Jinsi Kampuni za Simu zinavyowaibia wateja wao!

Jinsi Kampuni za Simu zinavyowaibia wateja wao!

kwa nini umesubiri kwa muda wa maika 10 ndipo unatueleza?Wakati ulipokuwa unapata mishahara kwa fedha za wizi,uliuchana.leo fedha zetu umeanzisha biashara unaamua kuwamwagia mchanga kitumbua wezi wenzako.miaka .10 kukaa kimya ni mingi sana.
 
yaani@voda ndo mababa wa utapeli mi siku hizi ni airtel afadhali

Skia mkuu,yan hii ni kwamakampun yote ya sim hapa Tanzania na bila ubishi vitu vyote alivyotaja mtoa mada vipo kwel na vinaonekana kwenye matumiz ya kila siku,kwaiyo uwezi kukoswa na mkono wa Escrow huu!!
 
Waziri wa tecnologia na mawasiliano na naibu wake yupo na wanayajua haya kisa10% alafu naibu waziri wa wizara husika anataka Urais kwa mtaji huu Urais asahau labda awe rais wa Bumbuli
 
TANU ilianza mwaka 1954 jamani TANU eeenhe iyeee iyee wimbo mzuri xana
 
Mzee hilo la kutokupewa taarifa kifurushi kinapokwisha ni la kweli kabisa. Mimi nishaliwa hela nyingi kwa mtindo. Kuna demu mmoja yeye alitaka kulia, alikua na laki mbili za salio kwenye simu yake. Sasa alijiunga na kifurushi so akawa comfortable kutumia internet. Wakati anaendelea kutumia kifurushi kikaisha na wazee wa mtandao wakaanza kumkata. Huwezi amini laki mbili zilikatwa usiku mmoja tu. Just imagine internet gani hiyo ya kumkata mtu laki mbili usiku mmoja!!!!

Sasa dawa yao ni moja tu. Mimi sasa hivi pesa zangu siweki salio moja kwa moja nazihifadhi kwenye tigopesa au easy pesa. Kila siku natoa 600 najiunga kifurushi, kikiisha simu inakuwa zero , najiunga tena.

duuuu mzee vocha ya laki 2 inafanya nn kwenye sim.....kama n kawaida yake......asingejutia......
any way...mchrzo uliishaje
 
tigo duka lao lililopo malindi Zanzibar ndio majambazi kabisa,vocha ikikwanguka vibaya ukiwapelekea ndio imekula kwako,niliwahi kuwapelekea vocha ya 5000 ilikwanguka vibaya.Walichofanya walinipa fomu nijaze ikisha wakaiambatanisha na hiyo vocha wakaniambia watanitumia basi mpaka leo mwaka wa pili huu.
 
tigo duka lao lililopo malindi Zanzibar ndio majambazi kabisa,vocha ikikwanguka vibaya ukiwapelekea ndio imekula kwako,niliwahi kuwapelekea vocha ya 5000 ilikwanguka vibaya.Walichofanya walinipa fomu nijaze ikisha wakaiambatanisha na hiyo vocha wakaniambia watanitumia basi mpaka leo mwaka wa pili huu.
 
Na kibaya ni kwamba kampuni hizi zimeunda partnership ya hatari sana kwa lengo la kuwakamua wateja wao bila huruma. Mwanzoni kila kampuni ilikuwa inafanya kazi zake kwa kujitegemea lakini baadaye waliamua kuungana ili wawadhibiti wateja vizuri zaidi. Mfano halisi ni kwamba kifurushi cha Tsh 500 kwa Voda na tiG0 ni dakika 8, sms 300 na 40MB…wamelinganisha viwango kwa makusudi! Hii maana yake ni kwamba wameweka viwango sawa ili wateja wakose pa kuponyokea…ukienda tigo unakula kirungu na ukirudi voda pia unakula kirungu hicho hicho! There is no way you can escape being exploited!

