ndayilagije
JF-Expert Member
- Nov 7, 2016
- 7,491
- 8,305
Natumaini mko salama mkizidi kulisongesha japo duh usawa mbovu huu, hatukawii kutumbuana ili tuonekane na sisi tupo tupo.
Napenda kuwapa hizi tips chache za kuweza kuishi kwa amani na hawa mabosi kazi wa kidjitali wasiojua kazi zao.
1.Kumbuka kutimiza wajibu wako na hata wake bila kinyongo.
2.Msifiesifie kuwa unajisikia raha sana kufanya kazi chini yake.
3.Mzibie mapengo ya ujinga wake.
4.Bila kutaja jina la mtu, mwambie kuna watu wanamroga lakini wewe utahakikisha anabakia hapo kwani babu yako ni fundi wa huo utaalam.
5.Kama ni mlevi hakikisha kila mara wageni hasa Madiwani na Mkurugenzi anapokuja unamtetea sana kuwa jana mmefanya kazi mpaka usiku mnene na sasa ameenda kuoga, maana ulimuacha kazini.
6.Kama ni mzinzi hakikisha michepuko yake haigongani kazini kwa kumshtua mapema.
7.Hata akiwa hajapendeza mwambie pamba zimemkaa vizuri mno.
8.Chekacheka naye hata kama unahisi kutapika.
Ukifanya hivi kila fursa atakupa.
Napenda kuwapa hizi tips chache za kuweza kuishi kwa amani na hawa mabosi kazi wa kidjitali wasiojua kazi zao.
1.Kumbuka kutimiza wajibu wako na hata wake bila kinyongo.
2.Msifiesifie kuwa unajisikia raha sana kufanya kazi chini yake.
3.Mzibie mapengo ya ujinga wake.
4.Bila kutaja jina la mtu, mwambie kuna watu wanamroga lakini wewe utahakikisha anabakia hapo kwani babu yako ni fundi wa huo utaalam.
5.Kama ni mlevi hakikisha kila mara wageni hasa Madiwani na Mkurugenzi anapokuja unamtetea sana kuwa jana mmefanya kazi mpaka usiku mnene na sasa ameenda kuoga, maana ulimuacha kazini.
6.Kama ni mzinzi hakikisha michepuko yake haigongani kazini kwa kumshtua mapema.
7.Hata akiwa hajapendeza mwambie pamba zimemkaa vizuri mno.
8.Chekacheka naye hata kama unahisi kutapika.
Ukifanya hivi kila fursa atakupa.