Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Karibuni Pasaka ndo inaanza hivi
 

Attachments

  • IMG_6409.jpeg
    IMG_6409.jpeg
    1.7 MB · Views: 23
SEASON 02:
A TRUE STORY BY INSIDER MAN

CHAPTER 01:

CONTINUE ……….
Simu yangu ilianza kuita pale na alikuwa ni Mama J akipiga na nilitabasamu kuona simu yake na niliipokea.

MIMI: “Baby nakuja kukuchukua turudi home na tukapate dinner ya pamoja.”

MAMA J: “Mbona ghafla sana na hujanipa taarifa mapema? na vipi kuhusu Junior atakaa na nani?”

MIMI: “Hutakiwi kuyakimbia matatizo inatakiwa ujue namna ya kuyakabili, siku kama bibi yake hayupo utafanyaje?.”

MAMA J: “Si unajua kesho natakiwa kureport chuo?“

MIMI: “Tutaongea haya” na nikakata simu.

Muda huu nilikuwa nawaza vitu vingi sana kichwani pale parking, ukweli moyo wangu ulianza kuumia kuona Iryn ananiacha na niliingiwa na wivu mkubwa sana juu yake, yaani nilitamani sana aendelee kubaki Dar. Nilikuwa siamini kama kweli Iryn anaondoka na ananiacha, nilihisi kama ndoto.

Wakati niko kwenye dimbwi la mawazo ujumbe uliingia kwenye simu yangu na ulitoka CRDB Bank ukionesha kiasi cha pesa kimeingizwa kwenye account yangu. Ni Iryn alikuwa kafanya muhamala, nilitabasamu na niliwasha gari nikaondoka kwa fujo sana pale JNIA.

Niliendesha gari kwa kasi sana barabarani kuelekea Boko kwa mama J, sasa wakati niko mwenge mataa, simu yangu ilianza kuita na ilikuwa ni namba mpya lakini haikuonekana kuwa ngeni kwangu na sikutaka kujiuliza sana na nikapokea simu.

“Hi Insider”

“Prisca”?

“Yes ni mimi, usinambie ushafuta namba yangu.”

“Hapana, nakusikiliza unashida gani?”

“Insider naomba kuonana na wewe please! please!.”

“Kuna nini Prisca, huwezi ongea kwa simu?”

“Ndio, ndomana nikaomba tuonane nakuomba sana.”

“Ok, nitakujulisha when and where.”

“Thank you, msalimie Junior.”

“Sawa zitafika usijali.”

Baada ya kuzungumza na Prisca nilijua fika huyu anaomba appointment na mimi lakini lazima litakuwa suala la mahusiano wala sio jambo lingine. Kwa upande wangu nilijisemea msimamo wangu utabaki ni uleule sitaki kujihusisha naye tena kwenye mahusiano ya aina yoyote ile.

Saa 1 usiku nilikuwa nimewasili pale ukweni na nilifungua gate nikaingiza gari ndani na bahati nzuri Junior alikuwa kibarazani anacheza peke yake. Baada ya kushuka kwa gari nilikwenda moja kwa moja nikambeba na yeye aliishia kufurahi na tukazunguka upande wa mbele.

Upande wa mbele kulikuwa na shemeji zangu wawili (Dada yake wife pamoja na mamdogo wake) wanakaanga maandazi. Ilikuwa ni muda sana toka tuonane na dada yake hata yeye alivyoniona aliishia kutabasamu, niliwasalimia wote na nilichukua andazi moja nikaanza kulila taratibu.

SHEM: ”Shem karibu…”

MIMI: “ Leo kama zari nimekuotea maana ni kitambo hatuonani.”

SHEM: ”Nipo sema tunapishana, naona unazidi kunawiri nipe siri ya mafanikio shem.”

MIMI: “Siri ya mafanikio muulize mdogo wako atakwambia.”

Na muda huu mama J alikuwa katoka nje,

SHEM: “Haya bhana karibu ndani shem, usiishie nje.”

MIMI: “Hapahapa nje panatosha tuendelee kupiga story, kwanza sikai sana maana nimekuja kuwabeba hawa warudi kwao.”

SHEM: “Mbona haraka hivyo na huyu mtoto mtafanyaje?”

MIMI: “Shem wewe usiwe na wasiwasi mama J anajua kila kitu.”

MAMA J: “Kwani ndo tunaondoka sahivi?”

MIMI: “Nimekwambia muda sana niko njiani ila hujawahi kuwa serious, anza kutoa vitu mimi nikusaidie kupeleka kwa gari tuondoke.”

SHEM: “Shem uko moto sana sijakuzoea hivi.”

MIMI: “Hahahaa sitaki wenye nyumba wanikute na hii ndo mida yao ndomana unaona niko moto, kwanza unakuja lini kwetu?”

SHEM: “Nitakuja shem kuwasalimia niyaone na makazi mapya.”

Tuliendelea kupiga story mbalimbali pale na utani mwingi mpaka mama J alivyomaliza kutoa vitu vyote na kuweka kwa gari ndo nikawaaga pale na sisi tukaondoka.

Wakati tumeingia kwa gari Mama J alianza kuniangalia sana na alionesha mtu ambaye anakitu cha kuongea na alikuwa anatabasamu, kwa upande wangu sikuwa hata nataka kumwangalia kabisa na yeye alianza kuongea,

WIFE: “Bae mke mwenza ameshaondoka tayari?”

