Jifunze hapa kuhusu ALBADIR

Jifunze hapa kuhusu ALBADIR

Al Badr kwetu sisi tusioamini kuwepo kwa Mungu haina ukweli kama "dua" inayojibiwa na Mungu (Mungu hayupo, hivyo hawezi kujibu dua hii).

Ila, ina maana kubwa sana katika jamii. Inaonyesha kwamba watu wamechoka kiasi kwamba Mungu angekuwepo na angeweza kusikiliza dua hii, wangeitumia.

Ni namna mojaya kuwa isolate na kuwa shame watu wanaotumia ugaidi kufikia malengo yao maovu.

Kwa hiyo hata mimi ambaye siamini kuwepo kwa Mungu, na siamini kwamba dua huwa zinajibiwa na Mungu,naweza kuona maana ya hii Al- Badr from a purely social-psychological/ non-religious context.

Ni namna fulani ya jamii kulaani vitendo viovu.

Mkuu hivi vitu vipo kwani kuna mbeba mizigo pale sokoni Tanga Mjini anaitwa Khalfani Kigozi
hii ilitokana na watu kwenda kuiba Nazi kwa Shariffu kikapu basi akawatwanga na al-Badr ya mguu mmoja basi kilichotokea ni kile chuma walichofulia Nazi kilikatika hadi kuku aliyekula machicha nae alitangulia mbele ya haki na huyo Khalfani kigozi alibeba tuu hizo Nazi sokoni akapata masaibu humuangalii mara mbili
 
Mkuu hivi vitu vipo kwani kuna mbeba mizigo pale sokoni Tanga Mjini anaitwa Khalfani Kigozi
hii ilitokana na watu kwenda kuiba Nazi kwa Shariffu kikapu basi akawatwanga na al-Badr ya mguu mmoja basi kilichotokea ni kile chuma walichofulia Nazi kilikatika hadi kuku aliyekula machicha nae alitangulia mbele ya haki na huyo Khalfani kigozi alibeba tuu hizo Nazi sokoni akapata masaibu humuangalii mara mbili
Unajuaje kwamba hayo mambo yalitokea kutokana na Al-Badr na si kitu kingine chochote?
 
Ikipata wasomaji wa ukweli kwa kukidhi vigezo vya kuwa wasomaji wa halbadir basi ina madhara ya kudumu...... Huku kwetu iliwahi kupigwa marufuku na serikali maana ilifikia mpaka mwizi wa kuku tu anasomewa....matokeo jogoo anawika tumboni kuanzia kwa mwizi,mnunuaji,mpikaji ,mlaji ,mpaka mtupaji wa hizo taka!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kusoma Halal Badiri au Albadiri (Ahlul-Badr) Kwa Ajili Ya Kinga Na Kuapiza Ni Shirki Na Dhambi Kuu!


Albadir imetoka katika lugha ya Kiarabu lakini kupotolewa au kuandikwa na kusomwa makosa katika Kiswahili. Wapo wanaosema Alibadirilakini makusudio ni Ahlul-Badr, yenye maana watu wa Badr (wale waliopigana vita vya Badr). Badr ni sehemu iliyo karibu na Madiynah na ndio iliyokuwa sehemu ambayo Waislamu wakiongozwa na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) walipambana na mushirikina wa Makkah katika vita vya kwanza baina ya pande hizo mbili. Waislamu waliohudhuria walikuwa baina ya 313 – 317, lakini pamoja na idadi yao ndogo hiyo waliweza kuwashinda washirikina waliokuwa na idadi kubwa ipatayo mara sita yao.



