Jiji la Mbeya kama kijiji

Jiji la Mbeya kama kijiji

ukisikia jiji la mbeya utafikiri bonge la jiji kumbe upuuzi mtupu. sasa hapa kati nilipata safari ya mbeya nikakwepa fastjet ile kutua kwa kweli uwanja wa songwe ni mzuri kiasi (pengine kwa sababu ya upya) sasa tukapanda shuttle kwenda mjini 10,000/= (bei ya kulangua) nikafika hoteli ambayo ndio wanaisifia ni classic (Mbeya hotel) duuh ni kama nyumba ya makumbusho nikamuambia dereva nipeleke nyingine tukaenda Paradise Hotel (nayo ya kipuuzi pia) nikaenda nyingine (GR City) daah ndo nikajua kumbe zile sifa za wanyakyusa hapo Dar kwao hamna lolote sasa sehemu ya kula ndo ishu yaani labda uende CITY PUB hakuna sehemu nzuri ya kupata varieties. Poor Mbeya inastahili kuitwa KIJIJI CHA MBEYA si JIJI LA MBEYA mmekalia UCHAWI tu.
Porojo nyiiiiiiingi halafu utakuta kwenu ni Mtwara, f.ala wewe
 
ni kweli mbeya haina hadhi ile ya juu ya jiji,lakini hii lugha uliyotumia si nzuri kabisa kama mbeya ambayo ni miongoni mwa majiji ya tz unatumia lugha hii sipati picha ukizungumzia mikoa kama lindi
 
andreakalima,

Kaka nina wasiwasi na uelewa wako kuhusu miji. Naamini kama umetembea duniani usingeongelea chochote kuhusu miji ya Tanzania hususani Mbeya. Unaposema hakuna hotel, unamaanisha kiwango kipi ukifananisha na ipi na iliyojengwa na nani? Na kwani mji kuwa jiji wanaangalia hotel tu? Tanzania tuko nyuma sana ukilinganisha na nchi ambazo zimetuzidi lakini na sisi tunawazidi wachache. Mbeya iko nyuma ukilinganisha na Dar es Salaam. Sasa wewe wataka ulichokiona Dar kiwepo Mbeya. Jengo la NSSF lililopo Dar likawepo Mbeya.

Mimi nimeishi Mbeya na ninajua vizuri sana historia ya huo mji na wafanyabiashara wake. Mbeya imejengwa na nguvu za wananchi tena wengi wao hawajafika hata Dar. Mbeya hakuna AICC. Mbeya hakuna jengo lolote kubwa la serikali. Kila unachokiona kimetokana na nguvu za wananchi.

Kuna wafanyabiashara wakubwa wamepata utajiri toka mikoani na kwenda kujenga Dar es Salaam. Wengi wanakimbia mikoani hasa Mbeya kwa kuwa TRA huwafuatilia sana. Ukifungua tu duka, kesho asubuhi vijana wa TRA watakuwa getini. Lakini ukienda kufungua biashara Dar, nani atakubughudhi. Hivyo wafanyabiashara wengi waliotajirikia mikoani hususani Mbeya wanaenda kujenga Dar es Salaam. Wanaiacha Mbeya ikijengwa na wafanyabiashara wadogo, wakulima wadogo na wafanyakazi wa taasisi za serikali.

Sasa ndugu nikuulize ulitaka ukutane na hotel ya nyota ngapi hapo Mbeya?
 
ni kweli mbeya haina hadhi ile ya juu ya jiji,lakini hii lugha uliyotumia si nzuri kabisa kama mbeya ambayo ni miongoni mwa majiji ya tz unatumia lugha hii sipati picha ukizungumzia mikoa kama lindi

Tanzania watu wanajifanya wanajua saana huku hawasomi. Watu wanataka ili mji kuwa jiji basi ufanane na Nairobi, Joburg n.k. Hawajui kwamba kila nchi ina vigezo vyake vya kulipa eneo hadhi ya jiji. Watu wajue kwamba kuna vigezo vinavyotumika kubadirisha mamlaka ya miji na vijiji. Wanaangalia vingi. Wanaangalia idadi ya watu; uwezo wa kiuchumi; uwezo wa eneo kuwa kituo chenye shughuli nyingi za kibiashara, kiuchumi na viwanda; uwezo wa eneo kujiendesha lenyewe, katika kutoa huduma za kijamii kama elimu na afya; uwezo wa eneo kuwa kituo cha utawala; eneo kuwa ni kituo na au makutano ya miundombinu ya usafiri na usafirishaji kama barabara, reli, bandari na kiwanja cha ndege.
 
Kaka andreakalima unataka ili mji kuwa jiji basi ufanane na Dar es Salaam, Nairobi Joburg n.k. Au hujui kwamba kila nchi ina vigezo vyake vya kulipa eneo hadhi ya jiji. Kwa hadhi ya hizo hotel utakazo ulipaswa ujue vigezo vinavyotumika kubadirisha mamlaka ya miji na vijiji. Labda nikupe somo kwamba ili kuupa mji hadhi fulani wanaangalia vingi, tena vyote havihusishi hoteli. Wanaangalia idadi ya watu; uwezo wa kiuchumi; uwezo wa eneo kuwa kituo chenye shughuli nyingi za kibiashara, kiuchumi na viwanda; uwezo wa eneo kujiendesha lenyewe, katika kutoa huduma za kijamii kama elimu na afya; uwezo wa eneo kuwa kituo cha utawala; eneo kuwa ni kituo na au makutano ya miundombinu ya usafiri na usafirishaji kama barabara, reli, bandari na kiwanja cha ndege. Tunategemea mtakao makubwa mjue hata madogo.
 
