Jirani yetu limbukeni anatuboa

Jirani yetu limbukeni anatuboa

hii makitu imekuwa tabu sana. yani kila kona ni tabu tupu. pale kwangu dah ni noma aisee..nimewambia lakini baada ya muda mfupi wanarudi hewani tena. huwa nafurahi sana umeme ukikatika napata muda wa kulala, sasa hapo JOTO kali hunisibu tena tabu nyingine hiyo.. mjini hapa kaz kwelikweli.
 
:A S angry::A S angry::A S angry: kwa kweli inatia hasira sana, Mimi jirani yangu pia alikuwa nafanya hivyo , nilimfuata nikamweleza, hakunijibu kitu ila aliendelea kufungulia kwa sauti kiasi kwamba hatuwezi hata kutizama TV maana hatusikii, nikaenda kwa mjumbe akaja akamweleza, akaacha kwa muda wa wiki akaanza tena, tena hapo ndipo alipoanza kuweka nyimbo za taarabu, basi nikaenda serikali za mtaa, nikawaambia wakaja wakamchukulia hatua, walimtoza faini ya sh 50,000/- pale pale na akaambiwa akiendelea atafungwa. Tangu siku ile mpk leo hii kakoma hafungulii tena mziki kwa sauti. KUISHI USWAHILINI NI NOMA!!!
 
Ningekuwa mimi dawa yao ni kuwa na mziki mkubwa zaidi yao,natafuta siku akiwa anaumwa nami nafungulia muziki kwa sauti ya juu,atajirekebisha tu.

Ha haa haa! Yaani kuna wakati natamani niwashe mziki mkubwa na kuziheuza spika kuelekea kwake, lkn naona tusije kuwa wote wajinga. Sijui watoto wake kama wanalala vizuri.
 
Enzi zangu nilikuwa nawakomesha wenye tabia hizo, baada yakuona nanyanyasika, niliamua kumfuata mshikaji wangu aliyekuwa na vyombo vya mziki vya kukodisha,

Nikamuomba viwe vinakaa kwangu,

Sasa limbukeni yule tuliyepanga nyumba moja akiwasha tu kiredio chake, mie namuwashia vyombo vyangu kwa mziki wa Bob Marley mpaka nyumba inatikisika!

Mbona aliamua yeye kwenda kwa mjumbe, mjumbe mwenyewe tayari nilishampa taarifa, hivyo akampuuza!

Mwisho aliama kuhama yeye!

Ha haa haa, hiyo tamu mkuu. Usiku huu, jamaa tayari kaanza, yaani yeye hana cha taarifa ya habari wala nini, yaani kama dala dala. Taabu kweli hii.
 
Hilo tatizo hata mimi linanisibu, nasubiria ushauri pia, manake mtu mzima kumfundisha kazi kweli kweli

Na wewe mwaga ugali akimwaga mboga!
Niliwahi kuishi Mwananyamala kisiwani mwaka 2006 jirani mmoja alikuwa na tabia hiyo. Nilichofanya baada ya kugundua kuwa radio yake ni ndogo kuliko yangu niliamua kumuonesha kazi. Niliweka spika usawa wa dirisha lake nikaweka plate zote cd nikafungulia sauti ya mwisho na kuweka repeat! Niliondoka kama masaa saba. Niliporudi nikazima na kusema wanafikiri wao tu ndo wanaradio, hadi nahama miezi sita baadaye sikuisikia tena radio yake!
 
Mimi pia hili tatizo jirani yangu ni mzaramo yaani tabu tupu toka anunue kamchina kake basi ni taabu kuna mida huwa natamani nikamtie vitasa,yaan hajui cha mchana wala usiku.kero
 
Hahahahahahahaha

Hahah kumbe ni Mdengereko....!!!
Baada ya ulimwengu kuhamia dijitali basi hata wao wamehama kutoka ngoma za "Mdundiko, Segere" nk na kuja kwenye ulimwengu wa kubofya...

