Jinsi nilivyowahi kutapeliwa, Wewe je?

Jinsi nilivyowahi kutapeliwa, Wewe je?

Kuna dogo alinitapeli pale Ubungo pamoja na kuishi kwangu mjini mda wote huu...

Aliniuzia sabuni badala ya simu alafu akakimbia

Nikaenda home na sabuni yangu kama simu nikaiweka juu ya kabati

Siku nasafiri nikaenda mpaka ubungo na sabuni yangu vile vile na yule dogo nikamkuta pale

Nilichomwambia tu ni chukua sabuni yako nipe hela yangu...wakaja maboss zake pale nikawaletea shida wakanipa hela nusu siku narudi tena Dar nikamdaka tena akanimalizia hela yangu.

Yule Dogo anatembea na hiziri kubwa sana mfukoni

Ila hakuna siku nilijiona mjinga kama siku ile...
 
Nilikuwa form two kipindi flani nkapewa hela ya kwenda kununua viatu vya shule nkafika kwa jamaa wa kiberiti wakazimaliza,sijawahi kucheza tena huo ujinga
Hawa jamaa viberiti vitatu ni ujanja tu, hawana dawa wala hirizi, isipokuwa wako makini na kazi yao, viberiti viwili havina njiti na kimoja kina njiti zilizopunguzwa urefu, ukifungua kwa upande mmoja unaziona, ila ukifungua kwa upande mwingine hauzioni, kwa sababu kimewekwa kaboksi katikati kutenganisha upande wenye njiti na upande usio na njiti, sasa anakuwa mjanja mchezeshaji, ukiweka pesa tu azingua anakufungulia upande mwingine wa kiberiti kilekile unakuta njiti hakuna, unakuwa umeliwa, halafu pale kundi kubwa wanakuwa ni wao tu, kwa hiyo kuchomoka inakuwa ngumu.
Daahhh nikikumbuka siku niliyotapeliwa huwa najiona mpumbavu kweli kweli.Ilikuwa maeneo ya mmanzi mmoja style ya utapeli huu ni ile ya kuopoa vikoponi kwenye kijimfuko ambavyo huwa na number ya bidhaa walizozipanga kama tv,deki,pasi,radio,jiko na vikorombwezo vingine kibao basi bwana nikatia mkono ndani nikaibuka na kuponi yenye number za music system wakadai thamani yake ni kama 1.7 ila sasa mimi itanipasa kutoa 150000K bahati nzuri sikuwa na hiyo hela nikikuwa na usd 30 na 10000k nikawapatia yote maana nilikuwa na njaa ya pesa kinyama pale pale nikaanza kuipigia hesabu ya matumizi ile 1.7ml ikaisha hata kabla sijajua kama nitaipata ama la,basi wakaendelea kunishawishi niongeze hela ifike mia hamsini bila mafanikio.Pembeni ya ile meza alikuwa amesimama kijana mmoja hivi akawa ananipa mahope kuwa nimeshawakamata hawana ujanja pesa nimepata basi mimi huku mapigo ya moyo yanaenda kasi kama saa ya automatic maana nikiangalia kikuponi number ndo ile ile nikajua mwanaume nimeula kumbe nimeliwa daahh kumbe yule jamaa aliyekuwa anani pump ni member pale,basi nikawakabizi ile $30 na 10000k ile wanafua vile vikupon nakuta number ni tofauti kabisaaaaaaaa pale ndo nikagutuka kuwa nimetapeliwa wala sikuuliza niliondoka maana ningeanzisha malumbano pale wangeweza pita watu wanaonifahamu wakaniona ikawa aibu mara mbili.
 
