Jinsi Kampuni za Simu zinavyowaibia wateja wao!

Jinsi Kampuni za Simu zinavyowaibia wateja wao!

Imefikia wakati napiga simu customer care..akipokea anajitambulisha...nachukua jina lake alafu nakata simu. Naanza kumpekua mitandaoni nikimfahamu namfuatilia.....ngoja niishie hapo. Ila hili jukumu nilianza baada ya kuona watoa huduma wengi wanavikauli vibaya pindi nipigapo simu...yaani naibiwa alafu napewa na maneno ya kejeli.....ngoja ninawe maji nitoe povu....ila hao one day watakufa
 
Wakuu ni takribani miaka 4 iliyopita tangu nianzishe uzi huu lakini mpaka leo TCRA hawajachukua hatua zozote kuwaadhibu hawa wezi wanaowaibia wananchi kila kukicha.

Takribani miezi 3 iliyopita mtakuwa mmegundua kwamba Vodacom Tanzania nao wameanza wizi kwenye bundles kama ilivyo kwa Halotel. Niliwakimbia Halotel nikahamia huku Vodacom lakini sasa naona ni afadhali nirudi Halotel kwa kuwa wizi wa Halotel unaonekana sio mkali sana kama huu wa Vodacom.

Kama mtakuwa wafuatiliaji wazuri, hasa wale wateja wa kudumu wa Vodacom, bila shaka mtakuwa mmegundua kuisha kwa bundle kusikokuwa kwa kawaida. Zamani nilikuwa nikinunua GB 2 za vodacom na kuzitumia kwa wiki nzima....nikidowload YouTube, kutazama TV, na kuperuzi mambo kibao...na bado chenji inabaki. Sasa hivi bundle hili huisha ndani ya siku moja na kama litadumu sana basi huchukua siku 2 tu (wakati matumizi ni yaleyale ya zamani).

Hii tasfiri yake ni nini? Tafsiri yake ni kwamba huu ni wizi wa mchana kweupe. Kuna uwezekanao mkubwa kwamba zile GB tunazopewa ni kanyaboya...ni maandishi tu lakini kiuhalisia unaweza ukute umepewa MB 100 tu! Tunaomba serikali iingilie kati wizi huu, otherwise wananchi tutaendelea kuibiwa na hawa makaburu hadi Yesu atakaporudi.

Nawasilisha.
 
Wakuu wizi mwingine huu hapa:

Rais Magufuli nakuomba uwashughulikie wahujumu uchumi hawa hapa!

Wakati kesi inayowakabili mabosi wa Haloteli kwa kutakatisha fedha na kuhujumu uchumi ikiwa haijafika tamati, kampuni hii ya simu imeanza tena wizi na utapeli kwa wateja wake. Nasema hili kwa kuwa mimi ni mteja wao na nina kipande cha ushahidi (a piece of evidence) na maelezo ya kutosha kuthibitisha haya ninayoyasema.

Mimi ninatumia data za Halotel kwenye modemu kwa takribani miaka mitano sasa. Hili neno “takribani|” naomba ulibold na kupigia mstari kwa kuwa hapa ndipo wizi wa Haloteli unapoanzia. Wakati naanza kutumia data za haloteli, mara kwa mara nilikuwa naambiwa kisi cha MB zilizobaki na muda zitakapoisha. Nilikuwa natumia meseji za kunikumbusha, hasa bando inapokaribia kuisha. Baada ya kuanza mchakato na hatimaye utekelezaji wa wizi wa bando za wateja, siku hizi hawatumi meseji tena. Wanachofanya ni kutuma meseji moja tu yenye utata na wizi ndani yake kama inavyoonekana hapo chini:

Halotel majizi wakubwa!.PNG


Mtu mwenye akili timilifu ukisoma hii meseji unaona kabisa ina wizi ndani yake kwa 100%. Kwanza imeandikwa kwa mafumbo na haionyeshi uhalisia wowote wa data zilizotumika na jinsi matumizi hayo yalivyofanyika. Twende taratibu. Mimi huwa nanunua bando ya Tsh 1500 yenye ujazo wa 1524 MB. Sasa tuje kwenye hiyo percentage yao. 90% ya 1524 MB = 1371.6 MB. Hii ina maana kuwa baada ya kutumia 1371.6 (90%) ya data kiasi kinachobaki ni 1524 - 1371.6 = 152.4 MB. Sasa tazama upya meseji yao kwennye kielelezo hapo juu. Kiasi cha data kinachotakiwa kubaki baada ya kutumia 90% ni 152.4 MB lakini wao wanasema ni 45 MB! Wezi wakubwa! Hapa wananipiga 152.4 MB - 45MB = 107.4 MB kwa mkupuo mmoja! Ina maana nikinunua bando ya Tsh 15000, kwa mfano, napigwa 10.74 GB. Huu ni wizi mchana kweupe pee!

Na kibaya zaidi, hii meseji inatumwa mwishoni kabisa. Kama sio wezi kwanini wasitume meseji kila ninapotumia labda 100 MB, kwa mfano? Na kwanini saliola data kwa mfumo wa asilimia? Je, ni wananchi wangapi wanaoweza kukokotoa hiyo asilimia? Kwa ujumla hawa jamaa ni wahuni, matapeli, na wezi wakubwa!

Aidha, kwenye meseji yao wanasema nimetumia takribani 90% ya kifurushi. Maana yake ni kuwa hata wao wenyewe hawana uhakika na kifurushi kilichobaki. Kama hawana uhakika mimi nitawaaminije? Hii ni sawa na kumpa shetani amlee mwanao. Ujanjaujanja na wizi wa aina hii haukubaliki hata kidogo hapa nchini Tanzania. Ikiwa sisi wananchi tunaibiwa kiasi hiki, je TRA wanaibiwa mapato kiasi gani?

Natoa wito kwa serikali, kupitia TCRA na TRA kuwachunguza Halotel ili kubaini kiasi cha fedha walizoiba tangu waanze wizi huu na kuwaamrisha wazirejeshe hazina pamoja na kuchukuliwa hatua kali za uhujumu uchumi haraka iwezekanavyo. Hatuwezi kukubali kuwafuga wezi, matapeli, na wahujumu uchumi wakati serikali haina fedha za kuleta maendeleo ya wananchi.

Nawasilisha.
 
Nimefanya kazi kwenye kampuni mbali mbali za simu hapa nchini kwa muda wa zaidi ya miaka 10, kabla ya kuamua kujiajiri mwenyewe. Katika muda wote huo nimeshuhudia kampuni hizi zikiwaibia wateja kwa namna mbalimbali.

Nimekaa na huu ushahidi kwa muda sasa lakini naona roho inanisukuma niuanike hadharani mbele za watanzania ili wafunguke macho na kufahamu UFISADI huu unaofanywa na kampuni za simu hapa nchini. Nitaanika wizi wote kadri nitakavyoweza kuukumbuka hapa:

Huduma za bure.

Kuna hizi huduma ambazo wanaziita huduma za "BURE" kana kwamba zinapatikana bure wakati si kweli! Kwa mfano, wateja hutumiwa SMS zinazowadanganya kwamba wanaweza kupata huduma za bure na ili wazipate wanaelekezwa kutuma ujumbe kwenda kwenye namba fulani.

Na mteja akisharogwa akatuma ujumbe kwenda kwenye namba husika, imekula kwake! Nyingi ya huduma hizi zinazoitwa za bure hugharimu fedha na mara ujiungapo hujikuta unakatwa salio lako kimya kimya.

Ni mara nyingi mtakuwa mmewahi kusikia mtu akilalamika kwamba salio lake limepungua….unaweka airtime ya Tsh 1000 leo bila kuitumia, ikifika kesho unakuta zimebaki sh 350! Tsh 650 zimeenda wapi? Zimekatwa kwenye zile huduma za "BURE" ulizotangaziwa.

Promosheni feki.

Promosheni nyingi zinazoanzishwa na makampuni ya simu zinalenga kuwanyonya na kuwakandamzia wateja. Mfano halisi ni pale wateja wanapotangaziwa kwamba huduma ya FESIBUKU inapatika bure! Thubutuuu! Hakuna kitu cha bure nchi hii, ndugu yangu.

