Jeshi la Israel limeanza kuingia Gaza

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,317
11,181
Kulingana na radio ya Israel vikosi vya IDF vimefanya mashambulizi makubwa ndani ya Gaza usiku wa kuamkia leo. Hata hivyo taarifa zaidi za mashambulio hayo dhidi ya Hamas hayajwekwa wazi.

Habari hizo zinafuatia ahadi ya hapo jana ya waziri mkuu wa nchi hiyo aliposema mashambulio ya kuingia Gaza yapo karibu kuanza lakini akasita kutaja ni siku gani yangeanza. Na pia yanakuja wakati viongozi wa nchi za Ulaya wakikutana kujadili vita hivyo na umuhimu wa kuruhusu misaada ya kibinadamu kwa Gaza.

Katika mkutano huo wa viongozi wa Ulaya,raisi Macron wa Ufaransa aliitahadharisha Israel kuwa kuingiza vikosi vya IDF itakuwa ni kosa kubwa itakalolifanya nchi ya Israel
Kwa takriban wiki mbili tangu patokee mashambulizi ya kushtukiza ya Hamas waziri mkuu wa Israel amekuwa katika malumbano na waziri wake wa ulinzi kuhusu uharaka wa kuingiza vikosi hivyo Gaza.

Wakati waziri wa ulinzi akihimiza kufanyika zoezi hilo kwa haraka kuokoa moyo wa kutaka kupiga wa askari wake walionao, waziri mkuu amekuwa akiakhirisha vita vya ardhini kwa kuhofia yatakayozuka hasa akiwafikiria Hizbullah.

Israeli army carries out a “relatively large” ground incursion into the Gaza Strip overnight to attack Hamas positions, according to the Israeli army radio.Aljazeera
1698301194349.png
 
Walipewa masharti nafuu sana kuwa wawaachie mateka mambo yaishe,
Msimamo wa Israel ni kwamba hata wakiwaachia mateka wote basi vita vitaendelea na hakuna kupelekewa misaada hasa mafuta.Sasa yanini Hamas wawachie na hakuna watakachokipata mwishowe.
 
Hamas wakubali wanawatesa wapalestina sana
Kati ya Hamas na Israel nani anamtesa mwenzake zaidi..
Wako waliotii amri za jeshi la IDF na bado wakauliwa kwenye mikokoteni na kwenye manyumba waliyofikia kusini ya Gaza.Kwa ufupi katika historia yote ya mayahudi hakuna kutekeleza ahadi wala kuheshimu mikataba.
 
Kulingana na radio ya Israel vikosi vya IDF vimefanya mashambulizi makubwa ndani ya Gaza usiku wa kuamkia leo. Hata hivyo taarifa zaidi za mashambulio hayo dhidi ya Hamas hayajwekwa wazi.

Habari hizo zinafuatia ahadi ya hapo jana ya waziri mkuu wa nchi hiyo aliposema mashambulio ya kuingia Gaza yapo karibu kuanza lakini akasita kutaja ni siku gani yangeanza. Na pia yanakuja wakati viongozi wa nchi za Ulaya wakikutana kujadili vita hivyo na umuhimu wa kuruhusu misaada ya kibinadamu kwa Gaza.

Katika mkutano huo wa viongozi wa Ulaya,raisi Macron wa Ufaransa aliitahadharisha Israel kuwa kuingiza vikosi vya IDF itakuwa ni kosa kubwa itakalolifanya nchi ya Israel
Kwa takriban wiki mbili tangu patokee mashambulizi ya kushtukiza ya Hamas waziri mkuu wa Israel amekuwa katika malumbano na waziri wake wa ulinzi kuhusu uharaka wa kuingiza vikosi hivyo Gaza.

Wakati waziri wa ulinzi akihimiza kufanyika zoezi hilo kwa haraka kuokoa moyo wa kutaka kupiga wa askari wake walionao, waziri mkuu amekuwa akiakhirisha vita vya ardhini kwa kuhofia yatakayozuka hasa akiwafikiria Hizbullah.

Israeli army carries out a “relatively large” ground incursion into the Gaza Strip overnight to attack Hamas positions, according to the Israeli army radio.Aljazeera
Bbc wanasemaje?
 
NILIPOKUA MDOGO MIAKA YA SITINI WAKATI HUO TANGANYIKA NDIO IMEUNGANA NA ZANZBAR NILIBAHATIKA KUONA HARAKATI ZA WARAABU PALE CAIRO NA DAMASCUS WAKATI WANAJIANDAA NA KUIVAMIA ISRAEL MWAKA 1967.
KILICHONIFURAHISHA NI ZILE NYIMBO ZAO ZA KISHUJAA KWENYE MIHADHARA.
"""" TUTAFIKA TEL AVIV KESHO"""
""""HAIFA TUTAFIKA JIONI"""
"NA JERUSALEM TUTAICHUKUA ASUBUHI"
NB : KILICHOWAKUTA MPAKA LEO HIZO NYIMBO WAMEZIFUTA KWENYE KUMBUKUMBU.NITAANDIKA HUU UZI KUELEZEA MADHARA YA KUONGEA SANA BILA VITENDO ILIVYOWAGHARIMU WAARABU 1967.
 
Hii sio akili ni maji ya mtaro
Sasa ulikuwa na haja gani ya kinikejeli hali ya kuwa nimekuuliza swali?

Nimekuuliza hivyo kwa sababu viongozi wa Israel wamesha sema kuwa mpaka hamas iangamizwe ndo vita ihishe sasa ww una tuambia kuwa waachie mateka ili vita iishe ,ndio maana nimekuuliza ya kuwa ajenda ya kuianfamiza hamas imewekwa pembeni?
 
Kati ya Hamas na Israel nani anamtesa mwenzake zaidi..
Wako waliotii amri za jeshi la IDF na bado wakauliwa kwenye mikokoteni na kwenye manyumba waliyofikia kusini ya Gaza.Kwa ufupi katika historia yote ya mayahudi hakuna kutekeleza ahadi wala kuheshimu mikataba.
Mkuu hiyo historia ya mayahudi na maarabu kuhusu mikataba umeisoma wapi na sisi tupate elimu kuwahusu hao mayahudi na maarabu.
 
Back
Top Bottom