Jina halisi la marehemu Eddy Shegy ni nani?

Jina halisi la marehemu Eddy Shegy ni nani?

dafity

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2008
Posts
1,881
Reaction score
2,091
Kuna mtu aliwahi kuniambia Jina lake ni EDWARD SHEKIONDO lakini akalifanyia usanii akajiita EDDY SHEGGY. Namzungumzia kaka wa Christian Sheggy, mwanamuziki wa zamani wa Orchestra Super Rainbow, na Washirika Tanzania Stars (Watunjatanjata). Ameshatangulia mbele za haki. Anayejua UHALISI WA JINA lake atujuze ili kuweka kumbukumbu sahihi.
 
ulivyombiwa ndivyo hivyo hivyo!kuna mwingine alikua anaitwa said salmin mziray yeye akajiita syllersaid mziray
 
ulivyombiwa ndivyo hivyo hivyo!kuna mwingine alikua anaitwa said salmin mziray yeye akajiita syllersaid mziray

umenikumbusha sheikh yahya, alitabir kuwa kw uchaguz mkuu wa 2010 kuna mgombea 1 wa urais atakufa. mara akafa huyu kocha mziray. sheikh yahya alipoulizwa vp akasema mauti ilikuwa inamtafuta mgombea 1 anaitwa peter kuga mziray
 
Kuna mtu aliwahi kuniambia Jina lake ni EDWARD SHEKIONDO lakini akalifanyia usanii akajiita EDDY SHEGGY. Namzungumzia kaka wa Christian Sheggy, mwanamuziki wa zamani wa Orchestra
Super Rainbow, na Washirika Tanzania Stars (Watunjatanjata). Ameshatangulia mbele za haki. Anayejua UHALISI WA JINA lake atujuze ili kuweka kumbukumbu sahihi.
MKUU huyu Mwanamuziki jina lake halisi alikua anaitwa EDWARD SHEMAHONGE, na sio SHEKIONDO kama ulivyoambiwa...!! duu umenikumbusha mbali wakati ule alipoibuka na wimbo wake maarufu uitwao "SHAKAZA PEE''.
 
walisemaaaaa dalili ya mvua ni mawinguuuuu,
nilimyempenda kanitoroka mamaaaaaaaaaaX 2

Nakumbuuka kuna mama yangu mdogo ndo alikuwa anaimba wakati huo enzi la club raha leo shooooooooooooooooooooo!
 
RIP Eddy Sheggy. Wimbo wa milima ya kwetu ulipangwa na kupangika vizuri sana!
 
No.
Its Edson Shekabughe na mdogo wake Christian Shekabughe

RIP nG'WOSHIE...........Edson

eddy+vijana.jpg
 
RIP nG'WOSHIE...........Edson

eddy+vijana.jpg


Jamaa alikuwa na sauti tamu huyu, sikiliza hizi nyimbo ndiyo utajuwa kuwa Tanzania tulikuwa na wanamuziki kweli si hawa wezi wa beats za watu na wauza unga.
Shakaza Pele (Bima Lee)
Milima Ya Kwetu (Super Rainbow)
Kumaliza Mwaka Taabu (Bima Lee)
Tangawizi (Super Rainbow)
Kapu La Mjanja original (Vijana Jazz)
Happy Massawe original (Vijana Jazz)
Wivu (Vijana Jazz)
Ngapulila, Pt. I (Vijana Jazz)
Mwisho Wa Mwezi (Vijana Jazz)

Kaka Eddy, unastahili pongezi na Mungu mwenyezi akuweke mahala pema peponi, Amina!
 
Eddy Sheggy,milima ya kwetu,r.i.p

Tancut Almas hii aisee ilkuwa kali sana na kama mtu yupo katika kipindi kigumu kama kapata msiba au amefulia anarudi nyumbani kwao kuna viashiria vinaonyesha kwamba anakaribia kufika hivyo akianza kuviona tu machozi yanamlengalenga
 
duu kweli muziki wa kale unamambo sii kidogo kumaliza mwaka mara mwisho wa mwezi..
 
Kwa hakika milima ya kwetu, mambo yote.

Kesho nitapita mitaani niitafute, maana inakila kitu na imekailika.

Eddy alikuwa wa aina ya pekee.
 
ulivyombiwa ndivyo hivyo hivyo!kuna mwingine alikua anaitwa said salmin mziray yeye akajiita syllersaid mziray

....na mwingine alikuwa mtangazaji wa RTD alikuwa anaitwa Benitho Kikoti yeye akajiita Ben Kiko.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom