Mkutano wa MEM Tarehe 24 Septemba, 2013, Katibu Mkuu MEM aliitisha mkutano kwa ajili ya kujadili maombi ya Serikali ya kuruhusu kutolewa kwa fedha za escrow. Mkutano huu ulimshirikisha Gavana wa BoT, Katibu Mkuu Hazina (PST), Mwakilishi wa AG na wawakilishi wa TANESCO. Katika mkutano huu, BoT ilitoa hoja ambazo ilitaka zizingatiwe kabla ya kutolewa kwa ruhusa ya kutolewa kwa fedha hizo. Hoja hizo ni: (i) (ii) Ushahidi kwamba hisa za Mechmar zinamilikiwa na PAP na ushahidi kwamba umiliki huo umesajiliwa na BRELA; Ushahidi wa suluhu ya mgogoro kuhusu tozo kati ya IPTL na TANESCO na kwamba suluhu hiyo imeamuliwa kwa manufaa ya (iii) IPTL; Iwapo IPTL na GoT wako tayari kusamehe riba inayotolewa kwa dhamana za Serikali ambako fedha za ¡ùEscrow¡ì zimewekezwa, endapo uwekezaji katika dhamana hizo utakatizwa kabla ya (iv) wakati (pre-mature redemption); Nini kauli ya Wizara ya Fedha kuhusiana na uamuzi wa kutolewa kwa fedha hizi na iwapo uongozi wa Kitaifa una habari na suala (v) hili; na Iwapo GoT imejihadhari na uwezekano wa madai yanayoweza kufunguliwa na wadai mbalimbali, wakiwemo Standard Chartered Bank (Hong Kong) ambao wanasemekana kuidai IPTL. 4.1. Timu ya Wataalam
Baada ya majadiliano, iliagizwa kwamba iundwe Timu ya Wataalam ili kuzifanyia kazi hoja zilizoibuliwa na kujadiliwa, na kuwasilisha Ripoti kwa PS ÿ MEM kwa ajili ya hatua muafaka. BoT iliwakilishwa katika timu hiyo ambayo iliwasilisha Ripoti yake tarehe 30 Septemba, 2013, ikiwa