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwanzoni,brother wangu alitapeliwa mnazi mmoja pale. Siku hiyo asubuhi aliaga anaenda shule boarding iringa,akaondoka na baraka zote za wazazi,ghafla saa nne asubuhi asharudi home anahema kichizi,wazee wakamuuliza kulikoni hujaenda shule?akawakusanya wazazi chumbani wakajifungia mi nikawa nachungulia ,bro akatoa kidude flan hivi nikamsikia anasema dhahabu,aisee wazee wakaenda funga mageti yote nje,bro akawaambia alikutana na msukuma stand eti aliokota hiko kidude ila yeye hakitaki kimeandikwa GOLD FIRST CLASS FROM ..nimesahau jina la mgodi akaamua mpa nauli ya ke ya bus to iringa na poketi money yote. Aisee ile ishu iliwachanganya wazee wakajua utajiri huu. Milango imefungwa home hamna wa kutoka mpaka mimi wanani ignore,ikafika usiku wa saa nne wakatoka kwenda kwa mzee jirani yeye mtaalam wa madini hahaha,yule mzee akawasha stovu akayaiunguza yale mawaya dooh yakawa meupe na biashara ikaishia hapo.
[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
kiberiti,sabuni,bahasha,mkanda na korokoro ninautaalamu navyo ila ninawasiwasi wa kuharibu biashara ya watu.mnanishaurije nimwage hapa?
Hata mimi navijua acha wapigwe si ujinga wao,usiharibu kabisa watu wanaishi kwa dili hizo!!
 
Hawa jamaa viberiti vitatu ni ujanja tu, hawana dawa wala hirizi, isipokuwa wako makini na kazi yao, viberiti viwili havina njiti na kimoja kina njiti zilizopunguzwa urefu, ukifungua kwa upande mmoja unaziona, ila ukifungua kwa upande mwingine hauzioni, kwa sababu kimewekwa kaboksi katikati kutenganisha upande wenye njiti na upande usio na njiti, sasa anakuwa mjanja mchezeshaji, ukiweka pesa tu azingua anakufungulia upande mwingine wa kiberiti kilekile unakuta njiti hakuna, unakuwa umeliwa, halafu pale kundi kubwa wanakuwa ni wao tu, kwa hiyo kuchomoka inakuwa ngumu.
Aisee umenifungua akili nilikuwa najiuliza huwa wanatumia ujanja gani hawa watu? Kumbe hiyo ndo trick yao.. Thank you mkuu.
 
Haaahaaa hawajakutoa na moshi?!
Umejuaje best!!! Alilamba kidole chake akasugua kwenye vumbi then akanisugua mkononi ukatoka moshi mwingiiiiiii huku anaongea makorokocho, hapo akili ikapaaa akanambia niende karibu na kanisa fulan eti nikifika niseme utukufu juu mbinguni na amani dunian ntaona Pete ya Bahati inashushwa! Daaah waliniweza wale jamaaa nikikumbuka nachekaa😀
 
Umejuaje best!!! Alilamba kidole chake akasugua kwenye vumbi then akanisugua mkononi ukatoka moshi mwingiiiiiii huku anaongea makorokocho, hapo akili ikapaaa akanambia niende karibu na kanisa fulan eti nikifika niseme utukufu juu mbinguni na amani dunian ntaona Pete ya Bahati inashushwa! Daaah waliniweza wale jamaaa nikikumbuka nachekaa😀
Yaani ule moshi aliutengeneza mwezio ambaye tayari alishakwenda kanisani kuna namna alivyorudi alimpa huyo muombeaji bila wewe kujua,hakuna uganga wala nini ni ujanja tu.
 
Yaani ule moshi aliutengeneza mwezio ambaye tayari alishakwenda kanisani kuna namna alivyorudi alimpa huyo muombeaji bila wewe kujua,hakuna uganga wala nini ni ujanja tu.

Du wanapigwa Sana pale msimbazi Makoro pgo za cmu unauziwa sabuni.au unanunua kiatu kumbe ugali wa juzi huwa nacheka Sana..
Hiyo inakuwaje?
 
Yaani ule moshi aliutengeneza mwezio ambaye tayari alishakwenda kanisani kuna namna alivyorudi alimpa huyo muombeaji bila wewe kujua,hakuna uganga wala nini ni ujanja tu.
Hahaaaa inakuwaje hapo
 
Yaani ule moshi aliutengeneza mwezio ambaye tayari alishakwenda kanisani kuna namna alivyorudi alimpa huyo muombeaji bila wewe kujua,hakuna uganga wala nini ni ujanja tu.
Mmmm wana umakini sana.... Kuja kujua ni matapeli ishakula kwako
 
Huu uzi wahusika wa u stick basi maana unatufunza mno tusije pigwa kama hao
 
  • Thanks
Reactions: Ok9
Back
Top Bottom