JF imevamiwa katika matangazo

JF imevamiwa katika matangazo

Tunzo

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2013
Posts
4,123
Reaction score
2,446
Kusema kweli nimeshafanya biashara na wakuu humu walio serious kwenye JF matangazo, ila sasa tumevamiwa humu, na Akina moderator watu wanajua hilo.

Tunatangaza biashara ila watu hawako serious unafikiri sio watu wazima, pia wengi ni ujinga wewe umeona gari imetangazwa ya M 55 alafu una comment nina M2, huo ni ujinga, usije ukaona watu watakusifu!

Kama huna pesa jiangalie hata pikipiki, hapo sasa pikipiki inatangazwa ya M1 na picha Juu tena namba kaweka mtu anacoment nitakupa elf 50 huo ni upumbavu, yani M1 mpaka 50.

Hebu wakuu tuwe serious na maisha, na alafu anayetangaza ana PhD alafu anaejibu kipumbavu hata six hajafika.

Usidhani mtu anaetangaza biashara ni hohehahe..
 
Niliweka Tangazo la mauzo ya nyumba, nikaweka picha, hizo picha moja ilipigwa ndani ya gari, wa kwanza kukoment, akahusisha utapeli sababu ya picha iliyopigwa ndani ya gari. Na waliofuata wengi wakaungana na yule wa kwanza. Bila kutoa vigezo vya maana, yani mtu sio mnunuzi, na wala uwezo wa. Kununua kinachouzwa hana ila anakua wa kwanza kuharibu, biashara za watu hapa.
 
Mkuu Tunzo,

Kwanza tunatoa pole sana kwa kukumbana na tatizo hilo. Hakika inakera na kukatisha tamaa.

Ifahamike kwamba tabia hiyo haikubaliki na ni kosa kwa mujibu wa JamiiForums Rules. Mwanachama yeyote akifanya mzaha kwenye uzi usiohitaji mizaha anakuwa ametenda kosa linaloweza kumpelekea kufungiwa.

Tunasisitiza, endapo mtakutana na wanachama wasio wastaarabu, tunaomba muwaripoti ili tuweze kushughulikia kwa haraka.

Tunaomba radhi kwa usumbufu mnaokumbana nao.

Wasalaam!
 
Niliweka Tangazo la mauzo ya nyumba, nikaweka picha, hizo picha moja ilipigwa ndani ya gari, wa kwanza kukoment, akahusisha utapeli sababu ya picha iliyopigwa ndani ya gari. Na waliofuata wengi wakaungana na yule wa kwanza. Bila kutoa vigezo vya maana, yani mtu sio mnunuzi, na wala uwezo wa. Kununua kinachouzwa hana ila anakua wa kwanza kuharibu, biashara za watu hapa.

Mkuu eeeh,naomba unielekeze jinsi ya kuweka picha kwenye version hii mpya ya JF,mm imenizingua sana
 
Mkuu eeeh,naomba unielekeze jinsi ya kuweka picha kwenye version hii mpya ya JF,mm imenizingua sana
Ingawa sio mwalimu mzuri nitajaribu. Kwa wanaotumia simu, iwapo umenzisha mada yako unataka kuweka picha au video, aidha unaka kuweka picha/video kwanza ama baada ya Maelezo. Nenda chini pandisha maabdishi huu chini utakuta maandishi yameandikwa, kushoto: Craete thread kulia: Upload a file bofya hapo kwenye upload a file itakupeleka moja kwa moja, sehemu ya mafaili yako simu unakohifadhia video/picha zako. Utachagua video/picha unayitaka utaipakia. Kama unachangia mada ya mtu unataka kuweka video/picha nenda kwenye send ambayo imeandikwa kwenye kisanduku cha bluu, huu take kulia Kuna mstari mweusi umejikunja Kama ofisi pini. Bofya hapo utakupeleka sehemu iliyoandikwa browse bonyeza hapo itakupeleka ulikotunza picha au video Na utaiweka.
wp_ss_20160223_0001.png
 
Tatizo watu hawajui matumizi ya haya majukwaa! Jukwaa la tangazo mtu analichukulia kama chit chat au hoja mchanganyiko! Na hawataki kuelewa hilo ! Pole sana ndugu, bado tunasafari ndefu
 
Ingawa sio mwalimu mzuri nitajaribu. Kwa wanaotumia simu, iwapo umenzisha mada yako unataka kuweka picha au video, aidha unaka kuweka picha/video kwanza ama baada ya Maelezo. Nenda chini pandisha maabdishi huu chini utakuta maandishi yameandikwa, kushoto: Craete thread kulia: Upload a file bofya hapo kwenye upload a file itakupeleka moja kwa moja, sehemu ya mafaili yako simu unakohifadhia video/picha zako. Utachagua video/picha unayitaka utaipakia. Kama unachangia mada ya mtu unataka kuweka video/picha nenda kwenye send ambayo imeandikwa kwenye kisanduku cha bluu, huu take kulia Kuna mstari mweusi umejikunja Kama ofisi pini. Bofya hapo utakupeleka sehemu iliyoandikwa browse bonyeza hapo itakupeleka ulikotunza picha au video Na utaiweka.View attachment 325007

Shukrani mkuu
 
Back
Top Bottom