Huu ni wizi wa mchana! Kupona kwako ni pale utakapotumia hiyo huduma ukiwa hauna salio kwa kuwa huwezi kupata access ya huduma husika (kama vile fesibuku, twita, nk).

Ikiwa utafungua huduma hiyo ukiwa na salio, salio lako lote litakombwa sawia! Kuna mtandao mmoja wa simu unajinadi kwamba unatoa huduma ya fesibuku bure wakati ni uongo mtupu. Ingia kwenye hiyo fesibuku uone utakavyoliwa fedha! Aidha kuna mtandao mmoja uliwahi kuwa na fesibuku ya bure siku za nyuma (kama mtakumbuka).

Kwa muda fulani huduma hii ilikuwa ikipatikana bure kabisa. Kumbe ilikuwa ni janja ya nyani…..baadaye ile "bure" ilifutwa kimya kimya, wateja wakaendelea kukamuliwa kama kawaida na mpaka leo hawajawahi kuwataarifu wateja wao kwamba hiyo "bure" imesitishwa! Kuna wateja wengi sana, hasa wa kule vijijini, ambao wanaendelea kukamuliwa kwa kujidanganya kwamba huduma ni ya bure hadi leo, kumbe ilishasitishwa kitambo sana!

Ulaghai wa Kimangungo.

Kuna wakati ambapo makampuni ya simu hupandisha tariffs kimya kimya bila kuwataarifu wateja wake na kuendelea kuwaibia bila kujua.


Mwaka 2006 gharama za kupiga simu, kutuma sms na kutumia data zilipandishwa kinyemela na wateja wakaendelea kukamuliwa fedha kimya kimya hadi pale baadhi yao waliposhtukia dili na kuja juu. Aidha, prosheni fulani zinapoanzishwa, kama vile punguzo la gharama za kupiga simu nyakati za usiku, pindi zinafikia tamati wateja hawapewi taarifa na kujikuta wakitumia fedha zaidi ya matarajio yao.

Promosheni inapoisha kampuni hizi huwakataza wafanyakazi wake wasiwaambie wateja ili waendelee kukamuliwa fedha kilaghai. Huu ni wizi, tena wa mchana na hauna tofauti na ufisadi wowote ule.

Kutotoa taarifa kwa wateja kwa makusudi.

Wateja wanapojiunga kwenye vifurushi mbalimabli huletewa taarifa immediately via SMS kwamba wamefanikiwa kujiunga lakini kifurushi kikiisha ama wateja huchelewa kutumiwa meseji ya taarifa au hawatumiwi kabisa. Hili tatizo huwakumba zaidi wale wateja wanaopenda kubaki na salio kubwa kwenye simu zao.

Kwa mfano, mtu unanunua vocha ya Tsh 2000 kisha unanunua kifurushi cha Tsh 500 na kubakiwa na Tsh 1500 kwenye simu. Pindi kifurushi cha 500 kikiisha hutatumiwa ujumbe wowote hadi utapokuwa umekausha 1500 zilizosalia kwenye simu.

Huu pia ni wizi wa mchana na unaofanywa kwa makusudi na kampuni za simu hapa nchini. Ninao ushahidi usiokuwa na mashaka katika huu wizi wa makusudi.

Njia nyingine inayotumika kuiba hapa ni kutotoa call details pindi upigapo simu. Ukimaliza kupiga simu ukiangalia call details unakuta inasoma 00:00:00! Details hizi zinafichwa kwa makusudi ili kujenga mazingira ya wizi.

Kwa mfano mtu unaongea kwa dakika 3, wao wanakata dakika 4.30 na kukuibia dakika 1.30! Matokeo yake unakuta muda wa hewani uliopewa wakati wa kujiunga umeibiwa na kampuni kwa maslahi yake binafsi. Lakini pia kuna wizi mwingine huu hapa: –

unaponunua kifurushi hupewa dakika ambazo ungetegemea zitozwe kwa sekunde (per second billing) lakini badala yake hutozwa kwa dakika (per minute billing) kinyume cha mkataba kwa lengo la kumkamua mteja kiujanja. Huu ni wizi na haukubaliki hata kidogo.

Kuvuruga mawasiliano kwa makusudi.

