MSIMISEKI
Senior Member
- Jul 30, 2011
- 123
- 34
Wakuu,
Haina shaka kwamba Hotuba ya Tundu Lissu imevuta hisia za washabiki wengi wa "Serikali 3/Nchi 3!" Pia nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa huyo kwa kuwasilisha maoni ya wachache na kuchambua Sheria akienda sambamba na historia ya Muungano wetu tangu kuundwa kwake mpaka leo.Mwanasheria huyo nguli, kama baadhi wanavyomwita ameenda mbali sana, bila kuuma maneno akidai kwamba Muungano wetu wa iliyokuwa Jamhuri ya Tanganyika na iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar hauna uhalali wowote wa kisheria kwa kuwa haukuridhiwa na Baraza la Wawakilishi, hata kama uliridhiwa na Bunge la Tanganyika tu!
Amedai pia kwamba kwa sasa tufute Sikukuu ya Muungano wetu na kuanzisha "Siku ya Shirikisho!"Kwa hoja hizo za Lissu mimi sina ubavu wa kuzipinga kwa kuwa ametaja na vifungu vya kisheria vya wakati huo, tukubali tu kwamba Muungano HAUNA UHALALI WOWOTE WA KISHERIA!
Hata hivyo, Tundu Lissu alifikiri kwamba hoja hiyo inamu-implicate tu Nyerere ambaye amemtaja mara nyingi kwamba mambo mengi ameyafanya kwa AMRI YA RAIS. Mambo hayo ni kamba vile:
1. Jina la Nchi,
2. Kuiua Tanganyika,
3. Nembo ya Taifa, nk.
Kama Muungano hauna uhalali wowote maana yake nini?
1. Ni kwamba Tundu Lissu alifanya makosa kugombea ubunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano "BATILI," kwa hiyo Ubunge wa Lissu mpaka sasa ni "BATILI!"
2. Kwamba, hata mchakato huu wa kuandika Katiba Mpya ni "BATILI" kwa kuwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba imetungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano" BATILI,"
3. Kwamba, Tundu Lissu amechangia kutunga Sheria "BATILI" za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa Bunge nalo ni "BATILI,"
4. Kwamba CHADEMA nacho ni chama "BATILI" kwa kuwa kimeundwa kwa Mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa ambayo imetungwa na Bunge "BATILI" la Muungano,
5. Kwamba, shughuli zote za kisiasa za Tundu Lissu hazina uhalali wowote wa Kisheria kwa kuwa zimefanywa kwa kufuata Sheria za Muungano "BATILI,"
6. Kama Lissu ana vyeti vya Shule za Tanzania navyo ni "BATILI" kwa kuwa vimetolewa na Serikali "BATILI,"
7. Kama Tundu Lissu amezaliwa baada ya Muungano na kupewa Cheti cha Kuzaliwa ahesabu kuwa ni "BATILI" mpaka sasa,
8. Kesi zote alizoshinda Tundu Lissu mahakamani ajue kwamba ni "UBATILI" mtupu maana" MUUNGANO HUU NI BATILI," kwa hiyo hata mahakama za Muungano ni "BATILI,"
9. Kama Tundu Lissu ameoa baada ya Muungano ajue kuwa ameumia, ni ndoa "BATILI" hiyo!!!
10..................
Hongera sana Tundu Lissu kwa Hotuba Murua...............Ila usiendelee kuwepo kwenye BUNGE hilo "BATILI" kwa kuwa limeundwa na Sheria "BATILI!!!" Tafadhali sana, I am not joking, this time around!
.....Panya kanywa mchuzi, Paka kala panya, kumbe paka kanywa mchuzi indirect.......?