Sipo
JF-Expert Member
- Jul 25, 2008
- 2,139
- 105
Nimeishi naye toka kabla sijazaliwa, ndio usishangae
Akanilea akanitunza, sikuona alipokosea
Sio Ukimwi, ni maneno ya watu ndio yanamchuria
Utanashati wake umemponza
Ustaarabu wake haukumlinda
Maisha yalipotononeka waswahili walifaidi kwa maneno
Sio Malaya ni nduguze, wabongo wameshupalia
Sio Ukimwi nasema aya ya kwanza nimemaliza
Chekechea hadi chuo kikuu ndie alinilinda
Wanae aliwapenda, kwa mkewe upendo ulianzia
Majirani wanamfahamu, wema wake wataunyumbua
Sio Ukimwi narudia aya ya pili imetimilika
Mawazo yalimganda, furaha ilimpotea
Wanafiki walifurahia, njaa ilipomwelemea
Wabongo walimponda Ukimwi umemnyemelea
Sio Ukimwi nakataa aya ya tatu ndio tamati
Sababu ninazo nyingi sio kidogo
Ingawa hampendi hapa ndio nazimwaga
Uchumi uliposinyaa familia ilidorora
Mke hana ajira, mwana wa kwanza kidato cha nne
Baba Mkwe kisukari kimemkaa, Bi Mkubwa presha juu juu
Sio Ukimwi mfunge yenu midomo mipana kama sufuria za shughuli
Aya ya nne kifungoni nimeitia
Ni kweli wembamba ulipamba na nguo kumpwaya
Peke yake barabarani alinongona, nywele hakutia kitana
Kosa sio lake uchumi ndio chanzo cha yote,
Kazi apate wapi pamoja na elimu kujaa tele
Sio Ukimwi nasema tena aya ya tano imeniponyoka
Familia aipeleke wapi?, Maulana ndio aliyomjalia
Akalime wapi ardhi ilishanyakuliwa vijijini
Akauze nini Kariakoo, Kilombero na Kisutu sokoni
Wachina wanauza hadi ubuyu na matango
Sio Ukimwi leo live nawapa mnaopenda majungu
Mbona hamkumsaidia mizigo ilipomwelemea
Jana usiku kaaga dunia maneno lukuki mwamtwisha kaburini
Sio Ukimwi nakataa, Ukweli nimewapasulia
Akanilea akanitunza, sikuona alipokosea
Sio Ukimwi, ni maneno ya watu ndio yanamchuria
Utanashati wake umemponza
Ustaarabu wake haukumlinda
Maisha yalipotononeka waswahili walifaidi kwa maneno
Sio Malaya ni nduguze, wabongo wameshupalia
Sio Ukimwi nasema aya ya kwanza nimemaliza
Chekechea hadi chuo kikuu ndie alinilinda
Wanae aliwapenda, kwa mkewe upendo ulianzia
Majirani wanamfahamu, wema wake wataunyumbua
Sio Ukimwi narudia aya ya pili imetimilika
Mawazo yalimganda, furaha ilimpotea
Wanafiki walifurahia, njaa ilipomwelemea
Wabongo walimponda Ukimwi umemnyemelea
Sio Ukimwi nakataa aya ya tatu ndio tamati
Sababu ninazo nyingi sio kidogo
Ingawa hampendi hapa ndio nazimwaga
Uchumi uliposinyaa familia ilidorora
Mke hana ajira, mwana wa kwanza kidato cha nne
Baba Mkwe kisukari kimemkaa, Bi Mkubwa presha juu juu
Sio Ukimwi mfunge yenu midomo mipana kama sufuria za shughuli
Aya ya nne kifungoni nimeitia
Ni kweli wembamba ulipamba na nguo kumpwaya
Peke yake barabarani alinongona, nywele hakutia kitana
Kosa sio lake uchumi ndio chanzo cha yote,
Kazi apate wapi pamoja na elimu kujaa tele
Sio Ukimwi nasema tena aya ya tano imeniponyoka
Familia aipeleke wapi?, Maulana ndio aliyomjalia
Akalime wapi ardhi ilishanyakuliwa vijijini
Akauze nini Kariakoo, Kilombero na Kisutu sokoni
Wachina wanauza hadi ubuyu na matango
Sio Ukimwi leo live nawapa mnaopenda majungu
Mbona hamkumsaidia mizigo ilipomwelemea
Jana usiku kaaga dunia maneno lukuki mwamtwisha kaburini
Sio Ukimwi nakataa, Ukweli nimewapasulia