kama mashine ya kusaga sasa wana dilute kelele kwa mziki
 
Ningekuwa mimi dawa yao ni kuwa na mziki mkubwa zaidi yao,natafuta siku akiwa anaumwa nami nafungulia muziki kwa sauti ya juu,atajirekebisha tu.

Miziki mikubwa hata sisi tunayo ila huwa inafanya kazi hapo kwa hapo! Meaning ukifungua yako anazima then kesho anarudia! Sanasana labda na wewe uwe unafungua kila siku! (Sasa sijui una muumiza au unajiumiza mwenyewe)
 
Ningekuwa mimi dawa yao ni kuwa na mziki mkubwa zaidi yao,natafuta siku akiwa anaumwa nami nafungulia muziki kwa sauti ya juu,atajirekebisha tu.

Yap yap sugu anakwambia Dawa ya bishoo ni kuwa bishoo zaidi yake,hata mie enzi hizo nipo uswazi kuna mtu alikuwa anasumbua sana na mziki wake nikaenda dukani nikanunua mziki wenye PMPO 30,000 wakati yeye PMPO 4500 mbona alikuwa afungulii....Dawa ya jeuri ni kiburi penda kusikiliza nyimbo za Sugu zinafunza sana!
 
Mkuu nenda kwao kawatie bakora familia nzima, ukishawatia mikwaju ya kutosha ndo uwaambie kwanini.... kesho hawatorudia tena kuweka sauti kubwa!!!!! :fencing:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom