OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,191
- 103,716
JamiiForums is Where we Dare to Talk Openly. Hii ndiyo slogan yetu,kufunguka. Tunafunguka katika nyanja zote kijamii, kisiasa, kimataifa, kimapenzi nk. Hata wale wasioweza kupata ujasiri wa kufunguka hadharani, Mkuu Melo na wenzie wametupa Jukwaa la kutema sumu.
Sasa basi, members kibao wamekuwa wakileta tuhuma nzito kuhusu mamlaka za serikali, taasisi na watu binafsi.
Kama hufahamu tuhuma hizi nzito zimekuwa mwiba mkali sana kwa wahusika. Msichukulie poa, misumari huwa inawaingia vizuri tu.
Binafsi nimeshuhudia paniki kibao katika maofisi ya umma kuhusu tuhuma za taasisi au mtumishi wa taasisi kuanikwa hapa JF.
Mara ya kwanza kuna bosi mmoja wa Halmashauri alituhumiwa kula watumishi wake, akatuhumiwa kutumia cheo chake kuchakaza kila mwanamke mwenye shida ya kiofisi. Asikwambie mtu, kesho yake ile ofisi ilikuwa kama imefiwa. Kikao kisicho rasmi kiliitishwa kujiuliza nani kamfunga paka kengere? Azimio ikawa kuna watu mlemle wameamua kukashfu na azimio ikawa kujibu na kukashfu wale waliohisiwa.
Baadae tena kikao cha kiofisi kikaitishwa ili kuwasiliana na JamiiForums kuwauliza nani kaleta tuhuma hizo. Nikaona hawa mabosi washamba.
Baadhi walikiri kuwa shutuma hizo ni za kweli ila ni mambo binafsi.
Kiufupi, stori za JF za kuanika uchafu wowote huwa zinaleta paniki kubwa sana huko field.
Vipi huko kwako, umewahi kushuhudia paniki yoyote ya mtu au taasisi baada ya uchafu wake kuletwa humu? Tuambie
Sasa basi, members kibao wamekuwa wakileta tuhuma nzito kuhusu mamlaka za serikali, taasisi na watu binafsi.
Kama hufahamu tuhuma hizi nzito zimekuwa mwiba mkali sana kwa wahusika. Msichukulie poa, misumari huwa inawaingia vizuri tu.
Binafsi nimeshuhudia paniki kibao katika maofisi ya umma kuhusu tuhuma za taasisi au mtumishi wa taasisi kuanikwa hapa JF.
Mara ya kwanza kuna bosi mmoja wa Halmashauri alituhumiwa kula watumishi wake, akatuhumiwa kutumia cheo chake kuchakaza kila mwanamke mwenye shida ya kiofisi. Asikwambie mtu, kesho yake ile ofisi ilikuwa kama imefiwa. Kikao kisicho rasmi kiliitishwa kujiuliza nani kamfunga paka kengere? Azimio ikawa kuna watu mlemle wameamua kukashfu na azimio ikawa kujibu na kukashfu wale waliohisiwa.
Baadae tena kikao cha kiofisi kikaitishwa ili kuwasiliana na JamiiForums kuwauliza nani kaleta tuhuma hizo. Nikaona hawa mabosi washamba.
Baadhi walikiri kuwa shutuma hizo ni za kweli ila ni mambo binafsi.
Kiufupi, stori za JF za kuanika uchafu wowote huwa zinaleta paniki kubwa sana huko field.
Vipi huko kwako, umewahi kushuhudia paniki yoyote ya mtu au taasisi baada ya uchafu wake kuletwa humu? Tuambie