Nilishtuka kusikia wife akiongea haya maneno ilibidi nimwangalie muda huu,

MIMI: “Mke mwenza kivipi? Sio bossy wangu tena?”

WIFE: “Hujanijibu swali kaondoka?”

MIMI: “Mama J maswali yako sometimes kama mtoto hata Junior atakuja kukuzidi, angekuwa hajaondoka ungeniona hapa? ndio ameondoka si alikuaga lakini?.”

WIFE: “Ndio aliniaga ndo kakuachia na gari?”

MIMI: “Hapana gari ya mama yake hii nitairudisha.”

Muda huu niliwasha gari na tukaanza safari,

WIFE: “Sawa na huyu Junior tunamfanyaje?”

MIMI:?“Junior asikupe shida twende kwanza sehemu tukae then tuanze maongezi.”

Niliendesha gari mpaka Whitesands hotel na tukaenda moja kwa moja mpaka restaurant kwaajili ya kupata Dinner, tuliagiza chakula na maongezi yakaendelea.

Tuliongea mambo mengi sana na kubwa nilimwambia sitaki kuona anakwenda kwao hovyohovyo bila sababu ya msingi maana haileti picha nzuri. Na kuhusu mtoto tulikubaliana nitakuwa ninakwenda naye kazini huku tukiendelea kufanya mawasiliano na Elena. Tulikubaliana kama Elena atarudi itabidi tuangalie namna ya kumpeleka shule hata akasomee fani yoyote ili iwe kama shukrani yetu kwake.

Hatukutumia muda mwingi sana hivyo tuliamua kuondoka kurudi home kulala na baada ya kuwasili home Asmah alinipigia simu kunijulia hali na nilimwambia itabidi tukae kikao next saturday na team kutoka salon zote. Baada ya kuzungumza na Asmah nilimtafuta Iryn ili kujua kama amefika salama lakini hakuwa online, hivyo nikajisemea atanitafuta akiwa online na mimi nikalala.

Jumanne tulikuwa tumeanza mwezi novemba ile asubuhi kama kawaida mapema niliamka na nilikwenda tizi baada ya kurudi nilikuta mam J akimwandaa mtoto ili tuondoke maana yeye alikuwa anakwenda chuo. Baada ya kupata breakfast tuliondoka na safari ilikuwa kumpeleka kwanza Mama J chuo na baada ya kumdrop mimi na Junior tuliamua kwenda ofisini Mikocheni.

Ndani ya dakika chache tulikuwa tumewasili pale ofisini na nilikwenda ndani kuendelea na ratiba zangu. Muda huu nilijikuta nam-miss Iryn hivyo nilitoa simu mfukoni nikampigia lakini hakuwa online. Nilianza kupatwa na wasiwasi why toka aondoke jana hajanitafuta wala kunipa taarifa yoyote? What’s really going on? na nikamtumia ujumbe ukisomeka,

"Hey baby, just wanted to check in and see how your journey to South Africa is going. I have been thinking about you and hope everything is going well. Let me know when you have a chance. Miss you!"

Haikuchukua muda Lucy akaingia ofisini na baada ya kumuona Junior aliishia kufurahi na alimbeba.

LUCY: “Insider mambo umekuja na mchumba wangu leo.”

MIMI: “Fresh tu, sikujua kama utakuwepo hapa nilijua utakuwa chuo.”

LUCY: “Nishakamilisha taratibu zote nasubiri timetable tu na lecture zianze kuchanganya.”

MIMI: “Vizuri, this weekend tutakuwa na kikao sijui unaratiba?”

LUCY: “Ndo unaniambia hapa now but haina shida na kitafanyikia wapi?”

MIMI: “Asmah atakucheki juu ya hili mtapanga nyie.”

LUCY: “Siamini Iryn kama kweli kaondoka.”

MIMI: “Bado unaota sindio?

LUCY: “No nakuonea huruma wewe utakuwa lonely.”

Ilibidi nicheke afu nikanyamaza na nikapotezea hii mada maana Lucy alianza kuvuka redline

MIMI: “Lucy chuo utakuwa unakwenda muda gani?”

LUCY: “Jioni saa 11, hakuna kitakachokuwa kinaharibika bossy.”

MIMI: “Sawa nakubali manager wangu.”

Hii siku nilishinda pale Mikocheni kwa upande wa Junior aliishia kuzurura mle ndani na nje na uzuri alikuwa anacheza na dada zake hivyo ilikuwa burudani maana walitokea kumpenda.

Mchana Iryn alinipigia simu kupitia whatsapp video na tuliongea kwa muda mrefu sana, kubwa aliniahidi mwezi huu mwishoni atakuja Dar kwa ajili yangu maana hawezi kukaa muda mrefu bila kuniona. Tuliongea mambo mengi sana likiwemo suala la yeye kuanza clinic pamoja na kuwapa taarifa wazazi wake kuhusu suala hili la mimba.

Baada ya kuongea na Iryn sikutaka kuendelea kupoteza muda pale ofisini, hivyo nilimuaga Lucy na sisi tuliondoka kwenda Mlimani city kupoteza muda huku tukiendelea kumsubiri mama yake atoke chuo. Junior hakuwa msumbufu kabisa kwanza ndo alikuwa anaona raha kuzurura na baba yake, haya mambo yeye ndo anatakaga unaweza kaa naye siku nzima na huwezi msikia akiulizia mama wala kulia.