Kuna wakati wahandisi wa kampuni husika hupewa jukumu la kuvuruga mawasiliano ya wateja ili watumie muda mwingi na pesa nyingi kwenye maongezi. Inakuwaje hapa? Inakuwa hivi: Ukimpigia mtu yeye anakuwa anakusikia lakini wewe humsikii au vice versa.

Hii husababisha kutumia muda mwingi kuelewana wakati huo salio likinyonywa kama kawaida – hata kama mkichukua muda mwingi kuelewana salio hutafunwa sawia! Njia nyingine inayotumika hapa ni kuvuruga access to customer care ili unapokuwa umepatwa na tatizo usiweze kuwafikia watu wa huduma kwa wateja kupata msaada.

Hii ndio sababu 90% ya wateja wenye matatizo genuine hawaipati namba 100. Mtu unaweza kupiga siku nzima na usiunganishwe kuongea na mshauri. Hatimaye wengi wao hukata tamaa na kuamua kukubali "kuliwa"!

Hii ni sehemu ya ushahidi ambao nimeukusanya while working with different mobile companies in Tanzania. Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

Nawasilisha.
Sasa hivi vifurushi vya mchongo ambavyo Nape na genge lake wameamua kuvifumbia mambo vitatuumiza aisee!!😱🙄😳🙄
 
Nimefanya kazi kwenye kampuni mbali mbali za simu hapa nchini kwa muda wa zaidi ya miaka 10, kabla ya kuamua kujiajiri mwenyewe. Katika muda wote huo nimeshuhudia kampuni hizi zikiwaibia wateja kwa namna mbalimbali.

Nimekaa na huu ushahidi kwa muda sasa lakini naona roho inanisukuma niuanike hadharani mbele za watanzania ili wafunguke macho na kufahamu UFISADI huu unaofanywa na kampuni za simu hapa nchini. Nitaanika wizi wote kadri nitakavyoweza kuukumbuka hapa:

Huduma za bure.

Kuna hizi huduma ambazo wanaziita huduma za "BURE" kana kwamba zinapatikana bure wakati si kweli! Kwa mfano, wateja hutumiwa SMS zinazowadanganya kwamba wanaweza kupata huduma za bure na ili wazipate wanaelekezwa kutuma ujumbe kwenda kwenye namba fulani.

Na mteja akisharogwa akatuma ujumbe kwenda kwenye namba husika, imekula kwake! Nyingi ya huduma hizi zinazoitwa za bure hugharimu fedha na mara ujiungapo hujikuta unakatwa salio lako kimya kimya.

Ni mara nyingi mtakuwa mmewahi kusikia mtu akilalamika kwamba salio lake limepungua….unaweka airtime ya Tsh 1000 leo bila kuitumia, ikifika kesho unakuta zimebaki sh 350! Tsh 650 zimeenda wapi? Zimekatwa kwenye zile huduma za "BURE" ulizotangaziwa.

Promosheni feki.

Promosheni nyingi zinazoanzishwa na makampuni ya simu zinalenga kuwanyonya na kuwakandamzia wateja. Mfano halisi ni pale wateja wanapotangaziwa kwamba huduma ya FESIBUKU inapatika bure! Thubutuuu! Hakuna kitu cha bure nchi hii, ndugu yangu.

Huu ni wizi wa mchana! Kupona kwako ni pale utakapotumia hiyo huduma ukiwa hauna salio kwa kuwa huwezi kupata access ya huduma husika (kama vile fesibuku, twita, nk).

Ikiwa utafungua huduma hiyo ukiwa na salio, salio lako lote litakombwa sawia! Kuna mtandao mmoja wa simu unajinadi kwamba unatoa huduma ya fesibuku bure wakati ni uongo mtupu. Ingia kwenye hiyo fesibuku uone utakavyoliwa fedha! Aidha kuna mtandao mmoja uliwahi kuwa na fesibuku ya bure siku za nyuma (kama mtakumbuka).

Kwa muda fulani huduma hii ilikuwa ikipatikana bure kabisa. Kumbe ilikuwa ni janja ya nyani…..baadaye ile "bure" ilifutwa kimya kimya, wateja wakaendelea kukamuliwa kama kawaida na mpaka leo hawajawahi kuwataarifu wateja wao kwamba hiyo "bure" imesitishwa! Kuna wateja wengi sana, hasa wa kule vijijini, ambao wanaendelea kukamuliwa kwa kujidanganya kwamba huduma ni ya bure hadi leo, kumbe ilishasitishwa kitambo sana!