Mfano mwingine: Hebu tazama ushahidi huu hapa jinsi walivyopanga ku synchronize huduma zao kwa lengo lilelile la kuwanyonya wateja kwa pamoja. Siku hizi hata promo wanapiga equally and at the same time:

******************************************************************************
Pata Sh1000 BURE kila uongezapo salio la Sh1000 au zaidi.Ongeza salio kwa Vocha,TigoPesa au TigoRusha.
******************************************************************************
Jaza kuanzia BUKU upate BUKU! Ongeza salio kuanzia Tsh.1000 upate nyongeza ya Tsh.1000 BURE ya Vodacom-Vodacom kwa saa 24. Maisha ni murua ukiwa na Vodacom.
 
kwa nini umesubiri kwa muda wa maika 10 ndipo unatueleza?Wakati ulipokuwa unapata mishahara kwa fedha za wizi,uliuchana.leo fedha zetu umeanzisha biashara unaamua kuwamwagia mchanga kitumbua wezi wenzako.miaka .10 kukaa kimya ni mingi sana.

Mkuu, napenda nikuhakikishie kwamba mimi sikuhusika kwa wizi huu hata kidogo. Mimi nilikuwa nafanya kazi kwenye kitengo cha Corporate Solution na Marketing....wanaofanya wizi huu hasa wapo kitengo cha IT na Network.
 
Na kibaya ni kwamba kampuni hizi zimeunda partnership ya hatari sana kwa lengo la kuwakamua wateja wao bila huruma. Mwanzoni kila kampuni ilikuwa inafanya kazi zake kwa kujitegemea lakini baadaye waliamua kuungana ili wawadhibiti wateja vizuri zaidi. Mfano halisi ni kwamba kifurushi cha Tsh 500 kwa Voda na tiG0 ni dakika 8, sms 300 na 40MB…wamelinganisha viwango kwa makusudi! Hii maana yake ni kwamba wameweka viwango sawa ili wateja wakose pa kuponyokea…ukienda tigo unakula kirungu na ukirudi voda pia unakula kirungu hicho hicho! There is no way you can escape being exploited!

Mfano mwingine: Hebu tazama ushahidi huu hapa jinsi walivyopanga ku synchronize huduma zao kwa lengo lilelile la kuwanyonya wateja kwa pamoja. Siku hizi hata promo wanapiga equally and at the same time:

******************************************************************************
Pata Sh1000 BURE kila uongezapo salio la Sh1000 au zaidi.Ongeza salio kwa Vocha,TigoPesa au TigoRusha.
******************************************************************************
Jaza kuanzia BUKU upate BUKU! Ongeza salio kuanzia Tsh.1000 upate nyongeza ya Tsh.1000 BURE ya Vodacom-Vodacom kwa saa 24. Maisha ni murua ukiwa na Vodacom.

tpaul big up bro.naona umeamua kuanika kila kitu. Ila Vipi hawa jamaa hawajakutafuta na kuanza kukuchimba mikwara kweli? Maana wengine wapo humu humu, kama hawa "kazi ni kwako"?
 
Last edited by a moderator:
tpaul big up bro.naona umeamua kuanika kila kitu. Ila Vipi hawa jamaa hawajakutafuta na kuanza kukuchimba mikwara kweli? Maana wengine wapo humu humu, kama hawa "kazi ni kwako"?

Mkuu, hao WAIZI bado hawajanighasi kwa kuwa wanafahamu kwamba nimesema ukweli ambao hawana uwezo wa kuukanusha. Tayari wadau wameishawaitwa waje kujitetea lakini wameingia mtini...WAIZI wakubwa!
 
