Jinsi nilivyokaa siku 100 bila kuangalia saa

Jinsi nilivyokaa siku 100 bila kuangalia saa

Napata picha unajiamkia tu asubuhi hujui ni saa ngapi hujui kama umechelewa kuamka ili ujue utajiandaa kwa muda gani,kituo cha kazi reporting time ni 08:30 asubuhi wewe uingie pale saa 09:40.

Yaani huyu jamaa sijamuelewa kabisa huyu.
ni ngumu sana kuelewa unaishije bila kuangalia muda,wazungu wanakuambia time is money 😂
 
Napata picha unajiamkia tu asubuhi hujui ni saa ngapi hujui kama umechelewa kuamka ili ujue utajiandaa kwa muda gani,kituo cha kazi reporting time ni 08:30 asubuhi wewe uingie pale saa 09:40.

Yaani huyu jamaa sijamuelewa kabisa huyu.

Atakua jobless huyu kijana
 
Swala Hapo Si Saa,,Swala Hapo Ni Muda...
###MudaHauitajiSaa###
###SaaNdioInahitajiMuda###
 
Kuna kitu nilifanya mwaka jana ambacho watu wengi waliniona kama nacheza mchezo wa ajabu kidogo.

Nilikaa siku 100 nzima bila kuangalia saa.

Hakuna sababu maalum. Sikuamka asubuhi nikasema tu moyoni, “leo naanza.” Nikajiambia nione kama inawezekana kuishi kawaida kabisa bila kujua muda ni saa ngapi.

Kitu cha kwanza nilifanya ni kuacha kabisa kuvaa saa ya mkononi. Ile saa ya ukutani nayo niliiondoa pale sebuleni kwa sababu nilijua macho yangu yataikimbilia tu bila kufikiria.

Simu yangu nayo nilijitahidi sana nisiangalie sehemu inayoonyesha muda.

Mwanzoni ilikuwa inanisumbua kidogo. Unajikuta mkono unaenda mfukoni kuchukua simu halafu ghafla unakumbuka, “hapana, leo siangalii saa.”

Lakini baada ya siku chache nikaanza kuzoea.

Nilianza kuamka tu bila kujua ni saa ngapi. Nikihisi njaa nakula. Nikihisi usingizi nalala. Siku zinaenda tu bila mimi kujua muda umefika wapi.

watu wengi walikuwa wanashangaa.

Mtu anakwambia, “sasa hivi ni saa ngapi?”
namwambia sijui.

Wengine walidhani natania.

Lakini ukweli ni kwamba kwa zile siku 100 sikujua kabisa muda ni saa ngapi kwa siku yoyote.

Na kitu nilichogundua ni hiki: baada ya muda mwili unaanza kujipangia mambo yake tu. Unahisi tu muda wa kula umefika, muda wa kupumzika umefika, au muda wa kwenda nje umefika.

Kuna siku nilikaa na watu wakawa wanabishana muda umeenda haraka au polepole. Mimi kichwani kwangu siku ilikuwa inaenda kawaida kabisa.

Changamoto pekee ilikuwa pale mtu anaponiambia tukutane saa fulani. Hapo nilikuwa namwambia tu anipigie au anifuate maana mimi sina habari na saa.

Baada ya kufika siku ya 100 ndipo nilipoamua kuangalia saa tena.

Nilihisi kama nimeingia tena kwenye ulimwengu ambao kila mtu anaishi akifuatilia namba tu ukutani.

Lakini ukweli ni huu…

Inawezekana kabisa kuishi bila kuangalia saa.

Na saivi nampango wa kukaa siku 300 kwamaana inatuliza akili
Mkuu ulijitahidi sana kwa mazingira ya sasa. Ila nikuambie... miaka wala siyo mingi sana iliyopita, hayo ndiyo yalikuwa maisha ya vijiji vingi Tanzania. Kuna watu wengi walikuwa wanaenda shambani, shule nk kwa kutumia majogoo, ndege, vivuli vya nyumba na hisia nyingine. Siyo ngumu kivile kama mtoto wa sasa wa Gen Z. anavyodhani.
 
Ila wengi ndivyo mumemsema kwa kutaka iwe kivyenu basi ndivyo mlivyo..

Badalahata ya kuuliza ilikuwaje? Kuna vitu aliona anakosa au kukosea kwa kutokujua muda... Ila, mjisikitikie

Kuna, jambo moja
Je, hajawahi kuamka, muda, fulani kimazoea hata iweje mtashtuka tu haswa kuamkia asubuhi? Na, ukiangalia saa muda ule ule mfano ndani ya -/+10mins
 
kuna watu hawaamini, hawa wana "trust issues" jaribu oekeyako hata wiki moja na utagundua inawezekana. mwili wenyewe una saa, binadamu tumeishi miaka mingi bila saa saa imekuja juzi tu, kuku na dege wanaamka asubui muda uleule bila saa, jogoo anawika sa tisa sa 12 etc, hakosei na hatumii saa, hata ukichunga n'gombe muda wao wa kurudi nyumbani hawakosei.

na binadamu tupo hivyo ststem nzima ilishakwepo tayari na ina ji update, ndo maana kuna muda unasikia usingizi hata ujizuie unalala, kuna muda usingizi unakata, kunamuda unasikia njaa

na matendo mengine yote yanaweza kuingia kwenye mfumo wa mwili ndani ya siku chache tu
 
Kwa nn ulirudi Tena kuangalia saa?
nilirudi kwasababu naishi kwenye dunia ambayo huo ndo utaratibu uliopo

ngoja nikuulize pia.. kwanini unafunga kipindi cha mfungo alafu baadae unaendelea na mambo yako ya kawaida ? hatakama wewe ukisema haufanyi hivo mbona wengi wanafanya na unaona ni sawa ?
 
Mada yako ni nzuri na inafikirisha , kiukweli tunaishi kwenye ulimwengu wa matrix, ukiweza kujitoa hapo maisha yako yanakua na uhuru wa asili sana
 
e0cfcc2d-245d-4a0c-be28-45543bca36b2.jpeg
 
Back
Top Bottom