Ulaghai wa Kimangungo.

Kuna wakati ambapo makampuni ya simu hupandisha tariffs kimya kimya bila kuwataarifu wateja wake na kuendelea kuwaibia bila kujua.


Mwaka 2006 gharama za kupiga simu, kutuma sms na kutumia data zilipandishwa kinyemela na wateja wakaendelea kukamuliwa fedha kimya kimya hadi pale baadhi yao waliposhtukia dili na kuja juu. Aidha, prosheni fulani zinapoanzishwa, kama vile punguzo la gharama za kupiga simu nyakati za usiku, pindi zinafikia tamati wateja hawapewi taarifa na kujikuta wakitumia fedha zaidi ya matarajio yao.

Promosheni inapoisha kampuni hizi huwakataza wafanyakazi wake wasiwaambie wateja ili waendelee kukamuliwa fedha kilaghai. Huu ni wizi, tena wa mchana na hauna tofauti na ufisadi wowote ule.

Kutotoa taarifa kwa wateja kwa makusudi.

Wateja wanapojiunga kwenye vifurushi mbalimabli huletewa taarifa immediately via SMS kwamba wamefanikiwa kujiunga lakini kifurushi kikiisha ama wateja huchelewa kutumiwa meseji ya taarifa au hawatumiwi kabisa. Hili tatizo huwakumba zaidi wale wateja wanaopenda kubaki na salio kubwa kwenye simu zao.

Kwa mfano, mtu unanunua vocha ya Tsh 2000 kisha unanunua kifurushi cha Tsh 500 na kubakiwa na Tsh 1500 kwenye simu. Pindi kifurushi cha 500 kikiisha hutatumiwa ujumbe wowote hadi utapokuwa umekausha 1500 zilizosalia kwenye simu.

Huu pia ni wizi wa mchana na unaofanywa kwa makusudi na kampuni za simu hapa nchini. Ninao ushahidi usiokuwa na mashaka katika huu wizi wa makusudi.

Njia nyingine inayotumika kuiba hapa ni kutotoa call details pindi upigapo simu. Ukimaliza kupiga simu ukiangalia call details unakuta inasoma 00:00:00! Details hizi zinafichwa kwa makusudi ili kujenga mazingira ya wizi.

Kwa mfano mtu unaongea kwa dakika 3, wao wanakata dakika 4.30 na kukuibia dakika 1.30! Matokeo yake unakuta muda wa hewani uliopewa wakati wa kujiunga umeibiwa na kampuni kwa maslahi yake binafsi. Lakini pia kuna wizi mwingine huu hapa: –

unaponunua kifurushi hupewa dakika ambazo ungetegemea zitozwe kwa sekunde (per second billing) lakini badala yake hutozwa kwa dakika (per minute billing) kinyume cha mkataba kwa lengo la kumkamua mteja kiujanja. Huu ni wizi na haukubaliki hata kidogo.

Kuvuruga mawasiliano kwa makusudi.

Kuna wakati wahandisi wa kampuni husika hupewa jukumu la kuvuruga mawasiliano ya wateja ili watumie muda mwingi na pesa nyingi kwenye maongezi. Inakuwaje hapa? Inakuwa hivi: Ukimpigia mtu yeye anakuwa anakusikia lakini wewe humsikii au vice versa.

Hii husababisha kutumia muda mwingi kuelewana wakati huo salio likinyonywa kama kawaida – hata kama mkichukua muda mwingi kuelewana salio hutafunwa sawia! Njia nyingine inayotumika hapa ni kuvuruga access to customer care ili unapokuwa umepatwa na tatizo usiweze kuwafikia watu wa huduma kwa wateja kupata msaada.

Hii ndio sababu 90% ya wateja wenye matatizo genuine hawaipati namba 100. Mtu unaweza kupiga siku nzima na usiunganishwe kuongea na mshauri. Hatimaye wengi wao hukata tamaa na kuamua kukubali "kuliwa"!