Last edited by a moderator:
Nimefanya kazi kwenye kampuni mbali mbali za simu hapa nchini kwa muda wa zaidi ya miaka 10, kabla ya kuamua kujiajiri mwenyewe. Katika muda wote huo nimeshuhudia kampuni hizi zikiwaibia wateja kwa namna mbalimbali. Nimekaa na huu ushahidi kwa muda sasa lakini naona roho inanisukuma
niuanike hadharani mbele za watanzania ili wafunguke macho na kufahamu UFISADI huu unaofanywa na kampuni za simu hapa nchini. Nitaanika wizi wote kadri nitakavyoweza kuukumbuka hapa:

Huduma za bure
Kuna hizi huduma ambazo wanaziita huduma za “BURE” kana kwamba zinapatikana bure wakati si kweli! Kwa mfano, wateja hutumiwa SMS zinazowadanganya kwamba wanaweza kupata huduma za bure na ili wazipate wanaelekezwa kutuma ujumbe kwenda kwenye namba fulani. Na mteja akisharogwa akatuma ujumbe kwenda kwenye namba husika, imekula kwake! Nyingi ya huduma hizi zinzoitwa za bure hugharimu fedha na mara ujiungapo hujikuta unakatwa salio lako kimya kimya. Ni mara nyingi mtakuwa mmewahi kusikia mtu akilalamika kwamba salio lake limepungua….unaweka airtime ya Tsh 1000 leo bila kuitumia, ikifika kesho unakuta zimebaki sh 350! Tsh 650 zimeenda wapi? Zimekatwa kwenye zile huduma za “BURE” ulizotangaziwa.

Promosheni feki
Promosheni nyingi zinazoanzishwa na makampuni ya simu zinalenga kuwanyonya na kuwakandamzia wateja. Mfano halisi ni pale wateja wanapotangaziwa kwamba huduma ya FESIBUKU inapatika bure! Thubutuuu! Hakuna kitu cha bure nchi hii, ndugu yangu. Huu ni wizi wa mchana! Kupona kwako ni pale utakapotumia hiyo huduma ukiwa hauna salio kwa kuwa huwezi kupata access ya huduma husika (kama vile fesibuku, twita, nk). Ikiwa utafungua huduma hiyo ukiwa na salio, salio lako lote litakombwa sawia! Kuna mtandao mmoja wa simu unajinadi kwamba unatoa huduma ya fesibuku bure wakati ni uongo mtupu. Ingia kwenye hiyo fesibuku uone utakavyoliwa fedha! Aidha kuna mtandao mmoja uliwahi kuwa na fesibuku ya bure siku za nyuma (kama mtakumbuka). Kwa muda fulani huduma hii ilikuwa ikipatikana bure kabisa. Kumbe ilikuwa ni janja ya nyani…..baadaye ile “bure” ilifutwa kimya kimya, wateja wakaendelea kukamuliwa kama kawaida na mpaka leo hawajawahi kuwataarifu wateja wao kwamba hiyo “bure” imesitishwa! Kuna wateja wengi sana, hasa wa kule vijijini, ambao wanaendelea kukamuliwa kwa kujidanganya kwamba huduma ni ya bure hadi leo, kumbe ilishasitishwa kitambo sana!

Ulaghai wa Kimangungo
Kuna wakati ambapo makampuni ya simu hupandisha tariffs kimya kimya bila kuwataarifu wateja wake na kuendelea kuwaibia bila kujua. Mwaka 2006 gharama za kupiga simu, kutuma sms na kutumia data zilipandishwa kinyemela na wateja wakaendelea kukamuliwa fedha kimya kimya hadi pale baadhi yao waliposhtukia dili na kuja juu. Aidha, prosheni fulani zinapoanzishwa, kama vile punguzo la gharama za kupiga simu nyakati za usiku, pindi zinafikia tamati wateja hawapewi taarifa na kujikuta wakitumia fedha zaidi ya matarajio yao. Promosheni inapoisha kampuni hizi huwakataza wafanyakazi wake wasiwaambie wateja ili waendelee kukamuliwa fedha kilaghai. Huu ni wizi, tena wa mchana na hauna tofauti na ufisadi wowote ule.