Usiku mida ya saa mbili Hilda alinipigia simu na muda huu nilikuwa nimekaa nje kibarazani na nilivyoiona simu yake nilishangaa sana maana ndo ilikuwa mara yake ya kwanza ananipigia simu usiku. Nilihisi atakuwa na shida hivyo niliipokea simu yake,

MIMI: “Hi Hilda za wewe.”

HILDA: “Safi Bossy, umepotea sana.”

MIMI: “Hapana nipo something wrong?”

HILDA: “Hapana nikasema nikusalimie pia nashukuru kwa kunichagua kuwa moja wa ambao tutapewa mafunzo.”

MIMI: “Usijali dear, tuko pamoja bado unakaa na Asmah?”

HILDA: “Ndio but nishapata kwangu tayari.”

MIMI: “Ooh hongera sana, umepata wapi?”

HILDA: “Morocco hapo by next week nitahamia.”

Baada ya kuona hana jambo la muhimu niliamua kukatisha maongezi,

MIMI: “Hongera sana kesho tutaongea vizuri, bye uwe na usiku mwema.”

Niliamua kukatisha maongezi maana muda ulikuwa ni usiku japo alionekana kuwa na maongezi zaidi na mimi.
*****
Asubuhi nilikwenda ofisini Masaki nikiwa na Junior kama kawaida na baada ya kufika pale ofisini team ilikuwa imewasili na baadhi walioniona waliishia kushangaa sana kuniona na mtoto. Kwa upande mwingine Hilda alikuwa pale reception na tukaanza story hata yeye alishangaa sana kuniona na mtoto uvumilivu ulimshinda ilibidi aniulize,

HILDA: “Bossy huyu ni mwanao? yaani mmefanana balaa huwezi kubisha hili.”

MIMI: “Hahaha mwanangu ndio, Junior kamsalimie mamdogo.”

HILDA: “Hongera sana so HB.”

MIMI: “Asmah kafika?”

HILDA: “Yeah yuko ndani.”

MIMI: “Sawa ngoja nikamuone afu nitarudi, pia jana kuna jambo ulitaka kuongea dizaini kama ulikuwa unaogopa kusema, leo utasema.”

HILDA: “Hahahaha sawa wewe nenda kwanza ukirudi tutaongea, utanikuta na dogo hapa.”

MIMI: “Angalia ni mtundu sana huyu, hachelewi kuchafua hali ya hewa.”

HILDA: “Nitam-mudu.”

Niliingia ndani na nilimkuta Asmah akionekana kuwa busy sana na baada ya kuniona alikunja laptop yake na tukasalimiana, nikakaa kwenye coach. Haikuchukua muda Asmah naye akaja akakaa kwenye coach na tukaanza story pale.

MIMI: “Nambie Bossy wangu.”

ASMAH: “Safi nimefurahi kukuona Insider, Iryn mzima?

MIMI: “Acha unafiki unataka kusema hajawasiliama na Iryn?”

ASMAH: “I did.”

MIMI: “So unanichora tu hapa. Aya niambie kikao cha weekend umepanga kifanyike lini? na wapi?”

ASMAH: “Siku iwe jumamosi ila place bado sija confirm but soon nitakupa update.”

MIMI: “Sawa mummy, nilitamani sana leo kuja kulala na wewe sema unaishi na Hilda.”

ASMAH: “Wewe Insider? akili yako iko sawa kweli?”

MIMI: “Kinachofanya uone akili yangu haiko sawa ni nini?”

ASMAH: “Insider yaani navyokuogopa kwasasa hivi naanzaje kulala na wewe?”

MIMI: “Ooh vizuri kama kweli umeanza kuniogopa na bado utaendelea kuniogopa zaidi, ngoja niwasalimie akina Rebby.”

Nilianza kuondoka pale na nilisikia akiniita

ASMAH: “Insider….umechukia?”

Nilitabasamu nikamkonyeza na nikafungua mlango nikatoka kwenda reception kwa Hilda lakini sikumkuta na niliamua kwenda kuwasalimia akina Rebby na niliwakuta wanacheza na Junior.

MIMI: “Hilda nilikuwa nakutafuta wewe kumbe umekuja huku.”

HILDA: “Mwanao ni mtundu sana hataki kushikwa kumuachia kaja huku.”

REBBY: “Insider kuanzia leo mimi nitakuwa mkwe wako, una mtoto mzuri hivi asee.”

MIMI: “Naona unaweka odda mapema ya kuwa lishangazi kwa mwanangu ausio.”

Kila mtu aliishia kucheka baada ya mimi kuongea hivi,

REBBY: “Jamani mbona mapovu?”

MIMI: “Thubutu.”

Nilimuacha Rebby akinisikitikia na niliondoka reception na tuliendelea mazungumzo yetu na Hilda.

MIMI: “Ongea sasa nataka kuondoka kama unaona aibu niandikie text.”

HILDA: “Hamna kuna kitu nilitaka kuomba but naona mapema sana.”

MIMI: “Ongea tu, usiwe na wasiwasi.”

ASMAH: “Nilikuwa nataka kuomba mkopo ili ninunue baadhi ya vitu nikahamie kwangu.”

MIMI: “Uko sahihi ni mapema sana kwakweli, ulitaka mkopo wa kiasi gani?”

HILDA: “Million 1 tu.”