Hii ni sehemu ya ushahidi ambao nimeukusanya while working with different mobile companies in Tanzania. Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

Nawasilisha.
Sasa hivi wamekuja na mtindo wa kukaa wote meza moja kupanga bei za vifurushi zinazofanana ili kuwabana wateja wakose mahali pa kukimbilia wakamuliwe vizuri. Mungu anawaona.
 
Wakuu wizi mwingine huu hapa:

Rais Magufuli nakuomba uwashughulikie wahujumu uchumi hawa hapa!

Wakati kesi inayowakabili mabosi wa Haloteli kwa kutakatisha fedha na kuhujumu uchumi ikiwa haijafika tamati, kampuni hii ya simu imeanza tena wizi na utapeli kwa wateja wake. Nasema hili kwa kuwa mimi ni mteja wao na nina kipande cha ushahidi (a piece of evidence) na maelezo ya kutosha kuthibitisha haya ninayoyasema.

Mimi ninatumia data za Halotel kwenye modemu kwa takribani miaka mitano sasa. Hili neno “takribani|” naomba ulibold na kupigia mstari kwa kuwa hapa ndipo wizi wa Haloteli unapoanzia. Wakati naanza kutumia data za haloteli, mara kwa mara nilikuwa naambiwa kisi cha MB zilizobaki na muda zitakapoisha. Nilikuwa natumia meseji za kunikumbusha, hasa bando inapokaribia kuisha. Baada ya kuanza mchakato na hatimaye utekelezaji wa wizi wa bando za wateja, siku hizi hawatumi meseji tena. Wanachofanya ni kutuma meseji moja tu yenye utata na wizi ndani yake kama inavyoonekana hapo chini:

View attachment 1588254

Mtu mwenye akili timilifu ukisoma hii meseji unaona kabisa ina wizi ndani yake kwa 100%. Kwanza imeandikwa kwa mafumbo na haionyeshi uhalisia wowote wa data zilizotumika na jinsi matumizi hayo yalivyofanyika. Twende taratibu. Mimi huwa nanunua bando ya Tsh 1500 yenye ujazo wa 1524 MB. Sasa tuje kwenye hiyo percentage yao. 90% ya 1524 MB = 1371.6 MB. Hii ina maana kuwa baada ya kutumia 1371.6 (90%) ya data kiasi kinachobaki ni 1524 - 1371.6 = 152.4 MB. Sasa tazama upya meseji yao kwennye kielelezo hapo juu. Kiasi cha data kinachotakiwa kubaki baada ya kutumia 90% ni 152.4 MB lakini wao wanasema ni 45 MB! Wezi wakubwa! Hapa wananipiga 152.4 MB - 45MB = 107.4 MB kwa mkupuo mmoja! Ina maana nikinunua bando ya Tsh 15000, kwa mfano, napigwa 10.74 GB. Huu ni wizi mchana kweupe pee!

Na kibaya zaidi, hii meseji inatumwa mwishoni kabisa. Kama sio wezi kwanini wasitume meseji kila ninapotumia labda 100 MB, kwa mfano? Na kwanini saliola data kwa mfumo wa asilimia? Je, ni wananchi wangapi wanaoweza kukokotoa hiyo asilimia? Kwa ujumla hawa jamaa ni wahuni, matapeli, na wezi wakubwa!

Aidha, kwenye meseji yao wanasema nimetumia takribani 90% ya kifurushi. Maana yake ni kuwa hata wao wenyewe hawana uhakika na kifurushi kilichobaki. Kama hawana uhakika mimi nitawaaminije? Hii ni sawa na kumpa shetani amlee mwanao. Ujanjaujanja na wizi wa aina hii haukubaliki hata kidogo hapa nchini Tanzania. Ikiwa sisi wananchi tunaibiwa kiasi hiki, je TRA wanaibiwa mapato kiasi gani?

Natoa wito kwa serikali, kupitia TCRA na TRA kuwachunguza Halotel ili kubaini kiasi cha fedha walizoiba tangu waanze wizi huu na kuwaamrisha wazirejeshe hazina pamoja na kuchukuliwa hatua kali za uhujumu uchumi haraka iwezekanavyo. Hatuwezi kukubali kuwafuga wezi, matapeli, na wahujumu uchumi wakati serikali haina fedha za kuleta maendeleo ya wananchi.