Kisomo cha Ahlul Badri inakuwa ni kutaja majina ya Maswahaba (Radhiya Allaahu ‘anhum) mmoja baada ya mwingine. Katika kutaja huko ni Imani ya mwenye kusoma hao Maswahaba (Radhiya Allaahu ‘anhum) wanamsaidia kwa njia moja au nyingine. Ima kupata kitu alichopoteza au kilichoibiwa au kulaaniwa aliyefanya. Na hii katika Uislamu ni njia moja ya shirki ambayo Allaah Aliyetukuka na Mtume Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wameikema na kuipiga vita sana. Allaah Aliyetukuka Anasema:

“Hakika Allaah Hasamehe kushirikishwa, na husamehe yaliyo duni ya hilo kwa Amtakaye. Na anayemshirikisha Allaah basi hakika amezua dhambi kubwa” (4: 48). Shirki ni dhuluma kubwa sana.
Wewe mbn una ipinga sana umeshiriki kulitenda hili jambo? Kama umeshiriki Mungu akuue na kama hujashiriki kwa kuwakingia waovu waendelee kudhulumu nafsi zisizo na hatia uwe kichaa. Nyamaza watu hawa na viobgozi wao washughulikiwe, wenye kibri ya kuwadhuru wenzao.
 
Sijui nn sasa we ndo ujui Mungu wetu ni mmoja na alisema Samehe saba mara sabini,.. Nyie na matakbir yenu mnaleta shida dunia nzima sio kila jambo unatakiwa ulipize kwa damu, vingine vya kukaa mezani yanaisha,mnajiita chinja chinja
Utakoma hiyo swala hata wateteaji kama wewe haiwaachi salama mnaua kwa kukataa kupingwa tu. Au kupewa ushauri anza kujiandaa kuwa chizi.
 
Nalazimisha kwa sababu al-badr ni uongo.

Kama unabisha soma hapa tui test.

Mkuu hio huwa haisomwi hivi hivi.hadi uwe umefanya maovu kwa mfano umeina au umemdhulumu mtu au umedhamiria kutoa nafsi ya mtu..
Hio dua maana yake Mtu aliefanyiwa maovu kama hayo ndio anamshatakia Mungu wake na hukumu anamwachia Mungu wake
%90 Hua inaleta Majibu yake,
Na mara nyingi msomaji anahakikisha ni kweli alichofanyiwa..
Ukisoma tu kua umeibiwa kumbe unaidanganya Uma hua inakurudia mwenyewe,,
Sasa Mkuu ningekushauri kua bisha kitu ili uwelewe sio ubishe kitu ili mradi tu unabisha
 
Ngoja mimi nitie neno tu maana sielewi nasubiria matokeo

Aslaam Waleykum
 
Duu kwa hiyo kesho kuna kisomo cha albadir kwa waliomfanyia ubaya Tundu lissu?
Yaani hawa watu akili zao wanazijua wenyewe, waliouwawa kibiti ni waislam lakini hawakuona umuhimu wa kuisoma tena waliuwawa zaidi ya watu 30 lakini Leo lisu kakoswakoswa wanasoma hiyo albadir yao
 
Albadiri ni uchawi. Haihusiani na dini

Sent using Jamii Forums mobile app
Hofu yako no ipi?? Na isomwe tu na hata kama michango itahitajika tujulishane ili kulifanikisha hili, kwani kutaka kutoa nafsi ya binadamu mwenzako ni zaidi ya uchawi.

Na isomwe tu na ikibidi zisomwe nyingi tu za kutosha na kila aliyeshiriki apate mapigo yeye na ukoo wake wote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waislamu kwa visasi utazani mnaenda mbinguni wote,

.aya ngoja tuyaone kesho ayo,
Hofu yako no ipi?? Na isomwe tu na hata kama michango itahitajika tujulishane ili kulifanikisha hili, kwani kutaka kutoa nafsi ya binadamu mwenzako ni zaidi ya uchawi.

Na isomwe tu na ikibidi zisomwe nyingi tu za kutosha na kila aliyeshiriki apate mapigo yeye na ukoo wake wote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwa maelezo yako ni dhambi kuisoma hiyo Ahlul-badr
Hofu yako no ipi?? Na isomwe tu na hata kama michango itahitajika tujulishane ili kulifanikisha hili, kwani kutaka kutoa nafsi ya binadamu mwenzako ni zaidi ya uchawi.

Na isomwe tu na ikibidi zisomwe nyingi tu za kutosha na kila aliyeshiriki apate mapigo yeye na ukoo wake wote

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom