Jifunze kitu kupitia ujasusi..

Jifunze kitu kupitia ujasusi..

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
2,569
Reaction score
4,441
##Jifunze kitu kupitia #ujasusi..
**Kwenye ujasusi Mkuu wa operesheni ,kiongozi wa serikali akitaka
kujua kama Afisa usalama au jasusi anamletea taarifa za uongo au za ukweli unatumia mbinu hii.
πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»
**Unatuma maofisa wa usalama au majasusi tofauti kama 5 bila wao wenyewe kujuana ili kuchunguza taarifa Moja inayofanana 🀣🀣🀣🀣🀣🀣🀣.
**Kitendo hiki kinaitwa Cross-checking au independent corroboration.
**Misingi ya mbinu hii ya maofisa Kutofahamiana au kujuana
kama kuna mtu mwingine anayefanya kazi ambayo wamepewa lengo ni kuzuia kupikwa taarifa kwa pamoja,Hii njia inaitwa #compartmentalization

**Pia njia hii inasaidia Kupima Ukweli (Collusion Prevention), maana inazuia mawakala kula njama au kupotosha ukweli kwa pamoja.

**Mkuu operesheni hulinganisha taarifa kutoka Kwa mawakala wote ambapo Taarifa ikifanikiwa kufanana au kuendana kutoka vyanzo visivyowasiliana au kufamiana huaminika kuwa ya ukweli.njia hiii inaitwa #corroboration

πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»πŸ‘‡πŸ»
Njia hii unaweza kutumika kwenye maisha yetu ya kawaida mfano
*Unataka taarifa za masoko juu biashara unayofanya kutoka eneo fulani unaweza kutumia watu 6 tofauti ambao hawafamiani na hawajuani kukupatia taarifa then utalinganisha hizo kama Zina ukweli.
*Pia njia hii unaweza kutumika kupata taarifa za mtu unayetaka kumuoa unatumia watu 5 ambayo hawafamiani na Kufatilia huyo mtu ili waweze kukuletea taarifa ambapo utalinganisha hizo taarifa na kufanya maamuzi ..
1787747830559.jpg
 
Kumbuka binadamu tuna kitu kinaitwa confirmation bias. Unaweza ukatuma watu 6 tofauti, watano wakakuletea ukweli unaouma lakini yule mmoja tu akakuletea uongo mtamu zaidi unaotaka kuusikia. Kisaikolojia lazima utamwamini yule mmoja tu na kuwapuuza wale watano, hapo ndipo ujajusi hautokusaidia chochote.
 
Kumbuka binadamu tuna kitu kinaitwa confirmation bias. Unaweza ukatuma watu 6 tofauti, watano wakakuletea ukweli unaouma lakini yule mmoja tu akakuletea uongo mtamu zaidi unaotaka kuusikia. Kisaikolojia lazima utamwamini yule mmoja tu na kuwapuuza wale watano, hapo ndipo ujajusi hautokusaidia chochote.
Kijasus taarifa zikipishana una wamwaga wote 5 unaweka wengine wapya,ujajusi ndo unavyo pata taarifa zake kamili ivyo
 
Hapo ndipo utakapothibitisha kwamba wewe mkuu wa operesheni huna uwezo wa kufanya critical evaluation.
Uwez elewa iv vitu ad uwe kwenye mfumo,unaweza ukapewa Kaz ukajua uko peke yake kumbe Kuna watu 20 nyuma yako wanakufatilia Sasa we jichanganye
 
Uwez elewa iv vitu ad uwe kwenye mfumo,unaweza ukapewa Kaz ukajua uko peke yake kumbe Kuna watu 20 nyuma yako wanakufatilia Sasa we jichanganye
Sawa, tuchukulie uko kwenye huo mfumo wako. Sasa kama mkuu wa operesheni ana uwezo wa kuweka watu 20 nyuma yangu bila mimi kujua, maana yake yeye mwenyewe hawaamini hao watu wake.
 
Kumbuka binadamu tuna kitu kinaitwa confirmation bias. Unaweza ukatuma watu 6 tofauti, watano wakakuletea ukweli unaouma lakini yule mmoja tu akakuletea uongo mtamu zaidi unaotaka kuusikia. Kisaikolojia lazima utamwamini yule mmoja tu na kuwapuuza wale watano, hapo ndipo ujajusi hautokusaidia chochote.
Kwe kazi hii lazima uwe makini na confirmation bias. Ukijifungia tu kwenye echo chamber utatoka nunge.
 
Kwamba ndiyo wapo wengi kiasi hicho unachotaka kutuaminisha!!!! Ama unazungumzia nchi za Dunia ya kwanza?
 
Kumbuka binadamu tuna kitu kinaitwa confirmation bias. Unaweza ukatuma watu 6 tofauti, watano wakakuletea ukweli unaouma lakini yule mmoja tu akakuletea uongo mtamu zaidi unaotaka kuusikia. Kisaikolojia lazima utamwamini yule mmoja tu na kuwapuuza wale watano, hapo ndipo ujajusi hautokusaidia chochote.
Na wewe ukiuamini upande wenye chanzo kimoja ambao unakufurahisha tu ujue hufai kuwa kiongozi
 
Back
Top Bottom