Jinsi counter wa baa alivyoibiwa pesa

Jinsi counter wa baa alivyoibiwa pesa

Una 'save' jina boss? Hapo lazima ulie.

Alitakiwa asave kwa jina lake huyo mmiliki.
Unadhan huyo tapeli alikua hana namba za huyo Boss..? Mtu akitaka kukupiga tukio anafanya research ya kutosha... Hata ungesevu kwa jina la ubatizo, yeye angeingiza namba za huyo boss kujua ameseviwa vipi... All in all ukiona mtu katapeliwa sio kwamba hana akili bali kazidiwa mbinu...
 
Ina maana huyo counter halijui jina halisi la bosi wake? Maana najua mawakala wengi umuuliza mteja jina linalotokea ndio alilokusudia kumtumia hizo pesa.
Muwe mnasoma habari nzima!!hayo ndio matatizo ya kusoma nusu nusu!!ameshakwambia kuwa huyo tapeli alimwambia tuma kwenye namba ....(ambayo ni nyingine)., ili awanunulie vinywaji kwa bei rahisi, wewe unauliza tena eti jina la boss?
 
Muwe mnasoma habari nzima!!hayo ndio matatizo ya kusoma nusu nusu!!ameshakwambia kuwa huyo tapeli alimwambia tuma kwenye namba ....(ambayo ni nyingine)., ili awanunulie vinywaji kwa bei rahisi, wewe unauliza tena eti jina la boss?
Wewe umeikuta story ameshai edit na mwenyewe amekiri usikosoe tu kitu ambacho huna uhakika nacho.
 
Manzi angu alitapeliwa ..siku hio nashangaa binti analia jioni shida nini mama,🤔 Hadi makamasi yanamtoka Kama kafiwa dhuu


Aliomba kazi sehemu wanauza simu hapo hapo ni wakala wa huduma za kifedha ikumbukwe alikuwa likizo Sasa kukaa home sio ishu akaamua jiongeza maana alikuwa anakaa kwa ndugu zake

Siku moja kazini kwake akaja mtu anataka fedha atumiwe sijui ilikuaje jamaa akasema hajaona na salio kwake hamna ikabdi jamaa apige simu huduma kwa wateja kumbe kampigia mwenzake wakaongea wee badae akamwambia embu mpe huyo dada ( wakala simu) .akapewa simu akapewa maelekezo kuwa bonyeza namba flani na flani kwanza akamuuliza salio Kuna sh ngap wakala akajibu laki 9 na point ..ebwana ee kufumba kufungua salio hakuna lote Yani ..badae ndo anagundua
 
Alienda mtu kunywa pombe ikumbukwe sio mteja wa pale hafahamiki. Akiendelea kunywa akaanza kumuomba counter amuazime simu ili mpigie mtu amletee hela aendelee kunywa mdada wa counter katika utetezi wake anadai Mara ya kwanza alimnyima kwa madai simu haina salio jamaa akaendelea kusihi apewe tu amtumie meseji.

Haifahamiki Kama ni uchawi ulitumika au sayansi ya kumnyenga mtu kwa kumpa offer za bia ila dakika ya mwisho dada alimpatia simu na jamaa bila kupoteza muda akabadilisha namba ya simu iliyoandika the boss yeye akaeidit ikawa namba yake za boss Tena zilikuwa Kama tatu akazibadilisha zote akamrudishia simu.wakaendelea kumwagilia moyo.

Asubuhi kufika meseji inaingia ikimtaka amwambie mauzo ya Jana kapata shingapi dada akastaajabu kwanini Leo iwe hivi wakati boss hanaga kawaida ya kuulizia mahesabu huwa anakuja mwenyewe kuyafuatilia Basi kwa kuwa boss ni boss akaambiwa ipo kiasi fulani laki tano..jamaa(boss) akamuamrisha aende kwa wakali atume fasta pesa kwenye namba fulani nyingine 07******** jina litakuja fulani fulani ili anunue vinywaji kwa Bei rahisi kwani Kuna mtu anataka afunge bar yake pesa ikatumwa maelezo baadae yanakuja kuwa mengi Ila ndo tayari kesi ya utapeli imeshatokea.