Last edited by a moderator:
Naona kiongozi unatumia fursa kuupa promo mji wako, safi Sana. Ila kwa uchafu hatuchekani.

Mkuu mwanzoni mwa mwakaa huu ilifanyika kitu inaitwa Operesheni Safisha jiji.....Dahhhh......Yani mji kwasasa ni msafi zaidi ya Moshi...

Wamachinga wote wamefukuzwa katikati ya Jiji....Karibu Arusha
 
acha ujinga.kwani ili mji uitwe jiji kigezo ni MAJENGO?pia mbeya ni sehemu ambayo huwezi jenga ghorofa zaidi ya sita..na baridi la kule linapelekea watu kutopendelea kushinda mahotelini ..hakuna idadi kubwa ya machangu na starehe kutokana na mazingira .mwisho si kila jiji lifanane na hapa dar ngugu
pole sana..na nazani bei ya tax tu ulibargain sijui kama uliweza kuzunguka na tax sehamu zote hizo usiku..

Kwenye red nipe sababu Mr,
 
Ozzie,

Huyu jamaa angeenda new york angeanza fananisha na dar...kweli mbeya ni nguvu za wananchi
 
Hahahaaaa...... Utakuwa umepigwa kibuti na toto la mbeya ww . Hanna jiji la maana km hili. Hizo hotel ulizozitaja inawezekana labda huna hadhi nazo ndo maana unalalamika hata bei ya 10'000 to town. We bonge la mshamba hata dar unaisikia tu kwenye redio yako ya mbao.
 
Wewe unaonekana lofa mmoja hivi hata labda ndio safari yako ya kwanza kwa ndege (fastjet ya bei chee) nje ya huko dar.
Hebu, tuambie, bei ya shuttle ulitaka iwe buku moja??
Kuna viroja sijawahi ona.

Pia ungetumia lugha ya kistaarabu mbona watu wangekuelewa tuu, matusi na kashfa za nini?

Atakuwa kashikishwa ukuta kapanic maana inaonesha anajifanya mjanja. Analijua jiji la wajanja Hutu?
 
ok.mbeya,iringa na maeneo mengine yamezungukwa na bonde la ufa.ni miaka ya nyuma tuliona ushahidi wa matetemeko ya ardhi
Idimi
vip kuhusu nchi zenye matetemeko makubwa kila wakati kama china,indonesia,japan n.k zimewezaje kujenga majengo marefu sana....je umeshawahi kusikia man-made island,vipo Dubai kimoja kinaitwa palm island,Dubai na nchi za mashariki ya kati zinakumbwa sana na matetemeko lakini wamejennga kitu ma-engineer wanaita MEGA STRUCTURE ENGINEERING,hicho kisiwa.

Lakini kwa taarifa hiyo kauli yako ilishakanushwa na serikali muda flani hivi(miaka kama 3 hivi imepita),ukienda kwa mkuu wa mkoa coz ndo alitolea ufafanuzi hili na ikatolewa kwenye gazeti-utapata maelezo mazuri au hata engineer wa majengo wa mkoa.Hiyo kitu haipo Mr,nyanyuenu gorofa hata 100 juu..

Kuna mmoja hapa amesema mby imejengwa na wananchi-hiyo inaweza kuwa ndo sahihi kwamba uwezo wa kujenga majengo marefu hawana na nafikiri ndo sababu iliyotolewa na RC wakati huo
 
ukisikia jiji la mbeya utafikiri bonge la jiji kumbe upuuzi mtupu. sasa hapa kati nilipata safari ya mbeya nikakwepa fastjet ile kutua kwa kweli uwanja wa songwe ni mzuri kiasi (pengine kwa sababu ya upya) sasa tukapanda shuttle kwenda mjini 10,000/= (bei ya kulangua) nikafika hoteli ambayo ndio wanaisifia ni classic (Mbeya hotel) duuh ni kama nyumba ya makumbusho nikamuambia dereva nipeleke nyingine tukaenda Paradise Hotel (nayo ya kipuuzi pia) nikaenda nyingine (GR City) daah ndo nikajua kumbe zile sifa za wanyakyusa hapo Dar kwao hamna lolote sasa sehemu ya kula ndo ishu yaani labda uende CITY PUB hakuna sehemu nzuri ya kupata varieties. Poor Mbeya inastahili kuitwa KIJIJI CHA MBEYA si JIJI LA MBEYA mmekalia UCHAWI tu.

Wewe ulimwambia dereva unataka hotel ya buku10 ulitegemea akupeleke wapi?:beer:🙂
 
The hammer,

Sijakurupuka.tecnolojia yetu haijafikia kama za nje..na mbeya maeneo makubwa tu yapo bado hivo haina ulazima wa kujenga kwenda juu sana kwa saaasa kwa kutumia tecnolojia za gharama ok?
 
Umepanic sana...watu wa mbeya bado washamba sana na mambo ya majiji
 
mie sio mwenyeji wa Mbeya but hizo hotel unazotaja hapa mbona wala sio za kiwango? wewe ulimwambia huyo dereva tax unataka ya kiwango gan in terms of money? kuna Hill View mfano, mbona ni kiwango tu? au wewe hukufika huko?

Hakufika huko huyo. Hill view nimelala recently, huduma zake kama za hoteli kubea za Dar. Lkn pia Soweto na Sae kuna hoteli nzuri za viwango. Why Mbeya Hotel?
 
Back
Top Bottom