MIMI: “Fanya hivi ongea na Asmah mshikaji wako akudhamini, hili litawezekana. Kama atakubali bhasi utanijulisha sawa?.”

HILDA: “Sawa haina shida nitaongea naye badae.”

MIMI: “Ok see you then.”

Niliondoka na Junior na safari yetu ilikuwa ni kuelekea kwenye apartment ambayo tulikuwa tunakaa na Iryn kabla hajaondoka na nilitakiwa kuikakabidhi apartment. Baada ya kuwasili maeneo yale nilikwenda moja kwa moja ndani na nilifungua makabati ya chumbani na kulikuwa na vitu ambavyo aliviacha kama viatu, nguo skin jeans, mikoba handbags na vitu vingine kibao.

Wakati nikiendelea kumsubiri Dalali kwa upande mwingine simu yangu ilianza kuita na ile kucheki ni mama Janeth alikuwa akinipigia simu. Nilipokea na tuliongea mambo mengi sana pamoja na utani mwingi, dizaini kama alikuwa anajua mimi ni mkwe wake tayari. Mama alinambia tuonane badae kuna mambo anataka tukazungumze nikiwa pamoja na Asmah.

Baada ya kuongea na Mama Janeth nilimpigia video call Iryn na uzuri alikuwa online na alipokea kwa haraka sana,

“Hi baba mtoto, I was thinking about you.”

“Unaendeleaje na mwanangu?”

“We good, nakuona upo na mwanangu Junior na nishaanza kuwa-miss”

“We miss you too, niko hapa kwa apartment naona kuna vitu ulisahau nikuwekee au?”

“No afu nilisahau kukwambia, hivyo viatu baadhi utampa Sumaiya, hizo skin mpe Hilda na Jack niliwapa ahadi, hizo handbags juu yako kama utampelekea mke mwenza au utazigawa.”

“Sawa baby.”

“Okay darling bye.”

Baada ya kuagana na Iryn kwa upande mwingine Dalali alikuwa kafika tayari hivyo tulifanya makabidhiano ya apartment na tukaagana pale na sisi tukaanza safari ya kurudi home.

Niliwasili home mapema sana na nilikuwa nimekaa kibarazani na muda huu nilikuwa nawaza namna ya kuzitumia pesa alizonipa Iryn. Nilikuwa nahitaji umakini wa hali ya juu sana kwenye hili jambo, niliwaza kumpa mtaji mama J kwenye biashara yake ya M-pesa na Tigopesa ili aanze kufanya na miamala ya Bank. Pia nilipata wazo kabla sijafanya haya maamuzi lazima kwanza nijue mipango yake ili nione kama naweza mpa pesa au laah.

Niliingia jikoni kwaajili ya kupika chakula cha mtoto pamoja na cha kwetu maana wife alikuwa hajarudi bado. Kwa upande mwingine Junior alikuwa nje anacheza na mtoto wa jirani yetu ni wa kike na mkubwa kidogo kwa Junior.

Saa moja usiku ndo muda ambao tulikwenda kwa mama Janeth pamoja na Asmah kuitikia wito. Baada ya kuwasili kwake tulikaribishwa ndani lakini tulikuta mama ana wageni hivyo ilitubidi tumsubiri kwa pale nje kibarazani mpaka amalize. Mimi sikuwa na story kabisa na Asmah muda huu na yeye alianzisha story,

ASMAH: “Insider are you okay?”

INSIDER: “Yeah kuna tatizo?”

ASMAH: “Seem hauko sawa, sorry kama nilikukwaza ile asubuhi ulikuwa utani tu.”

INSIDER: “Wasiwasi wako tu, mimi niko sawa.”

Akanisogelea karibu,

ASMAH: “Insider bado una deni kwangu.”

INSIDER: “Deni gani tena?”

ASMAH: “Kutoka out bado sijasahau ile siku uliyonizingua.”

INSIDER: “Hahahaa unawezaje kutoka out na mtu unayemwogopa?”

Maongezi yetu yalikatishwa baada ya mama Janeth kutokea,

“Wanangu poleni nafikiri tukae hapa wote na mazungumzo yetu tufanyie hapa au mnaonaje mtakuwa comfortable?”

“Hakuna shida mama hapa pametulia sana.”

Tulianza maongezi yetu pale kuhusu kuongeza mishahara kama alivyoahidi pamoja na suala la mafunzo. Mama alisema mtu atakayetoa mafunzo anatarajia kuwasili Dar jumapili hii na mafunzo yataanza jumatatu as planned.

Tuliongea masuala mengine mengine kuhusu kampuni pamoja na safari zake anazotarajia kuzianza soon za kwenda huko Ukraine na US. Kwa upande wake alisema atakuwa busy sana hivyo anatutegemea sana kwenye kusimamia hii kampuni.

Nilimwambia mama nimeleta na gari yake ambayo niliachiwa na Iryn lakini mama alisema ile gari sio yake bali yeye alimkabidhi Iryn kuwa mali yake hivyo niendelee kuitumia.

MAMA: “Mwanangu hio gari mimi nilimpa Iryn kuwa na amani endelea kuitumia nafikiri hata yeye anapenda ukiendelea kuitumia.”

MIMI: “Mhh hapana mama hakuwahi nambia hili, hii gari kwangu ni gharama siwezi kuimudu naomba niiache hapa.”

MAMA: “Kama ni gharama za mafuta hili ondoa shaka, sipendi haya magari yaendelee kukaa hapa yanaharibika bila sababu ndomana niliamua kumpa hio gari Iryn.”

