Nilikuwa nakuonyesha ni jinsi gani utofautishe kati ya Talmud na Tanakh, Tanakh ndio agano la kale kwenye Biblia yetu hii, mpangilio ndio unatofautiana lakini mambo ni yale yale, ambapo sisi tumepangilia namna hii, Fungu la 1 ni vitabu vya Musa, ambapo vipo vitano au sheria, Fungu la 2, vitabu 12 vya historia, Fungu la 3, vitabu 5 vya mashairi, Fungu la 4 vitabu 5 vya manabii wakubwa, Fungu la 5 vitabu 12 vya manabii wadogo...
Tanakh yenyewe imepangiliwa tofauti kidogo lakini kitu kilekile, Haya basi niambie Talmud ni maneno ya nani!? kwasababu kuna Mishnah pamoja na Gemara, ambapo ina jumuisha Babylon Talmud na Jerusalem Talmud, mi kwa mtazamo wangu naona Talmud haijakidhi hichi kigezo hapa chini
2 Timotheo 3:16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;