Jinsi ya Kusajili kampuni katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mchaga

JF-Expert Member
Apr 11, 2008
1,378
204
Wana JF naomba mwenye taarifa za taratibu za kusajili kampuni ya madini pale nyumbani Tanzania anisaidie.

Natanguliza shukrani zangu.

BAADHI YA MAJIBU YALIYOTOLEWA NA WADAU:
===
===
===
===
 
Uko nje ya nchi...unataka kuchimba madini...this is latest point ya mining....kwa maana halisi ni kwamba labda useme unataka kufanya exploration ya madini..tanzania..na hapo unasajili company ya exploration....

Unafanya utafiti maeneo yako then ukisha pata deposit ya kutosha ya madini kuweza kuchimba kwa mfani 5-10 Million Oz..(kipimo cha Gold)then unaweza ku apply Mining license.Ila unaweza at the same time ukawa na license mbili katika company moja nimeona kwenye company moja Tanzania royality company hawa wana licence ya mining and exploration..ila wamefanya kaujanja kamoja ka kuwa na company mbili katika mwamvuli mmoja.Moja ikiitwa mama na nyingine dada.

Kwa ushauli exploration mining tanzani ni ngumu sana hata ma kampuni makubwa sasa yanatapata shida kufanya kwa kuwa eneo kubwa la tanzania limeshafanyiwa utafiti unawe zakuwa na PL 100,100% ownership lakini ukifanya exploration kwa level ya kwanza haikupi matumaini kwenda level ya pili...at the end of the day inakuwa useless.

So kuwa makini sana unapo kuja kufanya mambo kam hii tanzania..most of wa wawekezaji wanakuja fanya JV(Join venture) na company zenye maeneo...kwani kuna about 50 - 100 exploration company kanda ya ziwa acha uko kusini mwa tanzania kwenye uranium.

Asubuhi njema
 
1. Kwanza chagua jina halafu nenda Brela kasajili jina. It's a one day process.

2. Baada ya kupata 'OK' ya jina. Nenda kwa mwanasheria akuandalie documents mbili muhimu. Hii ni The Memorandum of the Company na Articles of Association copy nne nne. This is a Two days Job.

3. Unarudi Brella na kujaza forms na ku-submit na hizo documents na unalipia - applicable fees. This is another two days job.

In total 5 working days zinatosha kusajili kampuni. Ukianza Jumatatu, unamaliza Ijumaa. Kama una mkono mrefu, unaweza kufanyiwa kwa Fast Track na ukamaliza mambo yote in a day or two.
 
1. Kwanza chagua jina halafu nenda Brela kasajili jina. Its a one day process.

Kwa nyongeza, hatua ya kwanza should be a "name search", kwahiyo ni lazima uende na barua uliyoiandika ukiomba kuangaliziwa jina. Kwa maana hiyo kwenye hiyo barua yako "utapropose" majina matatu ukiwa umeyapangilia kulingana na "priority order" yako.

Hao watu wa Brela wakishaipokea hiyo barua watakupa kama siku mbili ili waangalie kwenye database yao kama hayo majina (kufuatana na priority order yako) hayajatumika.Ukishajua ni jina lipi limekubaliwa ndipo sasa utatakiwa kuandaa Memorandum of Association na Articles of Associasion kwa kutumia jina lililokubaliwa.

Maelezo zaidi pata kwenye hii link.
 
Last edited:
Sasa hao BRELA wapo upande gani na jengo lipi hapa Dar es Salaam na Mikoani wana matawi? kuna Kigezo gani ukitaka Kampuni yako iwe LTD au Holdings,Enterprises etc. Samahani kwa swali la nyongeza mtatusidia wengi tu jamani lol!!!
 
Sasa hao BRELA wapo upande gani na jengo lipi hapa DSM na Mikoani wana matawi? kuna Kigezo gani ukitaka Kampuni yako iwe LTD au Holdings,Enterprises etc. Samahani kwa swali la nyongeza mtatusidia wengi tu jamani lol!!!

Mkuu umesoma hiyo link uliyopewa na Chibidu?
Wapo eneo la Mnazi Mmoja, mtaa wa Lumumba, jengo la Ushirika jijini Dar-es-salaam
 
Wataalam, asanteni sana. Hapa nimeelewa na nashukuru kwa link naona pia ina maelekezo niliyokuwa ninayahitaji. Nitawasiliana nikimaliza kusajili.
 
This is JF, Nami nilitaka fungua kampuni binafsi nadhani maelekezo haya yatanifaa sana. BIG THANKS...!
 
Yaani Mkuu nikushukuru sana kwa taarifa na link its very informative. Thanks.
 
Hizi biashara za kuonana na receptionist ndio zinaumiza wananchi!, haya mambo kama vipi yafanyike online tuu, kuna kila sababu ya kufanyia hizi issue online, sioni kwa nini lazima tuonane na watu. ndio maana rushwa haitokoma TZ. Tujifunze kuokoa muda.

B.
 
Kumbuka, baada ya kusajili kampuni (Incorporation) na kabla ya kuanza biashara utatakiawa kupata leseni ya biashara (business licence) na pia kujisajili kama mlipa kodi (TIN certificate).

Nakutakia mafanikio.

Je nikisha sajili hiyo kampuni natakiwa nilipe nini kwa TRA, na je consultancy firms nazo zinasajiliwa Brella??

Tafadhali wakuu nifahamisheni hapo.
 
Pasco kaizungumza hii ishu kama ni rahisi. Ebwana jiandae kuna watu wananuka rushwa pale. Mie aliremember, ilinichukua miezi 2 kukamilisha kuna danadana za kijinga saana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…