Nawasilisha.
Hawa HALOTEL ni majizi wa kutupwa. Mkumbuke pia mkurugenzi wa Halotel aliwahikukamatwa na serikali kwa shu ya utapeli. Ikiwa anaweza kuitapeli serikali atashindwaje kutapeli wateja?
 
Hivi huu wizi unaofanywa na tiGO na Halotel utakoma lini katika nchi hii ya kusadikika? Inauma sana.
 
Nimefanya kazi kwenye kampuni mbali mbali za simu hapa nchini kwa muda wa zaidi ya miaka 10, kabla ya kuamua kujiajiri mwenyewe. Katika muda wote huo nimeshuhudia kampuni hizi zikiwaibia wateja kwa namna mbalimbali.

Nimekaa na huu ushahidi kwa muda sasa lakini naona roho inanisukuma niuanike hadharani mbele za watanzania ili wafunguke macho na kufahamu UFISADI huu unaofanywa na kampuni za simu hapa nchini. Nitaanika wizi wote kadri nitakavyoweza kuukumbuka hapa:

Huduma za bure.

Kuna hizi huduma ambazo wanaziita huduma za "BURE" kana kwamba zinapatikana bure wakati si kweli! Kwa mfano, wateja hutumiwa SMS zinazowadanganya kwamba wanaweza kupata huduma za bure na ili wazipate wanaelekezwa kutuma ujumbe kwenda kwenye namba fulani.

Na mteja akisharogwa akatuma ujumbe kwenda kwenye namba husika, imekula kwake! Nyingi ya huduma hizi zinazoitwa za bure hugharimu fedha na mara ujiungapo hujikuta unakatwa salio lako kimya kimya.

Ni mara nyingi mtakuwa mmewahi kusikia mtu akilalamika kwamba salio lake limepungua….unaweka airtime ya Tsh 1000 leo bila kuitumia, ikifika kesho unakuta zimebaki sh 350! Tsh 650 zimeenda wapi? Zimekatwa kwenye zile huduma za "BURE" ulizotangaziwa.

Promosheni feki.

Promosheni nyingi zinazoanzishwa na makampuni ya simu zinalenga kuwanyonya na kuwakandamzia wateja. Mfano halisi ni pale wateja wanapotangaziwa kwamba huduma ya FESIBUKU inapatika bure! Thubutuuu! Hakuna kitu cha bure nchi hii, ndugu yangu.

Huu ni wizi wa mchana! Kupona kwako ni pale utakapotumia hiyo huduma ukiwa hauna salio kwa kuwa huwezi kupata access ya huduma husika (kama vile fesibuku, twita, nk).

Ikiwa utafungua huduma hiyo ukiwa na salio, salio lako lote litakombwa sawia! Kuna mtandao mmoja wa simu unajinadi kwamba unatoa huduma ya fesibuku bure wakati ni uongo mtupu. Ingia kwenye hiyo fesibuku uone utakavyoliwa fedha! Aidha kuna mtandao mmoja uliwahi kuwa na fesibuku ya bure siku za nyuma (kama mtakumbuka).

Kwa muda fulani huduma hii ilikuwa ikipatikana bure kabisa. Kumbe ilikuwa ni janja ya nyani…..baadaye ile "bure" ilifutwa kimya kimya, wateja wakaendelea kukamuliwa kama kawaida na mpaka leo hawajawahi kuwataarifu wateja wao kwamba hiyo "bure" imesitishwa! Kuna wateja wengi sana, hasa wa kule vijijini, ambao wanaendelea kukamuliwa kwa kujidanganya kwamba huduma ni ya bure hadi leo, kumbe ilishasitishwa kitambo sana!

Ulaghai wa Kimangungo.

Kuna wakati ambapo makampuni ya simu hupandisha tariffs kimya kimya bila kuwataarifu wateja wake na kuendelea kuwaibia bila kujua.


Mwaka 2006 gharama za kupiga simu, kutuma sms na kutumia data zilipandishwa kinyemela na wateja wakaendelea kukamuliwa fedha kimya kimya hadi pale baadhi yao waliposhtukia dili na kuja juu. Aidha, prosheni fulani zinapoanzishwa, kama vile punguzo la gharama za kupiga simu nyakati za usiku, pindi zinafikia tamati wateja hawapewi taarifa na kujikuta wakitumia fedha zaidi ya matarajio yao.