Kutotoa taarifa kwa wateja kwa makusudi
Wateja wanapojiunga kwenye vifurushi mbalimabli huletewa taarifa immediately via SMS kwamba wamefanikiwa kujiunga lakini kifurushi kikiisha ama wateja huchelewa kutumiwa meseji ya taarifa au hawatumiwi kabisa. Hili tatizo huwakumba zaidi wale wateja wanaopenda kubaki na salio kubwa kwenye simu zao. Kwa mfano, mtu unanunua vocha ya Tsh 2000 kisha unanunua kifurushi cha Tsh 500 na kubakiwa na Tsh 1500 kwenye simu. Pindi kifurushi cha 500 kikiisha hutatumiwa ujumbe wowote hadi utapokuwa umekausha 1500 zilizosalia kwenye simu. Huu pia ni wizi wa mchana na unaofanywa kwa makusudi na kampuni za simu hapa nchini. Ninao ushahidi usiokuwa na mashaka katika huu wizi wa makusudi.

Njia nyingine inayotumika kuiba hapa ni kutotoa call details pindi upigapo simu. Ukimaliza kupiga simu ukiangalia call details unakuta inasoma 00:00:00! Details hizi zinafichwa kwa makusudi ili kujenga mazingira ya wizi. Kwa mfano mtu unaongea kwa dakika 3, wao wanakata dakika 4.30 na kukuibia dakika 1.30! Matokeo yake unakuta muda wa hewani uliopewa wakati wa kujiunga umeibiwa na kampuni kwa maslahi yake binafsi. Lakini pia kuna wizi mwingine huu hapa: – unaponunua kifurushi hupewa dakika ambazo ungetegemea zizotozwe kwa sekunde (per second billing) lakini badala yake hutozwa kwa dakika (per minute billing) kinyume cha mkataba kwa lengo la kumkamua mteja kiujanja. Huu ni wizi na haukubaliki hata kidogo.

Kuvuruga mawasiliano kwa makusudi
Kuna wakati wahandisi wa kampuni husika hupewa jukumu la kuvuruga mawasiliano ya wateja ili watumie muda mwingi na pesa nyingi kwenye maongezi. Inakuwaje hapa? Inakuwa hivi: Ukimpigia mtu yeye anakuwa anakusikia lakini wewe humsikii au vice versa. Hii husababisha kutumia muda mwingi kuelewana wakati huo salio likinyonywa kama kawaida – hata kama mkichukua muda mwingi kuelewana salio hutafunwa sawia! Njia nyingine inayotumika hapa ni kuvuruga access to customer care ili unapokuwa umepatwa na tatizo usiweze kuwafikia watu wa huduma kwa wateja kupata msaada. Hii ndio sababu 90% ya wateja wenye matatizo genuine hawaipati namba 100. Mtu unaweza kupiga siku nzima na usiunganishwe kuongea na mshauri. Hatimaye wengi wao hukata tamaa na kuamua kukubali “kuliwa”!

Hii ni sehemu ya ushahidi ambao nimeukusanya while working with different mobile companies in Tanzania. Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

Nawasilisha.

Wanayo internet bila kikomo ya wizi
 
Jamani tutaponea wapi?

Wisi, wisi, wisi kila kona
 
Wizi mwingine, wakati mwingine ukijiunga bandle na mtandao unapotea hapohapo mpaka masaa 24 yanaisha na haurudishiwi chako
 
