JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

niwakati muafaka wa kuisoma na kuielewa ripoti nzima ili tutoe hukumu stahiki kwa kila mhusika... Rais ana vyanzo vingi sana vya kuthibitisha uhalisia wa jambo! something is wrong kwenye taasisi ya urais... namhurumia rais wangu, nawahurumia sana watanzania makabwela... Mkombozi Bank imulikwe kwa undani zaidi...
 
Sasa kama yana baraka za Rais kinamshinda nini kufanya maamuzi magumu mara moja tukamaliza hii sintofaham? Kwa hiyo unataka tuamini huko USA kaenda ili awaache walio chini yake (watoto) waparurane utadhani hakuna baba mwenye nyumba?
haya mambo yanafuata process sio kukurupuka,sasa ni mda wa bunge,part y rais kuact haijafika na hawezi kuingilia,ndo maana ya kuwepo PAC
 
Sijui kwa nini watu wanasubiri hadi wafukuzwe.

Hata kama haujahusika moja kwa moja suala la jina lako kuwepo tu kwenye taarifa hii na ahukuweza kuzuia uovu huu usitokee maana yake siku ya mwisho utakuwa umeshiriki.

Ingekuwa uwajibikaji tunaoongea kila siku ni kwa kila mtu, wote waliotajwa wangejiodokea kwa aibu iliyosababishwa na taasisi wanazo ziongoza. Lakini wa kwetu utasikia namsikiliza aliyeniteua aamuwe. Hiyo siyo kuwajibika bali kufukuzwa.
 
Tena kikwete ndo anabidi aanze yeye kuwajibika then wa chini watafuata.hawa BoT wapo smart sana kutokana na scandal za huko nyuma.
 
Mara nyingi huwa nalazimisha akili yangu kukataa ule usemi wenzetu wanaosema sisi mweusi ni baboon, sasa kwahaya niliyoyashuhudia Kwa kipindi cha takribani miaka kumi nafsi inanisuta
 
Tunasubiri, tukiwa hai ukweli utajulikana, lakini nionavyo nguvu inayotumika mitandaoni kuuaminisha uongo ni imesha flop na haina mshiko.

Ngoma ikivuma sana hupasuka.

Jitafakarini kwanini asilimia kubwa sana yamafisadi wanatokea Kidumu na nyie mnashangilia
 
Hivi anasubiri nini huko Marekani alipo,atapata heshima zaidi kama atampa msaiidizi wake ''RESIGNATION NOTICE'' ya saa 24 aikabidhi bungeni kabla hajaumbuka zaidi.Heshima yooooote aliyokuwa nayo kwa sasa imeyeyuka kama bonge la barafu.
Hakuwa na heshima yoyote huyu
 
Huu uzi simuoni mwenye id ya Faizafox....alikesha uzi mwengine unaofanana na huu akitetea serikali ya jk....

Hii kashifa sawa na Richmond ndo maana walishindwa kuvuana gamba....el akakanyaga moto chini akiutaka urais kama walivyokubaliana....sasa si jui bado anautaka au amebadilisha mawazo.
 
kama mkuu wa kaya alibariki basi ashughulikiwe tu,yeye amekua bingwa wa kuwadharau wazee walio mpokea ndani ya chama na kumpa fursa,kama akina mzee warioba,aliwapa kazi alafu akaenda wadhalilisha bungeni na juzi wanafanyiwa fujo amekaa kimya tu akimaanisha shauli yao sasa,kama amehusika bunge lijadili serikali iondoke tufanye uchaguzi.
 
Hamna kazi hapo ya kutafuta mbaya nani,
Inaskitisha pale wanapowajibishwa pasipo kufunguliwa mashitaka ya wizi.

Ni zaidi ya usanii, na hata maamuzi ya jambo hili yatakuwa ni ya kisanii tu.
 
Naanza kuunganisha dots kwa nini Rweyemamu ali disclose ugonjwa wa rais haraka haraka kitu ambacho si kawaida yake hasa ukizingatia ugonjwa wenyewe.

Mkuu we umeona mbali,ilikua ni ku draw our attention ili escrow ipite,tumeshituka.
 
Huu uzi simuoni mwenye id ya Faizafox....alikesha uzi mwengine unaofanana na huu akitetea serikali ya jk....

Hii kashifa sawa na Richmond ndo maana walishindwa kuvuana gamba....el akakanyaga moto chini akiutaka urais kama walivyokubaliana....sasa si jui bado anautaka au amebadilisha mawazo.

Sio ff tu wale wote wa lumumba hawatii mguu humu.
 
Back
Top Bottom