Wakuu wizi mwingine huu hapa:
Rais Magufuli nakuomba uwashughulikie wahujumu uchumi hawa hapa!
Wakati kesi inayowakabili mabosi wa Haloteli kwa kutakatisha fedha na kuhujumu uchumi ikiwa haijafika tamati, kampuni hii ya simu imeanza tena wizi na utapeli kwa wateja wake. Nasema hili kwa kuwa mimi ni mteja wao na nina kipande cha ushahidi (a piece of evidence) na maelezo ya kutosha kuthibitisha haya ninayoyasema.
Mimi ninatumia data za Halotel kwenye modemu kwa takribani miaka mitano sasa. Hili neno “takribani|” naomba ulibold na kupigia mstari kwa kuwa hapa ndipo wizi wa Haloteli unapoanzia. Wakati naanza kutumia data za haloteli, mara kwa mara nilikuwa naambiwa kisi cha MB zilizobaki na muda zitakapoisha. Nilikuwa natumia meseji za kunikumbusha, hasa bando inapokaribia kuisha. Baada ya kuanza mchakato na hatimaye utekelezaji wa wizi wa bando za wateja, siku hizi hawatumi meseji tena. Wanachofanya ni kutuma meseji moja tu yenye utata na wizi ndani yake kama inavyoonekana hapo chini:
View attachment 1588254
Mtu mwenye akili timilifu ukisoma hii meseji unaona kabisa ina wizi ndani yake kwa 100%. Kwanza imeandikwa kwa mafumbo na haionyeshi uhalisia wowote wa data zilizotumika na jinsi matumizi hayo yalivyofanyika. Twende taratibu. Mimi huwa nanunua bando ya Tsh 1500 yenye ujazo wa 1524 MB. Sasa tuje kwenye hiyo percentage yao. 90% ya 1524 MB = 1371.6 MB. Hii ina maana kuwa baada ya kutumia 1371.6 (90%) ya data kiasi kinachobaki ni 1524 - 1371.6 = 152.4 MB. Sasa tazama upya meseji yao kwennye kielelezo hapo juu. Kiasi cha data kinachotakiwa kubaki baada ya kutumia 90% ni 152.4 MB lakini wao wanasema ni 45 MB! Wezi wakubwa! Hapa wananipiga 152.4 MB - 45MB = 107.4 MB kwa mkupuo mmoja! Ina maana nikinunua bando ya Tsh 15000, kwa mfano, napigwa 10.74 GB. Huu ni wizi mchana kweupe pee!
Na kibaya zaidi, hii meseji inatumwa mwishoni kabisa. Kama sio wezi kwanini wasitume meseji kila ninapotumia labda 100 MB, kwa mfano? Na kwanini saliola data kwa mfumo wa asilimia? Je, ni wananchi wangapi wanaoweza kukokotoa hiyo asilimia? Kwa ujumla hawa jamaa ni wahuni, matapeli, na wezi wakubwa!
Aidha, kwenye meseji yao wanasema nimetumia takribani 90% ya kifurushi. Maana yake ni kuwa hata wao wenyewe hawana uhakika na kifurushi kilichobaki. Kama hawana uhakika mimi nitawaaminije? Hii ni sawa na kumpa shetani amlee mwanao. Ujanjaujanja na wizi wa aina hii haukubaliki hata kidogo hapa nchini Tanzania. Ikiwa sisi wananchi tunaibiwa kiasi hiki, je TRA wanaibiwa mapato kiasi gani?
Natoa wito kwa serikali, kupitia
TCRA na TRA kuwachunguza Halotel ili kubaini kiasi cha fedha walizoiba tangu waanze wizi huu na kuwaamrisha wazirejeshe hazina pamoja na kuchukuliwa hatua kali za uhujumu uchumi haraka iwezekanavyo. Hatuwezi kukubali kuwafuga wezi, matapeli, na wahujumu uchumi wakati serikali haina fedha za kuleta maendeleo ya wananchi.
Nawasilisha.