Na Yona Maro, Mwananchi

Ni dhahiri wengi tumewahi kupokea ujumbe mfupi wa maneno (sms) bila wenyewe kutaka, halafu hapo hapo utaona kiasi fulani cha fedha kimeondoka kutokana na ujumbe huu.
Wakati mwingine simu haina fedha lakini unapoingiza salio tu ujumbe utaingia na fedha hiyo itakatwa. Kwa Tanzania hivi sasa tabia hii imekuwa kama ada.
Wateja wanatumiwa sms wasizopenda, lakini kibaya zaidi ni namna fedha zao zinavyokatawa kienyeji na watoa huduma wa simu za mkononi.
Katika baadhi ya nchi wameanza kufikishana mahakamani kutokana na aina hizi za ujumbe wa promosheni. Watu wanataka haki zao za mawasiliano ziheshimiwe na waamue wenyewe kama wanataka kujiunga kwenye huduma fulani au la.
Mwanasheria mmoja nchini Uganda ameifikisha mahakamani kampuni ya MTN, kwa madai ya kumtumia ujumbe mfupi wa matangazo. Mwanasheria huyu anataka kampuni ya MTN Uganda kuacha mara moja kumtumia ujumbe mfupi wa matangazo.
Anasema yeye ni mtumiaji na amesajiliwa kutumia simcard ya mtandao wa MTN, sio kwa minajili ya kutumiwa matangazo na kwamba kitendo hicho ni kuvunja haki zake.
Mahakama imeitaka kampuni ya MTN Uganda kuwasilisha utetezi wake baada ya shauri hilo kupelekwa mahakamani.
Kabla ya suala hili la mahakamani , taasisi inayohusika na usimamizi wa mawasiliano nchini Uganda (Uganda Communications Commision) ilipiga marufuku utumaji wa ujumbe mfupi wa matangazo kwa watumiaji wa huduma za simu nchini humo. Marufuku hii ilianza kutumika tangu Juni 8 mwaka huu.
UCC imetaka kampuni zote za mawasiliano nchini Uganda kuandaa utaratibu wa jinsi zitakavyoendesha huduma kama hizo bila kusumbua watumiaji wa huduma za mawasiliano hasa kwenye suala la ujumbe mfupi.
Pamoja na yote hayo kuna masuala kama matatu ambayo wateja wengi wamekuwa wakiyalalamikia ambayo yanafanana na yanayotokea hapa nchini.
Moja ni mkataba au makubaliano kati ya mtumiaji wa namba husika na mtoa huduma wake; kwamba hakuna mkataba rasmi ambao unatamka rasmi kwamba mteja amekubali mwenyewe kutumia sms za matangazo au sms zozote zile kutoka kwa mtoa huduma. Kimsingi kunatakiwa kuwepo kwa mkataba kama huu ili mteja aamue mwenyewe kama anataka kujiunga ama la.
Pili ni suala la kampuni za simu kutumia mwanya huo wa kutokuwapo kwa mkataba kuanzisha promosheni na kuzituma kwa wateja wake, kwa sababu ya sheria mbovu za mawasiliano.
Kwa yanayaotokea Uganda, ni vyema tujiandae kujadili suala na hatimaye kuliingiza katika Sheria ya Mawasiliano kwa mjadala bungeni.
Japo inajulikana kuwa kampuni zinaweza kupinga kipengele hiki, kwa sababu ndicho wanachokitumia kupata faida nono, lakini bado ni suala muhimu kuwa mteja awe na haki ya kuamua kama anataka kupokea ujumbe au la. Kuwepo na uchaguzi wa aina gani ya ujumbe mteja anataka atumiwe.
Jambo hili limekuwa likipigiwa kelele na wadau kadhaa wa mitandao ya simu, lakini kampuni zinajitetea kuwa watumaji wa ujumbe ni wengine, wao wanawezesha tu utumaji.
Katika Sheria ya Mawasiliano kuna kipengele cha faragha. Hiki kinahusika na masuala binafsi ya kila mtumiaji wa huduma za mawasiliano na hapo ndipo tunapoweza kuongeza kipengele hiki cha kudhibiti matangazo au promosheni.
 
Unanunua bundle.......then network hakuna hadi muda wa bundle uishe.
Hebu tuwe tunaweka hayo matukio hapa...
 
Back
Top Bottom