Ila hao dawa yao ni moja tu, ongea na vishoka wa mtaani wapige shoti nyumbani kwake, hizo tabu hutazipata tena
 
Nunua na ww music system yenye akili. Fungulia mpaka mwisho na hutaisikia radio mkuluma yake.
Mwisho ataona aibu na kuizima radio yke inayokoroma kuipusha nyumba yake kupata nyufa.
 
Tabia zingine bwana sijui ni za asili? Tuna jirani yetu anatusumbua sana, yaani anasikiliza muziki kwa sauti kubwa sana na hana usiku wala mchana! Anaanza saa 11 asubuhi na anaweka sauti kubwa muda wote mpaka saa 5 au 6 usiku, yaani kelele tu. Yeye na mke wake wote wako hivyo na wana watoto wadogo sana, inanishangaza kwa kweli.

Mkewe huweka taarabu, mipasho kwa sauti kubwa sana, jamaa mwenyewe mfano asubuhi hii kaweka cd ya Remi Ongala (nafikiri kainunua jana) basi kaweka sauti kubwa sana wakati yeye mwenyewe kakaa nje ya nyumba yake akisikilizia. Jamaa ni Mndengereko, sasa sijui ni asili ya uswahili? Siku nyingi tu nilitaka nimfuate kumjulisha tatizo hili, lakini wife anasema huyu kuna analotafuta kwa majirani kwa hiyo tumuache tu na ulimbukeni wake.

Naomba ushauri wenu wadau, tutaishi hivi mpaka lini?

Mkuu Tanzania Mpya, laiti kama mngekuwa mmepanga kwenye nyumba moja na hiyo nyumbe isiwe na dari, Ungenunua kilo 2 za nyama unaziweka kwako bila kupika unafunga na kusafiri kwa wiki 2 unamwacha na yeye acheze na harufu ya uozoo kwa kipindi chote ukiwa likizo!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Tafuta fundi pikipiki aje hapo karibu na dirisha lake ,kila dakika unalipiga resi mwenyewe atakimbia na kuzima kiredio
 
Mimi nilikomesha tabia ya hivyo kwenye nyumba ninayoishi
watu walikua wanafungulia ufa mshenzi mm nikawa nakodi ufa
kubwa kwa jamaa yangu mmoja mwenye duka la electronics
nikawakomesha wenyewe wakaja kunifuata jamani sauti nikawaambia
waanze wao kwanza kuwa wastaarabu mpaka
leo heshima.

Impections should be allopwed to cancel themselves
 
Tabia zingine bwana sijui ni za asili? Tuna jirani yetu anatusumbua sana, yaani anasikiliza muziki kwa sauti kubwa sana na hana usiku wala mchana! Anaanza saa 11 asubuhi na anaweka sauti kubwa muda wote mpaka saa 5 au 6 usiku, yaani kelele tu. Yeye na mke wake wote wako hivyo na wana watoto wadogo sana, inanishangaza kwa kweli.

Mkewe huweka taarabu, mipasho kwa sauti kubwa sana, jamaa mwenyewe mfano asubuhi hii kaweka cd ya Remi Ongala (nafikiri kainunua jana) basi kaweka sauti kubwa sana wakati yeye mwenyewe kakaa nje ya nyumba yake akisikilizia. Jamaa ni Mndengereko, sasa sijui ni asili ya uswahili? Siku nyingi tu nilitaka nimfuate kumjulisha tatizo hili, lakini wife anasema huyu kuna analotafuta kwa majirani kwa hiyo tumuache tu na ulimbukeni wake.

Naomba ushauri wenu wadau, tutaishi hivi mpaka lini?


Unaonekana hauna self-confidence; Nenda kaishi Ulaya kwa wazungu wenzio
 
Dawa ni moja tu nunua yale maredio yenye maspika makubwa mawili marefuuuuu urefu unaolingana na mtoto wa darasa la tano na fungua mwenyewe atazima kimziki chake.
Pole sana tena ukizingatia kuwa siku hizi mambo ya startimes yanahusika basi kutwa kusikiliza taarab wakina gea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom