sele200000
Member
- Dec 24, 2013
- 85
- 23
No coment atal
Mhh sijii mie!!! Lini utakuja mjinii
Mbeya na wenyeji wa Mbeya wamelala FURSA za kmwaga hususani biashara ya hoteli na vyakula lakini ndo hivyo tena. Mpo strategic mno RELI YA TAZARA, SONGWE AIRPORT, LAKE NYASA na mnapakana na MALAWI, ZAMBIA/ZIMBABWE/CONGO DRC na ni mji unaopitiwa na barabara kuu ya kihistoria CAPE to CAIRO. Bado mnambwela mbwela
Nani kakwambia kipimo cha maendeleo kinaangalia maambukuzi mapya ya UKIMWI? Unajua maambukizi mapya Unguja, Pemba, Lindi na Mtwara yakoje?Kwa sasa Mbeya inaongoza kwa Maambukizi Mapya ya UKIMWI. Nafikiri hilo ndo wana MBEYA wanalifanya kwa ufanisi mkubwa. Zaidi ni lile la kuanzisha makanisa/madhehebu kila kukicha
tatizo la mbeya mzunguko wa pesa ni mdogo ndio maana huwezi linganisha na moshi, arusha na mwanza, hata dodoma tu. labda uwingi wa watu ila kwa uzuri wa jiji hakuna kitu pale. mi nimeishi san apale na nimeolea hukuhuko in short huko ni kwetu, bado tunahitaji mabadiliko makubwa.
Unakosea unapojadili utofauti wa miji negatively - inabidi uwe positive. ni kweli wewe ni mgeni mbeya lazima uone tofauti iliyopo na miji kama mwanza kwa mfano. Mambo uliyoyazungumza sikubaliani nayo yote hasa hili la uchawi ambalo tuliache kwanza.
mwanza nayo haikuwa hivi miaka kama 25 iliyopita - hoteli kumbwa sana za kujivunia ilikuwa Mwanza hotel na kidogo lake hotel. Pamba ilikuwa almost ni guest house ya hali ya juu. hizi hotel ndo ziko comaparable na hizi ulizozitaja za mbeya. na wakati wote wawekezaji wakuu wa mwanza wakitoka Bukoba, Musoma, Shinyanga na Tabora - mzee Makinda RIP, baba yake spika Anne, amabaye alikuwa RC wa Tabora enzi hizo (1970s) aliwasihi waarabu na wahindi wa Tabora kwamba wasisahau kuinvest Tabora na kukimbilia Mwanza. hadi sasa kuna wafanya biashara toka Mbeya wame invest Mwanza.
Investment ya juu na haraka kwa Mwanza imekuja baada ya upandikizaji na uvunaji wa Sangara, uvunaji wa madini ya dhahabu Geita, Kahama, Tabora, Mara nk. Angalia Tanga - ulikuwa ndo mji wa pili kwa Dar shauri ya mkonge na wazungu matajiri wakiwa Lushoto etc - lakini baada ya hapo mji umedorora ingawa kwa mbali unarudi tena. Maana yangu hapa ni kuwa unlike Mbeya Mwanza ina utajiri wa maeneo jirani tajiri ambayo yanakwenda kuinvest kule. Ukija kwenye population Wasukuma tu pekee ni wengi kuliko kabila lolote Tanzania na ni matajiri na watumiaji wazuri, acha wana Kagera, Mara etc
Mbeya imejikaza kuwa katika hali hiyo mbele ya policies ambazo zimewatimua wafanya biashara kadhaa ambao wameelekea Dar, Mwanza na kwingineko. Policies za Mbeya kwa wawekezaji ni HARSH = kwa mfano kuna mtu alitaka kujenga 5-star hotel eneo la gymkana kati ya uwanja wa Sokoine na mbeya peak hotel alipigwa vita tena na viongozi wenyeji wa Mbeya - ubovu wa mji wa Mbeya unaletelezwa na aina ya uongozi walionao. watu wamekalia kula pesa - miaka ile world bank ilikuwa na master plan ya kui modernize the notorious Mwanjelwa - hakuna kilichofanyika imebaki ni the best squatter ya Tanzania!!
hii thread yako inafaa isomwe na viongozi wa Mbeya masikio na macho yazibuke.
Kuhusu uchawi sikubaliani nawe - ukitoka mbeya wanasema pwani wana majini. ukifika pwani ya dar wanasema unguja. ukifika unguja wanasema pemba. pemba wanasema tanga etc.
Amina! Mihangaiko yangu yooote nikiritire ni Mwanza. Hali ya hewa nzuri, Mazingira safi, Mji Mtulivu, Watu wastaarabu, Maji ya Kumwaga. Bila kusahau samaki! Mwanza wanapigania maeneo ya wazi yabaki kuwa wazi, bustani za jumuiya zinaendelezwa na zinatunzwa! Nawapongeza sana.
View attachment 162576
View attachment 162577
Malafyale mwanafyaleMalafyale ulikuguu?
Nina hasiraaa ntarudi baadae........
Mimi nafikiri Arusha inajulikana kimataifa zaidi ya Miji yote Tanzania....DAhh...ninabahati kuzaliwa Arusha..
Bukoba kuna hoteli nzuri kuliko Mbeya...bisha?:A S 13:
Umepanic sana...watu wa mbeya bado washamba sana na mambo ya majiji
Mtoa mada hii ya kutudharau wewe kwenu wapi?