Jinsi nilivyoongea na viumbe wa ajabu

Venus Star

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
19,664
59,735
Nawasalimia kwa pamoja ndungu zangu wana JF.
Muda mrefu umepita nimekuwa nikiwaza sana kuhusu jambo hili lililonitokea tarehe 11/9/1990. Kila nikijaribu kumwambia mtu moyo unakataa nahisi kwamba hata nielewa na anaweza akaanza kuniogopa. Kipindi kile nilikuwa nilikuwa nimeingia kidato cha sita shule ya sekondari ya ILBORU nikiwa nasoma masomo ya sayansi.

Leo nimeona niandike humu huenda wapo watu watanielewa maana jambo hili nimekuwa nikiliwaza sana. Siku hiyo wanafunzi wote walikuwa wamelala ilikuwa usiku wa manane. Ghafla usingizi ulikata na nikapata msukumo wa kutoka kwenda nje. Basi nilifanya hivyo. Nikaenda kukaa kwenye mti ambao tulikuwa tunapendelea kukaa ili kupiga soga.

Ghafla nilipigwa mwanga usoni na kitu kilichotokea mbele yangu. Mwili wangu ukawa kama umepigwa shoti ya umeme, nywele zangu zote zikasimama, nikawa na jiona kama nimo ndani ya maji nikielea. Nikasikia sauti ikiniita jina langu J J J mara tatu. Naami nikaitika na kusema naam!!

Viumbe wawili wa ajabu walinisogelea mmoja akanigusa kichwani ndipo nguvu zikanijia. Wakaanza kunena na mimi; ni mambo mengi sana waliongea na mimi, lugha tuliyokuwa tunaongea nao kwakweli mpaka leo hii siwezi kuijua kuwa ni lugha gani. Bali tulikuwa tunaelewana. Walinipatia kanuni kadha wa kadha, ilinichukua muda kuzielewa.

Viumbe hao walinibeba kwenye chombo chao kilikuwa kinafanana na meli ambayo ni ya duara. Tuliondoka mpaka tukafika sehemu. Wakaniambia hapa ndipo chanzo cha nishati, wewe umeweza kuyaona haya tutakufunulia siri nyingi ili uweze kuwapatia wengi wajue ulimwengu huu. Wakasema sisi tunawaona mnahangaika sana elimu na ujuzi wenu bado upo chini sana maana hamuwezi hata kutuona sisi tukija huko. Uwezo wa macho yenu kuona ni mdogo sana, hata masikio yenu hayawezi kutusikia.

Viumbe hao wakanipatia formula mbalimbali na namna nitakavyo wafundisha wengine jinsi ya kujua siri nyingi. Nimejaribu kuzitumia formula kadha wa kadha naona zinafanya kazi.

Ninajitolea sasa kuanza kuwafundisha watu watakaokuwa tayari.

Kama kuna mtu mwenye swali karibu sana.
 
Kupata maswali ya maana ni vigumu maana maswali yangekuja ungeeleza hayo uliyofundishwa kuwajulisha wengine na hapo huenda ndiyo tungevutika kulingana na faida zake.
Sasa kisa hicho kifupi tutakuuliza nini ilihali hata lugha mliyoongea tu pia huijui.
 
Back
Top Bottom