MIMI: “Sawa mama nimekuelewa kama ni hivyo basi nitakuwa nakuja kuichukua mara moja moja lakini sio kukaa nayo, hapa kwako usalama upo.”

MAMA: “Nitaongea na Iryn akiridhia sawa ila kwasasa endelea kuitumia.”

Tuliagana na mama Janeth pale kwake na sisi tukaondoka na wakati tunatoka Asmah alisema tukapate dinner ya pamoja na atalipia.

MIMI: “Muda umekwenda Asmah tutatoka next time.”

ASMAH: “Unanipa lift mpaka home au niliquest uber?”

MIMI: “Fanya kurequest nataka niwahi home leo nimechoka sana.”

Japo alionesha kutofurahishwa na majibu yangu lakini sikuwa na jinsi. Nilipark gari pembeni tukiendelea na story na yeye alikuwa akisubiri usafiri.

ASMAH: “Insider una bahati sana yaani mpaka unalazimishwa kubaki na gari, mbona hii nyota wengine hatuna.?”

INSIDER: “Unataka kuwa na nyota ya aina gani? na huu uzuri wote ulionao huoni kama Mungu alikupendelea?”

Asmah ilibidi acheke maana hakutegemea kama ningempa jibu la namna hii,

ASMAH: “Kama mimi ni mzuri na Iryn aseme nini?”

INSIDER: “Seems hujiamini na hujikubali, ngoja leo nikwambie ukweli Asmah. Ukianza kujikubali hutakuwa unalalamika kwangu hutongozwi, sometimes unajiweka local sana mpaka uzuri na thamani yako inapotea. Embu mcheki mtoto Hilda anavyotupia viskin jeans na zinavyomkaa, mtoto kiuno huko, inshort anajipenda.”

Asmah alikuwa kimya kwa muda ni kama nilikuwa nimemchana ukweli, na dizanini alianza kuwa na aibu.

ASMAH: “Ushaanza kumtamani Hilda?”

INSIDER: “Nimekupa mfano namna anavyojipenda but you can do better than her you’re so beautiful.”

Asmah alinyamaza kimya ni kama alipatwa na aibu ghafla, na muda huu simu yake ilianza kuita na alikuwa ni dereva wa uber, alimuelekeza tulipo na baada ya uber kuwasili tuliagana na mimi nikaondoka kuelekea home.

Wakati niko njiani nilikumbuka suala la Prisca kuomba tuoanane na nikakumbuka kumpigia simu dogo ili anipe report ya upelelezi aliofikia mpaka sasa. Nilifanya mawasiliano na majibu niliyopata ni kwamba kwasasa hakuna taarifa yoyote maana vyuo vilikuwa vimefungwa na hajamuona Prisca kwa muda sana maeneo ya kule. Nilimsisitiza dogo aendelee na uchunguzi wake na pindi atakapopata taarifa mpya bhasi anijulishe na nilimwambia nitamtumia muamala sio muda mrefu.

*********
Jumamosi ya week ya kwanza ya mwezi November ilikuwa ndo siku ya kikao chetu na kubwa ilikuwa ni kwaajili ya kupeana majukumu mapya na kutambulishana management mpya ya kampuni.

Niliamka asubuhi na mapema kama kawaida nilikwenda jogging na baada ya kurudi na kujiandaa niliamua kwenda Mbweni kumsalimia Jane. Baada ya kuwasili pale home nilimkuta Jane na mama yake wako seblen na wageni. Niliwasalimia na mimi nilitoka nje kwenda kuangalia maendeleo ya mbwa wangu na walionekana kukua kwa kasi sana.

Baada ya dakika 10 nilisikia Jane akiniita na aliomba tukae garden ili tuongee, Jane akiniona huwa anafurahi sana na mimi kama kawaida yangu matani huwa siachi.

“Nakuona shem wangu unazidi kuwa mzuri.”

“Hahaha jamani huoni nilivyojichokea hapa shem.”

“Naona mambo si muda mrefu yatakuwa hadharani, na wanasemaje maendeleo.?”

“Yaani doctor anasema muda wowote tu naweza kushusha, nikianza kusikia dalili niwahi kwenda hospital.”

“Na wewe unampango wa kujifungulia wapi?”

“Rabininsia palepale naona ni pazuri.”

“Ukianza kuona dalili nijulishe mapema ili nije nikupeleke, sawa shem?”

“Usijali Insider, nashukuru sana kwa kunijali najua huyu mtoto atakupenda sana.”

“Hilo halina ubishi, mimi nilikuja kukujulia hali, pia nimekuja na vyakula vya mbwa na kama utahitaji kitu kingine nambie nikuletee.”

“Usiwe na wasiwasi kama kuna lolote nitakujulisha shem wangu.”

Niliendelea maongezi na Jane kuhusu masuala mbalimbali ya maisha na yeye alisisitiza sana akijifungua lazima afungue biashara kama tulivyokuwa tumepanga before. Jane alikuwa yuko hoi sana yaani alikuwa ni mtu ambaye anahesabu siku za kujifungua cha ajabu alikuwa anazidi kung’aa.

Niliagana na Jane na mimi niliamua kurudi kwanza home kupumzika na wakati nimefika home nilistaajabu sana kuona pale uwanjani nina park gari 3 (Audi, Dualis na ist). Nikajisemea Jane akijifungua tu nitamkabidhi gari yake na hii audi jumatatu lazima niirudishe kwa mama Janeth.