Promosheni inapoisha kampuni hizi huwakataza wafanyakazi wake wasiwaambie wateja ili waendelee kukamuliwa fedha kilaghai. Huu ni wizi, tena wa mchana na hauna tofauti na ufisadi wowote ule.

Kutotoa taarifa kwa wateja kwa makusudi.

Wateja wanapojiunga kwenye vifurushi mbalimabli huletewa taarifa immediately via SMS kwamba wamefanikiwa kujiunga lakini kifurushi kikiisha ama wateja huchelewa kutumiwa meseji ya taarifa au hawatumiwi kabisa. Hili tatizo huwakumba zaidi wale wateja wanaopenda kubaki na salio kubwa kwenye simu zao.

Kwa mfano, mtu unanunua vocha ya Tsh 2000 kisha unanunua kifurushi cha Tsh 500 na kubakiwa na Tsh 1500 kwenye simu. Pindi kifurushi cha 500 kikiisha hutatumiwa ujumbe wowote hadi utapokuwa umekausha 1500 zilizosalia kwenye simu.

Huu pia ni wizi wa mchana na unaofanywa kwa makusudi na kampuni za simu hapa nchini. Ninao ushahidi usiokuwa na mashaka katika huu wizi wa makusudi.

Njia nyingine inayotumika kuiba hapa ni kutotoa call details pindi upigapo simu. Ukimaliza kupiga simu ukiangalia call details unakuta inasoma 00:00:00! Details hizi zinafichwa kwa makusudi ili kujenga mazingira ya wizi.

Kwa mfano mtu unaongea kwa dakika 3, wao wanakata dakika 4.30 na kukuibia dakika 1.30! Matokeo yake unakuta muda wa hewani uliopewa wakati wa kujiunga umeibiwa na kampuni kwa maslahi yake binafsi. Lakini pia kuna wizi mwingine huu hapa: –

unaponunua kifurushi hupewa dakika ambazo ungetegemea zitozwe kwa sekunde (per second billing) lakini badala yake hutozwa kwa dakika (per minute billing) kinyume cha mkataba kwa lengo la kumkamua mteja kiujanja. Huu ni wizi na haukubaliki hata kidogo.

Kuvuruga mawasiliano kwa makusudi.

Kuna wakati wahandisi wa kampuni husika hupewa jukumu la kuvuruga mawasiliano ya wateja ili watumie muda mwingi na pesa nyingi kwenye maongezi. Inakuwaje hapa? Inakuwa hivi: Ukimpigia mtu yeye anakuwa anakusikia lakini wewe humsikii au vice versa.

Hii husababisha kutumia muda mwingi kuelewana wakati huo salio likinyonywa kama kawaida – hata kama mkichukua muda mwingi kuelewana salio hutafunwa sawia! Njia nyingine inayotumika hapa ni kuvuruga access to customer care ili unapokuwa umepatwa na tatizo usiweze kuwafikia watu wa huduma kwa wateja kupata msaada.

Hii ndio sababu 90% ya wateja wenye matatizo genuine hawaipati namba 100. Mtu unaweza kupiga siku nzima na usiunganishwe kuongea na mshauri. Hatimaye wengi wao hukata tamaa na kuamua kukubali "kuliwa"!

Hii ni sehemu ya ushahidi ambao nimeukusanya while working with different mobile companies in Tanzania. Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

Nawasilisha.
Tpaulo@ mimi najua kuwa wewe ulifurushwa kazini ila huku Jf unadanganya ! Yafaa nini?
 
Tpaulo@ mimi najua kuwa wewe ulifurushwa kazini ila huku Jf unadanganya ! Yafaa nini?
1. kufurushwa kazini kuna uhusiano gani na hoja inayohusu wizi wa kampuni za simu?
2. Kama nasema uongo nipinge kwa hoja sio kwa porojo. Hoja haipigwi rungu bali hupingwa kwa hoja iliyo bora/kweli zaidi (JK, 2020)
 
Back
Top Bottom