Jinsi ya kumjengea mwanao tabia ya kupenda kusoma vitabu

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
4,695
6,398
Mwanaharakati maarufu wa Marekani, Dr. Martin Luther King Jr. alishawahi kusema, "An idle mind is the workshop of the devil!". Mtu mmoja anisaidie kutafsiri kwa Kiswahili, tafadhali!🙏

Namna pekee ya kuiepusha akili kuwa "idle" ni kwa kuifanyisha kazi nzuri, na ili akili iweze kufanya kazi nzuri ni lazima uilishe taarifa nzuri kila siku.

Njia gani bora ya kuilisha akili ya mwanao taarifa nzuri zaidi ya vitabu vizuri?

Unaweza kumzoesha kuwa msomaji kwa kutumia njia zifuatazo:

1. Msomee kitabu kila siku mpaka atakapoweza kujisomea mwenyewe

Hili linaweza likafanyika tokea mtoto akiwa tumboni mwa mama yake. Tafuta vitabu vizuri na uanze kumsomea kwa sauti. Usifikiri kwamba haelewi. Utakachokuwa unakifanya kitakuwa kinarekodiwa kwenye akili yake, na kuchochea aina ya tabia atakayokuwa nayo maishani mwake.

Atakapozaliwa, uendelee kufanya hivyo. Mnaweza mkapeana zamu na mwenzi wako kumsomea kitabu Usiku wakati wa kulala, kwa kumsomea kwa sauti hadi asinzie.

2. Hakikisha kuna vitabu vya kutosha vya aina mbalimbali nyumbani kwako. Muhimu, vitabu hivyo viwe ni vitabu vizuri. Jihadhari na vitabu vinavyoweza kuwa hatari kwa afya ya akili ya mtoto.

3. Jijengee tabia ya kujisomea vitabu kila siku ukiwa naye. Wanasema, "like the father, like the son". Watoto wana tabia ya kuwaiga wazazi wao.

4. Mnunulie zawadi ya kitabu kila baada ya muda fulani, au wakati wa tukio fulani zuri. Kama una kawaida ya kumfanyia "birthday", usiishie tu kumlisha ngano na kuku, mpatie zawadi ya kitabu kizuri.

Ni gharama na usumbufu kufanya hivyo? Vyo vyote vile, lakini kama hiyo itamsaidia mwanao, kwa nini usifanye? Isitoshe, hautawafanyia hivyo milele. Wakishajua kusoma na kuandika, watakuwa wakijisomea wenyewe. Na itakuwa rahisi zaidi wao kufanya hivyo ikiwa ulishawazoesha tokea wakiwa watoto wachanga.

Ukiona vyaelea, ujue vimeundwa!

Unafikiri ni mbinu gani tena itakayomsaidia mtoto kuwa msomaji wa vitabu?
 
Mwanaharakati maarufu wa Marekani, Dr. Martin Luther King Jr. alishawahi kusema, "An idle mind is the workshop of the devil!". Mtu mmoja anisaidie kutafsiri kwa Kiswahili, tafadhali!🙏

Namna pekee ya kuiepusha akili kuwa "idle" ni kwa kuifanyisha kazi nzuri, na ili akili iweze kufanya kazi nzuri ni lazima uilishe taarifa nzuri kila siku.

Njia gani bora ya kuilisha akili ya mwanao taarifa nzuri zaidi ya vitabu vizuri?

Unaweza kumzoesha kuwa msomaji kwa kutumia njia zifuatazo:

1. Msomee kitabu kila siku mpaka atakapoweza kujisomea mwenyewe

Hili linaweza likafanyika tokea mtoto akiwa tumboni mwa mama yake. Tafuta vitabu vizuri na uanze kumsomea kwa sauti. Usifikiri kwamba haelewi. Utakachokuwa unakifanya kitakuwa kinarekodiwa kwenye akili yake, na kuchochea aina ya tabia atakayokuwa nayo maishani mwake.

Atakapozaliwa, uendelee kufanya hivyo. Mnaweza mkapeana zamu na mwenzi wako kumsomea kitabu Usiku wakati wa kulala, kwa kumsomea kwa sauti hadi asinzie.

2. Hakikisha kuna vitabu vya kutosha vya aina mbalimbali nyumbani kwako. Muhimu, vitabu hivyo viwe ni vitabu vizuri. Jihadhari na vitabu vinavyoweza kuwa hatari kwa afya ya akili ya mtoto.

3. Jijengee tabia ya kujisomea vitabu kila siku ukiwa naye. Wanasema, "like the father, like the son". Watoto wana tabia ya kuwaiga wazazi wao.

4. Mnunulie zawadi ya kitabu kila baada ya muda fulani, au wakati wa tukio fulani zuri. Kama una kawaida ya kumfanyia "birthday", usiishie tu kumlisha ngano na kuku, mpatie zawadi ya kitabu kizuri.