Wakati bado niko nje kibarazani nikiendelea kuwaza ghafla nilisikia Junior akiniita akitokea kwa jirani na akaja kwangu ameshika remote ya gari yake na alikuwa ananipa huku ananivuta. Mimi nilishamsoma anataka nikamwendeshe na nilikwenda mpaka kwa gari yake nikaanza kumwendesha pale, baada ya dakika kadhaa akaja rafiki yake wa kike naye akakaa pembeni nikaendelea kuwaendesha.

Baada ya muda nilisikia mtu akiniita “Jirani” na ile kugeuka alikuwa ni dada na tukasalimiana pale,

“Jirani habari yako.”

“Salama sana jirani, karibu niko na madogo hapa.”

“Nilikuja kumchukua huyu binti yangu ili akale ila kwasasa hawezi kubali.”

“Hapa itabidi uwe mpole hawezi kukuelewa, hongera una bint mzuri kama wewe.”

“Hahaa ahsante sana jirani hata wewe una kijana mzuri, si unaona bint yangu kila muda anamtaka Junior hahahaa. Toka uhamie hapa nakuonaga kwa mbali pia huonekaniki, karibu sana.”

“Ahsante sana jirani, nimekuwa na mambo mengi sana toka nihamie hapa lakini tuko pamoja, bila shaka mama yake Junior mmeonana.”

“Mama J tunaonana daily maana haipiti siku sijaja kwenu au yeye kuja kwangu kumuilizia mtoto.”

“Binti yako anaitwa nani?”

“Joana”

“Bhasi kuanzia leo nitakuwa nakuita Mama Joana.”

Tulishia kucheka wote pale na kila mmoja aliondoka na mtoto wake kuingia ndani maana nilikuwa nataka nipumzike before ya kwenda kwenye kikao Mikocheni.

Saa 12 jioni niliondoka kuelekea Regency hotel mikocheni kikao chetu ndo kilikuwa kinafanyika pale na nilikuwa nje na muda. Baada ya kuwasili na kuingia ndani, timu yote ilikuwa imewasili tayari nilikuwa ni mimi tu nasubiriwa ili kikao kianze.

Kikao kilianza na ni Asmah aliyeinuka na kuanza kuongea maana yeye alikuwa ndo katibu wa hiki kikao.

“Team habari za jioni kabla ya kuendelea naomba tufungue kikao chetu kwa sala.”

Baada ya sala Asmah aliendelea kuongea,

kama mnavyofahamu leo ndo kikao chetu na Agenda zote za kuhusu hiki kikao zinajulikana, hivyo mimi nitazungumza machache na mengine atazungumza manager wetu.”

Baada ya Asmah kumaliza kuongea alinikaribisha ili niweze kuzungumza na mimi sikutaka kupoteza muda nilianza kuongea.

Team habari yenu, nafurahi kuwaona kwa mara nyingine mkiwa mmependeza sana. Julieth hongera umependeza kushinda wote humu ndani.”

Waliishia kucheka na wote walifurahi baada ya kuongea haya maneno..

Guys sitaki tupoteze muda hapa ila dhumuni kubwa la hiki kikao ni kujadili kuhusu kubadilika kwa uongozi kama mlivyosikia kikao kilichopita bossy wetu Iryn kaenda masomoni, mama yetu pia atakuwa busy sana. Agenda ya pili itakuwa kuzungumzia suala la kuanza kwa mafunzo jumatatu na mafunzo yatakuwa pale kwa mama Janeth kwake hivyo wale mliochaguliwa zingatieni hili. Agenda yetu yetu ya tatu itakuwa ni kuhusu Sacoss yetu pamoja na kutoa maoni, ushauri na mapendekezo mbalimbali kuhusu kampuni yetu.”

Baada ya ukimya kadhaa niliendelea kuongea,

Ninaanza kutaja majina ya viongozi wenu na utaratibu uliotumika, tumezingatia uzoefu pamoja na elimu. Kuanzia leo Asmah ni HR wa kampuni matatizo yote ya kiofisi pamoja na yale binafsi mtakuwa mnamwona yeye na msaidizi wake atakuwa Hilda. Lucy atabaki kuwa manager wa branch ya Mikocheni na msaidizi wake atakuwa Julieth. Mimi Insider nitakuwa top manager hasa kwenye masuala ya fedha na maendeleo yote yanayohusu kampuni kwa ujumla.”

Niliongea masuala mengine mengi sana kuhusu maendeleo ya Saccos yetu bila kusahau mikakati na malengo ya kampuni. Baada ya kumaliza kuongea tulikaribisha maswali, maoni na ushauri na kila mmoja alifunguka kwa upande wake.

JULIETH: “Manager muda wa kumaliza mafunzo ni saa ngapi? na je tutatakiwa kwenda na nini? na kwa mama Janeth tunafikaje maana wengine hatukujui.”

ASMAH: “Muda wa kumaliza mafunzo ni saa 12 jioni na suala la chakula liko chini ya ofisi, pia tunaandaa bajeti ya nauli kwa ajili yenu lakini bado hatujafikia muhafaka na mama, baada ya hiki kikao tutakwenda kujadiliana naye na nitawapa mrejesho.”