Wale wenye biashara waambieni wanaowauzia wawe makini kuzoeana na mtu haraka maisha ya Sasa sio ya kumsaidia mtu simu yako usimuazime kabisa usije kupata shida ya matukio ya kihalifu.
Sishangai hakika visa hivi vipo sana
 
Alienda mtu kunywa pombe ikumbukwe sio mteja wa pale hafahamiki. Akiendelea kunywa akaanza kumuomba counter amuazime simu ili mpigie mtu amletee hela aendelee kunywa mdada wa counter katika utetezi wake anadai Mara ya kwanza alimnyima kwa madai simu haina salio jamaa akaendelea kusihi apewe tu amtumie meseji.

Haifahamiki Kama ni uchawi ulitumika au sayansi ya kumnyenga mtu kwa kumpa offer za bia ila dakika ya mwisho dada alimpatia simu na jamaa bila kupoteza muda akabadilisha namba ya simu iliyoandika the boss yeye akaeidit ikawa namba yake za boss Tena zilikuwa Kama tatu akazibadilisha zote akamrudishia simu.wakaendelea kumwagilia moyo.

Asubuhi kufika meseji inaingia ikimtaka amwambie mauzo ya Jana kapata shingapi dada akastaajabu kwanini Leo iwe hivi wakati boss hanaga kawaida ya kuulizia mahesabu huwa anakuja mwenyewe kuyafuatilia Basi kwa kuwa boss ni boss akaambiwa ipo kiasi fulani laki tano..jamaa(boss) akamuamrisha aende kwa wakali atume fasta pesa kwenye namba fulani nyingine 07******** jina litakuja fulani fulani ili anunue vinywaji kwa Bei rahisi kwani Kuna mtu anataka afunge bar yake pesa ikatumwa maelezo baadae yanakuja kuwa mengi Ila ndo tayari kesi ya utapeli imeshatokea.

Wale wenye biashara waambieni wanaowauzia wawe makini kuzoeana na mtu haraka maisha ya Sasa sio ya kumsaidia mtu simu yako usimuazime kabisa usije kupata shida ya matukio ya kihalifu.
Mtuhumiwa mbona napatikana tuu ,kama katumiwa kupitia miamala ,waende kwenye ofisi za kampuni ya mtandao husika...wanampata.
 
Kuna namba za watu wa karibu sana ambao nikiwagusa tu kwa msg huwa wanatuma hela bila kupiga simu, watu hao huwa sisevu namba zao. Mfano kaka, mama, dada, madogo nk.
Na wao wakigusa tu kwangu kwa msg, nitafanya jitihada hadi nitume.
 
Hamna muhudumu wa bar anayelipwa mshahara wa 250,000.
Counter huyo analipwa 250000 Mimi sisemi uwongo...stori yote nimeipata hivyo akawa anaomba akatwe 200000 abakishiwe 50000 kila mwezi nyingine atadanga kwa ma sponsor itajazwa...hio NI bar kubwa japo najua wahudumu wengi huwa 70000-150000
 
Mdada anamwambia boss amkate 200000 kila mwezi ambakishie 50000 Sasa sijajua itaishiaje hi kesi maana kesho wote na wahudumu wengine wanaitwa polisi wakatoe maelezo...ndo hapo nikapata nafasi pia ya kujua mshahara wa counter kumbe NI laki mbili na nusu
..me Nilikuwa najuaga labda laki moja tu
Hapa umetutia Kamba. Aina ya huo utapeli inaweza ikawa kweli upo, ila kusema Counter wa Bar au Muhudumu wa Bar analipwa laki mbili na nusu(250,000/=) huo ni uongo.

Kumbuka vinywaji kama bia, soda, some spirit vina faida ndogo sana. Sasa Boss anatoa wapi jeuri ya kulipa 250k kwa mwezi. Na hapo bado kodi ya jengi au frame hajalipa, umeme kwakuwa mafriji yanakula umeme unamuhusu na vitu vinginevingine.
 
Back
Top Bottom