Ni gharama na usumbufu kufanya hivyo? Vyo vyote vile, lakini kama hiyo itamsaidia mwanao, kwa nini usifanye? Isitoshe, hautawafanyia hivyo milele. Wakishajua kusoma na kuandika, watakuwa wakijisomea wenyewe. Na itakuwa rahisi zaidi wao kufanya hivyo ikiwa ulishawazoesha tokea wakiwa watoto wachanga.

Ukiona vyaelea, ujue vimeundwa!

Unafikiri ni mbinu gani tena itakayomsaidia mtoto kuwa msomaji wa vitabu?

Mfano Mimi Napenda Sana kusoma kuliko kutazama Tv hivyo Mimi nyumbani kulikuwa hamna Tv hiyo ilinijenga kupenda kusoma Sana Hadi leo


Ila ukiwa bookworm unafikia malengo yako haraka Sana na kuishi kwa uhuru ,upendo na Amani Sana . Binafsi mtoto wangu lazima nimjenge Apende kusoma VITABU njia mojawapo sinunui Tv nanunua Vitabu na radio na laptop Basi tu namuwekea Movie zakumjenga na soft copy books basi
 
Mfano Mimi Napenda Sana kusoma kuliko kutazama Tv hivyo Mimi nyumbani kulikuwa hamna Tv hiyo ilinijenga kupenda kusoma Sana Hadi leo


Ila ukiwa bookworm unafikia malengo yako haraka Sana na kuishi kwa uhuru ,upendo na Amani Sana . Binafsi mtoto wangu lazima nimjenge Apende kusoma VITABU njia mojawapo sinunui Tv nanunua Vitabu na radio na laptop Basi tu namuwekea Movie zakumjenga na soft copy books basi
Hongera mkuu, ila usiache kuwa na TV. Watoto wanaweza kutorokea kwa jirani kuangalia tv. Muhimu ni kuthibiti matumizi yake huku ukiendelea kumjengea tabia ya usomaji.
 
Rahisi tu mbona,hakuna MTU asiependa Fedha,kwa watoto Zawadi..Nunua Kila kitabu atakachomaliza kusoma kwa makubaliano ya pesa fulani or kumpatia Zawadi ambayo unamuahidi kuwa endapo atamaliza kusoma basi utampatia..

Hiyo ni baada ya kukueleza NN alichosoma na ameelewa NN Ktk hicho kitabu,n'a kwa vile ww mzazi pia ni msomaji WA vitabu inakuwa rahisi Kujua kama anachosema ni Kweli ama Laa..

Utaingia gharama kwa kipindi fulani anapoanza kujisomea Ili apate hizo Fedha or hizo Zawadi Ila utamu WA vitabu ukimnogea Hilo zoezi linakuwa halipo tena..

Nothing comes at easy,kama unavyotongoza tu Mwanamke unavyojikakamua mwanzoni Ili uonekane uko Vizuri kabla hujampata Ila ukishampata unarudi kwenye uhalisia wako,ndivyo hivyo hivyo tu Comrade..tumia approch hiyo.
 
Rahisi tu mbona,hakuna MTU asiependa Fedha,kwa watoto Zawadi..Nunua Kila kitabu atakachomaliza kusoma kwa makubaliano ya pesa fulani or kumpatia Zawadi ambayo unamuahidi kuwa endapo atamaliza kusoma basi utampatia..

Hiyo ni baada ya kukueleza NN alichosoma na ameelewa NN Ktk hicho kitabu,n'a kwa vile ww mzazi pia ni msomaji WA vitabu inakuwa rahisi Kujua kama anachosema ni Kweli ama Laa..

Utaingia gharama kwa kipindi fulani anapoanza kujisomea Ili apate hizo Fedha or hizo Zawadi Ila utamu WA vitabu ukimnogea Hilo zoezi linakuwa halipo tena..

Nothing comes at easy,kama unavyotongoza tu Mwanamke unavyojikakamua mwanzoni Ili uonekane uko Vizuri kabla hujampata Ila ukishampata unarudi kwenye uhalisia wako,ndivyo hivyo hivyo tu Comrade..tumia approch hiyo.
Ni kweli! Pesa ni kihamasishi kisichobagua umri. Shukran🙏
 
Hivi library hakuna yale madarasa ya jumamosi ya watoto. Zamani nilikuwa nampeleka dogo kila jumamosi anaimba na kusoma pale mpaka saa sita. Ile ilimjenga akawa msomqji mzuri wa vitabu.
Sikumbuki kama nilishawahi hata kusikia kuhusu hayo madarasa! Yalikuwaje?

Vipi dogo, aliweza kuendelea na hiyo tabia ya usomaji?
 
Mfano Mimi Napenda Sana kusoma kuliko kutazama Tv hivyo Mimi nyumbani kulikuwa hamna Tv hiyo ilinijenga kupenda kusoma Sana Hadi leo


Ila ukiwa bookworm unafikia malengo yako haraka Sana na kuishi kwa uhuru ,upendo na Amani Sana . Binafsi mtoto wangu lazima nimjenge Apende kusoma VITABU njia mojawapo sinunui Tv nanunua Vitabu na radio na laptop Basi tu namuwekea Movie zakumjenga na soft copy books basi
Mkuu,nunua vyote.
Ukimzuia mtoto wako kula nyumbani ni kwamba wewe umeamua kumnyima chakula chako (mchoyo) hivyo atapewa chakula na jirani yako.

