Idara ya usalama wa Taifa, iliondoka na Mwalimu Nyerere alipofariki mwaka 1999, baada ya kuondoka Mwalimu,Idara hiyo yenye majukumu nyeti sana kwa nchi,ikabadilisha kinyemela majukumu yake na kuwa usalama wa watawala wa CCM!
Hivi katika mazingira ya kawaida pesa zote hizo bilioni 321, ambazo zilipaswa zirejeshwe TANESCO, wajanja wachache wakaamua kuzi-hijack,na kuanza kuzigawa kama njugu, bila intelejinsia ya policcm wala usalama wa Taifa kustukia, hivi katika mazingira hayo waTZ, tuna haja gani ya kuendelea kukiita kitengo hicho Idara ya usalama wa Taifa,badala ya jina wanalostahili la Usalama wa watawala wa CCM?
Hata mkiangalia 'movements' zote zinazofanywa kwa sasa na Idara hiyo kwa sasa ni kufanya juhudi zote za kufa na kupona, kuhakikisha ripoti hiyo ya CAG haitingi bungeni tarehe 26 ili ijadiliwe,kwa lengo moja tu la kuwaokoa na dhahma inayoelekea kuwakuta watawala wa CCM kutokana na skandali hiyo ya Escrow/IPTL!