MIMI: “Afu kuhusu vitu ya kwenda navyo, msiwe na wasiwasi mtavipata kulekule. Naona tumalize kikao chetu na tusubiri dinna ya pamoja then tutaondoka kurudi makwetu.“

Wakati tukisubiri dinna pale story za hapa na pale zilikuwa zikiendelea pamoja na kupiga picha za pamoja kwa upande mwingine Iryn alikuwa akinipigia sana simu lakini sikutaka kupokea simu zake muda huu maana haikuwa sehemu sahihi ya kufanya maongezi.

Nilianza kupiga story na Hilda pale na mimi kama kawaida yangu nilianza kumzingua.

MIMI: “You look great today kama Kim K.”

HILDA: “Thank you bossy, hata wewe pia.”

MIMI: “Ushahamia kwako? nataka nije nilale kwako.”

HILDA: “Tayari, wewe karibu tu muda wowote.”

MIMI: “Unanihakikishia usalama wangu lakini?”

Hilda alianza kucheka,

HILDA: “Yeah why not?”

Baada ya dakika 10 chakula kilikuwa tayari na baada ya kumaliza kula mimi na Asmah ilibidi tuage team na tuliondoka kwenda kwa mama Masaki.

Ilituchukua muda mfupi sana kuwasili Masaki kwa mama na baada ya kukaribishwa ndani seblen ilimchukua dakika 5 mama kutoka ndani na tukaanza maongezi. Mama alisema trainer atawasili kesho akitokea Canada na mafunzo yatafanyikia palepale kwake floor ya juu ya nyumba yake. Suala lingine tulilojadili ni kuhusu nauli na posho kwa watakao hudhuria hii training na tuliona 50,000/= kwa siku ingependeza zaidi.

Yalikuwa ni mazungumzo ya kama lisaa kasoro na tuliagana na mama pale tukaondoka maeneo yale. Asmah hakuwa na mood ya kurudi home mapema hivyo alianza kunishawishi tutoke out na muda ulikuwa unasoma saa 3 usiku tayari.

ASMAH: “Insider si tunatoka out? Sijisikii kabisa kurudi home mapema hivi.”

INSIDER: “Si kuna Hilda kule home? atajiskiaje ukimwacha alone na umetoka out.”

ASMAH: “Hilda kashahamia kwake toka juzi.”

Wakati nikiendelea kujifikiria hili ukweli sikuwa na mood na mzuka wa kutoka out, na nilikuwa najifikiria kwa hili. Kwa upande wake simu yake ilianza kuita,

“Insider Iryn anapiga simu.”

MIMI: “Pokea ongea naye.”

Na mimi nilihisi tu Iryn anapiga simu kwa Asmah sababu mimi sipokei simu zake na nilimwambia Asmah aweke loudspeaker.

ASMAH: “Hi bossy.”

IRYN: “Fine, za wewe?”

ASMAH: “Safi dear.”

IRYN: “Sound great, upo ofisini?”

ASMAH: “Hapana tumetoka mapema sana leo maana tulikuwa na kikao.”

IRYN: “meeting? mbona sina hizi information?”

ASMAH: “Insider atakuambia nafikiri.”

IRYN: “Okay! na mmeshamaliza kikao chenu?”

ASMAH: “Yeah ni 30mns zimepita na mimi narudi home hapa. Nambie bossy wangu ushaanza masomo?”

IRYN: “Ndio kipenzi nakujulia hali mpenzi.”

ASMAH: “Thank you bossy mimi niko poa.”

Baada ya kumaliza mazungumzo Iryn alikata simu na Asmah alinigeukia akaanza kuongea,

ASMAH: “Insider nipeleke home nikalale.”

MIMI: “Umeghairi kutoka tena?”

ASMAH: “Wewe nipeleke tu sina hamu tena ya kutoka.”

Ilibidi nicheke kinafiki maana simu ya Iryn ni kama ilimpa warning juu ya next move aliyokuwa anaitaka kuifanya.

Tulielekea na usawa wa Toure road mpaka tunafika kwake cha ajabu njiani kila mtu alikuwa kimya na hakuna aliyekuwa anamwongelesha mwenzie. Asmah alishuka kwenye gari akaniaga na mimi nikaondoka kurudi home sikutaka kupoteza muda kabisa na saa yangu ilikuwa inasoma nne kasoro za usiku.

Nilirudi na Mwaikibaki road na baada ya kufika Nakiete pharmacy ilibidi nishuke ili ninue dawa ya mafua kwaajili ya Junior. Wakati niko mle ndani pharmacy simu ilianza kuita na alikuwa ni bossy lady akipiga sababu nilikuwa natoa maelezo kwa doctor sikutaka kuipokea simu yake, nikajisemea huyu nitaongea naye kwenye gari. Simu iliendelea kuita na kukata na aliendelea kupiga kwa fujo sana lakini sikuwa na nguvu ya kupokea simu yake maeneo haya.

Baada ya dakika 3 doctor alirudi na dawa na akawa ananipa maelekezo pale namna ya kutumia dawa kwa mtoto. Wakati natoka mle ndani kwenda parking kwaajili ya kuondoka simu yangu iliita tena na mara hii alikuwa anapiga kwa simu ya kawaida na baada ya kuingia kwa gari niliipokea simu yake.

IRYN: "Darling, why didn't you pick up my phone?"

MIMI: “I'm sorry, I was in a meeting and couldn't answer at the time.”

IRYN: “Why didn't you tell me?”