Vitu vingi pamoja na kwamba tabia hutegemea mazingira (mazoea) ila pia kupenda jambo flani ni asili ya mtu (nature (in born).
 
Sikumbuki kama nilishawahi hata kusikia kuhusu hayo madarasa! Yalikuwaje?

Vipi dogo, aliweza kuendelea na hiyo tabia ya usomaji?
Mimi mwenyewe nilikuwa member miaka ile nipo shule ya msingi na huyo dogo ni miaka 2006 tuu hapo.
Jumamosi watoto wa shule mbali mbali walikutana kuimba na kusoma vitabu asubuhi kuanzia saa tatu mpaka saa sita.
Mimi mwenyewe mpaka leo nasoma vitabu mfano votabi vyooote vya willy gamba nimevinunua na kurudia kuvosoma mara kadhaa. Sababu vilikuwa library enzi zile..
Dogo anasoma vitabi mpaka kesho na kwa sasa ni Engineer huko Afrika magharibi.
 
Mimi mwenyewe nilikuwa member miaka ile nipo shule ya msingi na huyo dogo ni miaka 2006 tuu hapo.
Jumamosi watoto wa shule mbali mbali walikutana kuimba na kusoma vitabu asubuhi kuanzia saa tatu mpaka saa sita.
Mimi mwenyewe mpaka leo nasoma vitabu mfano votabi vyooote vya willy gamba nimevinunua na kurudia kuvosoma mara kadhaa. Sababu vilikuwa library enzi zile..
Dogo anasoma vitabi mpaka kesho na kwa sasa ni Engineer huko Afrika magharibi.
Very inspiring! Congratulations👏👏👏🙏

NB. Kuna typing error kama 2 hivi kwenye comment yako:
1. Votabi
2. Vitabi

Lakini imeeleweka kuwa ulimaanisha VITABU!
🙏🙏🙏
 
Very inspiring! Congratulations👏👏👏🙏

NB. Kuna typing error kama 2 hivi kwenye comment yako:
1. Votabi
2. Vitabi

Lakini imeeleweka kuwa ulimaanisha VITABU!
🙏🙏🙏
Si unajua ukiandika kwa simu pole. Na asante kwa pongezi.
 
Mfano Mimi Napenda Sana kusoma kuliko kutazama Tv hivyo Mimi nyumbani kulikuwa hamna Tv hiyo ilinijenga kupenda kusoma Sana Hadi leo


Ila ukiwa bookworm unafikia malengo yako haraka Sana na kuishi kwa uhuru ,upendo na Amani Sana . Binafsi mtoto wangu lazima nimjenge Apende kusoma VITABU njia mojawapo sinunui Tv nanunua Vitabu na radio na laptop Basi tu namuwekea Movie zakumjenga na soft copy books basi
Nilikua msomaji mzuri ila sasa nimepoteza hamu ya kusoma kabisa nmekua mvivu sjui narudi vip
 
Nilikua msomaji mzuri ila sasa nimepoteza hamu ya kusoma kabisa nmekua mvivu sjui narudi vip
Ni rahisi sana!
1. Kika siku uamkapo, panga ratiba ya siku nzima (andika), na uhakikishe unajumuisha na alau lisaa kimoja la kusoma. Huo muda wa kusoma ukiwadia, tafuta sehemu ya "kujichimbia" na hakikisha hutoki mpaka muda uishe. Katika kipindi cha hilo lisaa kimoja, hakikisha unatumia kusoma na di vinginevyo. Soma hata kama ni kwa kuilazimisha.

2. Kuja utokapo nyumbani kwako, hakikisha una kitabu mkononi. Uzuri mmoja siku hizi kuna vitabu vya soft copy. Upatapo upenyo, uteseme upo kwenye daladala, ndege, su unasuburia kuingia kwenye ofisi fulani, uutumie huo muda kusoma, hata kama utasoma ukurasa mmoja tu.

Utashindwa kufanya hivyo?
 
Ni rahisi sana!
1. Kika siku uamkapo, panga ratiba ya siku nzima (andika), na uhakikishe unajumuisha na alau lisaa kimoja la kusoma. Huo muda wa kusoma ukiwadia, tafuta sehemu ya "kujichimbia" na hakikisha hutoki mpaka muda uishe. Katika kipindi cha hilo lisaa kimoja, hakikisha unatumia kusoma na di vinginevyo. Soma hata kama ni kwa kuilazimisha.

2. Kuja utokapo nyumbani kwako, hakikisha una kitabu mkononi. Uzuri mmoja siku hizi kuna vitabu vya soft copy. Upatapo upenyo, uteseme upo kwenye daladala, ndege, su unasuburia kuingia kwenye ofisi fulani, uutumie huo muda kusoma, hata kama utasoma ukurasa mmoja tu.

Utashindwa kufanya hivyo?
No siwezi shindwa ngoja nitafanyia kazi ushauri wako mkuu🙏
 
Back
Top Bottom