JESHI LA POLISI: kwepeni aibu Hii

JESHI LA POLISI: kwepeni aibu Hii

kasanga70

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2015
Posts
227
Reaction score
517
Wiki zima nimekuwa na safari za gongo la mboto to chanika! Aibuuu!
Kati ya g/mboto to chanika kuna kilomita kati ya 18/20 hv. Traffic police vituo 5
Nimeshuhudia haya kila Sikh
Gongo la mboto basi linasimamishwa traffic anakimbiziwa tsh elfu 2000, baghdad mwisho wa lami basi linasimamishwa traffic anapokea tsh 2000 pugu shuleni basi linasimamishwa traffic anapokea tsh 2000 kigogo fresh kituo cha kwa pinda basi linasimamishwa mikwara kibao anapewa elfu 2000 kabla ya Kwazoo opposite na Uhuru town basi linasimamishwa elfu 2000 inatoka hapa konda machozi yanamlengalenga anamwambia dereva akapaki gari kazi haifanyiki, kituo cha mwisho na cha sita magenge karibu na hospital mpya basi linasimamishwa dakika 10 elfu 3000 inatoka konda katepeta vibayaaa sana.

Jeshi letu nini hiki jmn!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Umbali wa km 18 vituo 6 Vya ukaguzi mmewahi kuona wapi jambo hili??? Askari ana mshahara konda hana mshahara hata hicho kdg kinanyang'anywa???? Bado hajapeleka hesabu! Kuweni watu basi huu ni unyama ambao hata shetani huwa anahuruma!
Imeniuma sana
 
Rushwa ni adui wa haki,,wasimamizi wa haki na sheria ndo wala rushwa wakubwa,,
Rushwa na Africa ni kama pete na kidole,
 
mbona hela enyewe kidogo tu?,elfu mbili si kwa ajili ya kiwi tu,mi kwakweli sioni tatizo,matrafic wetu wanafanya kazi kubwa sana barabarani,hiyo ni motisha tu
 
mbona hela enyewe kidogo tu?,elfu mbili si kwa ajili ya kiwi tu,mi kwakweli sioni tatizo,matrafic wetu wanafanya kazi kubwa sana barabarani,hiyo ni motisha tu
Daaa! Aisee
 
Gari kumi mara efu mbili kwa siku efu 20...
Kwa mwezi laki 6...
Ada ya mtoto shule mwaka mzimaaaa....
mbona hela enyewe kidogo tu?,elfu mbili si kwa ajili ya kiwi tu,mi kwakweli sioni tatizo,matrafic wetu wanafanya kazi kubwa sana barabarani,hiyo ni motisha tu
 
Duuuhhhhh! Hawa watu huwa najiuliza maswali mengi sana kuhusu wao. Je mshahara wao ni mdogo kiasi kwamba hauwatoshi au ni tabia zao tu?

Hawa ndiyo chanzo kikubwa cha ajari barabarani na si vinginevyo.
 
Nimeamua Kujipanga Kazi Ya Kutumbua Jipu
 
Duuuhhhhh! Hawa watu huwa najiuliza maswali mengi sana kuhusu wao. Je mshahara wao ni mdogo kiasi kwamba hauwatoshi au ni tabia zao tu?

Hawa ndiyo chanzo kikubwa cha ajari barabarani na si vinginevyo.
Kinachotia uvivu zaidi gari hiyohiyo inakaguliwa Lila Siku? Abiria mnapotezewa muda weee kumbe inahitajika elfu 2 tuu! Tunasafari ndefu sana
 
Wiki zima nimekuwa na safari za gongo la mboto to chanika! Aibuuu!
Kati ya g/mboto to chanika kuna kilomita kati ya 18/20 hv. Traffic police vituo 5
Nimeshuhudia haya kila Sikh
Gongo la mboto basi linasimamishwa traffic anakimbiziwa tsh elfu 2000, baghdad mwisho wa lami basi linasimamishwa traffic anapokea tsh 2000 pugu shuleni basi linasimamishwa traffic anapokea tsh 2000 kigogo fresh kituo cha kwa pinda basi linasimamishwa mikwara kibao anapewa elfu 2000 kabla ya Kwazoo opposite na Uhuru town basi linasimamishwa elfu 2000 inatoka hapa konda machozi yanamlengalenga anamwambia dereva akapaki gari kazi haifanyiki, kituo cha mwisho na cha sita magenge karibu na hospital mpya basi linasimamishwa dakika 10 elfu 3000 inatoka konda katepeta vibayaaa sana.

Jeshi letu nini hiki jmn!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Umbali wa km 18 vituo 6 Vya ukaguzi mmewahi kuona wapi jambo hili??? Askari ana mshahara konda hana mshahara hata hicho kdg kinanyang'anywa???? Bado hajapeleka hesabu! Kuweni watu basi huu ni unyama ambao hata shetani huwa anahuruma!
Imeniuma sana
Hzo 2000 inaanziaga kituo cha makumbusho pale kona ya kuingilia, kisha pale Kwa Manjunju anakaaga pia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom