Jinsi ya kuondoa umaskini tanzania .nini kifanyike?naomba maoni yenu

houseboy

Member
Jul 22, 2007
39
3
Tumekua tukishuudia jinsi umaskini unavyoizamisha Tanzania,asilimia 85%ya waTanzania wanaishi chini ya maisha ya umasikini mkubwa,uku baadhi ya viongozi na wafanyakazi wa umma wakiikwangua na kujikandamizia utajiri wa hali ya juu.viongozi wengi na wafanyakazi wa umma wengi wanachangia 100% kulididimiza taifa kwa wizi,ruswa,kubebana nk.kwa mtazamo wangu,inabidi sasa tuwe makini sana na tukifanya mchezo Bongo katika miaka 10 ijayo itakuwa imefirisika kabisa.nomba maoni yenu jinsi gani ya kulikwamua taifa letu kutoka tulipo sasa na kupigaga maendeleo,naomba watu wasifanye mchezo kwani nitachapisha maoni mazuri na kuyapeleka kwa wausika.
Kitu cha kwanza kwa maoni yangu nadhani tuanze na kupunguza ukubwa wa serikali,kwani tuna wizara nyingi sana na watu wanaofanya kazi kwenye wizara wanatumia mamilioni ya pesa nyinyi sana bila kuzalisha chochote kile,mimi naona kuwe na wizara 7 tu aya nimaoni yangu naomba tusifanye hii kuwa ndio ajenda ,nipe mawazo yako ili tuifanye bongo iwe mfano katika Africa tuna kila kitu na sababu ya kuwa taifa tajiri duniani,au tumetupiwa voodu nini?asanteni naomba maononi yenu .asanteni na karibuni
 
Houseboy
Muulize Kikwete maana 2005 alisema anajua matatizo ya Watanzania ingawa alipopanda ndege kwenda Ufaransa alisahau akasema hata yeye hajui kwanini Tanzania ni nchi maskini. Kwa kuwa tunaelekea 2010 labda sasa anajua
 
Umaskini wa Watanzania unaanzia na umaskini wa mawazo..ngazi zote na wakati mwingine umaskini wa roho.Mungu kajalia TZ kila kitu cha kuifanya nchi inyanyuke kwa spidi ya roketi lakini bado hakuna hata dalili.Baada ya Azimio la Arusha, Sera zililenga kuweka njia kuu za uchumi kwa serikali..lakini serikali ni nani? Ni watu..watu hao hawakuwa na nia ya kweli ya kulifanya taifa lifaidike na rasilimali.Kuhodhi bila kuzifanyia kazi zilete manufaa ni sawa na kuwa bila kitu.

Hapo hapo wajanja wachache wakachukulia "ujinga" wa Watz walio wengi kujinufaisha huku wakiwakaririsha watz kuwa kila kitu ni mali ya umma!Mali ya umma isiyokuwa na mwenyewe?Hulka ya umimi inayoendelea kujengeka hasa kwa wale wenye dhamana ya mali ya umma, nafasi na fursa zaidi ya wengine isipoangaliwa na kudhibitiwa basi tujiandae kuwa na taifa fukara lisiloweza kujikwamua tena kutoka katika rindi la umaskini uliokithiri.Rasilimali nazo zinaenda zikiisha ( depleted) wakati hatujaweza kujiwekea miundombinu sahihi ya kuleta maendelea kwa watanzania wali wengi.
Tutaweza kuwa na maendeleo kama atatokea kiongozi radical mwenye nia ya kweli ya kupambana na ufisadi, asiyekuwa na umimi, aliye tayari kuwabadilikia hata maswahiba ili kuondoa vizingiti vyote vinavyofanya mapinduzi ya kiuchumi yasiwezekane.Hapo ndipo pa kuanzia.Pili ni kuhakikisha kuwa waliokaa kwenye gari ni abiria sahihi, vinginevyo inabidi kuwashusha wale wasiostahili! This is the only way to move from good to great!
 
Umaskini wa Watanzania unaanzia na umaskini wa mawazo..ngazi zote na wakati mwingine umaskini wa roho.Mungu kajalia TZ kila kitu cha kuifanya nchi inyanyuke kwa spidi ya roketi lakini bado hakuna hata dalili.Baada ya Azimio la Arusha, Sera zililenga kuweka njia kuu za uchumi kwa serikali..lakini serikali ni nani? Ni watu..watu hao hawakuwa na nia ya kweli ya kulifanya taifa lifaidike na rasilimali.Kuhodhi bila kuzifanyia kazi zilete manufaa ni sawa na kuwa bila kitu.

Hapo hapo wajanja wachache wakachukulia "ujinga" wa Watz walio wengi kujinufaisha huku wakiwakaririsha watz kuwa kila kitu ni mali ya umma!Mali ya umma isiyokuwa na mwenyewe?Hulka ya umimi inayoendelea kujengeka hasa kwa wale wenye dhamana ya mali ya umma, nafasi na fursa zaidi ya wengine isipoangaliwa na kudhibitiwa basi tujiandae kuwa na taifa fukara lisiloweza kujikwamua tena kutoka katika rindi la umaskini uliokithiri.Rasilimali nazo zinaenda zikiisha ( depleted) wakati hatujaweza kujiwekea miundombinu sahihi ya kuleta maendelea kwa watanzania wali wengi.
Tutaweza kuwa na maendeleo kama atatokea kiongozi radical mwenye nia ya kweli ya kupambana na ufisadi, asiyekuwa na umimi, aliye tayari kuwabadilikia hata maswahiba ili kuondoa vizingiti vyote vinavyofanya mapinduzi ya kiuchumi yasiwezekane.Hapo ndipo pa kuanzia.Pili ni kuhakikisha kuwa waliokaa kwenye gari ni abiria sahihi, vinginevyo inabidi kuwashusha wale wasiostahili! This is the only way to move from good to great!

Ulichoandika hapo juu ndiyo ukweli halisi wa nchi yetu. Ahsante sana kwa mawazo yako mazuri na yaliyotulia.
 
Mimi nadhani kikubwa ni kuwa na serikali inayowajibika tu. Hili litafanikiwa pale kila mwananchi atakapotumia nafasi yake kuwajibika sawia pale alipo. Hii pia ihusishe kuishinikiza serikali isiyotaka kuwajibika ikiwa ni pamoja na kujenga mfumo shirikishi na usioegemea kikundi cha watu wachache wenye masilahi binafsi. Kuishikiza serikali kujenga mfumo sawa mbele ya sheria, na kuwapunguzia watu/tasisi (mfano rais) madaraka makubwa ambayo yanamfanya aendeshe nchi kama mradi wake na wapendwa wake. Hili likifanikiwa, hatuna sababu ya kutoendelea kwani rasilimali zote zitatumika kwa maslahi ya watanzania, ikiwa ni pamoja na kutoa fursa kwa wale wenye uwezo na wala sio kwa kigezo cha huyu kuwa mwenzetu.
 
I think we need visionary leaders, na sio wanao kwenda kufungua mafail tu.

A leader must have a vision,
 
I think we need visionary leaders, na sio wanao kwenda kufungua mafail tu.

A leader must have a vision,

Having a vision without action is a nightmare!
Nadhani kila kiongozi anayeingia madarakani atasema anayo vision....na ndio maana yuko madarakani.Aliuza sera kwa wananchi wakavutika na ndio maana wakampa dhamana.
What is lacking is actualising the vision through actions directed towards attaining the vision.Perhaps a steer with the buy-in of those he chooses to help him to realise goals.
 
Having a vision without action is a nightmare!
Nadhani kila kiongozi anayeingia madarakani atasema anayo vision....na ndio maana yuko madarakani.Aliuza sera kwa wananchi wakavutika na ndio maana wakampa dhamana.
What is lacking is actualising the vision through actions directed towards attaining the vision.Perhaps a steer with the buy-in of those he chooses to help him to realise goals.

Hizo vision za CCM za kuandikiwa sidhani kama ni vision bali ni ndoto tu walizo nazo. A man with a vision, first, he will tell us his vision; second, he will give us the way how he will execute hiyo vision, na sio kusema tu ataleta kazi milioni moja, bila ya kutuambia ni kivipi atazitengenza hizo kazi na zitawagusa wananchi kivipi?

Now, enforcing his vision hilo nalo ni jambo lingine ambalo viongozi wengi hawana, kwasababu hizo position wamepewa na watu, hivyo basi wapo tayari kucompromise na hao walio wapa, ulaji. When you enforce your vision, kumbuka kuwa wengi watakuona mbaya, lakini, mwishoni watu wataelewa kuwa ni kwa manufaa ya nchi.
 
Last edited:
Mengi yaliyosemwa kwenye thread hii ni ya kweli. Hata hivyo naona kuna jambo moja halijaangaliwa kiundani - ELIMU

85% ya wantanzania ni masikini, lakini utakumbuka kuwa 1% ya wanafunzi wanaomaliza darasa la 7 ndio wanaopata nafasi ya kuendelea na elimu ya juu (university education).

Maendeleo ya taifa hayawezi kufanywa na mtu mmoja, bali taifa kwa ujumla. Watu wakielimika, wataweza kutofautisha kati ya kiongozi mzuri na mbaya - kama leo hii wewe uliyeelimika unavyoweza kuona ubaya wa SISIEM au chama kingine chochote hapa Tanzania.

Pia kumbuka, KURA ya MJINGA na ya ALIYEELIMIKA zote zina uzito sawa. Usipomwelimisha mwenzako leo, kura yake kesho itakugharimu na wewe pia!
 
Back
Top Bottom