Jiji la Mbeya kama kijiji

Jiji la Mbeya kama kijiji

Mbeya kwa namna yoyote haipaswi kuwa jiji kabla ya Dodoma. Yaani ni ujinga ulifanyika kuipa hadhi ya jiji
 
Umepanic wewe,yani unalilia uzuri wa maeneo miaka ya leo!!! wenzako tunaishi vijijini huku hata umeme hakuna but hatuna wasiwasi.Kuanza kujadili uzur ama ubaya wa maeneo ni UTOTO wa hal ya juu.Jitafakari



Acha kuongea upuuzi....huku Dar Wanyakyusa utawasikia Mbeya bwana, kumbe ni upuuzi mtupu yaani hakuna lolote zaidi ya uchawi.
 
The hammer,

Ni kweli kuna matetemeko mengi sana maeneo hayo na wao hutumia teknolojia sophisticated kidogo kurefusha majengo yao, tofauti na wakazi wa Mbeya ambao hawana kipato kikubwa kurefusha majengo yao kwa teknolojia hiyo.
 
andreakalima,

Moyo ukizidi kukuuma sana nenda kawambie serikali wabatilishe uteuzi ili tuendelee kuishi kama zamani kwani sie hatukuomba tuwe jiji ila ilitokea automatically kutokana na kukidhi vigezo kama idadi ya watu ambao wako takribani Mil 2.5, Shughuli za kiuchumi hususani kilimo, Mchango wake katika pato la taifa, Miundombinu barabara, Uwepo wa taasisi mbalimbali nyeti zikiwemo za elimu, banking nk. Climatic condition. Hizo ni baadhi tu ya cretaria chache ambazo wanaangalia mambo ya uzuri wa majengo ni very minor sana ktk utambuaji wa majiji, kumbuka majengo ni culture.
 
Kweli sababu wana uchumi mkubwa na wamejitahidi kielimu na ulewa kuliko Mbeya! chezea wagogo na wadigo kwa Elimu wewe!
tafuta ramani ya mpango mji wa hiyo mikoa alafu utoe comment yako
 
Moyo ukizidi kukuuma sana nenda kawambie serikali wabatilishe uteuzi ili tuendelee kuishi kama zamani kwani sie hatukuomba tuwe jiji ila ilitokea automatically kutokana na kukidhi vigezo kama idadi ya watu ambao wako takribani Mil 2.5, Shughuli za kiuchumi hususani kilimo, Mchango wake katika pato la taifa, Miundombinu barabara, Uwepo wa taasisi mbalimbali nyeti zikiwemo za elimu, banking nk. Climatic condition. Hizo ni baadhi tu ya cretaria chache ambazo wanaangalia mambo ya uzuri wa majengo ni very minor sana ktk utambuaji wa majiji, kumbuka majengo ni culture.

acha uongo wewe mbeya kama jiji halina watu 2.5m, mwanza yenyewe ndio inakimbilia milioni, au wewe unaongelea idadi ya watu wa mkoa wa mbeya? wakati mwanza inapata hadhi ya jiji ilikuwa jinsi ilivyokuwa mbeya bado hata hadhi ile haijafika, kwa maana nyingine mwanza ya 2000 bado ni nzuri kuliko mbeya ya 2014, ni barabara tu za mwanza zilikuwa na vumbi. Mbeya ni mji uliojaa wala rushwa, soko la matola wao walienda kujenga la kushindana kariakoo badala ya kujenga kitu cha maana kama shopping malls, na kulimalizia wameshindwa nafikiri ni zaidi ya miaka 4 au 5 sasa, mwanza wamenza kujenga mall kubwa miaka miwili iliyopita mwaka huu inaisha, arusha wanajenga nayo itaisha ya mbeya bado, dodoma wanajenga itaisha mbeya bado, kwa hiyo miradi ya maendeleo wanairoga wenyewe,miji ifuatayo itaipita mbeya muda wowote, dodoma iringa, moshi na mtwara
 
Kwa walio tembelea j'burg, South Africa watakubaliana na ukubwa na mindombinu safi ya jiji lile.Sasa issue ya msingi ni kwamba majengo marefu na barabara nzuri zina msaada gani kwa wakazi na wananchi? Ni eneo lenye umaskin na utapeli.

Mbeya ndio mzalishaji mkuu wa vyakula vingi hapa tz,na karibu kila mkazi wa pale ana kazi,biashara,kilimo au vyote,uchumi wa mby uko mikonon mwa wakazi wake.Ukubwa wa wilaya ya kyela tu, Dsm inaingia mara 4!Kuona maendeleo ya mkoa ukubwa vile sio rahis kwa wewe wa kuja.
 
Hii ni changamoto kwa wana MBEYA mna fursa nyingi sana, ukizingatia mmepakana na nchi jirani (Zisizo na bandari) nyingi kuliko mkoa wowote Tanzania, mna ardhi yenye rutuba, ziwa nyasa, sasa uwanja wa Ndege lakin mmeendekeza uchawi, ngono & sifa za kijinga. BADILIKENI vinginevyo WACHAGA wakija kukamata fursa msilalamike.
 
Kwa sasa Mbeya inaongoza kwa Maambukizi Mapya ya UKIMWI. Nafikiri hilo ndo wana MBEYA wanalifanya kwa ufanisi mkubwa. Zaidi ni lile la kuanzisha makanisa/madhehebu kila kukicha
 
Hotel ungeenda Green View mkuu ipo uzunguni ni standard na iko poa. Then mji kupewa sifa ya kuwa jiji hawaangalii mazingira tuu peke yake. Kuna ishu kama wingi wa watu na hiyo ndio sifa kubwa ya jiji la mbeya.

Alitaka tujue hotel alizoenda
 
Mbeya na wenyeji wa Mbeya wamelala FURSA za kmwaga hususani biashara ya hoteli na vyakula lakini ndo hivyo tena. Mpo strategic mno RELI YA TAZARA, SONGWE AIRPORT, LAKE NYASA na mnapakana na MALAWI, ZAMBIA/ZIMBABWE/CONGO DRC na ni mji unaopitiwa na barabara kuu ya kihistoria CAPE to CAIRO. Bado mnambwela mbwela
 
Kwa sasa Mbeya inaongoza kwa Maambukizi Mapya ya UKIMWI. Nafikiri hilo ndo wana MBEYA wanalifanya kwa ufanisi mkubwa. Zaidi ni lile la kuanzisha makanisa/madhehebu kila kukicha

mikoa
inayoongoza kwa maambukizi ya Ukimwi na
kiwango kwa asilimia kwenye mabano kuwa ni
Njombe (14.8), Iringa (9.1), Mbeya (9.0),
Shinyanga (7.4) na Ruvuma (7.0).
 
Mbeya na wenyeji wa Mbeya wamelala FURSA za kmwaga hususani biashara ya hoteli na vyakula lakini ndo hivyo tena. Mpo strategic mno RELI YA TAZARA, SONGWE AIRPORT, LAKE NYASA na mnapakana na MALAWI, ZAMBIA/ZIMBABWE/CONGO DRC na ni mji unaopitiwa na barabara kuu ya kihistoria CAPE to CAIRO. Bado mnambwela mbwela

Fursa ziko kwa ajili ya watanzania wote haijalishi ni mkoa gani. Mtu yeyote yuko huru kuzitumia popote pale usijifiche kwenye mgongo wa wanambeya. Kama umeziona fursa zitumie. Watanzania tunaongea mambo kimkumbo ila hatujui tunachoandika. Hakuna mkoa Tanzania hii uliokosa fursa za kiuwekezaji kwa wazawa. Tatizo linaloikumba Tanzania ni porojo kama hizi. Hatukai tukatathimini ni maendeleo gani tuliyochangia sisi au mimi binafsi ndani ya nchi yetu. Hivi katika hizo hotel, magholofa, vyuo, vituo vya afya, kumbi za starehe na vingine vingi unavyoona vinakupaisha mkoani kwako kipi unamiliki wewe binafsi? Au ndo mnasifia mali za watu huku mnaishi kwenye vibanda? Ndio nyie mnaokazana kila siku ukoo wenu unahela wakati wewe huna kitu na ni maskini wa kutupwa katika ukoo wenu.

Jitolee mfano wewe usitumie watu wengine kujisifia kimaendeleo. Dar es salaam haijajengwa na wazaramo wala wandengeko, Dodoma haijajengwa na wagogo wala wadigo, hata mwanza vilevile haijapendezeshwa na wasukuma pekee. Huko kote watanzania wametumia fursa sio wenyeji tu. WATANZANIA TUMIENI HIZO FURSA MNAZOZIONA MSIBWETEKE.
 
Juzi tulikuwa na mada hii kwenye daladala pale mbeya....kiukweli ni hamna kitu, New York iitwe eti Mbeya nayo inaitwa City!!
 
Back
Top Bottom