nilishaga wahi kulizwa kwa njia ya mitandao m-pesa.
jamaa mmoja alihack(mpaka leo sijajua aliwezaje) namba ya bosi wangu, kisha jamaa akanitumia ujumbe huu' NITUMIE 130,000/= KWENYE NAMBA HII 075.......(nishaisahau) simu yangu imeshiwa moto".
siku ile sikuwa na balance salio kwenye simu, na niliona uvivu kuweka ili nimuulize, na kwa vile haikuwa mara ya kwanza kupokea ujumbe kama huo kutoka kwa boss wangu nikatuma kweli. daaah nilikuja kugundua kuwa nimeibiwa baada ya yule jamaa(tapeli) anani text sms ya kuniomba nimtumie tena 120,000/= ndipo nikastuka kwa vile boss wangu ataombaje hela nyingine ilihali fedha ya mauzo hata yeye anaijua ilikuwa 140K. NILILIA SANA kwa vile ndio kwanza nilikuwa natoka kijijin na mshahara wenyewe ni 50,000. ndipo iliponibidi nifanye kazi miezi mitatu bila malipo SITASAHAU!!