MIMI: “I apologize for not informing you earlier but everything is going well.”

IRYN: “Whenever I need to talk to you, you don't answer my calls on time. What’s wrong with you?”

Mpaka nafika home alikuwa analalamika sana na mimi niliendelea kumbembeleza na kuwa mpole maana sikupenda awe vile ukizingatia ana ujauzito. Baada ya kufika home nilipark gari pembeni maana sikutaka kuingia ndani ili niendelee kuyajenga na Iryn na tulikuwa tumeanza maongezi mengine.

MIMI: “So, baby mimba inazidi kukua na huwezi kuendelea kuhide ni bora ukawaambia wazee mapema before it’s too late.”

IRYN: “Mama yangu mdogo nimesha mpa taarifa tayari ila mzee bado hajui soon nitaongea naye, but kuna jambo nilitaka kukwambia ila ni busara tuongee tukionana.”

Muda huu simu ya Mary ilianza kuingia na mimi baada ya kuona Mary akipiga nilipoteza kabisa network.

MIMI: “Sawa baby.”

IRYN: “Baby good night see you tomorrow I love you”

Baada ya Iryn kukata simu ndo napata akili na kuanza kujiuliza hivi Iryn amesema kuna jambo la kuongea, hivi kwanini sijamuuliza ni jambo gani?. Nilianza kujilaumu lakini ikabidi niwe mpole na muda huu simu ilianza kuita tena ni Mary alikuwa akipiga. Ukweli niliona aibu hata kuipokea simu yake maana toka aondoke sikuwahi kuongea naye wala kumpigia simu na text zake sikuwa na jibu.

MIMI: “Mary..”

MARY: “Hi Insider, finally leo umepokea simu yangu.”

MIMI: “Nisamehe rafiki yangu, toka uondoke nimekuwa busy sana then nasahau kukurudia, umesharudi tayari?”

MARY: “Yeah nimerudi jana dear.”

MIMI: “Umerudi na zawadi yangu?”

MARY: “Yeah you know I do care about you.”

MIMI: “Thank you ukisema hivyo utafanya nijisikie vibaya mummy.”

MARY: “Kesho unaratiba gani? maana niliwishi sana nikuone maana nimekumiss sana.”

MIMI: “Sure kesho tutaonana usiwe na wasiwasi.”

MARY: “Nimefurahi kusikia hivyo byee Insider kesho tutaongea mengi tukionana. Angalia whatsapp kuna ujumbe wako.”

Baada ya kuagana na Mary na mimi nilifungua haraka whatsapp kuangalia Mary katuma nini?, damn alikuwa kanitumia picha zake akiwa amewaka sana na nikagundua Mary nje na kuwa Kenya pia alikwenda Europe. Niliishia kuziangalia zile picha kwa tamaa za kifisi na nikaingia ndani maana nilikuwa nimekaa pale nje kwa zaidi ya lisaa.

Baada ya kuingia ndani niliingia kuoga kwanza na nilirudi sebleni kuongea na mama J kuhusu suala la dada wa kazi wamefikia wapi? maana alisema kufikia jumatano Elena angekuwa amerudi lakini haikuwa hivyo.

Kutembea na Junior kila angle nilianza kuona ni mtihani maana Junior ni mtundu sana ukizubaa sekunde tu humwoni machoni pako, hivyo alikuwa anahitaji uangalizi wa karibu sana. Na pia sakala la kuanza kwa mafunzo jumatatu nilikuwa nahitajika kuwa karibu sana na mazingira ya ofisini, kuwa na Junior ingekuwa tatizo.

“Baby vipi kuhusu suala la dada umefanikiwa kuwapigia simu?”

“Nimetoka kupiga simu sio muda hapa lakini hazipatikani zote mpaka baba yake.”

“Aisee sasa hii hatari so tunafanyaje? maana kumpeleka shule huyu ni mdogo sana kwa umri wake.”

“Mama ananitafutia dada mwingine so tuwe na subira maana tukiharakisha tunaweza pata dada mbaya ikawa tatizo.”

“Jumatatu nitakuwa busy sana afu siwezi kwenda na Junior na wewe unakwenda chuo.”

“Nitaongea na bibi yake asubuhi nitakuwa nampeleka afu jioni navyotoka chuo nitakuwa napitia kumchukua.”

“Sipendi tumsumbue mama anashinda pia kwenye biashara zake huu mzigo ni wetu.”

“Dada yangu pia yuko home so hakuna tatizo hata yeye alikuwa tayari kukaa naye uzuri Junior sio mtoto wa kulialia.”

“Pia maendeleo ya biashara zako yakoje?”

“Maendeleo mazuri baba J, dogo wa bajaji hana shida kule dukani nako hakuna shida.”

“Una mpango gani na biashara zako

Baada ya kumsikiliza niliona anamipango mizuri sana na nikaona kuna haja ya kumpa pesa ili aongezee na uwakala wa bank hasa CRDB na NMB, japo sikumwambia chochote.

Mama J aliondoka kwenda chumbani na mimi nilibaki pale seblen nikiangalia match ya Barcelona. Baada ya dakika 15 nilisikia mlango ukigongwa na nikasimama kwenda kufungua, nilijua lazima atakuwa jirani. Baada ya kufungua mlango nilipigwa na butwaa kubwa sana na sikuamini nayemuona mbele yangu muda huu,

ITAENDELEA….
 
Back
Top Bottom